Mlenga ameyasema hayo wakati wa Siku ya Mtoto wa Afrika kimkoa iliyofanyika kwenye ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mjini Kibaha.
Mlenga amesema kuwa pia wasipokee zawadi au kuomba fedha kwa watu wasiowafahamu na wazazi wawalinde watoto kwa kutokuwa wakali na kuwahusisha na masuala ya dini ili wawe na hofu ya Mungu.
Akisoma risala ya watoto wa mkoa wa Pwani Evelin Mhema amesema kuwa baadhi ya changamoto ni pamoja kufanyiwa vitendo vya ukatili mimba za utotoni, ubakaji, vipigo na vitendo vingine vinavyowanyima haki zao.
Mhema amesema kuwa watashirikiana na viongozi wakiwemo walimu ili waweze kufikia ndoto zao walizojiwekea kwa kusoma kwa bidii na kutii wazazi na walezi wao.
Kwa upande wake Said Mwinjuma amesema kuwa matumizi ya dawa za kulevya yamekuwa changamoto kwa vijana na kusababisha mmomonyoko wa maadadili.
Mwinjuma amesema kuwa wazazi na walezi wanapaswa kuwalinda watoto wao kwa kuwapatia malezi bora ili wasijiingize kwenye matumizi ya dawa za kulevya na wasiwaache wajilee wenyewe na wawapatie elimu na stadi za kazi.
No comments:
Post a Comment