Monday, July 17, 2023
MAMLAKA YA UDHIBITI MBOLEA NCHINI TFRA YAHIMIZA UWEKEZAJI VIWANDA VYA MBOLEA NCHINI
PPRA YAWATAKA WADAU WAKE KUZINGATIA MAADILI
MAMLAKA ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) imewataka wanaojihusisha na Ununuzi wa Umma ikiwemo watumishi wa Umma na wazabuni kuzingatia maadili katika utendaji wao.
Sunday, July 16, 2023
MWENYEKITI WA UWT TAIFA CHATANDA AIELEKEZA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KUTATUA CHANGAMOTO ZA NDOVU LINDI
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa na Mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa CC Mary Chatanda ameiagiza Wizara ya Maliasili na Utalii kuhakikisha inashughulikia changamoto za ndovu waliovamia makazi ya watu Mkoani Lindi.
Ameyasema hayo leo katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Naipingo Wilaya ya Nachingwea Mkoani Lindi.
Amefafanua kuwa ndovu hao wamevamia makazi ya watu kutokana na wananchi kuingia katika maeneo ya Hifadhi.
"Wizara ya Maliasili Utalii shirikianeni na Wizara ya Mifugo muwatoe wafugaji walioingia kwenye maeneo ambayo ndovu wanakaa" Chatanda amesisitiza
Ameelekeza hatua za haraka zichukuliwe kuwatoa wananchi katika hifadhi ili kunusuru mazao ya wananchi yanayoliwa na ndovu pamoja na vifo vya wananchi.
Kufuatia hoja hiyo, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mary Masanja ameahidi Wizara ya Maliasili na Utalii kupeleka helikopta ya kufukuza ndovu ambayo itaweka kambi katika maeneo husika.
"Tutahakikisha tunaleta helikopta ambayo itakaa kuondoa ndovu hawa ili wananchi waishi bila taharuki" Mhe. Masanja amesisitiza.
Amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan inajua Changamoto zinazowakabili wananchi hivyo imepanga kuongeza idadi ya askari na kujenga vituo vya askari ili kuondokana na tatizo la ndovu.
Kuhusu malipo ya kifuta jasho/machozi, Mhe. Masanja amesema Serikali imetenga fedha kiasi cha shilingi milioni 612 kwa Wilaya ya Nachingwea mwaka ili kukabiliana na changamoto ya wanyamapori wakali na waharibifu hususan ndovu.
Pia amesema Serikali itachukua vijana kwenye maeneo yenye changamoto za ndovu na kuwapatia mafunzo ya kukabiliana na wanyamapori hao.
Thursday, July 13, 2023
TASAF YABADILISHA MAISHA YA AKINAMAMA WAJENGA NYUMBA ZA KISASA
MFUKO wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) umeleta mabadiliko makubwa kwa walengwa wake ambapo Zubeda Juma miaka (70) mkazi wa Kijiji cha Kisanga kata ya Masaki Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani amefanikiwa kujenga nyumba ya tofali kutoka nyumba ya udongo aliyokuwa anaishi awali.
Wednesday, July 12, 2023
WATUMISHI WAFANYE KAZI KIMKAKATI
Tuesday, July 11, 2023
VIKUNDI VYA UJASIRIAMALI VYA TASAF VIKOPESHWE ASILIMIA 10 ZA HALMASHAURI
NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejmenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ridhiwani Kikwete ameshauri Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha kuvipatia fedha za mikopo za asilimia 10 vikundi vya ujasiriamali vilivyopo kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)
MHE.MASANJA : FILAMU YA "THE ROYAL TOUR" IMEFANIKIWA KWA KIWANGO KIKUBWA SANA
NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) amesema filamu ya “The Royal Tour” iliyozinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanikiwa kwa kiwango kikubwa na kwamba kwa sasa watalii wameongezeka.
Mhe. Masanja ameyasema hayo leo Julai 11,2023 alipotembelea Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam maarufu kama Sabasaba yanayoendelea Jijini humo.
“Tunatambua kwamba ni nadra sana kumpata Kiongozi anayeamua kuongoza kwa vitendo kama alivyofanya Rais Samia, ametangaza kwa vitendo vivutio vyetu hivyo tunatakiwa kuvitembelea vivutio hivyo ili kumuunga mkono” Mhe. Masanja amesisitiza.
Mhe. Masanja ametumia nafasi hiyo kuwahimiza Watanzania kutembelea vivutio vya utalii vilivyoko nchini akitolea mfano wa maeneo ya Malikale, Misitu ya Asili, tamaduni za Kitanzania, historia za Tanzania za Waasisi wa Taifa na maeneo mengine ya utalii.
“Tutembelee vivutio vyetu, ukishakitembelea kile kivutio unakuwa umechangia pato la Taifa lakini hata wewe mwenyewe utakuwa umejifunza historia ya nchi ilivyo lakini pia utapunguza hata msongo wa mawazo” Mhe. Masanja amefafanua.