Na John Gagarini, Rufiji
Serikali kupitia wizara ya Ujenzi imetoa ufafanuzi juu ya suala la
fidia kwa wakazi wanaopitiwa na mradi wa ujenzi wa barabara ya Ndundu-Somanga iliyopo
kati ya Mikoa ya Pwani na Lindi.
Waziri wa ujenzi Pombe Magufuli akizungumzia suala hilo kwa
wananchi wakati akikagua barabara hiyo huku akiwa ameambatana na viongozi
mbalimbali wa Serikali,wakala wa Tanroads katika Mikoa ya Lindi na Pwani
alisema wale waliojenga nyumba zao ndani ya mita 22.5 hawatolipwa fidia
kutokana na kuvunja sheria.
Alieleza kuwa mbali ya kutolipwa fidia pia watu hao watatakiwa
kulipia gharama za mafuta ya greda ambalo litafanya kazi ya ubomoaji.
Magufuli Alielezea wale walio nje ya mita 22.5 na ambao makazi yao
yamejengwa nyuma ya mwaka 2007 ambapo watawekewa
alama ya X kwa rangi ya kijani ikiashiria hao ndio watalipwa fidia .
Aidha Waziri huyo wa Ujenzi alikemea tabia ya kuiba mafuta
inayofanywa na baadhi ya watumishi wa mkandarasi huyo sanjali na baadhi ya
wananchi kwani kwa kufanya hivyo ni kukwamisha kasi ya ujenzi wa barabara hiyo.
Alitoa rai hiyo baada ya kufikishiwa malalamiko hayo na baadhi ya
wananchi wa kijiji cha Manzese kilicho mpakani mwa mikoa ya Lindi na Pwani kuwa
kuna tabia ya kuibiwa mafuta jambo ambalo linasababisha ujenzi kusuasua.
Magufuli pia alimtaka mkandarasi wa barabara hiyo M.A Kharafi $
Sons Ltd kuwalipa fedha nzuri wafanyakazi wake ili waweze kuondokana na tamaa za kuiba mafuta
na vifaa vingine.
Mwishoni mwa wiki Magufuli alitoa siku 60 kwa Mkandarasi wa
barabara ya Ndundu-Somanga iliyopo kati ya Mikoa ya lindi na Pwani M.A Kharafi
$Sons Ltd kuhakikisha anamaliza ujenzi wa barabara hiyo .
Agizo hilo ni kuanzia sasa hadi mwezi wa 9 mwaka huu awe
ameshamaliza kazi hiyo na kama akizembea serikali itamchukulia hatua zaidi
kwani imeshamlipa kwa awamu nyingine Bil 8.91 hivyo hakuna kisingizio kingine.
Waziri Magufuli alisema mkandarasi huyo amekiuka mkataba hivyo serikali imechoshwa na usumbufu na visingizio vyake .
Waziri Magufuli alisema mkandarasi huyo amekiuka mkataba hivyo serikali imechoshwa na usumbufu na visingizio vyake .
Alisema Mkataba wake ulikuwa ukionyesha kuanza ujenzi mwaka 2009
na kukamilika 2011 kwa kujenga km 56.318 kwa kiwango cha lami lakini hadi sasa
km 10 bado hajazikamilika.
Sambamba na agizo hilo aliwaagiza mameneja wa wakala wa barabara
Tanroads ,Mikoa ya Lindi na Pwani kumbana Mkandarasi huyo ili kuhakikisha
hazembei kumaliza kazi hiyo kwa muda aliopewa.
Aidha alisema tayari kwasasa wizara imechukua hatua ya kumfukuza
kazi Mhandisi Msimamizi ushauri wa awali wa ujezi wa barabara hiyo Engineering
System Group –KSCC toka juni 8 mwaka huu .
Ambapo kwasasa barabara hiyo itasimamiwa na Wakala wa barabara
–Tanroads-yenyewe kupitia kitengo cha usimamizi wa kazi ndani ya wakala huo kwa
mujibu wa sheria namba 16 ya mwaka 1997.
"Wasimamiazi hao wamsimamie mkandarasi hadi atoke makamasi
,na ni lazima kuanzia sasa afanye kazi usiku na mchana,jumatatu hadi jumapili
ili amalize ujenzi kwa muda wa miezi hii miwili pekee”alisema Magufuli.
Alieleza kuwa ifikie hatua ya kusema basi kulea wakandarasi wasumbufu ili kuondoa changamoto zinazowakabili wananchi ikiwemo vumbi na kukwama kwa magari kutokana na uzembe wa mkandarasi husika.
Nae Mtendaji Mkuu wa wakala wa barabara Tanroads nchini ,Mhandisi
Patrick Mfugale alieleza mbali ya changamoto hiyo pia mkandarasi huyo
alishindwa kuendesha mradi kwa fedha zake mwenyewe hadi serikali ilipomwezesha.
Sababu nyingine ni kucheleweshwa kwa fedha kutoka kwa wachangiaji
wa fedha wengine katika mradi huo ikiwemo OPEC na Quwait fund .
Barabara ya Ndundu-Somanga ina urefu wa km 56.318 ,zilizokamilika ni km
42 huku km 10 zikiwa bado hazijakamilika,na hadi kukamilika kwa ujenzi
itagharimu kiasi cha sh. Bil 58.813 ambapo hadi sasa umegharimu sh.Bil 49.
Katika gharama hizo serikali itachangia asilimia 55,OPEC 14 na
Quwait Fund asilimia 31.
Mwisho
No comments:
Post a Comment