Saturday, September 12, 2026

NYIKA FC YAINGIA FAINALI MICHUANO MEETING POINT SUPER CUP

TIMU ya soka ya Nyika Fc imeifunga Kiduli Fc kwa penati 4-3 kwenye michuano ya Meeting Point Super Cup kwenye uwanja wa Mwendapole Kibaha. 

Timu hizo ziliingia kwenye hatua ya penati baada ya kufungana goli 1-1 hadi dakika 90 zilipotamatika kwenye mchezo huo.

Kutokana na matukio hayo Nyika imeingia hatua ya fainali ikisubiri mchezo kati ya Nyumbu na Baberian mchezo utakaopigwa kwenye uwanja huo huo wa Mwendapole.

No comments:

Post a Comment