Friday, February 28, 2025

CCM KATA YA MKUZA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 9.4

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya  ya Mkuza Wilayani Kibaha kimefanya ukaguzi wa miradi ya maendeleo yenye thamani ya shilingi bilioni 9.4 na kurudhishwa na kiwango cha utekelezaji wa miradi hiyo.

Akizungumza baada ya kukamilisha ziara ya Halmashauri ya Kuu ya Kata kutembelea miradi hiyo Mwenyekiti wa CCM Kata ya Mkuza Matata Ngolo amesema kuwa huo ni utekelezaji wa ilani ya CCM.

Ngolo amesema kuwa kabla ya kikao waliona ni vema wakatembelea miradi hiyo ya maendeleo ili kujionea uhalisia wa utekelezaji wa ilani ya CCM kwa kipindi cha miaka mitano.

Kwa upande wake diwani wa Kata ya Mkuza Fokas Bundala amesema  kuwa moja ya mafanikio makubwa ni ujenzi wa shule za sekondari mbili ambapo kiutaratibu kila kata inapaswa kujenga sekondari moja.

Bundala amesema kuwa changamoto kubwa iliyopo ni madawati na viti na meza lakini kwenye bajeti inayokuja fedha zimetengwa hivyo itapunguza changamoto hiyo.

Amesema kuwa katika kipindi hicho serikali kupitia mapato yake ya asilimia 10 ilitoa kiasi cha shilingi milioni 660 kwa ajili ya mikopo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kwa vikundi.

No comments:

Post a Comment