HALMASHAURI ya Mji Kibaha imewataka wavamizi waliovamia Shamba la Mitamba namba 34 kuondoa maendelezo waliyoyafanya kabla ya zoezi la kuwaondoa kufanyika ili wasipate hasara.
Monday, January 8, 2024
HALMASHAURI YAWATAKA WAVAMIZI SHAMBA LA MITAMBA KUONDOKA.
Saturday, January 6, 2024
TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE MKOA WA PWANI INATARAJIA KUJENGA KITUO WATOTO WANAOISHI KWENYE MAZINGIRA MAGUMU
Monday, January 1, 2024
TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE PWANI YATOA VYETI VYA PONGEZI KWA WADAU
TAASISI ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Mkoa wa Pwani imetoa vyeti vya shukrani kwa vyombo vya habari na wadau mbalimbali ambao ilishirikiana nao katika shughuli zake za maendeleo.
Akikabidhi vyeti hivyo hakimu mkazi mstaafu mkoa wa Pwani Stephen Mbungu amewataka waandishi wa habari na wadau kudumisha amani kwa kuzingatia maadili ya nchi.
Naye naibu katibu mkuu wa taasisi hiyo Neema Mkwachu alisema kuwa moja ya kazi zao ni kufundisha maadili kwa Watanzania ili nchi iendelee kuwa na amani.
Naye Mkurugenzi wa Huduma za Tathmini kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Dk Abdulsalaam Omar alisema kuwa wanashirikiana na taasisi na mashirika katika utoaji huduma ikiwa ni sehemu ya kuleta maendeleo.
Mwakilishi wa kamishna wa uhifadhi wa Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) Mathew Ntilicha aliwataka wananchi kulinda mazingira kwa kupanda miti na ufugaji wa nyuki.
Meneja wa Shirika la Ugavi la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Pwani Mhandisi Mahawa Mkaka alisema kuwa wataendelea kushirikiana na taasisi hiyo ili iendelee kuihudumia jamii.
Mwenyekiti wa (CCM) Mkoa wa Pwani Mwinshehe Mlao alisema kuwa elimu inapaswa kutolewa kwa viongozi wakiwemo madiwani na viongozi wa umma kwani baadhi hawana maadili mazuri.
Mhamasishaji wa taasisi hiyo kitaifa Jirabi alisema kuwa lengo kuu ni kuwaunganisha Watanzania ili kujua falsafa za Nyerere ambaye alikuwa akipambana na adui watatu wa Taifa ambao ni Ujinga, Maradhi na Umaskini.
Kwa upande wake katibu wa taasisi hiyo Mkoani Pwani Omary Punzi alisema kuwa wamefanya hafla hiyo ikiwa ni sehemu ya kutoa shukrani kwa wadau mbalimbali ambao imeshirikiana nayo katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo.
Sunday, December 31, 2023
ALIYEESHINDA TUZO YA MALKIA WA UINGEREZA ATAKA DIASPORA WAPEWE HADHI MAALUM WAWEZE KULETA MAENDELEO NCHINI.
MTANZANIA ambaye alipata Tuzo ya Malkia Elizabeth || wa Uingereza, Prudence Kimiti amesema kuwapa hadhi maalum Diaspora itasaidia waweze kuwekeza nchini.
Saturday, December 30, 2023
SIKU YA LISHE YA KIJIJI GAIRO DC
GAIRO DC
SIKU YA AFYA NA LISHE YA KIJIJI
NIMEPATA FURSA YA KUZUNGUMZA NA WAKINA MAMA.
NIMESISITIZA KUHUSU LISHE, NIMEWAKUMBUSHA MALEZI YA WATOTO KWA KUWALINDA DHIDI YA UKATILI. UZOEFU UNAONESHA KUWA MATUKIO MENGI YA UKATILI YANAANZIA KWENYE NYUMBA ZETU KWA KUWAAMINI NDUGU TUNAOWAKARIBISHA HADI KUWALAZA KITANDA KIMOJA NA WATOTO WETU.
GAIRO DC - KAZI INAENDELEA
@ortamisemi
@wizara_afyatz
@rs_morogoro
@jabiri_makame
Thursday, December 28, 2023
WATU WATATU WAMEFARIKI DUNIA BAADA YA GARI WALILOKUWA WAKISAFIRIA KULIGONGA GARI LINGINE KWA NYUMA
ReplyReply allForward Add reaction |
Saturday, December 16, 2023
ATFT KUENDELEZA VIPAJI KUPITIA KIPAJI BILA MIPAKA
KITUO cha kuendeleza vipaji Africa Talent Forum-TZ (ATFT) cha Mkoani Pwani imewakutanisha wasanii wa fani mbalimbali ili kujadili namna ya kuendeleza vipaji vya wasanii ili viweze kutoa ajira.