Na John Gagarini, Kibaha
WANANCHI wa eneo la Maili Moja wilayani Kibaha
mkoani Pwani wamelia na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) mkoa wa Pwani
kuwa wawafikirie kwa kuwalipa fidia wakati wa zoezi la bomobomoa ambalo
linatarajiwa kufanyika Novemba 23 mwaka huu.
Hataua hiyo imekuja baada ya TANROADS kutoa barua
kwa watu waliojenga kwenye eneo la hifadhi ya barabara inayomilikiwa na wakala
hiyo kwa wale waliojenga umbali wa mita 120 kwa kila upande wa barabara kuu ya
Dar es Salaam Morogoro kuanzia Kiluvya hadi Tamco waanze kubomoa kabla ya zoezi
hilo kwa kuwapa siku 90 kufanya hivyo.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mwenyekiti
wa chama cha ACT-Wazalendo mkoa wa Pwani Mrisho Swagala alisema kuwa mbali ya
kuwtowlaipa fidia pia eneo linalopitiwa na zoezi hilo ni kubwa sana
ikilinganishwa na maeneo mengine.
“Hatukati zoezi hilo kufanyika lakini wangeangalia
namna ya kuwafidia wananchi kwani kuwabomolae bila ya kuwapa fidi itakuwa ni
kitendo cha ukatili na kinakwenda kinyume cha haki za binaadamu kwani bomoa
hiyo itawaacha watu wengi wakiwa hawana mahali pa kuishi na kwa wafanyabiashara
hawatakuwa na sehemu ya kufanyia biashara,” alisema Swagala.
Alisema kuwa alisema kuwa sheria ya barabara
iliyotungwa mwaka 1932 ambapo inadaiwa kuwa watu walilipwa fidia jambo ambalo
kwa kipindi hicho fedha ilikuwa ni ndogo ukilinganisha hali halisi ya sasa
hivyo kuna haja ya kuwafikiria.
Naye Ally Gonzi mwenyekiti wa ushirika wa
wafanyabiashara wa soko la mkoa la Maili Moja alisema kuwa wao kama
wafanyabiashara wansikitishwa na hatua hiyo kwani hadi sasa hawajui watakwenda
kufanyia biashara wapi.
Gonzi alisema kuwa waliahidiwa kuwa watajengewa
soko la kisasa lakini hadi sasa soko halijajengwa ambapo wao wako hapo kwa
zaidi ya miaka 35 na Halmashauri ambao wao wako chini yao.
Kwa upande wake mwenyekiti wa Mtaa wa Maili Moja
Athuma Mkongota alisema kuwa wananchi wengi wamekwenda ofisini kwake kwenda
kulalamika juu ya zoezi hilo ambalo litawakumba watu wengi ambao wako katikati
ya mji huo.
Mkongota alisema kuwa ubomoaji huo umekuja baada ya
kuisha kwa kesi iliyofunguliwa na wananchi kupinga hatua hiyo lakini
walishindwa hata hivyo alisema kuwa hukumu ya kesi hiyo bado hajaipata.
Awali mkaguzi wa barabara wa mamlaka hiyo
Livingston Urio alisema kuwa kwa sasa wanaendelea na zoezi la kutoa barua
ambapo idadi kamili ya nyumba na vibanda vya biashara vitakavyobomolewa
itajulikana.
Urio alisema kuwa ilikuwa ifanyike mwezi Agosti
lakini waliongeza hadi Novemba lakini miaka ya nyuma tayari walishawawekea
alama ya X mwaka 2004 lakini zoezi hilo halikufanyika lakini kwa sasa zoezi
hilo linafanyika.
Alisema kuwa wananchi walipoenda mahakamani
walishinda na kuonekana kuwa eneo hilo ni mali ya mamlaka hiyo na kuwa eneo
hilo magari yanakwenda taratibu hivyo barabara kuharibika na baada ya bomoa
hiyo eneo hilo litawekwa stendi kubwa na patapangwa vizuri ili mji uonekane
vizuri.
“Kulingana na sheria ya barabara ya mwaka 1932 na
kufanyiwa marekebisho 1958 kifunga na 52 na marekebisho ya sheria ya barabara
na 13 ya mwaka 2007 sambamba na taratibu za sheria za usimamizi wa barabara
kifungu na 30 (b) eneo la hifadhi ya barabara sehemu iliyotajwa hapo juu ni
mita 120 sawa na futi 400 kwenda kila upande kutoka katikati ya barabara ni
marufuku kufanya maendelezo yoyote katika eneo hilo,” alisema Urio.
Mwisho.