Wednesday, July 2, 2014

WASOMALI 11 WADAKWA




Na John Gagarini, Kibaha

HUKU zoezi la kuandikisha usajili na utambuzi wa watu mkoa wa Pwani kuanza zoezi hilo Julai 2 mwaka raia 11 wa Ethiopia wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani humo kwa kuingia nchini bila ya kibali.

Kwa mujibu wa kamanda wa Polisi mkoani humo kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi (SACP) Ulrich Matei alisema kuwa raia hao walikamatwa kwa kushirikiana na rai wema.

Kamanda Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea Julai Mosi mwaka huu majira ya saa 3 usiku Kijiji cha Ukuni kata ya Dunda Tarafa ya Mwambao wilaya ya Bagamoyo.

Amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Amoree Achem (22), Worko Hule (26), Basiad Tekiara (38), Anamaiyo Ramri (21), Fekri Angole (23), Kassa Dewenj (28) na Antiosogaso Suraj (20).

Wengine ni Abara Charkiso (30), Mmbarak Diljigab (30), Nichacho Abiche (32) na Kafasa Serecho (40).

Aidha alisema kuwa watuhumiwa hao watakabidhiwa idara ya uhamiaji kwa taratibu zingine za kisheria ili wajibu tuhuma zinazowakabili za kuingia nchini bila ya kibali.

Mwisho.      

No comments:

Post a Comment