SHIRIKA lisilokuwa la Kiserikali la (YODAMEFO) la Picha ya Ndege Wilayani Kibaha linahitaji kiasi cha shilingi milioni 10 kwa ajili ya kujenga kituo cha ufundi kwa vijana.
Tuesday, July 9, 2024
YODAMEFO YAHITAJI MILIONI 10 UJENZI KITUO
Saturday, July 6, 2024
WATUMISHI WA HALMASHAURI WATOA MISAADA MAKAO TISA YA WATOTO
WATUMISHI wa Halmashauri ya Mji Kibaha kwa kushirikiana na Watumishi wa Shirika la Elimu Kibaha pamoja na wadau wa maendeleo ikiwemo Benki ya CRDB wametoa vifaa mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni 4.2 kwa makao tisa ya vituo vya kulea yatima.
Friday, July 5, 2024
KPC YATAKA WATOTO KUJILINDA
MAREKANI YAADHIMISHA SIKU YA UHURU WAKE
Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mhe Dkt Michael Battle akitoa hotuba yake kwa Kiswahili jana jioni katika hafla ya kuadhimisha siku ya Uhuru wa Marekani maarufu kama Julai 4, katika makazi yake Oysterbay jijini Dar es salaam.
Julai 4 ndio siku kuu ya nchini Marekani, ikiadhimisha kupitishwa kwa Tamko la Uhuru mnamo Julai 4, 1776 na Rais Thomas Jefferson, alipottangaza kupatikana kwa uhuru wa koloni kumi na tatu za Marekani kutoka utawala wa Uingereza.
Umuhimu wa Julai 4 kwa Wamarekani unatokana na sababu kadhaa kuu. Katika siku hii, Kongresi yao ilipitisha rasmi Tamko la Uhuru, ambalo lilielezea matamanio ya koloni kuunda taifa tofauti lililo huru kutoka utawala wa Uingereza.
Tamko hilo la Uhuru lilikuwa alama ya uhuru kamili na demokrasia. Liliainisha misingi ya msingi ya uhuru, usawa, na kutafuta furaha, ambayo ina maana kubwa kwa maadili ya Marekani.
Kupitishwa kwa Tamko kuliweka msingi wa Vita vya Mapinduzi, hatimaye kupelekea kuanzishwa kwa Marekani kama taifa huru. Ushindi katika vita na mkataba wa amani uliofuata na Uingereza ulithibitisha Julai 4 kama tarehe muhimu katika historia ya Marekani.
Kwa Wamarekaniu, kuadhimisha siku ya Uhuru Julai 4 kumekuwa jadi ya muda mrefu, ikitia nguvu umoja wa kitaifa na uzalendo.
Siku hiyo huadhimishwa na sherehe mbalimbali, ikiwemo fataki, gwaride, matamasha, na mikusanyiko ya familia, ambayo huleta watu pamoja kusherehekea urithi wao wa pamoja.
Ingawa tarehe nyingine, kama vile kusainiwa kwa Katiba au kumalizika kwa Vita vya Mapinduzi, pia ni muhimu, Julai 4 ina umuhimu wa kipekee wakati ambapo koloni za Marekani zilichukua msimamo thabiti kwa uhuru wao. Siku hii tangu hapo imekuwa sikukuu ya kitaifa inayoheshimu misingi ya nchi na roho ya kudumu ya watu wake.
Thursday, July 4, 2024
UMAUKI WAPANDA MITI KWENYE MAENEO YALIYOCHIMBWA MCHANGA
Hayo yamesemwa na Meneja wa chama hicho Hay Mshamu wakati wa unzinduzi uliofanyika Mwendapole Kibaha.
Mshamu amesema kuwa chama kimeendelea na shughuli za kudhibiti uharibifu wa Mazingira unaotokana na sababu mbalimbali zikiwemo uchimbaji wa mchanga kiholela, ukataji wa miti hovyo na uharibifu wa vyanzo vya maji.
"Tulitekeleza mradi wa upandaji wa miti ya kivuli na matunda kuzunguka katika mipaka na katikati mwa eneo la shule ya Msingi Muungano,"amesema Mshamu.
Amesema kuwa mradi ambao umekamilika kwa 100 na sasa watoto wetu wananufaika na uwepo wa miti hiyo tumeendelea kufanva kazi mbalimbali rafiki wa mazingira hadi kufikia sasa.
Aidha amesema kuwa pia wanajihusisha na uvuvi, ufugaji wa nyuki lengo likiwa ni kulinda mazingira ili yawe salama na kurejesha uoto wa asili ambao umetoweka kutokana na uharibufu wa mazingira.
"Tunahitaji kiasi cha shilingi milioni 6.5 kwa ajili ya mradi wa kilimo cha matunda ya pasheni na papai ambapo tulianzisha kuanzia miche hadi kupanda lakini nguvu imeishia hapo huku tukihitaji kupata uzalishaji mzuri,"amesema Mshamu.
Kwa upande wake Kaimu Ofisa Kilimo Halmashauri ya Mji Kibaha Suzana Mgonja amesema kuwa chama hicho kinapaswa kutumia wataalam wa kilimo ili waweze kuzalisha kwa ubora.
Mgonja amesema kuwa wao wako tayari kushirikiana na wakulima ili kuhakikisha wanainuka na kulima kilimo bora na chenye manufaa siyo kilimo kisicho na tija.
Wednesday, July 3, 2024
MTAA MAILI MOJA A WAJENGA OFISI
UONGOZI wa Mtaa wa Maili Moja A umetimiza ahadi yake ya kujenga ofisi ambapo Diwani wa Kata ya Maili Moja aliizindua ofisi hiyo na kuondokana na ofisi waliyokuwa wamepanga.
Tuesday, July 2, 2024
KAMATI YA BUNGE YAISHAURI TARURA UBORESHAJI BARABARA ZAKE
WAKALA wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) Mkoa wa Pwani kwa kushirikiana na mkoa huo wametakiwa kuandika ombi maalumu la fedha kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya barabara kwenye maeneo ya uwekezaji.
Hayo yemesemwa Mjini Kibaha na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Denis Londo wakati wa majumuisho ya ziara ya siku moja kutembelea barabara zilizojengwa na Tarura Mkoa huo.
Londo amesema kuwa kutokana na mkoa huo kuwa na uwekezaji mkubwa hasa wa viwanda ambao una manufaa kwa Taifa ni vema wakaomba maombi maalumu ya fedha kwa ajili ya miundombinu ya barabara badala ya kuomba kidogo kidogo.
"Angalieni mahitaji ya barabara zote ambazo zinahitajika kwenye maeneo muhimu ya uwekezaji badala ya kuomba sehemu chache ili muweze kuboresha kwa pamoja,"amesema Londo.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kukiwa na miundombinu mizuri ya barabara kwenye maeneo hayo kutakuwa ni kivutio kwa wawakezaji kuendelea kuwekeza.
Kunenge amesema kuwa Tarura imeweza kujenga barabara yenye urefu wa Kilometa 12.5 kwenye eneo la viwanda la Zegereni yenye thamani ya shilingi bilioni 16.4 ambayo imekamilika kwa sasa ikiwa kwenye muda wa matazamio.
Naye Meneja wa Tarura Mkoa wa Pwani Mhandisi Leopold Runji alisema miradi mitatu ambayo imetembelewa na kamati hiyo ni kutoka barabara ya Morogoro kwenda Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha yenye urefu wa mita 300 na umekamilika unathamani ya shilingi milioni 500.
Runji alisema kuwa barabara nyingine ni Visiga Zegereni ni eneo la viwanda kiwango cha lami kilometa 12.5 tunamshukuru kutoa fedha bilioni 16.4 na umekamilika sasa kipindi cha matazamio barabara nyingine ni ya Picha ya Ndege Boko Timiza kilometa 7.8 ambapo hadi sasa zimekamilika kilometa 1.2 awamu ya kwanza milioni 950 kwa awamu ya kwanza ujenzi huku ukiwa na awamu tatu.
Mjumbe wa Kamati hiyo Saasisha Mafuwe alisema kuwa katika ujenzi wa barabara zinazosimamiwa na Tarura kuwe na kiwango maalum cha gharama za ujenzi ijulikane mfano kwa kilometa na kuwe na bei maalumu siyo kila mtu kujenga kwa utashi ambapo gharama zinatofautiana kutoka sehemu moja hadi nyingine.
Kamati hiyo ilitembelea barabara za Picha ya Ndege-Boko Timiza, barabara kuelekea ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha na Visiga Zegereni na kuridhishwa na ujenzi wa barabara hizo.