KIWANDA cha Keds Tanzania Company Ltd kimesema kitaendelea kuzalisha bidhaa zenye ubora na bei nafuu kulingana na hali ya soko.
Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Mkurugenzi wa kiwanda hicho Bob Cheng alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.
Cheng amesema kuwa katika utengenezaji wa bidhaa zao wanazingatia ubora ili kuendelea kuwa na soko kwa kuwapatia wananchi kitu kilicho bora.
"Malengo ya kuanzishwa kiwanda ni kukuza uchumi wa wananchi kwa kutoa ajira kwa watu wengi pia kutengeneza bidhaa bora zinzokubalika,"amesema Cheng.
Amesema kuwa malengo yao ni kutengeneza bidhaa nyingine lakini kwa sasa wanafanya kwanza utafiti ili kujua ni bidhaa gani watakayoizalisha.
"Kiwanda kinajihusisha na uzalishaji wa sabuni za unga, vipande, pampasi na pedi za akinamama na kinashirikiana na serikali kwa kufuata taratibu zote za kisheria,"amesema Cheng.
Aidha amesema kuwa kiwanda kinashirikiana na jamii kwa kurudisha kwa jamii kwa kusaidia kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni pamoja na kwenye sekta za elimu, afya, barabara na sekta mbalimbali.
"Kuhusu maji yanayotoka kiwandani hayana athari zozote za kiafya na kimazingira ambapo hata wafanyakazi wetu wanaishi jirani na kiwanda ni asilimia 60 hivyo hayana tatizo lolote,"amesema Cheng.
Kiwanda hicho kinauza bidhaa zake kote nchini pamoja na nchi za jirani baadhi zikiwa ni Uganda, Kenya na Malawi.
No comments:
Post a Comment