Wednesday, September 9, 2026

ULEGA ATAKA MIUNDOMBINU ITOE HUDUMA KIPINDI CHA MVUA ZA ELNINO.

WAZIRI wa Ujenzi Abdala Ulega ametaka hatua za haraka kuchukuliwa ili miundombinu ya barabara iendelea kutoa huduma hata wakati wa mvua kubwa za Elnino zinazotarajiwa kuanza kunyesha hivi karibuni kote nchini.

Ulega ametoa maelekezo hayo akiwa mkoani Pwani katika ziara yake aliyoianza ya ukaguzi wa maandalizi ya kimiundombinu kufuatia maelekezo ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa watendaji wa Serikali kuhakikisha nchi inakingwa na athari za mvua zinazoweza kujitokeza wakati huo.

Amesema kuwa inapaswa kufanyika kwa ukaguzi wa barabara na madaraja kote nchini kama sehemu ya maandalizi dhidi ya mvua kubwa za Elnino zinazotarajiwa kuanza hivi karibuni.

Aidha amesema kuwa ukaguzi huo ndiyo utakuwa msingi wa kufahamu ni wapi na wapi panahitaji kufanyiwa kazi ili mvua hizo zisiathiri mzunguko wa watu na biashara.

"Naagiza Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) kuhakikisha barabara na madaraja yote nchini yanakaguliwa na hatua za haraka kuchukuliwa ili miundombinu hiyo iendelea kutoa huduma hata wakati wa mvua kubwa zinazotarajiwa kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini",amesema Ulega.

Amesisitiza kuwa pamoja na uwepo wa vifaa ³na mitambo utayari wa wataalam na watendaji ndio msingi wa kuhakikisha nchi inapita salama katika kipindi cha mvua hizo.

"Wizara ya Ujenzi kwa kushirikiana na TANROADS kufanya tathmini ya kila wiki katika mikoa yote nchini ili kubaini maeneo yoyote yanayohitaji kuongezewa nguvu kwa wakati ili kuhakikisha huduma za dharura zinafika kila kona ya nchi,"amesema Ulega.

Aliingeza kuwa TANROADS mejipanga katika kanda mbalimbali na Mkoa wa Pwani ndiyo kitovu cha kanda zote kwa ajili maandalizi ya tahadhari ya mvua za Elnino.

Pia alikagua pia vifaa mbalimbali vitakavyotumika kufanya matengenezo ya dharura katika miundombinu ya barabara na madaraja nchini
kote.

Meneja wa TANROADS Mkoa waPwani Mhandisi Joel Mwambungu amesema kuwa wamejipanga kukabiliana na athari za mvua hizo kwa ununuzi na usambazaji wa vifaa vya dharura katika maeneo mbalimbali nchini.

Mwambungu amesema kuwa TANROADS tayari ina kalavati za chuma zenye jumla ya urefu wa mita 5,638 zitakazotumika katika maeneo ambayo barabara au madaraja yanaweza kupata athari kutokana na mvua hizo.

mwisho.

No comments:

Post a Comment