Thursday, July 27, 2023

MRADI MKUBWA WA KILIMO CHA VANNILA WAZINDULIWA DODOMA UNAKWENDA KUGHARIMU ZAIDI YA BIL 30 ZA KITANZANIA.

 


KAMPUNI ya Vanilla international Limited imezindua Mradi wa kilimo cha Vanilla Mkoani Dodoma Vanilla village Dodoma katika Kitongoji cha Zamahero Kata ya Mayamaya Wilaya ya Bahi.

Uzinduzi huo umeambatana na utoaji Elimu kwa wananchi wa eneo hilo kuhusu kilimo cha Vanilla ambao umefanyika Julai 22 2023 katika shamba la kitalu (green House)kubwa ya kilimo hicho inayotumia njia za kisasa.

Mkurugenzi Mtendaji na muasisi wa makampuni ya Vanilla international Limited ,Simon Mkondya amesema shamba kitalu lipo kilomita 40 kutoka katikati  ya JIJI la Dodoma barabara kuu ya kwenda Arusha lenye ukubwa wa hekta 125.

Mkondya amesema uwekezaji huo unakuja baada ya mafanikio makubwa yaliyopatikana kupitia kilimo hicho katika kisiwa cha Zanzibar.

JWT YAVUTIWA UTALII UWEKEZAJI YAWATAKA WAFANYABIASHARA WAKAWEKEZE

 

KATIKA kuunga mkono jitihihada za Rais Dk Samia Suluhu Hassan kutangaza utalii Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) Mkoa wa Pwani imetembelea vivutio vya utalii na kutambua fursa za uwekezaji zilizopo Wilayani Bagamoyo.

Akizungumza mara baada ya kutembelea vivutio vya utalii na fursa za uwekezaji mwenyekiti wa Jwt Abdala Ndauka alisema kuwa baada ya ziara hiyo wameweza kutambua fursa mbalimbali kupitia utalii.

Ndauka alisema kuwa fursa kwa wafanyabiashara ni nyingi sana kwenye utalii pamoja na fursa nyingine kwenye sekta mbalimbali zikiwemo za utoaji huduma.

Kwa upande wake kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Majid Mhina alisema kuwa changamoto kubwa waliyonayo ni maeneo mengi yanamilikiwa na watu binafsi.

Naye ofisa biashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Magdalena Kitilla alisema kuwa kuhusu uwekezaji wametenga eneo lenye ukubwa wa hekta 9,800 ambalo linahitaji wawekezaji.

Kitilla alisema kuwa sekta ya utalii ina fursa nyingi ambapo kwenye sekta ya uvuvi kupitia uchumi wa buluu bado haujatumika ipasavyo ambapo kuna ufugaji wa vizimba baharini kunakofanyika ufugaji wa majongoo bahari ambapo ni mwekezaji ni mmoja tu.

Moja ya wafanyabiashara Fihiri Msangi alisema kuwa ziara hiyo wamejifunza mambo mengi ambayo watayafanyia kazi ili waangalie namna ya kuweza kuwekeza.

Msangi alisema kuwa fursa hizo watazitumia vizuri ili kuinua uchumi wa Mkoa huo ambao unategemea uwekezaji kwenye maeneo mbalimbali na pia unauwekezaji mkubwa wa viwanda.

JWT WAVUTIWA NA VIVUTIO VYA UTALII NA UWEKEZAJI BAGAMOYO

KATIKA kuunga mkono jitihihada za Rais Dk Samia Suluhu Hassan kutangaza utalii Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) Mkoa wa Pwani imetembelea vivutio vya utalii na kutambua fursa za uwekezaji zilizopo Wilayani Bagamoyo.

Akizungumza mara baada ya kutembelea vivutio vya utalii na fursa za uwekezaji mwenyekiti wa Jwt Abdala Ndauka alisema kuwa baada ya ziara hiyo wameweza kutambua fursa mbalimbali kupitia utalii.

Ndauka alisema kuwa fursa kwa wafanyabiashara ni nyingi sana kwenye utalii pamoja na fursa nyingine kwenye sekta mbalimbali zikiwemo za utoaji huduma.

Kwa upande wake kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Majid Mhina alisema kuwa changamoto kubwa waliyonayo ni maeneo mengi yanamilikiwa na watu binafsi.

Naye ofisa biashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Magdalena Kitilla alisema kuwa kuhusu uwekezaji wametenga eneo lenye ukubwa wa hekta 9,800 ambalo linahitaji wawekezaji.

Kitilla alisema kuwa sekta ya utalii ina fursa nyingi ambapo kwenye sekta ya uvuvi kupitia uchumi wa buluu bado haujatumika ipasavyo ambapo kuna ufugaji wa vizimba baharini kunakofanyika ufugaji wa majongoo bahari ambapo ni mwekezaji ni mmoja tu.

Moja ya wafanyabiashara Fihiri Msangi alisema kuwa ziara hiyo wamejifunza mambo mengi ambayo watayafanyia kazi ili waangalie namna ya kuweza kuwekeza.

Msangi alisema kuwa fursa hizo watazitumia vizuri ili kuinua uchumi wa Mkoa huo ambao unategemea uwekezaji kwenye maeneo mbalimbali na pia unauwekezaji mkubwa wa viwanda.

Wednesday, July 26, 2023


KATIKA kuhakikisha wafanyabiashara wanaondokana na changamoto mbalimbali Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) imejipanga kuhakikisha inakabili kero na kuzifikisha sehemu husika.

Hayo yamesemwa na  Mwenyekiti wa Jumuiya ya  Wafanyabiashara Tanzania Hamis Livembe wakati wa mkutano wa wafanyabiashara mkoani Tanga.

Amewataka wafanyabiashara hao kuungana na kuwa na sauti ya pamoja katika kuhakikisha wanajenga jumuiya yao kwa kutetea masilahi ya biashara zao.

Livembe amesema kuwa umoja wa wafanyabiashara unasaidia katika kutatua kero na kuisaidia serikali katika kutatua changamoto za wafanyabiashara pamoja na kuundwa kwa sera bora ya biashara.

"Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ipo katika kusaidia na kutatua kero za wafanyabiashara kwa makundi siyo kwa mtu mmoja mmoja ndiyo maana waliunda kamati maalum ambayo lengo lake lilikuwa ni kukusanya na kuchakata na kuwasilisha kwa serikali," amesema Livembe.

Awali katibu wa JWT Mkoa wa Tanga Ismail Masod amesema kuwa hadi sasa bei ya vitenge imeshuka ambapo awali ilikuwa kati ya shilling milioni 200 na milioni 300 lakini kwa sasa ni shilingi milioni 60 kwa kontena ambayo hiyo ni kazi ya kamati iliyoundwa.

Masod amewataka wafanyabiashara wa Tanga watumie fursa ambazo serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imeziweka kwa kuagiza mizigo China kutokana na mfumo mzuri ambao serikali wameutengeneza.

Naye Mwenyekiti wa Kariakoo Martin Mbwana amesema kuwa serikali ipo pamoja na Jumuiya hiyo hivyo ametoa wito kwa wafanyabiashara watambue fursa na thamani ambayo Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan ambayo ameitoa kwa wafanyabiashara hao.

WATAKIWA KUINGIA MIKATABA NA WAWEKEZAJI KWENYE ARDHI BADALA YA KUIUZA

NAIBU Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Omar Kipanga amewataka wananchi wa Mafia wanaomiliki mashamba na viwanja vilivyopo karibu na ufukwe wa bahari kutokuyauza maeneo yao badala yake waingie ubia.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopo kwenye Kata ya kirongwe Vijiji vya Banja na Jojo.

Kipanga alisema kuwa baadhi ya wananchi wa Mafia wamekuwa wakiuza maeneo yao kwa wanaowaita  wawekezaji ambao wanavutiwa na maeneo hayo.

"Wananchi wanapaswa kuyakodisha maeneo hayo au wangie mikataba kwa kugawana asilimia angalau nusu kwa nusu ili kupata faida zaidi kuliko kuyauza,"alisema Kipanga.

Alisema kuwa mashamba/viwanja ni vyao lakini kwa Sasa utaratibu mzuri wa kupata maendeleo ya ardhi yako sio kuuza bali ni kuingia ubia na wawekezaji.

"Acheni kabisa tabia hii siyo nzuri itafika hatua ardhi yote ya maeneo ya Pwani ya Mafia itakuwa inamilikiwa na wageni na wenyeji watakua hawana ardhi wakati ni sasa kila mmoja apate faida ya ardhi katika uwekezaji,"alisema Kipanga.

Aidha alisema kuwa Serikali ya Rais Samia na Chama Cha Mapinduzi (CCM) inaboresha barabara za Mafia ni wazi maeneo hayo yanaenda kupanda thamani hivyo ni muhimu kuwawekea na kizazi cha baadae kupitia makubaliano kwenye ardhi.

JUMUIYA YA WAFANYABIASHARA TANZANIA (JWT) KUPAZA SAUTI

 

JUMUIYA ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) imejipanga kuhakikisha inakabili kero za wafanyabiashara na kupokea maoni na mapendekezo ya wafanyabiashara wote nchini na kuzifikisha sehemu husika.

Hayo yameyasema na Mwenyekiti wa wafanyabiashara Tanzania Hamis Livembe wakati wa mkutano wa wafanyabiashara mkoani Tanga.

Amewataka wafanyabiashara hao kuungana na kuwa na sauti ya pamoja katika kuhakikisha wanajenga jumuiya yao kwa kutetea masilahi ya biashara zao.

Livembe amesema kuwa umoja wa wafanyabiashara unasaidia katika kutatua kero na kuisaidia serikali katika kutatua changamoto za wafanyabiashara pamoja na kuundwa kwa sera bora ya biashara.

"Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ipo katika kusaidia na kutatua kero za wafanyabiashara kwa makundi siyo kwa mtu mmoja mmoja ndiyo maana waliunda kamati maalum ambayo lengo lake lilikuwa ni kukusanya na kuchakata na kuwasilisha kwa serikali," amesema Livembe.

Awali katibu wa JWT Mkoa wa Tanga Ismail Masod amesema kuwa hadi sasa bei ya vitenge imeshuka ambapo awali ilikuwa kati ya shilling milioni 200 na milioni 300 lakini kwa sasa ni shilingi milioni 60 kwa kontena ambayo hiyo ni kazi ya kamati iliyoundwa.

Masod amewataka wafanyabiashara wa Tanga watumie fursa ambazo serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imeziweka kwa kuagiza mizigo China kutokana na mfumo mzuri ambao serikali wameutengeneza.

Naye Mwenyekiti wa Kariakoo Martin Mbwana amesema kuwa serikali ipo pamoja na Jumuiya hiyo hivyo ametoa wito kwa wafanyabiashara watambue fursa na thamani ambayo Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan ambayo ameitoa kwa wafanyabiashara hao.

Monday, July 24, 2023

URAIA WETU YAZINDULIWA

SHIRIKA la Maendeleo ya Vijana (YPC) la Kibaha Mkoani Pwani limeingia mkataba wa miaka mitatu na Shirika la The Civil Society (FCS) chini ya udhamini wa Jumuiya ya Ulaya (EU) wa kutoa elimu Utawala wa Kidemokrasia kupitia mradi wa Uraia Wetu.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha Mkurugenzi wa YPC Israel Ilunde amesema kuwa mradi huo utatekelezwa kwenye mikoa minne ya Kanda ya Mashariki.

Ilunde amesema kuwa mradi huo una lengo la kuendeleza mazingira wezeshi kwa ajili ya utawala wa kidemokrasia nchini ambapo kwa kanda ya mashariki ni mikoa ya Pwani, Dar es Salaam, Lindi na Morogoro.

Amesema kuwa mradi utawezesha majadiliano kati ya serikali na azaki kwa ajili ya uchechemuzi (ushawishi na utetezi) wa masuala wa kidemokrasia, maendeleo na kuboresha mahusiano na ushirikiano wa kikazi.

Aidha amesema kuwa mradi utatoa fursa wa azaki kujengewa uwezo kujiendesha kupitia shughuli zao ili kuwanufaisha wananchi wa kanda hiyo na Watanzania kwa ujumla.