AMWUA MKEWE KWA WIVU WA MAPENZI
KIJANA aliyetambuliwa kwa jina la Omary Molel
mkazi wa Kijiji cha Mwanabwito kata ya Ruvu wilayani Kibaha mkoani Pwani
anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka (25) anatuhumiwa kumwua mchumba wake Sina
Hamis (21) kwa kumchoma kisu kutokana na wivu wa mapenzi.
Mtuhumiwa huyo ambaye alikuwa akifanya kazi ya
kusimamia shamba la mtu pamoja na kufanya kazi ya bodaboda anatuhumiwa kufanya
mauaji hayo nyumbani kwa wakwe zake baada ya kuona kuwa mkewe amegoma kwenda
kwake kutokana na ugomvi uliokuwepo baina yao.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia
ya simu mwenyekiti wa Kijiji cha Boko Mnemela Hassan Mohamed amesema kuwa tukio
hilo limetokea Julai 27 majira ya saa mbili asubuhi.
Mohamed amesema kuwa siku moja kabla ya tukio
hilo Julai 26 mtuhumiwa huyo akiwa na amesindikizwa na mtu mmoja ambaye jina
lake bado halijapatikana walikuwa na kikao cha kusuluhishwa baada ya
kuhitilafiana na kikao hicho kilifanyika
nyumbani kwa wazazi wa marehemu.
Amesema kuwa Kwa mujibu wa watu waliohudhuria
kikao hicho wamesema kuwa kikao hicho kilifanyika kuanzia majira ya saa 2 usiku
hadi saa 5 usiku ambapo hata hivyo mwafaka haukuweza kufikiwa kwani marehemu
alikataa kwenda kwa mume wake.
Aidha amessema kuwa siku iliyofuata watu
waliokuwa wakihusika kusuluhisha waliondoka na yeye pamoja na mtu aliyeambatana
naye waliondoka lakini ghafla alirudi akidai kuwa anafuata betri ya simu
aliyoisahau nyumbani kwao na marehemu.
Alimkuta mkewe akipepeta mchele jikoni na kuanza
kumbembeleza lakini inaonekana aligoma kabisa kurudi kwa mumewe hali ambayo ili
mkasirisha mumewe na kuanza kumchoma kwa kutumia kisu huko jikoni kisha
wakatoana nje huku marehemu akipiga kelele.
Ameongeza kuwa Mtuhumiwa alimchoma marehemu
kwenye ziwa la upande wa kulia na kwenye uti wa mgongo karibu na bega la upande
wa kushoto na alimchoma kisu mbele ya bibi yake mama yake wa kufikia na mdogo
wake ambao walipiga kelele na kushindwa kumsaidia ambapo mtuhumiwa huyo
alikimbia maporini.
Mwenyekiti huyo alipoulizwa juu ya chanzo cha
mauaji hayo amesema kuwa kwa mujibu wa watu waliokuwa wakijua ugomvi wao
walisema kuwa mtuhumiwa alikerwa na tabia ya mkewe kurudishiwa zaidi chenchi
anapokwenda kwenye duka lililopo kijijini hapo.
Ameongeza kuwa Marehemu alikuwa akimjulisha
mumewe juu ya hali hiyo ambapo inasemekana aligoma kurudi kutokana na kuambulia
vipigo na kutishiwa kuuwawa na mwanaume huyo na kupelekea kufanyika kikao cha
usuluhishi na muuza duka kifanyika ili kupata mwafaka lakini ikashindikana na
kutokea mauaji hayo ya kusikitisha.
Kwa upande wa kamanda wa Polisi mkoani Pwani
Kamishna Msaidizi Mwanadamizi wa Polisi (SACP) Ulrich Matei amekiri kutokea kwa
tukio hilo na kusema kuwa mtuhumiwa huyo anatafutwa ambapo jitihada hizo bado
hazijazaa matunda.
No comments:
Post a Comment