Na John Gagarini, Kibaha
JESHI la Polisi mkoani Pwani linawashikilia wakazi wawili wa Kijiji
cha Mwetemo wilaya ya Bagamoyo mkoani humo kwa tuhuma za kulima shamba
la bangi hekari mbili kwenye shamba la mahindi.
Watuhumiwa hao walibainika baada ya askari wa jeshi hilo kufanya doria
ya kusaka makosa mbalimbali wilyani humo ili kukamata wahalifu.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo jana mjini Kibaha kamanda wa
polisi mkoani humo Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa polisi (SACP)
Ulrich Matei alisema kuwa msako huo ni wa kawaida.
Kamanda Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea Mei 19 mwaka huu
majira ya saa 9 alasiri huko kijiji cha Mwetemo- Kiwangwa Tarafa ya
Msata wilayani humo.
Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Musa Zahoro (20) na Asher Mbuya (29)
ambapo watuhumiwa hao watafikishw amahakamani mara upelelezi
utakapokamilika.
Kwenye tukio lingine Jeshi hilo linamshikilia Omary Sultan (32)
mkulima wa mkazi wa Kijiji cha Kauzeni wilaya ya Kisarawe kwa tuhuma
za kupatikana na pombe ya Moshi lita 12 na mtambo wa kutengenezea
pombe hiyo.
Alisema kuwa tukio hilo lilitokea Mei 19 majira ya saa 6:00 Kijijini
hapo na mtuhumiwa anatarajiwa kufikishwa mahakamani mara uchunguzi wa
tukio hilo utakapokamilika.
Mwisho.
Wednesday, May 21, 2014
MFUKO WA MWENYEKITI WAKATALIWA
Na John Gagarini, Kibaha
MKOA wa Pwani umeingia umeingia mkataba na wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa halmashauri na wenyeviti wa halmashauri juu ya utekelezaji wa mpango wa kupunguza vifo vya mama wajawazito watoto wachanga na wale wenye umri chini ya miaka mitano.
Pia mkoa umeingia na viongozi hao kwenye mkataba kwa ajili ya makusanyo ya mapato ambayo waliyapitisha kuwa wana uwezo wa kuyakusanya kwenye halmashauri za wilaya saba za mkoa huo katika kipindi cha bajeti ya mwaka 2014-2015.
Tukio hilo la kihistoria la kusaini mikataba hiyo ya kazi kwa viongozi hao ndani ya mkoa wa Pwani lilifanyika juzi mjini Kibaha na lilisimamiwa na mkuu wa mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza na mwanasheria wa mkoa Mohamed Magati ambapo viongozi hao endapo watashindwa kufikia malengo yaliyowekwa itawabidi kujieleza.
Wakuu wa wilaya ambao waliingia mikataba hiyo na wilaya zao ni pamoja na Mercy Silla wilaya ya Mkuranga, Fatuma Kimariyo Kisarawe, Nurdin Babu Rufiji, Sauda Mtondoo wilaya ya Mafia, Ahmed Kipozi wilaya ya Bagamoyo na Halima Kihemba wilaya ya Kibaha.
Akizungumza na watendaji hao kuhusiana na mikata hiyo walioingia na mkoa Mahiza alisema kuwa mikataba hiyo itasaidia uwajibikaji kwa watendaji hao ambao wanawatumikia wananchi katika kuwaletea maendeleo.
“Mikataba hii ni changamoto kwa watendaji wetu hawa na endapo watashindwa kutekeleza majukumu yao kama mkataba unavyoonyesha itabidi wajieleze kwani hata mimi nishaingia mikataba na mamlaka za juu hivyo kila mtu lazima atimize wajibu wake,” alisema Mahiza.
Mahiza alisema kuwa kwa upande wa vifo vya mama wajawazito, watoto wa changa na wale wenye umri chini ya miaka mitano ni tatizo kubwa hivyo mkataba huo utasaidia kupunguza vifo hivyo visivyo vya lazima.
“Kwa upande wa makusanyo kila halmashauri ilileta makadirio yake ya kukusanya mapato kwenye bajeti ya mwaka 2014- 2015 hivyo ni lazima watimize kusudio lao na hakuna sababu ya kusema wameshindwa kuyafikia malengo hayo ya ukusanyaji wa mapato,” alisema Mahiza.
Halmashauri hizo kila moja imejiwekea kiwango chake cha kukusanya kutegemeana na vyanzo vyake vya mapato ambapo Bagamoyo watakusanya bilioni2.6, Kibaha Mjini, bilioni 4.2, Kibaha Vijijini bilioni 2.6, Kisarawe bilioni 3.8, Mafia bilioni 1, Mkuranga bilioni 2.1 na Rufiji bilioni 2.7 ambapo jumla ya makusanyo hayo kwa wilaya zote za mkoa huo itakuwa ni bilioni 8.7
Naye mganga mkuu wa mkoa wa Singida ambaye alishinda tuzo ya Rais ya kupunguza vifo vya makundi hayo Dk Doroth Gwajima alisema kuwa vifo vingi vinatokana na uzembe wa baadhi ya watumishi wasio na maadili ya kazi.
Dk Gwajima aliwataka wahudumu wa afya kwenye mkoa huo wa Pwani kumtanguliza Mungu wakati wa utendaji wao wa kazi pia kuzingatia maadili ya kazi zao kwani baadhi ya vifo vinatokana na uzembe na si mapenzi ya Mungu.
Mwisho.
Thursday, May 15, 2014
WACHEZAJI WAMIMINIKA RUVU SHOOTING KUOMBA USAJILI
Na John Gagarini, Kibaha
JUMLA ya wachezaji 251 wamejitokeza kufanya majaribio kwenye
kikosi cha Ruvu Shooting ya Wilayani Kibaha mkoani Pwani ili kusajiliwa na timu
hiyo waweze kupata nafasi kwenye timu hiyo kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu
ya Voda Com.
Akizungumza na wachezaji hao kwenye uwanja wa Ruvu Kocha Mkuu
Tom Olaba alisema kuwa lengo la kutangaza nafasi hiyo ya kuwaita
wachezaji ni kuwapatia fursa chipukizi wenye uwezo wa kusakata soka ili waweze
kutoa mchango wao kwenye kikosi hicho kinachojiandaa na Ligi Kuu ya msimu ujao.
Olaba alisema kuwa wamewaita wachezaji hao kufanya majaribio ili wataofanikiwa majaribio hayo waweze kupata nafasi ya kukitumikia kikosi chetu ya Ruvu Shooting tayari kwa Ligi Kuu ya Vodacom msimu ujao unaotaraji kuanza kutimua vumbi mwezi wa 8 mwaka huu, hivyo wanapaswa kuonesha uwezo na watakaofaulu watapata nafasi bila ya upendeleo.
“Mazoezi haya yataendelea kwa wiki mbili ambayo yatakuwa yanachezwa kwa mtindo wa bonanza ikiwa na lengo la kuwapatia nafasi nzuri zaidi wachezaji kuonesha uwezo wao wa kucheza soka na hatimye wapatikane wachezaji wenye vipaji,” alisema Olaba.
Naye Mkuu wa Kikosi cha Ruvu kilichopo kikosi hicho Luteni Kanali Charles Mbuge alisema kuwa uongozi huo bado unaendelea kuwataka vijana zaidi wajitokeze kwani lengo ni kuhakikisha wanapata wachezaji wenye uwezo watakaosajiliwa kwa
ajili ya Ligi Kuu na wale wenye chini ya umri wa miaka 20.
"Lengo kubwa ni kuhakikisha tunapata wachezaji ambao wataisaidia timu ili iweze kufanya vyema kwenye ligi ijayo pamoja na kuwaandaa vijana wengine watakaoitumikia timu miaka ya baadaye kwenyeligi zijazo," alisema Luteni Mbuge.
Kanali Mbuge.
Aidha Luteni Mbunge alitoa shukrani kwa jopo la makocha mbali ya Olaba na msaidizi wake Seleman Mtungwe ambao wamejipanga vizuri katika kuhakikisha zoezi hilo linakwenda kama lilivyopangwa na hatimaye kupatikana kwa wachezaji bora zaidi watakaoongezea ushindani katika kikosi hicho kwenye kinyang'anyiro kijacho.
MWISHO
Olaba alisema kuwa wamewaita wachezaji hao kufanya majaribio ili wataofanikiwa majaribio hayo waweze kupata nafasi ya kukitumikia kikosi chetu ya Ruvu Shooting tayari kwa Ligi Kuu ya Vodacom msimu ujao unaotaraji kuanza kutimua vumbi mwezi wa 8 mwaka huu, hivyo wanapaswa kuonesha uwezo na watakaofaulu watapata nafasi bila ya upendeleo.
“Mazoezi haya yataendelea kwa wiki mbili ambayo yatakuwa yanachezwa kwa mtindo wa bonanza ikiwa na lengo la kuwapatia nafasi nzuri zaidi wachezaji kuonesha uwezo wao wa kucheza soka na hatimye wapatikane wachezaji wenye vipaji,” alisema Olaba.
Naye Mkuu wa Kikosi cha Ruvu kilichopo kikosi hicho Luteni Kanali Charles Mbuge alisema kuwa uongozi huo bado unaendelea kuwataka vijana zaidi wajitokeze kwani lengo ni kuhakikisha wanapata wachezaji wenye uwezo watakaosajiliwa kwa
ajili ya Ligi Kuu na wale wenye chini ya umri wa miaka 20.
"Lengo kubwa ni kuhakikisha tunapata wachezaji ambao wataisaidia timu ili iweze kufanya vyema kwenye ligi ijayo pamoja na kuwaandaa vijana wengine watakaoitumikia timu miaka ya baadaye kwenyeligi zijazo," alisema Luteni Mbuge.
Kanali Mbuge.
Aidha Luteni Mbunge alitoa shukrani kwa jopo la makocha mbali ya Olaba na msaidizi wake Seleman Mtungwe ambao wamejipanga vizuri katika kuhakikisha zoezi hilo linakwenda kama lilivyopangwa na hatimaye kupatikana kwa wachezaji bora zaidi watakaoongezea ushindani katika kikosi hicho kwenye kinyang'anyiro kijacho.
MWISHO
MLINZI ANYONGWA
Na John Gagarini, Kibaha
MLINZI Bakari Mape (70) mkazi wa Mlandizi wilaya ya Kibaha mkoa wa Pwani
ameuwawa kwa kunyongwa na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi.
Watu hao ambao idadi yao haikuweza kufahamika mara moja walimwua mlinzi
huyo kwa kumvunja shingo kisha kuiba kwenye duka ambalo mlinzi huyo alikuwa
akililinda.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa Polisi mkoani humo Kamishna
Mwandamizi Msaidizi (SACP) Ulrich Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea Mei
14 mwaka huu majira ya saa 8 usiku eneo la sokoni Mlandizi wilayani hapa.
Kamanda Matei alisema kuwa watu hao baada ya kumwua marehemu ambaye alikuwa
akilinda duka la Conrad Masawe (53) mkazi wa Mtongani Mlandizi, waliiba kiasi
cha shilingi milioni 5.2.
"Walipomwua walingoa bati kisha kuingia ndani na kuiba fedha hizo na
kutoweka kusikofahamika huku wakimwacha marehemu hapo," alisema Kamanda
Matei.
Alisema kuwa kutokana na tukio hilo wanamshikilia mtu mmoja aitwaye Omary
Rajabu kuhusiana na suala hilo.
"Mwili wa marehemu ulikabidhiw andugu kwa ajili ya mazishi baada ya
uchunguzi wa daktari na tutawasaka watu walihusika na tukio hilo ili mkondo wa
sheria uweze kuchukua hatua kwani kitendo hicho ni ukatili ndani ya
jamii," alisema Kamanda Matei.
Aidha aliwataka wafanyabiashara waajiri watu weny umri wa kati ili waweze
kukabiliana na matukio kama hayo na kuacha kuajiri watu wenye umri mkubwa sana
kwani ni vigumu kukabiliana na matukio kama hayo.
mwisho.
Friday, May 9, 2014
VIJANA KUSAIDIWA NA RED CROSS
Na John Gagarini, Kibaha
ASASI isiyo ya Kiserikali ya Amani Development Organization (ADEO) la Kibaha mkoani Pwani limetenga kiasi cha shilingi milioni 10 kwa ajili ya kuwakopesha wasichana waliokuwa wakifanyabiashara ya ngono na matumizi ya dawa za kulevya zaidi ya 20.
Mbali ya kuwakopesha fedha hizo pia shirika hilo linawapatia elimu ya kuepukana na mambo hayo ambayo yamekuwa chanzo cha maambukizi ya magonjwa ukiwemo UKIMWI.
Akizungumza jana mjini Kibaha kwenye mkutano shirikishi wa utekelezaji wa programu ya vijana kupambana na UKIMWI inayofadhiliwa na Sat Tanzania, mratibu wa shirika hilo Jane Apollo alisema kuwa lengo la kuwakopesha fedha hizo ni kuwapatia njia mbadala ili wajiepushe na vitendo hivyo.
Apollo alisema kuwa kupitia mpango huo umeweza kuwafikia vijana wa ndani na nje ya shule 3,817 ambapo kati yao wasichana wanaofanya biashara ya ngono 41 wanaume 11 wanaofanya mapenzi ya jinsia moja, vijana 63 wanaotumia dawa za kulevya na machimbo sita ya mchanga.
"Lengo ni kuwafanya vijana kuachana na vitendo vya matumizi ya dawa za kulevya na biashara ya ngono na kuwafundisha shughuli za ujasiriamali ili kuinua kipato chao na kupunguza umaskini katika maisha yao," alisema Apollo.
Moja ya waischana waliokuwa wakifanya biashaya ya ngono (Subira Hatibu) Jasmini siyo jina halisi alisema kuwa alikuwa akiishi Jijini Dar es Salaam na kujiuza kwa wanaume ambapo kwa siku alikuwa akitembea na wanaume watatu au wanne.
"Nilikuwa nikifanya biashara ya kujiuza kuanzia shilingi 50,000 hadi 30,000 kwa mtu mmoja ambapo nilifanya biashara hii kwa muda mrefu lakini sikuona faida yake zaidi ya kupata matatizo," alisema Jasmini.
Naye kijana aliyejitambulisha kwa jina la Omary Mkumba alisema kuwa alikuwa akijihusisha na uvutaji wa bangi pamoja na dawa za kulevya ambazo zilimsababisha kupata ugonjwa wa kifua kikuu lakini baada ya kupatiwa elimu aliamua kuachana na matumizi hayo.
Shirika hilo lilianzishwa mwaka 2010 na linajihusisha na mapambano dhidi ya dawa za kulevya, UKIMWI, biashara ya ngono, mimba za utotoni, ndoa kwenye umri mdogo na afya ya uzazi.
mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA cha Msalaba Mwekundu mkoani Pwani kimtoa misaada ya viatu na vifaa vya shule kwa wanafunzi wa shule ya sekondari Nyumbu na vituo vya kulelea watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu.
Chama hicho kilitoa misaada hiyo kwa lengo la kuwawezesha wanafunzi hao waweze kusoma kwa kuwa na mahitaji muhimu ili kufanikisha masomo yao.
Akizungumza na waandishi wa habari jana mara baada ya sherehe ya siku ya chama hicho inayoadhimishwa kila mwaka ambapo bkitaifa ilifanyika mkoani Mbeya, katibu msaidizi wa msalaba mwekundu mkoani humo, Felisiana Mmasi alisema kuwa waliamua kuadhimisha siku hiyo kwa kuwasaidia wanafunzi.
Mmasi alisema kuwa lengo la chama hicho ni kuwasaidia watu wenye matatizo mbalimbali kwenye jamii ikiwa ni pamoja na kutoa msaada kwenye majanga na maafa yanoyojitokeza ikiwa ni pamoja na ajali, mafuriko na kwenye vita.
"Mbali ya kutoa viatu pia tumetoa madaftari na kalamu ambapo vituo vya watoto waishio kwenye mazingira magumu vya THADEI na Buloma wamenufaika na misaada hiyo," alisema Mmasi.
Naye mratibu wa mradi wa Life kupitia chama hicho Kibaha Mjini Agnes Lubogo alisema kuwa mbali ya kusaidia kutoa misaada mbalimbali pia wanasaidia kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI walio majumbani.
Lubogo alisema kuwa wanahudumia wagonjwa ambao watoro ambao hawapati huduma mahospitalini hivyo kuwafuata huko waliko ambapo wana wahudumu wa nyumbani wapatao 73.
Aliwataka watu kujiunga na chama hicho ili waweze kuisaidia jamii ambayo inahitaji misaada mbalimbali ya kiutu ikiwa ni pamoja na kujitolea damu kwa ajili ya kuwasaidia wagonjwa.
mwisho.
ASASI isiyo ya Kiserikali ya Amani Development Organization (ADEO) la Kibaha mkoani Pwani limetenga kiasi cha shilingi milioni 10 kwa ajili ya kuwakopesha wasichana waliokuwa wakifanyabiashara ya ngono na matumizi ya dawa za kulevya zaidi ya 20.
Mbali ya kuwakopesha fedha hizo pia shirika hilo linawapatia elimu ya kuepukana na mambo hayo ambayo yamekuwa chanzo cha maambukizi ya magonjwa ukiwemo UKIMWI.
Akizungumza jana mjini Kibaha kwenye mkutano shirikishi wa utekelezaji wa programu ya vijana kupambana na UKIMWI inayofadhiliwa na Sat Tanzania, mratibu wa shirika hilo Jane Apollo alisema kuwa lengo la kuwakopesha fedha hizo ni kuwapatia njia mbadala ili wajiepushe na vitendo hivyo.
Apollo alisema kuwa kupitia mpango huo umeweza kuwafikia vijana wa ndani na nje ya shule 3,817 ambapo kati yao wasichana wanaofanya biashara ya ngono 41 wanaume 11 wanaofanya mapenzi ya jinsia moja, vijana 63 wanaotumia dawa za kulevya na machimbo sita ya mchanga.
"Lengo ni kuwafanya vijana kuachana na vitendo vya matumizi ya dawa za kulevya na biashara ya ngono na kuwafundisha shughuli za ujasiriamali ili kuinua kipato chao na kupunguza umaskini katika maisha yao," alisema Apollo.
Moja ya waischana waliokuwa wakifanya biashaya ya ngono (Subira Hatibu) Jasmini siyo jina halisi alisema kuwa alikuwa akiishi Jijini Dar es Salaam na kujiuza kwa wanaume ambapo kwa siku alikuwa akitembea na wanaume watatu au wanne.
"Nilikuwa nikifanya biashara ya kujiuza kuanzia shilingi 50,000 hadi 30,000 kwa mtu mmoja ambapo nilifanya biashara hii kwa muda mrefu lakini sikuona faida yake zaidi ya kupata matatizo," alisema Jasmini.
Naye kijana aliyejitambulisha kwa jina la Omary Mkumba alisema kuwa alikuwa akijihusisha na uvutaji wa bangi pamoja na dawa za kulevya ambazo zilimsababisha kupata ugonjwa wa kifua kikuu lakini baada ya kupatiwa elimu aliamua kuachana na matumizi hayo.
Shirika hilo lilianzishwa mwaka 2010 na linajihusisha na mapambano dhidi ya dawa za kulevya, UKIMWI, biashara ya ngono, mimba za utotoni, ndoa kwenye umri mdogo na afya ya uzazi.
mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA cha Msalaba Mwekundu mkoani Pwani kimtoa misaada ya viatu na vifaa vya shule kwa wanafunzi wa shule ya sekondari Nyumbu na vituo vya kulelea watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu.
Chama hicho kilitoa misaada hiyo kwa lengo la kuwawezesha wanafunzi hao waweze kusoma kwa kuwa na mahitaji muhimu ili kufanikisha masomo yao.
Akizungumza na waandishi wa habari jana mara baada ya sherehe ya siku ya chama hicho inayoadhimishwa kila mwaka ambapo bkitaifa ilifanyika mkoani Mbeya, katibu msaidizi wa msalaba mwekundu mkoani humo, Felisiana Mmasi alisema kuwa waliamua kuadhimisha siku hiyo kwa kuwasaidia wanafunzi.
Mmasi alisema kuwa lengo la chama hicho ni kuwasaidia watu wenye matatizo mbalimbali kwenye jamii ikiwa ni pamoja na kutoa msaada kwenye majanga na maafa yanoyojitokeza ikiwa ni pamoja na ajali, mafuriko na kwenye vita.
"Mbali ya kutoa viatu pia tumetoa madaftari na kalamu ambapo vituo vya watoto waishio kwenye mazingira magumu vya THADEI na Buloma wamenufaika na misaada hiyo," alisema Mmasi.
Naye mratibu wa mradi wa Life kupitia chama hicho Kibaha Mjini Agnes Lubogo alisema kuwa mbali ya kusaidia kutoa misaada mbalimbali pia wanasaidia kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI walio majumbani.
Lubogo alisema kuwa wanahudumia wagonjwa ambao watoro ambao hawapati huduma mahospitalini hivyo kuwafuata huko waliko ambapo wana wahudumu wa nyumbani wapatao 73.
Aliwataka watu kujiunga na chama hicho ili waweze kuisaidia jamii ambayo inahitaji misaada mbalimbali ya kiutu ikiwa ni pamoja na kujitolea damu kwa ajili ya kuwasaidia wagonjwa.
mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
ASASI isiyo ya Kiserikali ya Amani Development Organization (ADEO) la Kibaha mkoani Pwani limetenga kiasi cha shilingi milioni 10 kwa ajili ya kuwakopesha wasichana waliokuwa wakifanyabiashara ya ngono na matumizi ya dawa za kulevya zaidi ya 20.
Mbali ya kuwakopesha fedha hizo pia shirika hilo linawapatia elimu ya kuepukana na mambo hayo ambayo yamekuwa chanzo cha maambukizi ya magonjwa ukiwemo UKIMWI.
Akizungumza jana mjini Kibaha kwenye mkutano shirikishi wa utekelezaji wa programu ya vijana kupambana na UKIMWI inayofadhiliwa na Sat Tanzania, mratibu wa shirika hilo Jane Apollo alisema kuwa lengo la kuwakopesha fedha hizo ni kuwapatia njia mbadala ili wajiepushe na vitendo hivyo.
Apollo alisema kuwa kupitia mpango huo umeweza kuwafikia vijana wa ndani na nje ya shule 3,817 ambapo kati yao wasichana wanaofanya biashara ya ngono 41 wanaume 11 wanaofanya mapenzi ya jinsia moja, vijana 63 wanaotumia dawa za kulevya na machimbo sita ya mchanga.
"Lengo ni kuwafanya vijana kuachana na vitendo vya matumizi ya dawa za kulevya na biashara ya ngono na kuwafundisha shughuli za ujasiriamali ili kuinua kipato chao na kupunguza umaskini katika maisha yao," alisema Apollo.
Moja ya waischana waliokuwa wakifanya biashaya ya ngono (Subira Hatibu) Jasmini siyo jina halisi alisema kuwa alikuwa akiishi Jijini Dar es Salaam na kujiuza kwa wanaume ambapo kwa siku alikuwa akitembea na wanaume watatu au wanne.
"Nilikuwa nikifanya biashara ya kujiuza kuanzia shilingi 50,000 hadi 30,000 kwa mtu mmoja ambapo nilifanya biashara hii kwa muda mrefu lakini sikuona faida yake zaidi ya kupata matatizo," alisema Jasmini.
Naye kijana aliyejitambulisha kwa jina la Omary Mkumba alisema kuwa alikuwa akijihusisha na uvutaji wa bangi pamoja na dawa za kulevya ambazo zilimsababisha kupata ugonjwa wa kifua kikuu lakini baada ya kupatiwa elimu aliamua kuachana na matumizi hayo.
Shirika hilo lilianzishwa mwaka 2010 na linajihusisha na mapambano dhidi ya dawa za kulevya, UKIMWI, biashara ya ngono, mimba za utotoni, ndoa kwenye umri mdogo na afya ya uzazi.
mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA cha Msalaba Mwekundu mkoani Pwani kimtoa misaada ya viatu na vifaa vya shule kwa wanafunzi wa shule ya sekondari Nyumbu na vituo vya kulelea watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu.
Chama hicho kilitoa misaada hiyo kwa lengo la kuwawezesha wanafunzi hao waweze kusoma kwa kuwa na mahitaji muhimu ili kufanikisha masomo yao.
Akizungumza na waandishi wa habari jana mara baada ya sherehe ya siku ya chama hicho inayoadhimishwa kila mwaka ambapo bkitaifa ilifanyika mkoani Mbeya, katibu msaidizi wa msalaba mwekundu mkoani humo, Felisiana Mmasi alisema kuwa waliamua kuadhimisha siku hiyo kwa kuwasaidia wanafunzi.
Mmasi alisema kuwa lengo la chama hicho ni kuwasaidia watu wenye matatizo mbalimbali kwenye jamii ikiwa ni pamoja na kutoa msaada kwenye majanga na maafa yanoyojitokeza ikiwa ni pamoja na ajali, mafuriko na kwenye vita.
"Mbali ya kutoa viatu pia tumetoa madaftari na kalamu ambapo vituo vya watoto waishio kwenye mazingira magumu vya THADEI na Buloma wamenufaika na misaada hiyo," alisema Mmasi.
Naye mratibu wa mradi wa Life kupitia chama hicho Kibaha Mjini Agnes Lubogo alisema kuwa mbali ya kusaidia kutoa misaada mbalimbali pia wanasaidia kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI walio majumbani.
Lubogo alisema kuwa wanahudumia wagonjwa ambao watoro ambao hawapati huduma mahospitalini hivyo kuwafuata huko waliko ambapo wana wahudumu wa nyumbani wapatao 73.
Aliwataka watu kujiunga na chama hicho ili waweze kuisaidia jamii ambayo inahitaji misaada mbalimbali ya kiutu ikiwa ni pamoja na kujitolea damu kwa ajili ya kuwasaidia wagonjwa.
mwisho.
ASASI isiyo ya Kiserikali ya Amani Development Organization (ADEO) la Kibaha mkoani Pwani limetenga kiasi cha shilingi milioni 10 kwa ajili ya kuwakopesha wasichana waliokuwa wakifanyabiashara ya ngono na matumizi ya dawa za kulevya zaidi ya 20.
Mbali ya kuwakopesha fedha hizo pia shirika hilo linawapatia elimu ya kuepukana na mambo hayo ambayo yamekuwa chanzo cha maambukizi ya magonjwa ukiwemo UKIMWI.
Akizungumza jana mjini Kibaha kwenye mkutano shirikishi wa utekelezaji wa programu ya vijana kupambana na UKIMWI inayofadhiliwa na Sat Tanzania, mratibu wa shirika hilo Jane Apollo alisema kuwa lengo la kuwakopesha fedha hizo ni kuwapatia njia mbadala ili wajiepushe na vitendo hivyo.
Apollo alisema kuwa kupitia mpango huo umeweza kuwafikia vijana wa ndani na nje ya shule 3,817 ambapo kati yao wasichana wanaofanya biashara ya ngono 41 wanaume 11 wanaofanya mapenzi ya jinsia moja, vijana 63 wanaotumia dawa za kulevya na machimbo sita ya mchanga.
"Lengo ni kuwafanya vijana kuachana na vitendo vya matumizi ya dawa za kulevya na biashara ya ngono na kuwafundisha shughuli za ujasiriamali ili kuinua kipato chao na kupunguza umaskini katika maisha yao," alisema Apollo.
Moja ya waischana waliokuwa wakifanya biashaya ya ngono (Subira Hatibu) Jasmini siyo jina halisi alisema kuwa alikuwa akiishi Jijini Dar es Salaam na kujiuza kwa wanaume ambapo kwa siku alikuwa akitembea na wanaume watatu au wanne.
"Nilikuwa nikifanya biashara ya kujiuza kuanzia shilingi 50,000 hadi 30,000 kwa mtu mmoja ambapo nilifanya biashara hii kwa muda mrefu lakini sikuona faida yake zaidi ya kupata matatizo," alisema Jasmini.
Naye kijana aliyejitambulisha kwa jina la Omary Mkumba alisema kuwa alikuwa akijihusisha na uvutaji wa bangi pamoja na dawa za kulevya ambazo zilimsababisha kupata ugonjwa wa kifua kikuu lakini baada ya kupatiwa elimu aliamua kuachana na matumizi hayo.
Shirika hilo lilianzishwa mwaka 2010 na linajihusisha na mapambano dhidi ya dawa za kulevya, UKIMWI, biashara ya ngono, mimba za utotoni, ndoa kwenye umri mdogo na afya ya uzazi.
mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA cha Msalaba Mwekundu mkoani Pwani kimtoa misaada ya viatu na vifaa vya shule kwa wanafunzi wa shule ya sekondari Nyumbu na vituo vya kulelea watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu.
Chama hicho kilitoa misaada hiyo kwa lengo la kuwawezesha wanafunzi hao waweze kusoma kwa kuwa na mahitaji muhimu ili kufanikisha masomo yao.
Akizungumza na waandishi wa habari jana mara baada ya sherehe ya siku ya chama hicho inayoadhimishwa kila mwaka ambapo bkitaifa ilifanyika mkoani Mbeya, katibu msaidizi wa msalaba mwekundu mkoani humo, Felisiana Mmasi alisema kuwa waliamua kuadhimisha siku hiyo kwa kuwasaidia wanafunzi.
Mmasi alisema kuwa lengo la chama hicho ni kuwasaidia watu wenye matatizo mbalimbali kwenye jamii ikiwa ni pamoja na kutoa msaada kwenye majanga na maafa yanoyojitokeza ikiwa ni pamoja na ajali, mafuriko na kwenye vita.
"Mbali ya kutoa viatu pia tumetoa madaftari na kalamu ambapo vituo vya watoto waishio kwenye mazingira magumu vya THADEI na Buloma wamenufaika na misaada hiyo," alisema Mmasi.
Naye mratibu wa mradi wa Life kupitia chama hicho Kibaha Mjini Agnes Lubogo alisema kuwa mbali ya kusaidia kutoa misaada mbalimbali pia wanasaidia kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI walio majumbani.
Lubogo alisema kuwa wanahudumia wagonjwa ambao watoro ambao hawapati huduma mahospitalini hivyo kuwafuata huko waliko ambapo wana wahudumu wa nyumbani wapatao 73.
Aliwataka watu kujiunga na chama hicho ili waweze kuisaidia jamii ambayo inahitaji misaada mbalimbali ya kiutu ikiwa ni pamoja na kujitolea damu kwa ajili ya kuwasaidia wagonjwa.
mwisho.
Tuesday, May 6, 2014
WASAIDIZI WA SHERIA WATAKA KUTAMBULIWA
Na John Gagarini, Kibaha
KITUO cha Msaada wa Kisheria wilayani Kibaha mkoani Pwani kimeiomba serikali kuwatambua wasaidizi wa kisheria ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi.
Kutokana na changamoto nyingi za kisheria kuikabili jamii na watu wengi kukosa haki zao kwa kushindwa kujua sheria ambazo ndo msingi wa haki za binadamu wasaidizi hao.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mafunzo kwa wasaidizi wa kisheria wa wilaya ya Kibaha ambayo yalitolewa na kituo cha msaada wa kisheria kwa wanawake (WLAC), mwenyekiti wa kituo hicho Israel Sazia alisema kuwa wasaidizi hao bado hawajatambuliwa rasmi na serikali.
Sazia alisema kuwa endapo wasimamizi wa msaada wa kisheria watatambuliwa wataweza kuisaidia jamii kutambua sheria mbalimbali ambazo zitawafanya wapate haki zao mara inapotokea migogoro kwenye jamii.
"Endapo watatambuliwa itasaidia hata kuwapatiwa misaada na fursa mbalimbali kutoka serikalini kupitia kwenye halmashauri kwa ajili ya kuiwezesha jamii katika masuala yanayohusu sheria," alisema Sazia.
Alisema kuwa wananchi wengi hawajui taratibu za kutafuta haki ikiwa ni pamoja na wanawake kwenye masuala mbalimbali endapo watashindwa kuendelea kuishi na mume wake pamoja hivyo kudai talaka.
"Kumekuwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na masuala ya mirathi, haki za watoto, migogoro ya ardhi na masuala ya ndoa ambazo zimekuwa zikileta migogoro mingi kwenye jamii," alisema Sazia.
Aidha alisema kuwa kituo chao kilichoanzishwa mwaka 2001 kimekuwa na changamoto kubwa ya wasaidizi hao kulegalega katika utendaji kazi kutokana na wengi wao kushindwa kujitolea hivyo kushindwa kufanya kazi kikamilifu.
Aliwataka wasaidizi hao wa kisheria kufanya kazi kwa kuzingatia weledi wa kazi zao ili kuweza kuisaidia jamii ambayo ina mahitaji makubwa ya kujua sheria mbalimbali katika maeneo yao ili waweze kupata haki zao za msingi.
Baadhi ya masomo waliyofundishwa ni pamoja na uelewa kuhusu dhana ya ya msaidizi wa kisheria, misingi na vyanzo vya sheria, sheria ya ndoa, sheria ya mirathi na taratibu za ufunguaji wa mirathi, sheria ya ardhi sura namba 113, sheria ya utatuzi wa migogoro ya ardhi ya mwaka 2002, haki ya mtoto ya mwaka 1999 na ukusanyaji na utunzaji wa taarifa za wateja na uandishi wa ripoti ya mwezi. Mafunzo hayo yaliwahusisha wasaidizi zaidi ya 30.
mwisho.
KITUO cha Msaada wa Kisheria wilayani Kibaha mkoani Pwani kimeiomba serikali kuwatambua wasaidizi wa kisheria ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi.
Kutokana na changamoto nyingi za kisheria kuikabili jamii na watu wengi kukosa haki zao kwa kushindwa kujua sheria ambazo ndo msingi wa haki za binadamu wasaidizi hao.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mafunzo kwa wasaidizi wa kisheria wa wilaya ya Kibaha ambayo yalitolewa na kituo cha msaada wa kisheria kwa wanawake (WLAC), mwenyekiti wa kituo hicho Israel Sazia alisema kuwa wasaidizi hao bado hawajatambuliwa rasmi na serikali.
Sazia alisema kuwa endapo wasimamizi wa msaada wa kisheria watatambuliwa wataweza kuisaidia jamii kutambua sheria mbalimbali ambazo zitawafanya wapate haki zao mara inapotokea migogoro kwenye jamii.
"Endapo watatambuliwa itasaidia hata kuwapatiwa misaada na fursa mbalimbali kutoka serikalini kupitia kwenye halmashauri kwa ajili ya kuiwezesha jamii katika masuala yanayohusu sheria," alisema Sazia.
Alisema kuwa wananchi wengi hawajui taratibu za kutafuta haki ikiwa ni pamoja na wanawake kwenye masuala mbalimbali endapo watashindwa kuendelea kuishi na mume wake pamoja hivyo kudai talaka.
"Kumekuwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na masuala ya mirathi, haki za watoto, migogoro ya ardhi na masuala ya ndoa ambazo zimekuwa zikileta migogoro mingi kwenye jamii," alisema Sazia.
Aidha alisema kuwa kituo chao kilichoanzishwa mwaka 2001 kimekuwa na changamoto kubwa ya wasaidizi hao kulegalega katika utendaji kazi kutokana na wengi wao kushindwa kujitolea hivyo kushindwa kufanya kazi kikamilifu.
Aliwataka wasaidizi hao wa kisheria kufanya kazi kwa kuzingatia weledi wa kazi zao ili kuweza kuisaidia jamii ambayo ina mahitaji makubwa ya kujua sheria mbalimbali katika maeneo yao ili waweze kupata haki zao za msingi.
Baadhi ya masomo waliyofundishwa ni pamoja na uelewa kuhusu dhana ya ya msaidizi wa kisheria, misingi na vyanzo vya sheria, sheria ya ndoa, sheria ya mirathi na taratibu za ufunguaji wa mirathi, sheria ya ardhi sura namba 113, sheria ya utatuzi wa migogoro ya ardhi ya mwaka 2002, haki ya mtoto ya mwaka 1999 na ukusanyaji na utunzaji wa taarifa za wateja na uandishi wa ripoti ya mwezi. Mafunzo hayo yaliwahusisha wasaidizi zaidi ya 30.
mwisho.
Subscribe to:
Posts (Atom)