Tuesday, March 12, 2024

EWURA KUMTUA MWANAMKE KUNI KICHWANI

Na Wellu Mtaki, Dodoma

MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Dkt. James Andilile,amesema mamlaka hiyo ina wajibu kuhakikisha wanamtua mwanamke kuni na mkaa kichwani kwa kuhakikisha wanatoa leseni kwa wakati kwa wawekezaji wanaokuja nchini kuwekeza katika nishati safi ya kupikia.

Dkt. Andilile ameyasema hayo Machi 9,2024 jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari katika banda la Mamlaka hiyo kwenye Kongamano la wanawake la kugawa mitaji na vitendea kazi vya nishati safi ya kupikia.

Amesema taifa bado linatumia nishati isiyosafi kwa kupikia hivyo EWURA itahakikisha ina wajibu wa kuhakikisha inatekeleza mikataba ya kukabiliana na changamoto zinazojitokeza ikiwemo uharibifu wa mazingira na madhara ya afya yanayosababidhwa na moshi wakati wa matumizi ya kuni na mkaa.

“EWURA tutahakikiha tunahamasisha uwekezaji katika nishati safi kwa kutoa leseni kwa wawekezaji kwa wakati ili wawekeze katika eneo hilo, pia tunaangalia upatikanaji wake katika maeneo mengi kwa kuangalia mwenendo wa bei za bidhaa hiyo,” amesema Dkt. Andilile.

Ameongeza kuwa:”Sisi kama EWURA tutahakikisha kama ilivyo dhamira ya Rais kumtua ndoo mama kichwani, tutamtua mwanamke kuni kichwani kwa kuhakikisha anatumia nishati ambayo itamrahisishia kupata maendeleo badala ya kuhangaika na nishati chafu ya kupikia,”.

Monday, March 11, 2024

TISA WAFA AJALINI BAGAMOYO

WATU tisa wamefariki dunia na wengine watatu kujeruhiwa baada ya basi dogo la abiria aina ya Toyota Coaster kugongana uso kwa uso na lori.

Kwa mujibu wa kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani SACP Pius Lutumo amesema kuwa ajali hiyo ilitokea Machi 10 majiira ya saa 11:15 jioni huko Kiromo Wilaya ya Bagamoyo barabaraba kuu ya Bagamoyo Dar es Salaam.

Lutumo amesema kuwa ajali hiyo ilihusisha basi hilo dogo lenye namba za usajiliT676 DSM likiendeshwa na dereva aitwaye Juma Mackey akitokea Dar es Salaam kuelekea Bagamoyo ambapo dereva huyo na yule wa lori ni miongoni mwa waliofariki dunia.

Ametaja gari lingine lililohusika na ajali hiyo kuwa ni lori aina ya Howo mali ya VGK Limited lenye namba za usajili T 503 DRP na tela namba T 733 DUa likierndeshwa na dereva aitwaye Apolo Mgomela (52) mkazi wa Kibaha likitoka Bagamoyo kwenda Dar es Salaam.

Waliokuta ni wanaume saba na wanawake yawawili ambapo majeruhi walipelekwa Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo kwa matibabu na pamoja na marehemu," amesema Lutumo.

Ametaja chanzo cha ajali hiyo kuwa ni uzembe wa dereva wa lori kuyapita magari menginep asipokuchukua tahadhari na kuligonga basi ambalo lilikuwa linakuja mbele yake ambapoa metoa wito kwa wananchi na watumiaji wote wa barabara hasa madereva kufuata sheria zau salama barabarani ili kuepusha ajali zinazogharimu maisha ya watu.

KATA YA MAILI MOJA WAELEZEA MAFANIKIO NA CHANGAMOTO

KATA ya Maili Moja Wilayani Kibaha Mkoani Pwani imeelezea mafanikio na changamoto huku wakiitaka Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) kukarabati miundombinu ya barabara ambayo imeharibika vibaya.

Diwani wa Kata hiyo Ramadhan Lutambi ameelezea baadhi ya mafanikio na changamoto mbele ya Katibu Tawala wa Wilaya ya Kibaha Moses Magogwa ambaye alimwakilisha mkuu wa Wilaya ya Kibaha wakati wa mkutano wa hadhara kwenye mtaa wa Uyaoni.

Lutambi amesema baadhi ya mafanikio ni kwenye sekta ya elimu ambapo kwenye sekondari ya Bundikani kwenye matokeo ya kidato cha nne mwaka jana wamefanikiwa kuondoa daraja sifuri na ujenzi wa madarasa mapya.

Amesema kwa upande wa shule za msingi wamefanikiwa kuanzisha shule mpya ya Muheza, shule za Maendeleo na Maili Moja zimejengewa madarasa mapya, kwa upande wa serikali za mitaa kujenga ofisi zake badala ya kupanga.

"Kuna baadhi ya changamoto lakini kubwa ni miundombinu ya barabara hii ni tatizo kwa mitaa yote suala la urasimishaji, umeme kukatika mara kwa mara, baadhi ya maeneo kukosa maji na umeme na mikopo ya kausha damu,"amesema Lutambi.

Kwa upande wake katibu tawala wa Wilaya ya Kibaha Moses Magogwa amesema kuhusu changamoto ya barabara atawaelekeza Tarura ili wakae na wananchi ili kuangalia vipaumbele vya barabara ili zianze kufanyiwa marekebisho.

Magogwa amesema kuhusu urasimishaji wote waliopewa hiyo kazi wakutane naye ofisini ili kuangalia namna ya kutatua changamoto hiyo ili kuondoa malalamiko ya wananchi.

Amesema kuhusu mikopo ya kausha damu viongozi wa mitaa wakae na wamiliki wa taasisi hizo za mikopo ili kuangalia namna ya kudai marejesho badala ya kuwadhalilisha watu.

Ameongeza kuwa serikali inasikiliza kero za wananchi ili kuzitatua kwani Rais Dk Samia Suluhu Hassan anapambana kuhakikisha wananchi wanaishi kwenye mazingira mazuri.

Saturday, March 9, 2024

BAWACHA YAWATAKA WANAWAKE WANAOLEA WATOTO PEKE YAO KUOMBA MSAADA


Na, Wellu Mtaki, Dodoma 

Mwenyekiti wa Baraza la wanawake wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA (BAWACHA) Sharifa Suleiman amewakumbusha wazazi wanaoleo watoto peke yao kuomba msaada wa malezi  kwani kumekuwa na wimbi kubwa la watoto kukosa malezi ya wazazi wote wawili

Bi. Sharifa ameyasema hayo Jijini Dodoma wakati wa maadhimisho ya  siku ya Wanawake Duniani ambapo kitaifa yamefanyika Jijini Dodoma huku akiongeza kuwa suala la malezi na makuzi linahitajika kwa pande zote mbili kwani wanategemeana kwenye malezi.

Aidha ameongeza kuwa changamoto ya afya ya akili imefanya wazazi wengi kukimbia familia zao jambo linalofanya hali ya familia kwasasa kuwa katika hali mbaya.

Naye Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe amewasisitiza wanawake kuwa na udhubutu wa kugombea nafasi mbalimbali za uongozi serikalini.

Nao baadhi ya wahudhuriaji katika maadhimisho hayo wamezungumzia kuhusiana na kitu kinachosababisha wanaume wengi kukimbia familia zao na kushindwa kutimiza jukumu lao la malezi.

Friday, March 8, 2024

WANAWAKE WATAKIWA KUWA NA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA

 

Na Wellu Mtaki, Dodoma

WANAWAKE nchini wametakiwa kutambua suala la matumizi sahihi ya fedha ili kuweza kujiongezea kipato zaidi na kujikwamua kiuchumi.

Hayo yameelezwa na  Mkurugezi Msaidizi sehemu ya usimamizi Rasilimali watu Wizara ya fedha Bi, Faudhia Nombo wakati akimwakilisha katibu mkuu wizara ya fedha katika  maonesho ya banda la wizara hiyo  leo Machi 7  siku ya ufunguzi  wa maonyesho ya wanawake  kuelekea maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani.

Nombo amesema wizara inaendelea kutoa Elimu kwa wanawake kujiandaa wakati wa kustafu kazi katika kipindi cha uzee pamoja na suala la kutunza fedha 

"Wizara haitokaa kimya ila itahakikisha inaendelea kutoa Elimu kwa wanawake ili pindi wanapostafu kazi wapate fedha za kujikimu kipindi chote cha uzee , wapo wanawake wanatumia fedha katika majukumu ambayo si sahihi na mwisho wa siku fedha hupotea na kuelekea mwisho mbaya uzeeni," amesema Nombo.

Aidha amesema kuwa wanawake wengi wanatamani kuingia katika vikoba ili kuweza kujikimu kiuchumi ila wanashidwa kutambua namna ya utunzaji wa fedha hivyo wizara imeona watoe mafunzo ya namna ya kutunza fedha katika maonesho ya siku ya wanawake Dunia.

Pia ametoa wito kwa wanawake wa Dodoma kutambua fursa zilizopo katika wizara hiyo na kutumia kiusahihi ili kufanikisha shughuli zao za kiuchumi.

KUNDO ATAKA VYOMBO VYA HABARI NCHINI KUANZISHA VIPINDI VYA KUHAMASISHA MILA NA DESTURI ZA WATANZANIA.

NAIBU Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Mathew Kundo amevitaka vyombo vya habari kuanzisha vipindi vinavyohamasisha mila na Destiri ya mtanzania ili kuwaelimisha vijana kuhusu tamaduni zao.

Mhandisi Kundo ametoa kauli hiyo Leo Februari 13,2024 Jijini Dodoma , alipomwakilisha Waziri wa Habari,Mawasiliano na Teknolojia ya habari Mhe. Nape Nnauye, katika ufunguzi wa Mkutano wa Mwaka wa Vyombo vya Utangazaji Nchini ulioenda sambamba na kilele cha maadhimisho ya siku ya Utangazaji Duniani

“Ni muhimu sana kwenu TCRA kuliangalia suala hili kwa umakini mkubwa kwani Mkifanya hivi itawasaidia sana kufanya kazi kwa ufanisi,na Sisi kama Serikali tunawaahidi kuendeleza ushirikiano uliopo ili kuleta maendeleo kwa jamii, "amesema Mhandisi Kundo

Pia Mhandisi Kundo ameiagiza Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA),kuhakikisha inajitathmini Mara kwa Mara ili kujua ni wapi kuna mapungufu na kuweza kuyafanyia kazi mapungufu hayo.

Katika hatua nyingine Mhandisi Kundo amebainisha kuwa katika kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa Vyombo vya Habari vinatakiwa kuwa mstari wa mbele katika kuzingatia Maadili na kanuni za utoaji Habari kwa jamii kwa maslahi ya Taifa.

“Vyombo vya habari vina wajibu mkubwa katika Taifa letu hivyo Ni muhimu kila mmoja kuzingatia taaluma na kutimiza majukumu yake kwa weledi mkubwa,amesisitiza Naibu Waziri

Aidha amewaasa Waandishi wa habari kuhakikisha wanazingatia usawa katika kuripoti matukio ya kampeni za Uchaguzi na matokeo Yake bila upendeleo

Kwa upande Wake Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania( TCRA )Jones Kilimbe amewataka watangazaji na waandishi wa habari kuzingatia Madili na kanuni ya kazi zao.

Amegusia pia uchaguzi  wa Serikali za mitaa kuwa,vyombo vya habari vina jukumu la kutoa elimu kwa wapiga kura ikiwa ni pamoja na kuhabarisha umma kuhusu mwenendo mzima wa kampeni bila upendeleo na kutoa ripoti sahihi za siku ya kupiga kura.

Amesema TCRA kama wadau wa Utangazaji watahakikisha wanakuwa bega kwa bega na vyombo vya Utangazaji kwa kuhakikisha wanatoa mwelekeo wa maudhui yenye ubora bila upotoshaji.

Thursday, February 29, 2024

BMH YAENDELEA KUPANDIKIZA BETRI KWENYE MOYO



Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) ya jijini Dodoma imefanya upandikiza betri kwenye moyo kwa watu watatu.

Upandikizaji wa betri kwenye moyo ambao kitaalamu unaitwa _pacemakers_  _implantation_ unafanyika kwa watu wenye matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo na kusababisha mapigo ya moyo kuwa chini ya kiwango kinachotakiwa kwa mtu wa kawaida ambayo ni 60-100 kwa dakika.Wengi wao huwa ni chini ya 40.

Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Moyo wa BMH, Daktari Bingwa wa Moyo, Happiness Kusima, amesema leo kuwa BMH imefikisha upandikizaji kwa watu 18 toka huduma ianzishwe mwaka 2021.

"Jana tumepandikiza watu watatu (3), leo tumepandikiza watu wawili," amesema Daktari huyo Bingwa wa Moyo.

Dkt Happiness amesema upandikizaji huu umefanyika kwenye kambi ya Madaktari Bingwa wa Moyo wa BMH kwa kujengewa uwezo na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) ya jijini Dar es Salaam.