Baadhi ya madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani wakiwa kwenye kikao cha baraza hilo kilichofanyika leo mjini Kibaha |
ZOEZI la kuchagua kamati mbalimbali za baraza la madiwani wa
halmashauri ya Mji wa Kibaha wilayani humo mkoani Pwani limekumbwa na
mtafaruku baada ya baadhi ya madiwani kupinga taratibu za kuwachagua
viongozi na wajumbe wa kamati hizo.
Mtafaruku huo ulitokea baada ya baadhi ya madiwani kulalamika kuwa
wengi wao walipewa kamati nzuri kwa upendeleo na kuwaweka madiwani
wengine kwenye kamati ambazo si nzuri.
Sakata hilo lilitokea jana wakati wa kikao cha baraza la madiwani wa
Halmashauri ya Mji huo lililofanyika mjini Kibaha ambapo madiwani hao
walidai kulikuwa na upendeleo wakati wa kuchagua wajumbe na wenyeviti
wa kamati hizo.
Walisema kuwa uchaguzi huo uliambatana na upendeleo mkubwa ambapo
baadhi ya madiwani wamekuwa wakichaguliwa kwenye moja hasa ile ya
Mipango Miji na Mazingira ambapo wako kwenye kamati hiyo kwa vipindi
vinne mfululizo ambapo wao walitaka wabadilishwe na kuwekwa kwenye
kamati zingine.
“Baadhi ya madiwani wamechaguliwa kutokana na urafiki baadhi
tunateuliwa kwenye kamati ambazo si nzuri inasikitisha sana lazima
kuwe na mabadiliko kama vipi sisi wengine tutajitoa kwenye kamati na
kubaki na udiwani pekee,” walisema madiwani hao.
Hata hivyo hali ilikuwa mbaya zaidi ambapo baadhi walidai kuwa wengine
walichaguliwa kwenye kamati hiyo ya mipango miji kama kulipa fadhila
baada ya kumpa mmoja wa viongozi kwenye uchaguzi wa chama.
“Watu walihongwa fedha ili wamchague mtu ushahidi upo sisi hatukubali
tunaona kuwa baada ya uchaguzi ule leo jana wanalipana fedhila
hatutaweza kufanikiwa tunachotakiwa ni kuwahudumia wananchi,” walisema
madiwani hao.
Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri Addhu Mkomambo alisema kuwa
uchaguzi huo haukuwa na upendeleo na kama kuna tatizo wanapaswa
kupeleka ofisini kwake na si kuunda vikundi.
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Abdala Mdimu alisema kuwa
amesikitishwa na madiwani hao kufikia hatua ya kusema mambo ambayo
hayakupaswa kusemwa hapo badala yake yangepelekwa kwenye chama kwa
hataua.
Mdimu alisema kuwa atakaa na madiwani hao ili kuzungumzia masuala hayo
ambayo yalionekana kumsononesha na kusema kuwa hali hiyo imemsikitisha
sana.
Mwisho.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Addhu Mkomambo kulia akihutubia kwenye kikao hicho kushoto ni mkurugenzi wa halmashuri hiyo Jenifa Omolo |
DIWANI wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kata ya Tumbi
Mbena Makala jana aliondolewa kwenye kikao cha madiwani wa baraza la
madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha wilayani Kibaha mkoani Pwani
kutokana na utovu wa nidhamu.
Kikao hicho cha kawaida cha robo tatu ya mwaka ambacho kilifanyika
jana ilimbidi mwenyekiti wa Halmashauri Addhu Mkomambo kumtoa nje ya
ukumbi baada ya kumtaka diwani huyo kukaa chini baada ya hoja yake
kutakiwa kupatiwa ufumbuzi wakati mwingine na si kwenye kaikao hicho.
Diwani huyo alitoa hoja ambapo alisema kuwa wananchi wake walikuwa
wakihitaji eneo kwa ajili ya kufanya soko huku eneo hilo likitakiwa
kufanyiwa jambo jingine na si soko na watafute sehemu nyingine na hapo
patawekwa kitega uchumi kingine.
“Wananchi walikubaliana eneo hilo la (Community Centre) lijengwe soko
kutokana na kata hiyo kutokuwa na soko ambapo wananchi mbali ya
kuliandaa pia walichanga fedha kwa ajili ya kulirekebisha kwa ajili ya
shughuli hiyo,” alisema Makala.
Makala alisema kuwa wananchi walishakubaliana juu ya eneo hilo
kufanywa ujenzi wa soko lakini cha kushangaza Halmashauri inakataa na
kuwataka watafute sehemu nyingine.
Akijibu hoja hiyo Mwenyekiti Mkomambo alisema kuwa eneo hilo haliwezi
kuwekwa soko na badala yake kiwekwe kitega uchumi kingine hivyo
watafute eneo mbadala kwa ajili ya shughuli hiyo ya soko na nyumba
zilizopo hapo zibomolewe.
Kutokana na majibu hayo ndipo diwani huyo alipoamka na kusema kuwa
miezi michache iliyopita Mwenyekiti alikuwa kwenye ziara na kusema
kuwa soko litajengwa iweje leo anakana kauli yake hivyo hawezi
kukubaliana na maelezo hayo.
Mwenyekiti huyo baada ya maelezo kutoafikiwa na diwani huyo alimwambia
kuwa suala hilo alipeleke kwenye kamati ya mipango miji na mazingira
ili lipatiwe majibu na majibu hayataweza kutolewa hapo.
“Ni kweli nilikuja kwenye kata yako lakini masuala haya itabidi
uyapeleke kwenye kamati ya mipango miji naamini utapata majibu pia
sasa imepita miezi saba tangu nilipotembelea kwanini hukuleta hoja
hizo mapema leo ndiyo unataka majibu hapa ili upate majibu ya uhakika
fuata hizo taratibu nilizokuambia,” alisema Mkomambo.
Kutokana na majibu hayo diwani huyo aliendelea kutoa maneno na
kutakiwa akae lakini alikataa na ndipo mwenyekiti alipomwamuru atoke
nje hadi pale atakapojirekebisha jambo ambalo lilimfanya diwani huyo
atoke nje na kuondoka kabisa eneo la viwanja vya halmashauri.
Mwisho.
Mbena Makala jana aliondolewa kwenye kikao cha madiwani wa baraza la
madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha wilayani Kibaha mkoani Pwani
kutokana na utovu wa nidhamu.
Kikao hicho cha kawaida cha robo tatu ya mwaka ambacho kilifanyika
jana ilimbidi mwenyekiti wa Halmashauri Addhu Mkomambo kumtoa nje ya
ukumbi baada ya kumtaka diwani huyo kukaa chini baada ya hoja yake
kutakiwa kupatiwa ufumbuzi wakati mwingine na si kwenye kaikao hicho.
Diwani huyo alitoa hoja ambapo alisema kuwa wananchi wake walikuwa
wakihitaji eneo kwa ajili ya kufanya soko huku eneo hilo likitakiwa
kufanyiwa jambo jingine na si soko na watafute sehemu nyingine na hapo
patawekwa kitega uchumi kingine.
“Wananchi walikubaliana eneo hilo la (Community Centre) lijengwe soko
kutokana na kata hiyo kutokuwa na soko ambapo wananchi mbali ya
kuliandaa pia walichanga fedha kwa ajili ya kulirekebisha kwa ajili ya
shughuli hiyo,” alisema Makala.
Makala alisema kuwa wananchi walishakubaliana juu ya eneo hilo
kufanywa ujenzi wa soko lakini cha kushangaza Halmashauri inakataa na
kuwataka watafute sehemu nyingine.
Akijibu hoja hiyo Mwenyekiti Mkomambo alisema kuwa eneo hilo haliwezi
kuwekwa soko na badala yake kiwekwe kitega uchumi kingine hivyo
watafute eneo mbadala kwa ajili ya shughuli hiyo ya soko na nyumba
zilizopo hapo zibomolewe.
Kutokana na majibu hayo ndipo diwani huyo alipoamka na kusema kuwa
miezi michache iliyopita Mwenyekiti alikuwa kwenye ziara na kusema
kuwa soko litajengwa iweje leo anakana kauli yake hivyo hawezi
kukubaliana na maelezo hayo.
Mwenyekiti huyo baada ya maelezo kutoafikiwa na diwani huyo alimwambia
kuwa suala hilo alipeleke kwenye kamati ya mipango miji na mazingira
ili lipatiwe majibu na majibu hayataweza kutolewa hapo.
“Ni kweli nilikuja kwenye kata yako lakini masuala haya itabidi
uyapeleke kwenye kamati ya mipango miji naamini utapata majibu pia
sasa imepita miezi saba tangu nilipotembelea kwanini hukuleta hoja
hizo mapema leo ndiyo unataka majibu hapa ili upate majibu ya uhakika
fuata hizo taratibu nilizokuambia,” alisema Mkomambo.
Kutokana na majibu hayo diwani huyo aliendelea kutoa maneno na
kutakiwa akae lakini alikataa na ndipo mwenyekiti alipomwamuru atoke
nje hadi pale atakapojirekebisha jambo ambalo lilimfanya diwani huyo
atoke nje na kuondoka kabisa eneo la viwanja vya halmashauri.
Mwisho.