Na John Gagarini, Kibaha
HALMASHAURI kote nchini zimetakiwa kupima maeneo ya shule ili kuepuka
kuvamiwa kwani hazina hati za kumiliki maeneo hayo kisheria na kuepuka
wavamizi.
Akizungumza wakati wa kufunga mashindano ya Umoja wa Michezo na
Taaluma kwa Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) Waziri wa Tawala za
Mikoa n Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Hawa Ghasia alisema kuwa maeneo
mengi ya shule hayajapimwa.
Ghasia asliema kuwa anashangaa ni kwa nini halmashauri hazipimi maeneo
ya shule hivyo kuwa rahisi kuvamiwa na watu kwa ajili ya kuyatumia kwa
shughuli za kimaendeleo.
“Inashangaza kuona kuwa maeneo mengi ya shule hayajapimwa na
halmashauri zinaangali tu hali hii ni mbaya kwani mtu anaweza kuvamia
bila ya woga na kwa kuwa hakuna hati miliki hivyo ni rahisi kuichukua
ardhi ya shule,” alisema Ghasia.
Alisema kuwa maeneo hayo nayo yanapaswa kuwa na hati miliki kama
ilivyo umiliki wa watu binafsi au taasisi za serikali.
“Nawaomba wakurugenzi kutekeleza hili ili kuondoa uporwaji wa maeneo
ya shule kwani kwa sasa migogoro ni mingi baina ya mashule na wananchi
ambao wanavamia maeneo hayo,” alisema Ghasia.
Aidha alsiema kuwa halmashauri ziepukane na mawazo ya kuyatoa maeneo
hayo kwa wawekezaji kwa ajili ya kufanyia shughuli za biashara au
matumizi mengine.
“Maeneo kwenye halmashauri yako mengi kwa nini waone maeneo ya shule
ndiyo sehemu ya kuwekeza hilo ni kosa kama wanahitaji maeneo wapewe
maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya uwekezaji,” alisema Ghasia.
Alizitaka halmashauri kuyalinda maeneo ya shule ambayo yamekuwa
yakivamiwa na watu bila ya kuwa na woga wowote licha ya kuwa ni
kinyume cha sheria.
Mwisho.
Sunday, July 7, 2013
Monday, July 1, 2013
TAPELI AWACHIMBISHA KABURI WATU, ATOWEKA NA SIMU ZAO NA KAMERA
Na John Gagarini, Kibaha
MTU mmoja aliyetambuliwa kwa jina la Abdul Ramadhan (35)
amewatapeli baadhi ya wakazi wa Kwa Mathias wilayani Kibaha mkoani Pwani kwa
kuwachimbisha kaburi kisha kutoweka na kuwaachia kaburi tupu bila ya kuzikwa
marehemu kama alivyowaomba azike ndugu yake.
Tukio hilo lilitokea juzi kwenye mtaa huo baada ya mtu huyo
kufika hapo na kuomba kusaidiwa kumzika mfanyakazi wake ambaye alidai kuwa hana
uwezo wa kumsafirisha kwani kwao ni mbali.
Mbali ya kuwachimbisha kaburi wakazi hao pia alifanikiwa
kuwaibia simu mbili pamoja na kamera moja pamoja na kuacha deni kwenye vyakula
ambavyo vilitumiwa na wachimba kaburi huku kingine kikiwa kimeandaliwa bila ya
kuliwa.
Akielezea mkasa huo Ustaadhi wa Masjid Kadiriya uliopo Kwa
Mathias Said Omary alisema kuwa mtu huyo alifika msikitini hapo na kukutana na
kiongozi kasha kuomba kuwa asaidiwe kuzikiwa mfanyakazi wake, msikiti
ukamkubalia na taratibu zikaanza kufanyika.
Omary alisema kuwa baada ya kuelekezwa na mkuu wake alitakiwa
ashughulikie suala hilo na kwenda na mtu huyo kwenye makaburi ya mambo akiwa na
watu wengine watatu kwa ajili ya kuchimba kaburi kwa ajili ya kumsitiri
marehemu.
“Tulikwenda makaburini na wachimbaji wakaanza kazi ya
kuchimba kaburi akawaletea chain a maandazi 20 wakanywa wakaendelea na kazi yao
mimi akaniambia twende hospitali ya Tumbi aliko marehemu kwa ajili ya kumwandaa,”
alisema Omary.
Alisema wakiwa njiani alimwambia kuwa anaomba simu yake ili
awasiliane na ndugu zake kwani ya kwake imeisha chaji pia amtafutie mpiga picha
kwa ajili ya tukio hilo kwa ajili ya kuwaonyesha ndugu juu ya mazishi hayo.
“Tulikwenda kwa mpiga picha wakakubaliana apige picha akasema
kabla ya kwenda Tumbi wakachukue nyama na vitu vingine kwa ajili ya msiba huo
na walipofika Maili Moja wakachukua nyama kilogramu 25 na,”alisema Omary.
Aliongeza kuwa wakati
wameshapima nyama aliwaambia ngoja akanunue viungo vingine lakini hakurudi tena
na kutoweka kusikojulikana huku kaburi likiwa limeshachimbwa na liko wazi hadi
sasa.
Kwa upande wake mpiga picha Jum Said ambaye yeye aliibiwa
kamera na simu alisema kuwa walikubaliana apige picha 36 hadi 40 ambazo gharama
yake ni sawa na shilingi 36,000 au 40,000.
Alisema wakati wako kwenye harakati ya kunua nyanya
alimwachia begi likiwa na kamera na simu lakini aliporudi hakumkuta akiwa yeye
na Ustaadhi na dereva wa teksi ambayo aliikodisha kwa shughuli za mazishi hayo.
“Alituacha mimi na ustaadhi tukiwa na nyama huku tukimsubiria
hali amabyo ilitufanya tuingie matatani kwani wauzaji nyama ilibidi watubana
ndipo tulipowaelewesha juu ya hali halisi ndiyo ikawa salama kwetu na kuondoka,”
alisema.
Watu waliokumbwa na hali hiyo walisema kuwa mbali ya
kudanganya mambo yote hayo pia aliweka oda ya chakula sahani 20 kwenye hoteli
lakini hakuonekana tena, katika kufuatilia walibaini jina la mtu huyo kwani
siku moja kabla ya tukio hilo alilala kwenye nyumba ya kulala wageni ya Iwawa
iliyopo mtaa wa Kwa Mbonde jirani na hapo wakazi hao walitoa taarifa kwenye
kituo cha polisi Kwa Mathias juu ya tukio hilo.
Mwisho.
Friday, June 7, 2013
SUMATRA KUDHIBITI MADEREVA PWANI
Na John
Gagarini, Kibaha
MAMLAKA ya Udhibiti
wa usafiri Majini na Nchini Kavu (SUMATRA) imefungua ofisi yake mkoani Pwani na
kuwataka wananchi kutoa taarifa za mabasi yanayokatisha ruti na kutotoa tiketi
kwa abiria.
Akizungumza na
waandishi wa habari ofisini kwake ofisa mwandamizi wa SUMATRA wa mkoa Iroga
Nashoni alisema kuwa abiria wanapaswa kukitumia chombo hicho ili kuondoa kero
kwa wasafiri.
Iroga alisema
kuwa ofisi hiyo imefunguliwa mwezi uliopita kwa lengo la kusogeza huduma kwa
wateja wao ambapo inaendelea kujitanua kwenye mikoa, mingine ikiwa ni Singida,
Iringa, Musoma na Rukwa.
Alisema kuwa
changamoto kubwa waliyoiona ni mabasi mengi ya abiria kushindwa kumalizia
safari zao Kukatisha Ruti) na kutotoa tiketi kwa abiria jambo ambalo ni kinyume
cha sheria ambapo watawapiga faini hata ikibidi kuwafungia leseni madereva
watukutu.
“Changamoto
hiyo inakuwa kubwa kutokana na abiria wengi kutokuwa na elimu ya kujua haki zao
za msingi wanapokuwa wanasafiri hivyo kuwapa mwanya madereva kufanya watakavyo,”
alisema Iroga.
Aliongeza kuwa
wataendelea kutoa elimu kwa pande zote ikiwa ni pamoja na abiria, madereva na
wamiliki wa mabasi hayo ili waweze kufuata sheria bila ya kushurutishwa.
“Jana tulifanya
operesheni kukamata magari yenye makosa mbalimbali ambapo magari manne
yamekutwa na makosa na kupigwa faini kutegemea na makosa,” alisema Iroga.
Alibainisha kuwa
wataendelea kufanya operesheni za kushtukiza za mara kwa mara ili kukabiliana
na madereva wengi kukiuka sheria za barabarani na kuwataka wananchi kutoa
taarifa na si kulalamika bali wachukue hatua.
Mwisho.
MBUNGE AMWAGA VIFAA TIMU YA UMISSETA
Na John Gagarini, Kibaha
MBUNGE wa Jimbo la Kibaha mkoani Pwani Silvestry Koka ametoa seti za
jezi kwa timu za mpira wa pete na soka za mkoa huo zinazojiandaa na
mashindano ya Umoja wa Michezo na Sanaa kwa Shule za Sekondari
Tanzania (UMISSETA) Kanda ya Mashariki inayotarajiwa kutimua vumbi
hivi karibuni mjini Kibaha.
Jezi hizo zimekabidhiwa kwa timu hiyo na mke wa mbunge huyo Selina
Koka kwenye kambi ya timu hiyo iliyopo kwenye shule ya Filbert Bayi
iliyopo wilayani Kibaha.
Mbali ya jezi hizo pia timu ya mkoa iliahidiwa kupatiwa mipira ya
michezo hiyo, mchele, kilogramu 100, mafuta ya kupikia, maji na sukari
pamoja na kumkabidhi mwalimu wa timu hiyo Loyd Mgombele kiasi cha
shilingi 100,000 kwa ajili ya shughuli za kuratibu timu hiyo.
Akiwakabidhi manahodha wa timu ya mpira wa pete na mpira wa miguu Koka
alisema kuwa lengo la kutoa vitu hivyo ni kuhamasisha timu hiyo ili
iweze kufanya vizuri kwenye michezo yake dhidi ya mkoa wa Morogoro ili
kuunda timu ya Kanda.
Koka alisema kuwa mkoa wa Pwani ni wenyeji wa mashindano hayo
wanapaswa kuwa na maandalizi mazuri ili kuweza kuwakilisha vema mkoa
na baadaye Taifa ambapo michuano hiyo itafanyika kwenye viwanja vya
Shirika la Elimu Kibaha Tumbi.
Aliwataka wachezaji hao kujituma kuzingatia yale wanayofundishwa na
walimu wao ili kuhakikisha wanafanya vyema na kutoa wachezaji wazuri
ili kuunda timu ya Kanda inayoundwa na mikoa ya Pwani na Morogoro.
Kwa upande wake ofisa elimu taaluma mkoa wa Pwani Godwin Mkaruka
ambaye aliwakilisha mkoa huo alisema kuwa ana mpongeza mbunge huyo kwa
kuisaidia timu ya mkoa ili iweze kuwakilisha vema mkoa huo.
Aliwataka wadau mbalimbali kujitokeza kuisaidia timu hiyo kwa hali na
mali kama alivyojitolea Mbunge huyo ili iweze kuuletea mkoa ushindi
katika michuano hiyo ambayo hufanyika wilayani humo kila mwaka.
Mwisho.
MBUNGE wa Jimbo la Kibaha mkoani Pwani Silvestry Koka ametoa seti za
jezi kwa timu za mpira wa pete na soka za mkoa huo zinazojiandaa na
mashindano ya Umoja wa Michezo na Sanaa kwa Shule za Sekondari
Tanzania (UMISSETA) Kanda ya Mashariki inayotarajiwa kutimua vumbi
hivi karibuni mjini Kibaha.
Jezi hizo zimekabidhiwa kwa timu hiyo na mke wa mbunge huyo Selina
Koka kwenye kambi ya timu hiyo iliyopo kwenye shule ya Filbert Bayi
iliyopo wilayani Kibaha.
Mbali ya jezi hizo pia timu ya mkoa iliahidiwa kupatiwa mipira ya
michezo hiyo, mchele, kilogramu 100, mafuta ya kupikia, maji na sukari
pamoja na kumkabidhi mwalimu wa timu hiyo Loyd Mgombele kiasi cha
shilingi 100,000 kwa ajili ya shughuli za kuratibu timu hiyo.
Akiwakabidhi manahodha wa timu ya mpira wa pete na mpira wa miguu Koka
alisema kuwa lengo la kutoa vitu hivyo ni kuhamasisha timu hiyo ili
iweze kufanya vizuri kwenye michezo yake dhidi ya mkoa wa Morogoro ili
kuunda timu ya Kanda.
Koka alisema kuwa mkoa wa Pwani ni wenyeji wa mashindano hayo
wanapaswa kuwa na maandalizi mazuri ili kuweza kuwakilisha vema mkoa
na baadaye Taifa ambapo michuano hiyo itafanyika kwenye viwanja vya
Shirika la Elimu Kibaha Tumbi.
Aliwataka wachezaji hao kujituma kuzingatia yale wanayofundishwa na
walimu wao ili kuhakikisha wanafanya vyema na kutoa wachezaji wazuri
ili kuunda timu ya Kanda inayoundwa na mikoa ya Pwani na Morogoro.
Kwa upande wake ofisa elimu taaluma mkoa wa Pwani Godwin Mkaruka
ambaye aliwakilisha mkoa huo alisema kuwa ana mpongeza mbunge huyo kwa
kuisaidia timu ya mkoa ili iweze kuwakilisha vema mkoa huo.
Aliwataka wadau mbalimbali kujitokeza kuisaidia timu hiyo kwa hali na
mali kama alivyojitolea Mbunge huyo ili iweze kuuletea mkoa ushindi
katika michuano hiyo ambayo hufanyika wilayani humo kila mwaka.
Mwisho.
E89A0881.jpg 1311K View Share Download |
E89A0882.jpg 1162K View Share Download |
E89A0874.jpg 1 |
WANAFUNZI WATAKIWA KULALA ILI WASISIKILIZE WENZAO WAKIFUNDIHSWA
Na John Gagarini, Bagamoyo
SHULE ya Msingi Ludiga wilayani Bagamoyo mkoani Pwani
inakabiliwa na uhaba wa madarasa hali ambayo inasababisha baadhi ya wanafunzi
wa madarasa mawili kusoma chumba kimoja cha darasa huku wengine wakitakiwa
kulala ili wasisikilize wanachofundishwa wenzao.
Akizungumza mbele ya mbunge wa Jimbo la Chalinze Said
Bwanamdogo alipotembelea Kijiji cha Talawanda kata ya Talawanda, mwalimu mkuu msaidizi wa shule hiyo Selestin Casian
alisema kuwa shule hiyo ina madarasa matatu tu.
Casian alisema kuwa mbali ya wanafunzi wa madarasa mawili
kusomea chumba kimoja pia wanafunzi wengine husomea nje kwenye miti kutokana na
upungufu huo wa vyumba vya madarasa.
“Inabidi tuwaambie wanafunzi wa darasa moja walale ili
wasisikilize kinachofundishwa na mwalimu ambaye yuko darasani hasa pale mwalimu
mwingine anapokuwa bado hajaingia,” alisema Casian.
Aidha alisema kuwa licha ya shule hiyo kuwa na mwaka wa 10
sasa tangu kuanzishwa kwake shule hiyo ina walimu watano ambapo ina jumla ya
wanafunzi 320.
“Kwa kweli tunachangamoto kubwa ya madarasa hali ambayo
inasababisha wanafunzi kutopatiwa elimu ipasavyo hivyo tunaiomba halmashauri
kutusaidia ili tuweze kuepukana na adha hii kwani wanafunzi wanashindwa kusoma
vema,” alisema Casian.
Kwa upande wake mbunge wa Bwanamdogo alisema kuwa atapeleka
suala hilo halmashauri ili iweze kutatua changamoto hiyo ambayo inakabili
baadhi ya shule za Jimbo hilo.
“Changamoto ya madarasa na walimu ni kubwa katika Jimbo la
Bagamoyo, lakini kama mnavyojua tatizo kubwa ni fedha kwani halmashauri yetu
haina fedha za kutosha hata hivyo tutaendelea kuhimiza ujenzi kwa kushirikiana
na wananchi,” alisema Bwanamdogo.
Aliitaka jamii kujitolea kwenye ujenzi wa madarasa na si
kuisubiri serikali kwani nayo inakabiliwa na mambo mengi ya kimaendeleo hivyo
wahimizane kuchangania kujenga madarasa.
Mwisho.
Sunday, May 26, 2013
DKT AISHI CHUMBA CHA KUZALISHIA
Na John Gagarini, Bagamoyo
WANANCHI wa Kijiji cha
Msinune kata ya Kiwangwa wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wameiomba serikali
kuwasaidia kujenga nyumba ya mganga ambaye anaishi kwenye chumba cha kuzalishia
kwenye zahanati ya kijiji hicho.
Akizungumza mbele ya mbunge wa Jimbo la Chalinze Said
Bwanamdogo wakati wa kikao cha Halamshauri ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kata ya
Kiwangwa, mwenyekiti wa Kijiji hicho Kesi Hassan alisema mganga huyo inabidi afanye
hivyo kutokana na kukosa nyumba.
Hassan alisema kuwa mganga pamoja na muuguzi wanatumia
wanaishi humo kutokana na uhaba wa nyumba za watumishi katika kijiji hicho.
“Tunaiomba serikali na kwa kupitia kwako kutusaidia ujenzi wa
nyumba za watumishi kwani kutumia chumba kinyume na matumizi si sawa na
haipendezi mazingira ni magumu,” alisema Hassan.
Aidha alisema kuwa watumishi wengi hawana nyumba za kuishi
hivyo kuwapa wakati mgumu katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku ya
kuwahudumia wananchi.
“Suala la nyumba za watumishi ni changamoto ambayo inatukabili
hivyo ni vema kukawa na nguvu ya ziada kutoka juu ili kutusaidia watumishi wetu
waweze kukaa kwenye mazingira mazuri.
Kwa upande wake Bwanamdogo alisema kuwa suala hilo amelipata
na ataangalia jinsi gani ya kuweza kulifanyia kazi ili mganga huyo na watumishi
wengine waweze kuweza kuwa na nyumba.
Bwanamdogo aliwataka viongozi na wananchi kwenye vijiji vya
Jimbo hilo kujitolea kwa kutumia nguvu zao ili kuanzisha ujenzi wa nyumba za
watumishi na ofisi yake itachangia.
Mwisho.
DKT AISHI CHUMBA CHA KUZALISHIA
Na John Gagarini, Bagamoyo
WANANCHI wa Kijiji cha
Msinune kata ya Kiwangwa wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wameiomba serikali
kuwasaidia kujenga nyumba ya mganga ambaye anaishi kwenye chumba cha kuzalishia
kwenye zahanati ya kijiji hicho.
Akizungumza mbele ya mbunge wa Jimbo la Chalinze Said
Bwanamdogo wakati wa kikao cha Halamshauri ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kata ya
Kiwangwa, mwenyekiti wa Kijiji hicho Kesi Hassan alisema mganga huyo inabidi afanye
hivyo kutokana na kukosa nyumba.
Hassan alisema kuwa mganga pamoja na muuguzi wanatumia
wanaishi humo kutokana na uhaba wa nyumba za watumishi katika kijiji hicho.
“Tunaiomba serikali na kwa kupitia kwako kutusaidia ujenzi wa
nyumba za watumishi kwani kutumia chumba kinyume na matumizi si sawa na
haipendezi mazingira ni magumu,” alisema Hassan.
Aidha alisema kuwa watumishi wengi hawana nyumba za kuishi
hivyo kuwapa wakati mgumu katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku ya
kuwahudumia wananchi.
“Suala la nyumba za watumishi ni changamoto ambayo inatukabili
hivyo ni vema kukawa na nguvu ya ziada kutoka juu ili kutusaidia watumishi wetu
waweze kukaa kwenye mazingira mazuri.
Kwa upande wake Bwanamdogo alisema kuwa suala hilo amelipata
na ataangalia jinsi gani ya kuweza kulifanyia kazi ili mganga huyo na watumishi
wengine waweze kuweza kuwa na nyumba.
Bwanamdogo aliwataka viongozi na wananchi kwenye vijiji vya
Jimbo hilo kujitolea kwa kutumia nguvu zao ili kuanzisha ujenzi wa nyumba za
watumishi na ofisi yake itachangia.
Mwisho.
Subscribe to:
Posts (Atom)