Wednesday, March 5, 2025

DOWEICARE YATOA YATOA MSAADA WA FEDHA UJENZI WA DARAJA LULANZI


KIWANDA cha Doweicare cha Kibaha Mkoani Pwani kimetoa fedha kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa daraja la Mtaa wa Lulanzi-Matunda ili kuboresha barabara ya mtaa huo.

Akikabidhi fedha hizo kwa uongozi wa Serikali ya Mtaa wa Lulanzi Mkurugenzi wa Kiwanda hicho Bob Chen amesema kuwa wameamua kutoa fedha hizo ili kukabili changamoto za jamii.

Amesema kuwa Kiwanda chao kimekuwa kikitoa misaada mbalimbali kwenye jamii ikiwa ni sehemu ya kurudisha kwa jamii kama sehemu ya huduma za jamii ambapo fedha hizo ni asilimia 57.5 ya fedha za mradi huo.

"Tunashirikiana na jamii kwenye masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja elimu, afya, barabara na masuala yanayohusu jamii,"amesema Chen.

Naye Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Lulanzi Thobias Shilole amesema kuwa wanakishukuru kiwanda hicho kwa msaada walioutoa utasaidia sana ujenzi wa daraja hilo.

Shilole amesema wananchi wamekuwa wakijitolea fedha kwa ajili ya ujenzi huo hivyo hiyo itakuwa imewaongezea nguvu kwenye kuanza ujenzi wa daraja ili kupunguza changamoto kwa wananchi wanaotumia barabara hiyo.

Amewataka wadau mbalimbali wa maendeleo kuendelea kuchangia ujenzi huo ili upunguze changamoto kwa watu wakiwemo wanafunzi wakati wakienda na kurudi shule.


No comments:

Post a Comment