Monday, March 3, 2025

SERA YA TAIFA YA MAENDELEO YA VIJANA 2007 YAENDELEA KUNADIWA

Leo tarehe 3.3.2025 Ndugu Omary Abdul Punzi Mwanadiplomasia na Mratibu wa Makongamano ya Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana Mwaka 2007 toleo la Mwaka 2024 katika kamati ya Vijana Wazalendo waliopewa kibali Maalumu na Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu 

Kwa ajili ya Kuinadi na kuineza Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana 

Amemtembelea Mheshiwimiwa Godfrey Eliakimu Mzanva Mkuu wa Wilaya ya Moshi kwa ajili ya kumpongeza kwa Kuaminiwa na Mheshiwimiwa Dk Samia Suluhu Hasani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya.

Unakumbuka kuwa Mheshiwimiwa Godfrey Eliakimu Mzanva ni miongoni mwa wakimbiza mwenge mwaka 2024 waliofanya vizuri katika kuendesha Makongamano ya vijana.

Aidha mazungumzo hayo yalitoa mwafaka wa Kuandaa Kongamano la Vijana Kuhusu Umuhimu wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Ambalo litajikita zaidi kuelezea historia ya Tanzania, Itifaki, Maadili na Uzalendo kwa Vijana,Madhara ya matumizi ya madawa ya kulevya, utunzaji wa Mazingira na Fursa zinatopatikana Wilaya ya Moshi Mkoa wa Kilimanjaro

No comments:

Post a Comment