Monday, March 31, 2025

NMB KUTUMIA ZAIDI YA BILIONI 6 MIRADI YA MAENDELEO

BENKI ya inatarajia kutumia kiasi cha shilingi bilioni 6.4 kwa ajili ya kuchangia shughuli za maendeleo kwa mwaka wa 2025.

Hayo yalisemwa na Meneja wa benki hiyo Kanda ya Dar es Salaam ambaye aliwakilishwa na meneja wa tawi la Mlandizi Wilayani Kibaha William Marwa wakati wa Kongamano la Vijana juu ya umuhimu wa kushiriki mbio za mwenge mkoa wa Pwani 2025.

Alisema vijana wanapaswa kujua historia ya mbio za mwenge wa uhuru na fursa zilizopo kupitia mwenge ambao ni alama ya mshikamano wa kuleta maendeleo ya nchi.

"Tangu mwenge umeanza mbio zake kwa sasa ni miaka 61 na pia tunakumbuka kifo cha mwasisi wa Taifa letu miaka 26 iliyopita lazima tumjue kwani aliifanyia nchi hii mambo makubwa,"alisema Marwa. 

Akizungumzia benki hiyo ambayo ni kubwa kuliko zote nchini imekuwa ikichangia maendeleo na ni chachu kwa kuchangia kwenye sekta ya afya, elimu na kutoa mkono wa pole kwa wananchi wanaopata majanga.

"Benki imekuwa ikirudisha sehemu ya faida kwa kuchangia suala la maendeleo kupitia sekta mbalimbali kwani wao ni sehemu ya wateja kwani ina matawi wilaya zote nchini,"alisema Marwa.

Alisema kuwa benki hiyo ina matawi 241 Atm 720 mawakala 50,000 na wateja milioni 8.7 kote nchini na bado inaendelea kuboresha huduma zake kimtandao.

No comments:

Post a Comment