Saturday, February 15, 2025

WAANDISHI WA HABARI WAJENGEWA UWEZO JUU YA MALEZI MAKUZI MAENDELEO YA WATOTO

WAANDISHI wa Habari nchini wametakiwa kuleta mabadiliko chanya kwenye masuala ya malezi na makuzi ya watoto ili kuja kupata viongozi bora wa baadaye.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Osifa Programu kutoka Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) Victor Maleko ambaye alikuwa mwezeshaji wa mafunzo kuhusu uandishi wa habari zinazohusu Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (MMMAM).

Maleko alisema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa ukuaji wa watoto ambao wanatakiwa kupata huduma muhimu katika ukuaji wao ili wawe na makuzi mazuri.

No comments:

Post a Comment