Wednesday, July 2, 2014

PWANI WAANZA UANDIKISHAJI VITAMBULISHO VYA TAIFA




Na John Gagarini, Kibaha
Mkuu wa mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza amewataka wakazi wa mkoa huoa kujitokeza kwenye zoezi la uandikishaji wa vitambulisho vya Taifa linaloanza leo mkoani humo kwani  zoezi hilo ni muhimu sana linasaidia na ni  mfumo mkuu wa utambuzi na usajili wa watu na mifumo mingine ya serikali.
Mahiza amesema kuwa vitambulisho vitasaidia kupunguza riba ya mikopo ya benki, kuondoa ukiritimba wa kufungua akaunti, kutambua wakwepaji wa kurejesha mikopo ya benki, kupunguza wafanyakazi hewa, kupata malipo ya pensheni, haki za matibabu, kuwatofautisha wageni na wakimbizi na rai wa Tanzania.
Ameyasema hayo mjini Kibaha wakati wa uzinduzi wa zoezi la usajili na utambuzi wa watu mkoa wa Pwani uliowahusisha wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa halmashauri, wanasiasa na viongozi wa dini.
Kutokana na kutotambulika wananchi hao kumesababisha wameshindwa kujiongezea uwezo wa kipato chao pamoja na cha Taifa hali ambayo imefanya uchumi  kushindwa kukua.
Kwa upande wake mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa Dickson Maimu amesema kuwa Maimu amesema kuwa kutokana na wananchi hao kutokuwa na utambulisho imesababisha kushindwa kunufaika na rasilimali fedha na fursa zingine kutokana na kutotambuliwa rasmi na mifumo husika.
Amesema Kutokana na hali hiyo serikali imaenza kutoa vitambulisho vya Utaifa ambavyo sasa vitawafanya wananchi wa Tanzania kutambulika na wale wasio raia nao watatmbuliwa hivyo kila kundi litajulikana.
Aidha amesema kuwa wananchi hao endapo watapatiwa vitambulisho wataweza kujijengea uwezo wao wenyewe kupitia taasisi za kifedha na sehemu nyingine hivyo kufanya uchumi wan chi kukua pia kwa wale wanaokopa mkopo utachukua muda mfupi.
Amebainisha kuwa Wananchi wanapaswa kujitokeza kutoa taarifa zao ili waweze kupata vitambulisho hivyo vya utaifa kwani mtu kama utaifa wako hautambuliki basi inakuwa ni tatizo na kushindwa kupata fursa mbalimbali.
Zoezi hilo lilianza mkoa wa Dar es Salaam na Zanzibar na sasa limeanza mkoa wa Pwani tangu Julai Mosi mwaka huu na na baadaye Lindi, Mtwara, Morogoro, Tanga na Kilimanjaro ambapo wananchi wanatakiwa kutoa taarifa sahihi ili kuweza kupatiwa vitambulisho vya Utaifa.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment