Tuesday, July 9, 2024

YODAMEFO YAHITAJI MILIONI 10 UJENZI KITUO










SHIRIKA lisilokuwa la Kiserikali la (YODAMEFO) la Picha ya Ndege Wilayani Kibaha linahitaji kiasi cha shilingi milioni 10 kwa ajili ya kujenga kituo cha ufundi kwa vijana.

Akizungumza na waandishi wa habari Mjini Kibaha Mwanzilishi wa kituo hicho Anne Balisidya alisema kuwa wameshaanza kutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa baadhi ya vijana wanaolelewa na kituo hicho.

Balisidya alisema kuwa kwa sasa wanatumia eneo dogo ambalo halitoshelezi kwa ajili ya shughuli hizo ambazo zinawaandaa vijana kuwa na ujuzi mbalimbali.

"Malengo ni kuwa na kituo kikubwa ambacho kitawakusanya vijana na kuwapatia mafunzo mbalimbali ya ufundi lakini kwa kuanzia tumeanza na masuala ya ujasiriamali ikiwemo utengenezaji wa batiki, sabuni za maji na bidhaa nyingine ,"alisema Balisidya.

Alisema kuwa kwa sasa wanaendelea na vikao kwa ajili yafanya maandalizi ya chakula hicho cha hisani na wadau mbalimbali wa maendeleo ili kufanikisha shughuli hiyo.

"Tumeona kuna faida kubwa kwa vijana kujifunza ujasiriamali kwani wameshaanza kuzalisha na wanauza wanapata fedha hivyo tukiwa na eneo maalum kwa ajili ya vijana kupata ujuzi,"alisema Balisidya.

Naye Mkurugenzi wa shirika hilo Ndesario Materu alisema kuwa changamoto kubwa inayowakabili ni ukosefu wa fedha hivyo kusababisha kushindwa kutekeleza majukumu yao.

Materu alisema kuwa hawana wafadhili hivyo hujikuta wakitekeleza majukumu yao kwa ugumu kutokana na kutokuwa na vyanzo vya mapato ya kufanyia shughuli zao.

Kwa upande wake Sechelela Ndyanao alisema kuwa wanahidumia watoto waishio kwenye mazingira magumu wakiwemo wasichana walioshindwa kuendelea na masomo kutokana na kupata ujauzito.

Ndyanao alisema kuwa wanawapatia ujuzi ambao utawasaidia kuwapatia kipato ili kiwasaidie na watoto wao na kwa wale wavulana waweze kujitegemea.

No comments:

Post a Comment