Sunday, September 13, 2026

NYIKA NA BABERIAN KUKIPIGA FAINALI MEETING POINT SUPER CUP 2026

TIMU za soka za Nyika na Baberian zinatarajiwa kuchuana kwenye hatua ya fainali ya kinyanganyiro cha Meeting Point Super Cup baada ya kushinda michezo yao ya hatua ya nusu fainali.

Nyika ilifanikiwa kuifunga Kiduli kwa mikwaju ya penati 4-3 kwenye nusu fainali ya kwanza na Baberian waliifunga Nyumbu kwa mabao 2-0 michezo yote ilifanyika uwanja wa Mwendapole Kibaha.

Mchezo huo wa hatua ya fainali utachezwa kwenye uwanja wa Mwendapole ambapo mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu ndiyo utaanza kati ya Kiduli na Nyumbu.


No comments:

Post a Comment