Sunday, August 6, 2023
UMWELANI WATWAA KOMBE MICHO CUP
Saturday, August 5, 2023
WAKULIMA WATAKIWA KULIMA KILIMO CHA KIBIASHARA NA SIYO CHA KUJIKIMU
SEARIKALI imepanga kubadilisha kilimo kutoka kuwa cha kujikimu na kuwa kilimo cha biashara ambapo mabadiliko hayo yanafanyika kwa kuzingatia malengo ya kitaifa kama yalivyoainishwa kwenye dira ya taifa ya maendeleo 2025 na kuhakikisha kilimo ichangie ipasavyo Katika vita dhidi ya umasikini na kulenga kukuza sekta hiyo kufikia asilimia 10 ifikapo Mwaka 2030.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Pindi Chana katika ufunguzi wa kongamano la zao la Mtama Jijini Dodoma kwenye maonesho ya nanenane.
Chana amesema kuwa mipango hiyo yote ya kitaifa imeweka mkazo kwenye mapinduzi ya viwanda na kubainisha sekta ya Kilimo kama mhimili imara utakaowezesha upatikanaji wa maligrafi za viwanda.
Amesema kuwa Mikoa ya kanda ya kati kama iliyo kwa Nchi na Dunia nzima inakabiliwa na mabadiliko ya tabia Nchi ambapo Mkoa wa Dodoma na Singida imeamua kwa dhati kuendeleza zao la Mtama ambalo limekuwa likistawi vizuri kwa hali ya hewa ya Mikoa hiyo.
Kanda ya kati imeamua kufanya uhamasishaji kupitia kongamano Hilo kuhusu matumizi ya teknolojia Bora Katika uzalishaji wa Zao la Mtama lengo likiwa ni kuunga mkono na kutekeleza kwa vitendo jitihada za Dkt. Mhe. Samia Suluhu Hassan Katika kuongeza Kasi ya ukuaji wa sekta ya Kilimo kutokana na kuhakikisha usalama wa chakula na kipato kwa wananchi.
Thursday, August 3, 2023
WANNE WAFA AJALINI PWANI
MKURUGENZI wa benki ya APSA Nechi Msuya (45- 50) mkazi wa Dar es Salaam na watu wengine watatu wamefariki dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuligonga gari lingine uso kwa uso.
Monday, July 31, 2023
MAKONGAMANO YA NANE NANE KUWA NA TIJA
Na Manase Madelemu, Dodoma
MKUU wa mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamle amesema kuwa tofauti na maonesha ya miaka iliyopita ya nane nane mwaka huu 2023 yatahusisha matukio muhimu na makongamano yanayoongeza wigo wa uzalishaji bora.
Senyamule amesema hayo leo julai 31,2023 jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea Maadhimisho ya nane nane mwaka kikanda.
Amesema kutakuwa na makongamano ya tasnia ya alizeti,kongamano la zao la mtama ambapo mikoa ya Dodoma na singida ilikabidhiwa jukumu la kuzalisha alizeti Kwa wingi ili kupunguza nakisi ya mafuta ya kula nchini na hivyo kuokoa fedha za kigeni.
Aidha ameongeza kuwa kutakuwepo na siku maalumu ya uhamasishaji uzalishaji kuku wa kienyeji hasa katika mkoa wa Singida unafahamika katika mikoa mbalimbali hapa nchini hadi kufikia watu kuwaita kuku wa Singida
Pia Senyamule amesema kuwa Katika maonesho ya mwaka huu kutakuwa na huduma za Afya na matibabu ya kibingwa zitakazotolewa na madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa na huduma hizi zitatolewa bure.
Kauli mbiu ya maonesha na sherehe za nane nane kitaifa Kwa mwaka 2023 ni Vijana na wanawake ni Msingi Imara wa Mifumo Endelevu ya Chakula"na kauli mbiu kikanda Kilimo ni Biashara, Biashara ni Uwekezaji.
Saturday, July 29, 2023
PINDA KUZINDUA MAONYESHO NANE NANE KANDA YA MASHARIKI
WAZIRI Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye maonyesho ya wakulima nane nane Kanda ya Mashariki Mkoani Morogoro Agosti Mosi mwaka huu.
Friday, July 28, 2023
WAZIRI MKUU MSTAAFU PINDA MGENI RASMI NANE NANE KANDA YA MASHARIKI
TASAC KUNUNUA BOTI ZA UOKOZI ZIWA VICTORIA
SHIRIKA la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limesema limejipanga kununua boti tatu za uokozi katika Ziwa Victoria ambazo zitakwenda kusaidia kutatua changamoto ambazo zimekuwa zikijitokeza pindi ajali zinapotokea
Hayo yamesemwa jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Bw.Kaimu Abdi Mkenyenge wakati akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa majukumu ya mamlaka hiyo na mwelekeo wa utekelezaji wa mwaka wa fedha 2023/2024 .
Amesema katika boti hizo tatu zitakazonunuliwa mbili zitakuwa ni za mwendonkasi kwaajili ya ukokozi na Moja itakuwa kwaajili ya kubebea majeruhi na wagonjwa (Ambulance) .
“Boti hizi tatu zitatumika kufanya uokozi katika ajali ambazo zimekuwa zikitokea katika Ziwa Victoria ambapo mbili zitakuwa ni za meendo kasi na Moja itatumika kama ambulance kwa ajili ya majeruhi”amesema
Aidha amesema TASAC imeendelea kuimarisha udhibiti huduma za usafiri majini, na kuhakikisha kuna ushindani sawia miongoni mwa watoa huduma.
Amesema kuwa linafanya ufuatiliaji, tathmini na kutoa maelekezo kuhusu utekelezaji wa vigezo na viwango vya ubora wa huduma (performance standards and Benchmarks) kwa watoa huduma za bandari na usafiri majini.
“Tunaendelea kuratibu maombi ya tozo za usafiri wa meli katika Maziwa (Victoria na Nyasa) na kuhakikisha viwango vya tozo vinavyotumika haviathiri ushindani wa kibiashara;
“Lakini pia zoezi la urasimishaji wa bandari bubu Tanzania bara ambapo bandari bubu kumi na tatu (13) zilizowasilishwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) kwa ajili ya urasimishaji zilikaguliwa na kufanyiwa tathmini ya kina kwa kushirikiana na TPA, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Baraza la Usimamizi wa Mazingira (NEMC)”amesema Mkeyenge
Kadhalika amesema bandari bubu kumi zilionekana kukidhi vigezo hivyo na kupendekezwa kwa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Uchukuzi) (WUU-U) kwa ajili ya kurasimishwa kwa mujibu wa sheria
“waendeshaji wa zilizokuwa bandari bubu binafsi tano (05) za Mwanza ambazo ni miongoni mwa zilizokuwa bandari bubu ishirini (20) zilizorasimishwa kupitia Tangazo la Serikali (GN) namba 293/2022 wamepewa leseni za uendeshaji huku TPA wakielekezwa kusimamia kwa karibu bandari kumi na tano (15) zilizobakia.
Akizungumzia kuhusu Kuboresha usalama, ulinzi kwa usafiri majini na kudhibiti uchafuzi wa mazingira baharini utokanao na meli amesema Shirika limetimiza lengo hilo la kimkakati kwa kuendelea kusimamia usalama wa vyombo vya usafiri majini kwa kufanya ukaguzi wa meli kubwa na vyombo vidogo vya majini.
“Shirika lilifanya kaguzi za usalama kwa meli kubwa zibebazo tani 50 au zaidi ili kuhakikisha kuwa ni salama na zinaendeshwa na mabaharia wenye sifa katika mikoa ya Dar es Salaam, Mtwara, Tanga, Mwanza, Kagera, Kigoma na Mbeya ambapo katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Juni, 2023, Shirika lilifanya jumla ya kaguzi za meli kubwa 288 ambapo kaguzi 165 zilikuwa za meli za kigeni na kaguzi 123 zilikuwa meli za ndani.”amesema
Kuhusu uratibu Shughuli za Utafutaji na Uokoaji Majini amesema Kituo cha Utafutaji na Uokoaji Majini kilichopo Dar es Salaam kinachoratibiwa na TASAC kiliendelea kufanya shughuli zake katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Juni, 2023 ambapo kituo kilipokea taarifa 4 za ajali zilizohusisha vyombo vya majini ambazo zilitokea katika eneo la maji ya Tanzania.
Katika ajali hizo jumla ya watu 61 walihusika ambapo watu 58 sawa na 95% waliokolewa na watu 3 sawa na 5% walipoteza maisha.
Naye Mkurugenzi wa Idara ya Habari -Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa amesema Serikali inataka kushirikiana na sekta binafsi kuendesha Bandari, mikataba nwatakaoendesha bado haijasainiwa.
“Sasa hivi ndio wataalamu wako mezani kuzungumza kuhusu mikataba, muda na gharama lakini hakuna bandari iliyouzwa, wataalamu watakapokamilisha majadiliano tutaangalia maslahi yetu yako wapi na maoni yanayotolewa na Watanzania yatazingatia Serikali iko macho wakati wote kuhakikisha maslahi ya Watanzania yanalindwa”amesema Msigwa.






