Monday, December 2, 2024
MAONYESHO YA WIKI YA UWEKEZAJI NA BIASHARA PWANI KUFANYIKA MAILI MOJA KIBAHA KUANZIA DESEMBA 16 HADI 20 MWAKA HUU
Friday, November 29, 2024
WENYEVITI WAAPISHWA WATAKIWA WASIUZE ARDHI
DK ALICE AWASHUKURU WANANCHI KWA KUWAPATIA USHINDI CCM UCHAGUZI SERIKALI
Monday, November 18, 2024
VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VINAVYOSIMAMIA ULINZI NA AMANI KUSINI MWA AFRIKA (SADC) ZIANDAE MITAALA KUZINGATIA MATISHIO YANAYOZIKABILI NCHI WANACHAMA
Mkuu wa Kamandi ya Vikosi chini ya Makao Makuu Meja Jenerali Iddi Said Nkambi amevitaka Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Taasisi za Serikali na Kiraia zinazohusika na Ulinzi wa Amani chini ya Mwavuli wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika ( SADC) kuhakikisha zinandaa mitaala ya kuendeshea mafunzo ya Ulinzi wa Amani kwa kuzingatia matishio yanayozikabili nchi wanachama.
Meja Jenerali Nkambi ameyasema hayo leo tarehe 18 Novemba 2024 wakati wa ufunguzi wa Semina fupi ya siku 5 inayohusu uwasilishaji wa mitaala mipya ya mafunzo itakayotumika kuandaa Majeshi ya SADC, semina inayofanyika katika Kituo cha Mafunzo ya Ulinzi wa Amani (PTC) kilichopo Kunduchi Jijini Dar es salaam.
Semina hiyo inayoendeshwa na Chuo cha Ulinzi wa Amani cha Kikanda chenye Makao Makuu yake nchini Zimbabwe inahudhuriwa na washiriki kutoka nchi wanachama wa SADC ikiwa na lengo la kuwajengea uwezo katika kukabiliana na matishio pindi wanapokuwa katika majukumu ya Ulinzi wa Amani ndani ya ukanda wa SADC na sehemu zingine watakapopewa jukumu.
Tuesday, November 5, 2024
TAKUKURU PWANI KUTOA ELIMU KUPAMBANA NA RUSHWA
Friday, November 1, 2024
WAHITIMU MAFUNZO JESHI LA AKIBA WAOMBA AJIRA HALMASHAURI

Tuesday, October 29, 2024
VIJANA NCHINI KUPEWA ELIMU SERA YA VIJANA
ILI kuwapa ufahamu juu ya Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana ya mwaka (2007) toleo la mwaka 2024 Kamati ya Vijana Wazalendo itafanya makongamano kwenye mikoa 10 hapa nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari mratibu wa Kamati ya Vijana Wazalendo Omary Punzi amesema kuwa Makongamano hayo yatakutanisha makundi ya vijana ambayo yatapatiwa elimu juu ya sera hiyo.
Punzi amesema kuwa sera hiyo ya vijana ni nzuri lakini vijana wengi hawaifahamu hali ambayo inawafanya vijana wengi kutotambua haki zao za msingi na makongamano hayo yatawafikia vijana zaidi ya milioni nane na tisa.
Mwenyekiti wa Kamati ya vijana Wazalendo Farida Kongoi amesema kuundwa kwa sera ya taifa ya maendeleo ya vijana lengo lilikuwa ni vijana wapate mwongozo wa kuendana na masuala ya siasa na kijamii ikiwa ni pamoja na mwelekeo wa kiteknolojia.
Mwanasheria wa Kamati ya vijana Wazalendo Godfrey Kizito amesema pia vijana watafafanuliwa kuhusu Sheria zinazohusu haki na masuala ya vijana.
Naye Mkurugenzi wa Great leaders organization na Mratibu na Mwandaaji wa kongamano la Wazazi na Walezi nchini Dubai Dk Debora Nyamlundwa amesema katika kongamano hilo kuna kujifinza fursa mbalimbali zilizopo katika taifa hilo kuja kuendeleza hapa nchini