Wednesday, July 3, 2024

MTAA MAILI MOJA A WAJENGA OFISI

 





UONGOZI wa Mtaa wa Maili Moja A umetimiza ahadi yake ya kujenga ofisi ambapo Diwani wa Kata ya Maili Moja aliizindua ofisi hiyo na kuondokana na ofisi waliyokuwa wamepanga.

Akiwaaga wananchi wa Mtaa huo kwente mkutano wa hadhara Mwenyekiti wa Mtaa huo Yassin Mudhihiri amesema wanawashukuru wananchi kwa kufanikisha ujenzi huo.

Mudhihiri amesema kuwa ujenzi huo umekamilika kwa asilimia 95 lakini imeanza kutumika na wananchi wanapata huduma kwenye ofisi hiyo iliyoko eneo la Minazini.

"Tumemalia muda wetu wa uongozi wa kipindi cha miaka mitano ambapo mafanikio mengine ni kupata mradi wa barabara za lami, kurasimisha ardhi, kudhibiti wizi, kupata mradi wa Tasaf wa ujenzi wa barabara na mambo mengine ya maendeleo,"amesema Mudhihiri. 

Kwa upande wake Diwani wa Kata hiyo Ramadhan Lutambi akizindua ofisi hiyo amesema kuwa  uongozi uliomaliza muda wake umefanya kazi kubwa ya kujenga ofisi hiyo.

Lutambi amesema kuwa mtaa utapunguza gharama za kila mwezi za kulipa kodi hivyo fedha walizokuwa wakilipa kodi zitatumika kwenye matumizi mengine.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Maili Moja Methew Mkayala amesema kuwa mafanikio yote hayo yanatokana na utekelezaji wa ilani ya Chama.

Mkayala amesema kwa sasa wanajiandaa na uchaguzi wa wenyeviti wa serikali za Mitaa utakaofanyika hivi karibuni na kuwa wamejipanga vizuri kuhakikisha wanashinda kwa kishindo. 


No comments:

Post a Comment