Tuesday, December 9, 2025

TANZANIA AND U.S. MOVE TO FINALISE MAJOR INVESTMENT AGREEMENTS

Her Excellency Dr. Samia Suluhu Hassan, President of the United Republic of Tanzania, today held talks with the Acting United States Ambassador to Tanzania, Andrew Lentz, at Chamwino State House to advance key areas of bilateral cooperation and reaffirm the shared commitment to a modern, mutually beneficial partnership.

Ambassador Lentz—accompanied by the Counselor for Political and Economic Affairs—underscored Washington’s determination to reset the relationship and deepen economic, political, and security collaboration with Tanzania.

“The United States is committed to a partnership based not on aid dependency but on shared prosperity,” Ambassador Lentz said.

The discussions centred on ongoing negotiations involving major U.S.-linked strategic investments. Both sides acknowledged that talks on two flagship projects—the LNG Project and Tembo Nickel Project—are now in their final stages, pending formal signing. A third investment, the Mahenge Graphite Project, remains under active technical review.

President Samia welcomed Washington’s renewed commitment and assured the delegation that Tanzania remains focused on completing the remaining procedural steps.

“As a non-aligned nation, Tanzania is open, ready, and committed to working with all partners who respect our sovereignty and share our vision for prosperity,” the President said.

“These strategic projects are of national importance, and we are determined to finalise them so they can unlock jobs, investment, and sustainable prosperity for our people.”

The President highlighted that more than 400 American companies currently operate in Tanzania—reflecting the country’s stability, openness to investment, and strong historical ties with the United States.

Beyond investments, the meeting touched on broader areas of cooperation, including political stability, regional security, economic reforms, private-sector growth, health-sector partnerships, and people-to-people exchanges.

Ambassador Lentz congratulated President Samia for her vision and long-term national planning through Vision 2050, noting the U.S. Government’s readiness to support its implementation and reinforce the President’s 4R philosophy of reconciliation, resilience, reforms, and rebuilding trust.

Both sides agreed that strengthened communication, consistent engagement, and timely action on pending agreements are key to unlocking the full potential of U.S.–Tanzania relations.

This meeting marks a pivotal moment in redefining and revitalising the U.S.–Tanzania relationship. The reaffirmed commitment from both governments signals the emergence of a modern, transparent, private-sector-driven partnership rooted in shared prosperity, mutual respect, and long-term strategic cooperation.

Flagship Projects

1. LNG Project — Estimated Value: USD 42 Billion

A transformative natural gas development involving leading international energy companies. The project aims to unlock Tanzania’s vast offshore gas reserves, boost national revenue, create thousands of jobs, and position the country as a major global LNG supplier.

2. Tembo Nickel Project — Value: USD 942 Million

A major critical-minerals investment in Ngara focused on nickel—an essential component in electric-vehicle batteries. The project will support global clean-energy supply chains, stimulate industrialisation, and expand Tanzania’s export base.

3. Mahenge Graphite Project — Value: USD 300 Million

One of the world’s largest high-grade graphite deposits, positioned to serve the fast-growing battery and renewable-energy sectors. The project will reinforce Tanzania’s role as a leading supplier of battery-grade minerals.



Sunday, October 5, 2025

BILIONI 44 ZATOLEWA KWA TASAF PWANI 2020/2025.

SERIKALI imetoa zaidi ya shilingi bilioni 44 kuwezesha Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Mkoa wa Pwani ili kutekeleza miradi ya kunusuru kaya maskini katika kipindi cha miaka mitano 2020/2025.

Aidha jumla ya vikundi 1,601 vyenye wanachama 16,495 kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) vikiwa na mtaji wa kiasi cha shilingi milioni 330.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Mratibu wa Tasaf Mkoa wa Pwani Roseline Kimaro wakati wa kikao kazi cha mwaka cha Utekelezaji wa (TASAF III – Awamu ya Pili).

Kimaro alisema kuwa fedha hizo ni za ruzuku kwa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kupitia miradi ya Afya na Elimu, miradi hii ni miradi ya ajira za muda, mitaji kwa ajili ya biashara ndogo ndogo.

Alisema kuwa vikundi hivyo vina jumla ya wanawake 14,568 ambapo idadi hiyo ni hadi kufikia Juni 2025 ambapo vimeanzisha miradi mbalimbali ya kiuchumi.

"Vikundi hivyo kupitia wanachama wake vinafanya miradi ikiwemo ile ya kilimo, ufugaji, biashara ndogondogo, ushonaji, usindikaji wa bidhaa na ufumaji,"alisema Kimaro.

Alisema kuwa Mkoa ulitekeleza miradi ya maendeleo katika sekta za afya na elimu katika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na ujenzi wa zahanati, wodi, mabweni na nyumba za watumishi.


"Haya ni mafanikio yaliyopatikana nani ni matokeo ya ushirikiano wa karibu kati ya Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, viongozi wa jamii na wanufaika wenyewe,"alisema Kimaro.


Aliongeza kuwa mpango huo unatarajiwa kuendelea kuleta mabadiliko chanya na kuchochea maendeleo endelevu ya Mkoa wa Pwani kwa kuboresha maisha ya wananchi.

Wednesday, October 1, 2025

WAWEKEZAJI WAITWA WAZAWA WAPEWA KIPAUMBELE HEKARI 100 ZATENGWA KONGANI YA KWALA.

WATANZANIA wametakiwa kwenda kuwekeza kwenye eneo la Kwala Wilayani Kibaha ambapo zimetengwa hekari 100 wawekezaji wanapewa hekari moja bure na sharti ni mtaji pekee.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye kituo cha Kwala Industry Park (KIP) Kaimu Meneja wa Mawasiliano kwa Umma na Habari Adelina Rushekya kutoka Mamlaka ya Uwekezaji na Kanda Maalum za Kiuchumi Tanzania (TISEZA) amesema kuwa wanawahamasisha Watanzania kuchangamkia fursa hiyo ya uwekezaji.

Rushekya amesema kuwa wameanzisha kampeni ya kuwataka Watanzania kuwekeza kwenye maeneo ambayo yametengwa kwa ajili ya uwekezaji ikiwemo Kongani ya Viwanda Kwala badala ya kuwaachia wageni kufanya uwekezaji.

"Hadi sasa kuna wawekezaji 10 wameonyesha nia ya kuwekeza wengi wakiwa ni wazawa pamoja na wageni ambapo wawekezaji hao wameonyesha nia kuwekeza kwenye sekta za kilimo, umeme jua na vifaa vya majumbani,"amesema Rushekya.

Naye msimamizi wa kiwanda cha kuunganisha majokofucha Snowsea Tanzania Co Ltd kilichopo kwenye eneo la kituo hicho cha Uwekezaji cha Kwala Gerald Tilia amesema kuwa wana uwezo wa kuunganisha majokofu 10 hadi 15 kwa siku.

Tilia amesema kuwa wafanyakazi wanaofanya kazi hiyo ya kuunganisha majokofu ni wazawa baada ya kupatiwa mafunzo kutoka kwa Wachina na hadi sasa kuna wafanyakazi 30.


Wednesday, August 27, 2025

GRACE JUNGULU ARUDISHA FOMU UDIWANI KATA YA PICHA YA NDEGE

DIWANI Mteule kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Picha ya Ndege Grace Jungulu amerudisha fomu ya udiwani na kuwataka wana CCM kujitokeza kwa wingi kupiga kura Oktoba mwaka huu.

Jungulu amerudisha fomu kwenye ofisi ya Kata ya Picha ya Ndege Manispaa ya Kibaha huku akisindikizwa na wanachama na wananchi wa Kata hiyo.

Amewataka wanaccm na wananchi kwa ujumla kuhakikisha Oktoba wabakipigia kura za kishindo chama ili kiendelee kuongoza serikali.


KOKA ACHUKUA FOMU UBUNGE KIBAHA MJINI

MBUNGE Mteule wa Jimbo la Kibaha Mjinj kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Silvestry Koka amewataka wale waliowania nafasi hiyo na kura hazikutosha washirikiane ili chama kipate ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi Mkuu Oktoba mwaka huu.

Koka aliyasema hayo mjini Kibaha wakati akichukua fomu kuwania nafasi hiyo kupitia CCM na kuwa ni wakati wa kuungana ili kuleta ushindi wa chama.

Alisema kuwa kama kulitokea kutofautiana kwa namna moja au nyingine ni kusameheana na kuungana wakati wa kutafuta kura za chama.

"Huu ni wakati wa kuungana na kuondoa tofauti ambazo zilijitokeza wakati wa ndani ya chama ambapo kila mmoja alikuwa akitafuta namna ya kushinda,"alisema Koka.

Alisema kuwa kilichoshinda ni hivyo kusiwe na kuona kuwa fulani kashinda wote ni wana ccm hawapaswi kutofautiana wote wanakipambania chama.

"Tuungane ili kuhakikisha tunakipatia ushindi chama kuanzia Urais, Ubunge na Udiwani tunataka ushindi uwe mkubwa na wakishindo na kuweka historia,"alisema Koka.

Aidha alisema kuwa wanaccm wahakikishe ushindi wa asilimia 100 kama ilivyokuwa kuwa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na kwenye kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura.

Kwa upande wake Alhaji Mussa Mansour ambaye alikuwa moja ya wagombea wa nafasi hiyo alisema kuwa uchaguzi ndani ya chama umekwisha kinachofuata ni kuzitafuta kura za CCM.

Naye mgombea wa nafasi hiyo Abubakar Allawi alisema kuwa baada ya uchaguzi ndani ya chama kwisha watashirikiana na mgombea huyo kuhakikisha anashinda na nafasi nyingine za Urais na Udiwani ili chama kiendelee  kushika dola.

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani Hawa Mchafu alisema kuwa anawapongeza wawania nafasi ya ubunge hao kwa kuonyesha ushirikiano na kukipa urahisi chama kupata ushindi itakapofika Oktoba.

mwisho.

Thursday, June 26, 2025

DMI MISSION TANZANIA KUKABILI MIMBA NDOA ZA UTOTONI









SERIKALI imesema kuwa elimu ni nguzo ya kuwalinda watoto na ukatili ndoa na mimba za utotoni na kuwataka wazazi na walezi kuhakikisha wanatimiza haki ya msingi ya mtoto kupata elimu.

Hayo yamesemwa na Madina Mussa ambaye alimwakilisha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha wakati wa kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika iliyoandaliwa na DMI Mission Tanzania.

Mussa amesema kuwa ili kutekeleza mazingira rafiki kwa watoto waweze kupata haki hiyo ya msingi imejenga miundombinu mizuri ya watoto kujisomea.

"Katika kukabiliana na ukatili na ndoa za utotoni wazazi na walezi lazima washirikiane na serikali kuhakikisha haki za msingi za mtoto zinalindwa ikiwa ni pamoja na elimu, kumlinda na ukatili na kuishi katika mazingira mazuri kwani haki za mtoto zinaanzia nyumbani,"amesema Madina.

Awali Mkurugenzi wa DMI Mission Tanzania Sister Fathima Jacintha Ran amesema kuwa dhima ya siku hiyo ni Kupanga bajeti na kuweka bajeti kwa haki za watoto.

Ran amesema kuwa lengo ni kuhakikisha ustawi, elimu, na hatma njema za watoto ikiwa ni kukumbusha wajibu wa pamoja kuhakikisha watoto wa Afrika wanapata haki za msingi za elimu bora, huduma za afya, ulinzi na fursa ya kukua.

Naye Ofisa Maendeleo ya Jamii kitengo cha watoto Halmashauri ya Mji Kibaha Hanifa Mruma amesema kuwa mradi ulioanzishwa na shirika hilo wa kupambana na mimba za utotoni ni mzuri na utasaidia kukabiliana na changamoto hiyo.

Kwa upande wake moja ya wanufaika kwenye mradi huo wa Klabu za Wanawake Vijana Chiku Hamis amesema kuwa wanalishukuru shirika hilo kwa kuwapatia vifaa kwa ajili ya kutengeneza batiki na sabuni kwa ajili ya mafunzo ya utengenezaji vitu hivyo. 

Mradi huo wa kupunguza mimba za utotoni unatekelezwa kwenye Kata tatu za Pangani, Tumbi na Kongowe.

Wednesday, June 25, 2025

MATUMLA PROMOTION KUINUA VIPAJI VYA NGUMI KIBAHA

MATUMLA Promotion ya Kibaha imeandaa pambano la ngumi kati ya Abdully Said au Dully Bwengo na Rashid Hassan au Makali litakalopigwa kwenye baa ya UEFA Kongowe Kibaha Juni 28 mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na pambano hilo ambalo litasindikizwa na mapambano mengine matano Mkurugenzi wa Matumla Promotion Abuu Matumla amesema kuwa maandalizi ya awali yamekamilika.

Matumla amesema kuwa maandalizi yakiwemo ya kuwalipa fedha za awali yameshafanyika na mabondia hao watakamilishiwa fedha zao baada ya pambano hilo kukamilika.

"Taratibu za awali zimekamilika ikiwa ni pamoja na malipo ya awali kwa mabondia, vibali na ulinzi vyote viko tayari kinachosubiriwa ni siku ya pambano hilo,"amesema Matumla.

Alisema kuwa malengo ya kuandaa mapambano hayo ni kuhamasisha mchezo huo kwa vijana wa Kibaha kwani mchezo huo ni ajira na kujenga afya bora na kuwaondoa vijana kwenye vitendo hatarishi.

"Tunataka tuinue mchezo wa ngumi Kibaha ambapo pia kutakuwa na pambano la wanawake ikiwa ni sehemu ya kuwahamasisha wanawake nao washiriki mchezo huo kwani hata wao wanauwezo wa kushiriki mchezo huo,"amesema Matumla.

Aidha alisema kuwa mbali ya mapambano hayo pia kutakuwa na burudani za muziki zikiongozwa na mkali wa Singeli Yuda Msaliti na waimbaji wengine wakali wa miondoko hiyo ya singeli.

"Nawaomba wapenzi wa mchezo wa ngumi kujitokeza kwa wingi kushuhudia vipaji vya vijana wao ili kuwapa hamasa wapende mchezo huo ambao umekuwa ukipendwa na wengi,"amesema Matumla.