Wednesday, December 24, 2014

BEI ZA BIDHAA ZA VYAKULA HAZIJAPANDA X-MASS

Na John Gagarini, Kibaha
HUKU leo ikiwa ni sikukukuu ya kumbukumbu ya kuzaliwa Yesu Kristo X-MASS ikiwa inaadhimishwa duniani kote wakazi wa wilaya ya Kibaha mkoani Pwani wanasherehekea kwa furaha kutokana na bei za bidhaa za vyakula zikiwa hazijapanda kama inavyokuwa miaka ya nyuma.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa bei za bidhaa za vyakula hazijapanda kama miaka ya nyuma kwani nyingi ziko vilevile hali amabyo imefurahiwa na wananchi wengi.
Akizungumza na gazeti hili mjini Kibaha mkazi wa Maili Moja Kibena Mtoro alisema kuwa wanasherehekea sikukuu hii huku bei za bidhaa za vyakula zikiwa ni za kawaida.
“Miaka ya nyuma beiza bidhaa za vyakula zilikuwa zinapanda mara dufu lakini mwaka huu tunamshukuru Mungu kwani bei ni zilezile,” alisema Mtoro.
Mtoro alisema kipindi cha nyuma baadhi ya watu wenye kipato cha chini walikuwa hawaifurahii sikukuu kutokana na bei kuwa juu.
“Kutokana na hali ya kiuchumi kuwa mabaya na bei kuwa za kawaida ni dhahiri tunasherehekea sikuku hii kwa furaha kwani kila mtu anamudu kununua chakula,” alisema Mtoro.
Kwa upande wake katibu wa soko kuu la wilaya ya Kibaha Maili Moja, Muhsin Abdu alisema kuwa kwa mwaka huu bei hazijapanda kabisa.
Abdu alisema kuwa bei ya ndizi pekee ndiyo iliyopanda ambapo mkungu umepanda bei kutoka shilingi 20, 000 hadi 35,000 kwa mkungu pamoja na tanagawizi toka shilingi 3,000 kwa kilo hadi 4,500.
“Bei haijapanda kwa sababu mojawapo ni wakulima wengi kuleta bidhaa toka mashambani na kuja kuziuza mjini tofauti na kipindi cha nyuma ambapo wafanyabiashara walikuwa wakileta bidhaa na kuuza kwa bei kubwa,” alisema Muhsin.
Alisema kuwa wafanyabiashara ndiyo walikuwa wakipandisha bei kwa kuficha bidhaa ili wauze kwa bei kubwa wakitoa visingizio mbalimbali.
“Kipindi kile bei zilikuwa juu na zinakuwa adimu lakini safari hii vyakula vingi na bado vinakuja kwa wingi hata sisi tunafurahia hali kwani bei zikiwa juu hata uuzaji unakuwa mgumu,” alisema Abdu.
Mwisho.

BIDHAA ZA VYAKULA HAZIJAPANDA X-MASS 2014

Na John Gagarini, Kibaha
HUKU leo ikiwa ni sikukukuu ya kumbukumbu ya kuzaliwa Yesu Kristo X-MASS ikiwa inaadhimishwa duniani kote wakazi wa wilaya ya Kibaha mkoani Pwani wanasherehekea kwa furaha kutokana na bei za bidhaa za vyakula zikiwa hazijapanda kama inavyokuwa miaka ya nyuma.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa bei za bidhaa za vyakula hazijapanda kama miaka ya nyuma kwani nyingi ziko vilevile hali amabyo imefurahiwa na wananchi wengi.
Akizungumza na gazeti hili mjini Kibaha mkazi wa Maili Moja Kibena Mtoro alisema kuwa wanasherehekea sikukuu hii huku bei za bidhaa za vyakula zikiwa ni za kawaida.
“Miaka ya nyuma beiza bidhaa za vyakula zilikuwa zinapanda mara dufu lakini mwaka huu tunamshukuru Mungu kwani bei ni zilezile,” alisema Mtoro.
Mtoro alisema kipindi cha nyuma baadhi ya watu wenye kipato cha chini walikuwa hawaifurahii sikukuu kutokana na bei kuwa juu.
“Kutokana na hali ya kiuchumi kuwa mabaya na bei kuwa za kawaida ni dhahiri tunasherehekea sikuku hii kwa furaha kwani kila mtu anamudu kununua chakula,” alisema Mtoro.
Kwa upande wake katibu wa soko kuu la wilaya ya Kibaha Maili Moja, Muhsin Abdu alisema kuwa kwa mwaka huu bei hazijapanda kabisa.
Abdu alisema kuwa bei ya ndizi pekee ndiyo iliyopanda ambapo mkungu umepanda bei kutoka shilingi 20, 000 hadi 35,000 kwa mkungu pamoja na tanagawizi toka shilingi 3,000 kwa kilo hadi 4,500.
“Bei haijapanda kwa sababu mojawapo ni wakulima wengi kuleta bidhaa toka mashambani na kuja kuziuza mjini tofauti na kipindi cha nyuma ambapo wafanyabiashara walikuwa wakileta bidhaa na kuuza kwa bei kubwa,” alisema Muhsin.
Alisema kuwa wafanyabiashara ndiyo walikuwa wakipandisha bei kwa kuficha bidhaa ili wauze kwa bei kubwa wakitoa visingizio mbalimbali.
“Kipindi kile bei zilikuwa juu na zinakuwa adimu lakini safari hii vyakula vingi na bado vinakuja kwa wingi hata sisi tunafurahia hali kwani bei zikiwa juu hata uuzaji unakuwa mgumu,” alisema Abdu.
Mwisho.

POLISI KUWEKA ULINZI MKALI SIKUKUU ZA X-MASS NA MWAKA MPAYA

Na John Gagarini, Kibaha
JESHI la Polisi mkoani Pwani limewataka wananchi kutumia vikundi vya ulinzi shirikishi ili kukabiliana na uhalifu katika kipindi hichi cha sikukuu za X-Mass na mwaka mpya.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha, kamanda wa Polisi mkoani hapa Ulrich Matei alisema kuwa wamejipanga vyema kudhibiti vitendo viovu kwa kushirikiana na wananchi.
Matei alisema kuwa katika kukabiliana na matukio ya uhalifu kipindi cha sikukuu kwa kutumia ulinzi shirikishi, ulinzi jirani na mgambo.
“Tutashirikiana na wananchi katika ulinzi ili washerehekee kwa amani na utulivu na tutakaowabaini wanaofanya matukio ya uhalifu,” alisema Matei.
Alisema kuwa katika ulinzi jirani wananchi wanatakiwa kuacha tabia ya kuondoka nyumbani bila ya kuacha mtu au hata kama wanatoka wawajulishe majirani zao.
“Baadhi ya vitendo viovu vinavyofanyika ni pamoja na uchomaji matairi ni kinyume cha sheria na hairuhusiwi kufanya hivyo,” alisema Matei.
Aidha alisema kuwa wazazi wanapaswa kutowaacha watoto wao kwenda kwenye maeneo ya starehe peke yao kwani ni hatari.
Aliwataka madereva kuhakikisha wanaendesha magari wakiwa hawajalewa ili kuepukana na ajali pia watawapima ulevi madereva hao kwani vifaa vya kupimia sasa wanavyo vya kutosha.
Mwisho.

Tuesday, December 23, 2014

AMWUA MWANAE KWA KUMNYONGA ADAKWA NA HEROIN

Na John Gagarini, Kibaha
ESTER Endrew (23) mkulima mkazi wa Tabata Jijini Dar es Salaam anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Pwani kwa tuhuma za kumwua mwanae Marko Elibariki (2) kwa kumnyonga kwa kutumia mikono.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha, kamanda wa polisi mkoani hapa Ulrich Matei alisema kuwa tukio hilo linahusishwa na wivu wa kimapenzi.
Kamanda Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea saa 2 asubuhi eneo la Wipas mtaa wa mkoani B kata ya Tumbi wilayani Kibaha.
“Mtuhumiwa baada ya kutekeleza tukio hilo naye alijichoma tumboni kwa kisu hali iliyosababisha apate majeraha,” alisema Kamanda Matei.
Alisema kuwa mtuhumiwa huyo baada ya tukio baadhi ya majirani waligundua kutokana na kulalamika huku damu zikimtoka.
“Alijijeruhi tumboni kwa kisu akitaka kujiua lakini hata hivyo licha ya kujichoma hakufa na kuanza kupiga kelele ndipo majirani walipotoa taarifa polisi na mtuhumiwa kuja kuchukuliwa ambapo ilibainika kuwa alikuwa akimlaumu mumewe kuwa na mke mwingine,” alisema Kamanda Matei.
Aidha alisema mtuhumiwa amelazwa kwenye hospitali ya Rufaa ya mkoa ya Tumbi kwa matibabu huku akiwa chini ya ulinzi.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
SHAMBA Malela (20) mkazi wa Nianjema wilayani Bagamoyo mkoani Pwani anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kupatikana na kete 136 za dawa aina ya Heroin.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoani Pwani Ulrich Matei alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa na polisi waliokuwa doria.
Kamanda Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea Desemba 22 mwaka huu majira ya saa 7:45 mchana huko Nianjema kata ya Magomeni wilaya ya Bagamoyo.
“Mtuhumiwa baada ya kutiliwa mashaka alikwenda kupekuliwa nyumbani kwake na kukutwa na dawa hizo ambazo zinadhaniwa kuwa ni za Heroin ambapo hata hivyo thamanai yake haikuweza kufahamika mara moja.
Alisema kuwa jeshi hilo linafanya doria kwenye maeneo mbalimbali ya wilaya za mkoa huo ili kukabiliana na matukio mbalimbali ya uhalifu.
Mwisho.

Sunday, December 21, 2014

Saturday, December 20, 2014

RIDHIWANI AKARIBISHWA KIJIJINI MSOGA KWA SHEREHE ZA JADI

Na John Gagarini, Chalinze

MBUNGE wa Jimbo la Chalinze Wilayani Bagamoyo mkoani Pwani  Ridhiwani Kikwete juzi alifanyiwa sherehe za jadi za kabila la Kikwere kama kiongozi baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge.

Sherehe hizo za jadi ambazo zilifanyika kijijini kwao Msoga ziliambatana na kukabidhiwa vitu mbalimbali vya kijadi kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.

Baadhi ya vitu alivyoakabidhiwa na mzee wa kabila hilo Zaidi Rufunga ni pamoja na fimbo kama kiongozi, kitanda cha kamba, msuli, kigoda na kinu pamoja na vitu mbalimbali.


Sherehe hizo za kijadi ziliamabatana na ngoma ya Kikwere na ulaji wa chakula kiitwacho Bambiko ambacho hutumiwa na kabila hilo. 

 Mzee Zaidi Rufunga kulia akimkabidhi vyungu mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete wakati wa sherehe za jadi za kumkaribisha nyumbani zilizofanyika juzi kijiji cha Msoga. 




 Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani  akielekezwa jambo na mzee Zaidi Rufunga  kabla ya kula chakula cha jadi cha kabila la Wakwere kiitwacho Bambiko baada ya kukaribishwa nyumbani na kufanyiwa sherehe za jadi za kikabila zilizofanyika kwenye Kijiji cha Msoga.




Baadhi ya akina mama wakila chakula mcha jadi cha kabila la Kikwere kiitwacho Bambiko mara baada ya kumkaribisha nyumbani Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani

 Baadhi ya akina mama wakila chakula mcha jadi cha kabila la Kikwere kiitwacho Bambiko mara baada ya kumkaribisha nyumbani Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani

Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete kushoto na katikati diwani wa kata ya Msoga Mohamed Mzimba na baadhi ya wageni wakila chakula cha jadi kiitwacho Bambiko mara baada ya sherehe za jadi za kumkaribisha nyumbani kwenye Kijiji cha Msoga .


Friday, December 19, 2014

HABARI ZA PWANI

Na John Gagarini, Chalinze
KATIKA kutekeleza mpango wa Matokeo ya haraka (BRN) Wizara ya Afya imesema kuwa iko katika maongeza na wafadhili kwa ajili ya kujenga viwanda vya kuzalisha dawa kwa ajili ya kutibu magonjwa mbalimbali badala ya kutegemea kuagiza dawa kutoka nje ya nchi.
Asilimia 80 ya dawa zinaotumika zinaagizwa toka nje ya nchi na kuifanya nchi kutumia gharama kubwa kwa ajili ya kuagiza dawa hizo ambapo endapo kutakuwa na viwanda vingi kutasaidia kupunguza gharama.
Hayo yalisemwa na katibu mkuu wa Wizara ya Afya Donan Mmbando, kwenye Kijiji cha Msoga alipotembelea ujenzi wa kituo cha afya cha kijiji hicho na kusema kuwa dawa bado ni changamoto kubwa.
“Mpango huu kama ulivyo kwenye sekta nyingine utatupima kwa kipindi cha miaka mitatu kutuona je temeweza kufikia malengo ambapo kati ya malengo hayo ni kuhakikisha upatikanaji wa dawa, upatikanaji wa vifaa tiba na mambo mengine,” alisema Mmbando.
Alisema BRN itafanikiwa endapo kutakuwa hakuna tatizo la upatikanaji wa dawa pamoja na vifaa tiba ambavyo vimeonekana kuwa ni changamoto kubwa.
“Mbali ya changamoto ya upatikanaji wa dawa pia kuna baadhi ya watumishi wanaojihusisha na wizi wa dawa hawa sasa tutawakamata na kuwatangaza kwenye vyombo vya habari,” alisema Mmbando.
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete alisema kuwa ujenzi wa Kituo hicho cha afya ambacho ni cha kisasa ni ukombozi kwa watu wa Jimbo hilo ambao hutegemea kuwapeleka wagonjwa kwenye hospitali ya Tumbi.
Ridhiwani alisema kuwa pia majeruhi wa ajali ambao walikuwa wakipelekwa Tumbi sasa watapata huduma hapo ambapo wanatarajia kituo hicho kufunguliwa mwezi Machi mwakani.
Naye diwani wa kata ya Msoga Hussein Mzimba alisema kuwa kituo hicho kinajengwa kwa nguvu ya wananchi, serikali pamoja na wadau wa maendeleo wa kata na wilaya hiyo.
Mwisho.

19,Des
Na John Gagarinii, Chalinze
KITUO cha Afya cha Chalinze wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani kinakabiliwa na ukosefu wa gari la kubebea wagonjwa kwa kipindi cha miezi mine jambo ambalo linasababisha wagonjwa kukodisha magari kwa ajili ya kupelekwa kwenye hospitali kubwa ikiwemo ya Tumbi.
Hayo yalisemwa na Mganga mkuu mfawidhi wa kituo hicho, Dk Victor Bamba wakati wa ziara ya mbunge wa jimbo la Chalinze,Ridhiwani Kikwete alipotembelea kituo hicho na kuangalia changamoto zinazoikabili sekta ya afya.
“Changamoto hii imetokana na imetokana na gari la wagonjwa lililopo kuwa kwenye matengenezo kwa muda wote huo,” alisema Dk Bamba.
Kwa upande wake Ridhiwani alisema kuwa tayari kuna mkakati wa kuhakikisha kunakuwepo na magari ya kubebea wagonjwa matatu mkakati utakaotekelezwa mapema mwaka ujao.
“Magari hayo yatagawiwa katika kituo cha afya Chalinze, Miono na kituo cha afya Msoga ambacho kinatarajia kukamilika hivi karibuni,” alisema Ridhiwani.
Kituo cha afya Chalinze kinakabiliwa na changamotombalimbali ikiwa ni pamoja na uhaba wa madawa, chumba cha kuhifadhia maiti, vifaa vya kujifungulia mama wajawazito ambapo kwa miezi 12 sasa havijasambazwa katika kituo hicho.
Mwisho.


Na John Gagarini, Kibaha
IMEELEZWA kuwa ajali kwa sasa zinaonekana kama ugonjwa usioambukiza ambao unaua watu wengi kwa sasa hapa nchini.
Hayo yalisemwa jana mjini Kibaha na mkurugenzi wa Elimu Mafunzo na Uenezi wa kamati ya usalama Barabarani Taifa Henry Bantu, wakati wa kilele cha siku ya usalama barabarani mkoani Pwani.
Alisema kuwa ajali kwa sasa zinaelekea kuwa ugonjwa unaoua kuliko magonjwa mengine kwani mwelekeo ndiyo unaoonekana.
“Endapo jitihada za kuzuia ajali hazitafanyika ajali ndiyo zitakuwa ni ugonjwa usioambukiza unaoua watu wengi nchini kwa sasa lakini hata hivyo baraza linajitahidi kuhakikisha ajali zinapungua,” alisema Bantu.
Bantu alisema kuwa madereva wanapaswa kuwa makini katika uendeshaji wa magari ili kupunguza ajali zisizo za lazima.
“Ajali nyingi siyo bahati mbaya kama wanavyosema watu bali ajali zinatokana na uzembe na si mpango wa Mungu hivyo umakini unatakiwa kuwepo,” alisema Bantu.
Awali akisoma risala ya kamati ya usalama barabarani mkoa Shaban Nkindwa alisema kuwa katika kipindi cha Januari Mosi hadi Novemba 30 jumla ya watu 556 walifariki dunia.
Nkindwa alisema kuwa ajali kwa jumla zilikuwa 1,859 za vifo zilikuwa 424 huku zilizojeruhi zikiwa 1,126 na watu waliojeruhiwa walikuwa 2,601.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
JESHI la Polisi mkoani Pwani limekusanya kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni mbili kutokana na makosa madogo madogo ya usalama barabarani yaliyotokea kwa kipindi cha Januari hadi Novemba mwaka huu.
Akisoma risala ya kamati ya usalama barabarani mkoa wa Pwani, wakati wa kilele cha siku ya usalama barabarani zilizofanyika jana mjini Kibaha, Shaban Nkwinda alisema kuwa fedha hizo zilitokana na makosa yaliyotokana na makosa yaliyofanywa na madereva.
Nkwinda alisema kuwa makosa yaliyokamatwa yalikuwa 80,786 ambapo ni ongezeko la ajali 23,839 sawa na asilimia 41.8 ikilinganishwa na mwaka jana.
“Makosa yaliyolipiwa yalikuwa 80,259 ikiwa ni ongezeko la ajali 24,293 sawa na asilimia 43.4 ikilinganishwa na mwaka jana,” alisema Nkwinda.
Alisema kuwa kwa kipindi cha mwaka jana mkoa uliweza kukusanya kiasi cha shilingi zaidi ya bilioni moja kutokana na makosa 56,946 kutokana na makosa yaliyolipiwa na 55,966.
Mwisho.