Sunday, April 26, 2026

INTRNATIONAL

 


SHULE KIMATAIFA

 


ZINGATIENI DIRA YA MAENDELEO

WIZARA ya Elimu Sayansi na Teknolojia imezitaka Shule za Kimataifa nchini kujisajili kwenye mifumo na miongozo ya elimu na kiserikal ili kukidhi matakwa ya kisheria.

Hayo yalisemwa na Dk Maulid Maulid aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara Caroline Nombo wakati wa kufunga mafunzo ya siku nne kwa wamiliki wa shule hizo juu ya namna ya uendeshaji wa shule hizo mafunzo yaliyofanyika kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere Kibaha.

Maulid alisema kuwa ili elimu inayotolewa na shule hizo za kimataifa lazima zihakikishe zinafanya usajili wao kupitia mifumo iliyowekwa ili kuendana na mfumo wa elimu wa nchi.

"Wamiliki wa shule hizi wanapaswa kufanya usajili kwenye mifumo ya elimu ili elimu inayotolewa itambulike na iwe na ubora unaotambulika na ushindani kimataifa kwa kuzingatia mitaala ya nchi yetu,"alisema Maulid.

Alisema kuwa shule hizo zinapaswa kujisajili kwenye mamlaka mbalimbali za taasisi za elimu ili ziweze kuendana na mifumo iliyopo ikiwemo kwenye Baraza la Mitihani NACTE na mamlaka za serikali.

"Lazima wafuate mifumo yote ya kiithibati na ubora bila kusahau kuzingatia sera ya elimu ambayo ndiyo inayotoa mwongozo wa elimu kwa taasisi za kielimu,"alisema Maulid.

Aidha alisema kuwa pia mitaala yao iendane na Dira ya Taifa ya Maendeleo ili wanafunzi wawe na uelewa wa juu ya Dira hiyo ambapo kwa sasa ni ya 2050.

"Mitaala yao iendane na Dira ya Maendeleo kwani inazingatia utoaji elimu bora ambayo inaangalia viaumbele vya nchi katika kuleta maendeleo kwa wananchi,,'alisema Maulid.

Kwa upande wake moja ya washiriki wa mafunzo hayo ambaye ni mhasibu wa shule ya kimataifa ya Renie Joshua John alisema kuwa mafunzo hayo yatakuwa chachu kwa shule yake kwani amepata elimu ya namna ya kuweka vizuri masuala ya fedha.

John alisema kuwa wamepata uelewa mzuri wa namna ya kuendesha shule zao na kwa kuzingatia taratibu na miongozo ya kisheria ambayo wanapaswa kuifuata.

Mafunzo hayo yaliandaliwa na Tanzania School Leadership Institute (TSLI) na kusimamiwa na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia waliwahusisha wamiliki, walimu wakuu, wahasibu na viongozi wa shule za kimataifa hapa nchini

SHULE ZA KIMATAIFA ZATAKIWA KUJISAJILI KIKIDHI MATAKWA YA KISHERIA

WIZARA ya Elimu Sayansi na Teknolojia imezitaka Shule za Kimataifa nchini kujisajili kwenye mifumo na miongozo ya elimu na kiserikal ili kukidhi matakwa ya kisheria.

Hayo yalisemwa na Dk Maulid Maulid aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara Caroline Nombo wakati wa kufunga mafunzo ya siku nne kwa wamiliki wa shule hizo juu ya namna ya uendeshaji wa shule hizo mafunzo yaliyofanyika kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere Kibaha.

Maulid alisema kuwa ili elimu inayotolewa na shule hizo za kimataifa lazima zihakikishe zinafanya usajili wao kupitia mifumo iliyowekwa ili kuendana na mfumo wa elimu wa nchi.

"Wamiliki wa shule hizi wanapaswa kufanya usajili kwenye mifumo ya elimu ili elimu inayotolewa itambulike na iwe na ubora unaotambulika na ushindani kimataifa kwa kuzingatia mitaala ya nchi yetu,"alisema Maulid.

Alisema kuwa shule hizo zinapaswa kujisajili kwenye mamlaka mbalimbali za taasisi za elimu ili ziweze kuendana na mifumo iliyopo ikiwemo kwenye Baraza la Mitihani NACTE na mamlaka za serikali.

"Lazima wafuate mifumo yote ya kiithibati na ubora bila kusahau kuzingatia sera ya elimu ambayo ndiyo inayotoa mwongozo wa elimu kwa taasisi za kielimu,"alisema Maulid.

Aidha alisema kuwa pia mitaala yao iendane na Dira ya Taifa ya Maendeleo ili wanafunzi wawe na uelewa wa juu ya Dira hiyo ambapo kwa sasa ni ya 2050.

"Mitaala yao iendane na Dira ya Maendeleo kwani inazingatia utoaji elimu bora ambayo inaangalia viaumbele vya nchi katika kuleta maendeleo kwa wananchi,,'alisema Maulid.

Kwa upande wake moja ya washiriki wa mafunzo hayo ambaye ni mhasibu wa shule ya kimataifa ya Renie Joshua John alisema kuwa mafunzo hayo yatakuwa chachu kwa shule yake kwani amepata elimu ya namna ya kuweka vizuri masuala ya fedha.

John alisema kuwa wamepata uelewa mzuri wa namna ya kuendesha shule zao na kwa kuzingatia taratibu na miongozo ya kisheria ambayo wanapaswa kuifuata.

Mafunzo hayo yaliandaliwa na Tanzania School Leadership Institute (TSLI) na kusimamiwa na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia waliwahusisha wamiliki, walimu wakuu, wahasibu na viongozi wa shule za kimataifa hapa nchini


Thursday, April 23, 2026

MITAALA YA SHULE ZA KIMATAIFA YAVUTIA WANAFUNZI KUTOKIMBILIA KUSOMA NJE YA NCHI


KWA kipindi cha miaka ya nyuma baadhi ya wazazi walikuwa na kasumba ya kupeleka watoto wao kusoma nje ya nchi kwa imani huko ndiko kuna elimu bora tofauti na hapa nchini.

Aidha baada ya maboresho mbalimbali kwenye shule za kimataifa hapa nchini kwa sasa wazazi wanawapeleka watoto wao kwenye shule za hapa nchini ambazo zinatoa elimu bora.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Elimu ya Ualimu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Mathias Mvula akimwakilisha Naibu Waziri wa Elimu Wanu Ameir wakati akifungua mafunzo ya wadau wa Shule za Kimataifa nchini kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Kibaha.

Mvula amesema kuwa Shule hizo zinafundisha kwa kuzingatia mitaala ya nchi na ile ya kimataifa ili elimu inayotolewa kuwa na ushindani na ile inayotolewa nje.

Naye Hassan Masawe kutoka Tanzania School Leadership Institute (TSLI) amesema kuwa mafunzo hayo yana lengo la kuboresha elimu inayotolewa na shule hizo kuwa na ubora baina ya elimu ya nchini na ile ya nje ya nchi.

Kwa upande wake Calista Mungwe Mkurugenzi wa shule ya Renie International ya Jijini Dar es Salaam amesema kuwa mafunzo hayo yatawasaidia kuboresha uendeshaji wa Shule zao.


Wednesday, April 22, 2026

VIJANA WASEMA BENKI YA VIJANA ITAKUZA MITAJI YAO YA BIASHARA


MPANGO wa kuanzisha benki ya vijana ni jambo zuri kwani watanufaika na kuweza kukuza mitaji na biashara zao hivyo wataweza kujiajiri na kuajiriwa kwa wingi.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Kata ya Tangini Lazaro Benjamin Wilayani Kibaha Mkoani Pwani akizungumzia kuhusu bajeti ya vijana iliyowasilishwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana Dk Joel Nanauka Jijini Dodoma.

Benjamin amesema kuwa benki hiyo itatoa mikopo rahisi na yenye masharti nafuu ikiambatana na riba ndogo pamoja na dhamana rahisi.

"Benki hiyo itaenda kuondoa changamoto za mitaji kwa vijana na itasaidia kuongeza nafasi ya kufadhiliwa,"amesema Benjamin.

Aidha amesema kuwa benki hiyo itasaidia kuwapatia vijana elimu ya biashara na uwekezaji na matumizi sahihi ya fedha.

"Itapunguza vijana kutokuwa na ajira kwani watajiajiri kupitia mikopo ambayo itawapatia mitaji na kupata elimu ya matumizi ya fedha,"amesema Benjamin.

Saturday, April 18, 2026

MWENGE KUPITIA MIRADI YA MAENDELEO 68 YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 263.1

MWENGE wa Uhuru umeanza mbio zake Mkoani Pwani ambapo utapitia miradi ya Maendeleo 68 yenye thamani ya shilingi bilion 263.1 

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge aliyasema hayo Mapinga Wilayani Bagamoyo wakati akiupokea Mwenge huo kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila.

Kunenge alisema kuwa kati ya hiyo miradi 23 itawekewa mawe ya Msingi miradi 21
itazinduliwa na miradi 24 itakaguliwa.

"Miradi hiyo imechangiwa na Serikali Kuu bilioni 16.2 Halmashauri za Wilaya zimechangia kiasi cha shilingi bilioni 1.62,"alisema Kunenge.

Alisema kuwa wananchi na wawekezaji wamechangia kiasi cha shilingi bilioni 180.7 wadau wa Maendeleo bilioni 64.3 na michango ya Mwenge milioni 38.8.

"Ujumbe Mkuu wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026 unalenga katika ujenzi wa Amani Umoja na Mshikamano wa Kitaifa chini ya Tanzania ni yetu sote tushikamane pamoja kuleta maendeleo,"alisema Kunenge.

Alisema kuwa kauli mbiu hiyo inalenga kujenga na kuimarisha Umoja wa Kitaifa na kuutumia Mwenge wa Uhuru kuwaenzi na kuwatia moyo wazalendo wa kweli na makundi mbalimbali.

"Makundi haya yana mchango mkubwa katika kulinda Amani, Umoja na Mshikamano wa Kitaifa katika kuijenga Tanzania imara kimaadili, kidiplomasia na kiuchumi ndani na nje ya mipaka,"alisema Kunenge.

Aidha alisema Mkoa unachukua hatua kupitia ujumbe wa kudumu katika mapambano dhidi ya Vvu/Ukimwi, dawa za kulevya, malaria, rushwa na changamoto za lishe.

Naye kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa Wazo Mwangonda alisema kuwa taarifa zinazoonyesha namna wanawake na makundi maalumu namna gani wanavyonufaika na zabuni.

Mwangonda kuwa Mwenge ni wawananchi yapangwe maeneo ambayo wananchi wataukimbiza.