Kunenge ameyasema hayo Mjini Kibaha wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo ya siku tisa ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Mkoani Pwani.
Amesema kuwa kampeni hiyo ni nzuri na itawasaidia wananchi wanyonge ambao hawana uwezo wa kulipia gharama za kisheria na kumshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kubuni kampeni hiyo.
Kwa upande wa Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Jumanne Sagini amesema kuwa kampeni hiyo ni kuwezesha wanyonge wanapata haki zao kwa wakati.
Naye Naibu Waziri wa maendeleo ya jamii jinsia wanawake na makundi maalum Mwanaid Khamis amesema kuwa kumekuwa na changamoto ya ukatili wa kijinsia, matunzo ya watoto, ardhi na ubakaji.
Mwakilishi wa bodi ya ushauri wa msaada wa kisheria Nuru Awadh amesema kuwa siku tisa ni chache kwani changamoto ya masuala ya kisheria ni kubwa sana hivyo ili kuwafikia wananchi wengi hivyo huduma ziendelee kutolewa.
Mkurugenzi wa mashirika yanayotoa msaada wa kisheria (TANLAP) Christina Ruhinda amesema kuwa kila kata ina wasaidizi wa kisheria nchi nzima ambao wanasaidia kutoa elimu na msaada wa kisheria.