MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amekabidhi magari mawili kwa wakuu wa Wilaya za Kisarawe na Bagamoyo kwa ajili ya urahisishaji utekelezaji wa majukumu yao ya kazi.
Wakuu waliokabidhiwa magari hayo aina ya Toyota yaliyotolewa na Serikali ni Petro Magoti wa Wilaya ya Kisarawe na Halima Okashi wa Wilaya ya Bagamoyo.
Kunenge alikabidhi magari hayo Mjini Kibaha mbele ya wakuu wengine wa Wilaya za Mkoa huo alisema yatawasaidia kufanya kazi zao kwa uharaka katika kuwatumikia wananchi.
Alisema kuwa mkoa una wilaya saba ambapo gari moja litakuja na manne yatakuja kwa bajeti ya mwaka huu ambapo hata wao wamepata magari kuhudumia wananchi.
"Kupata magari haya yatasaidia kuwafikia wananchi kwa urahisi kwani upatikanaji wa magari hayo ni sehemu ya kurahisisha njia ya kuwafikia wananchi,"alisema Kunenge.
Aidha alisema kuwa wanampongeza Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuwapa magari hayo ili kuwarahisishia usafiri kwenda kuwatumikia wananchi.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Okashi alisema kuwa magari hayo yatawasaidia kuketa ufanisi watayatunza ili waweze kuwafikia wananchi kwa urahisi na kwa wakati ili watatue changamoto zinazo wakabili.
Alisema kuwa magari hayo watayatunza kwani ni kwa ajili ya kuhudumia wananchi na wanaipongeza serikali kwa kuwapatia magari hayo.
Kwa upande wake Magoti alisema kuwa usafiri huo utawasaidia kuwafikia wananchi waliomoko hata maeoneo yaliyoko mbali watayafikia kwa urahisi na kutoa huduma bora.
Magoti alisema kuwa sasa hatarudi nyumbani kwani atahakikisha anawafikia wananchi na kuwasikiliza wananchi maeneo mbalimbali.
No comments:
Post a Comment