Saturday, March 11, 2023

KIKWETE ATAKA BARUA ZA KIUTUMISHI KUJIBIWA KWA WAKATI

MHE. RIDHIWANI AELEKEZA BARUA ZA MASUALA YA KIUTUMISHI KUJIBIWA KWA WAKATI KUEPUKA MALALAMIKO YASIYO YA LAZIMA

NAIBU Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amewataka watumishi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma kujibu kwa wakati barua za masuala ya kiutumishi ili kuepuka malalamiko yasiyo ya lazima ambayo yamekuwa yakielekezwa katika Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Mhe. Kikwete ametoa maelekezo hayo Jijini Dodoma wakati wa kikao kazi chake na watumishi wa idara hiyo kilicholenga kufahamu majukumu yanayotekelezwa na kuhimiza uwajibikaji.


Mhe. Kikwete amewasisitiza watumishi wa idara hiyo ya Utawala wa Utumishi wa Umma kutosita kujibu barua za wadau kwa wakati hata kama zina mapungufu, ili wahusika wafahamu mapungufu yaliyopo kwenye masuala yao ya kiutumishi ambayo yamewasilishwa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa ajili ya kupata kibali au kutolewa maamuzi.

“Natambua kuna mapungufu ya masuala ya kiutumishi katika barua mnazolalamikiwa kutozijibu kwa wakati, lakini mnapaswa kuzijibu kwani msipofanya hivyo, mnatoa mwanya kwa wahusika kuilalamikia ofisi na hatimaye kuichafua taswira nzuri ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,” Mhe. Kiwete amefafanua.

Aidha, amewataka watumishi wa idara hiyo kuchakata  utoaji wa vibali vya uhamisho wa watumishi wa umma kwa kuzingatia takwimu zinazoainishwa na Mfumo wa Tathmini ya Hali na Mgawanyo wa Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma ili vibali vya uhamisho vinavyotolewa visiathiri utendaji kazi wa baadhi ya taasisi katika eneo la utoaji huduma bora kwa wananchi.


Kuhusiana na utendaji kazi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma kwa ujumla, Mhe. Kikwete amewapongeza watumishi wa idara hiyo kwa kutekeleza majukumu yao kikamilifu licha ya kuwa ni mengi na yenye changamoto nyingi.


Mhe. Kikwete ameongeza kuwa, watumishi wa idara hiyo wanatakiwa kuendelea kufanya kazi kwa bidii na weledi ili kutimiza azma ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kutoa huduma bora kwa wananchi.

Friday, March 10, 2023

CHAMA CHA MADEREVA WANAWAKE TANZANIA KUJA NA MRADI WA USAFIRISHAJI

CHAMA Cha Madereva Wanawake Tanzania (CWMT) kinatarajia kuanzisha kampuni ya usafirishaji ili kujiongezea kipato na kutoa ajira kwa wanachama wake.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa chama hicho Naetwe Ihema alisema kuwa lengo ni kumkwamua mwanamke ili ajitegemee na asiwe tegemezi.

Ihema ambaye ni dereva wa mabasi ya Mwendokasi alisema kuwa madereva wanawake kwa sasa ni wengi ambao wanafanya kazi kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo kwenye Taasisi za serikali na binafsi lakini walikuwa hawana Umoja wao.

"Tumeanzisha chama hichi ambacho mwanzo ilikuwa ni kikundi tukaona tujiongeza na kuwa chama ambacho kimesajiliwa na moja ya malengo yetu ni kuwa na kampuni ya usafirishaji kwa mabasi ya kwenda mikoani na daladala ambapo wanachama wetu watakuwa ndiyo madereva,"alisema Ihema.

Alisema kuwa wanatarajia kuongea na watu wenye kampuni za mabasi kwa kuanzia mabasi madogo (daladala) ili waingie makubaliano kama ni kuwakopesha au njia yoyote ili waweze kupata mabasi ili waanze kufanya hiyo kazi.

"Tutaanzisha hiyo kampuni ya usafirishaji kwani ajira kwa madereva wanawake ni changamoto ambapo waajiri wanakuwa hawawaamini wanawake lakini ni madereva wazuri na uwezo wao ni mkubwa,"alisema Ihema.

Aidha alisema kuwa madereva wanawake hawasababishi ajali kutokana na kuwa makini na hofu ya kuogopa kupoteza uhai wa watu ndiyo sababu udereva wao ni wa kujihami na siyo kujiamini.

"Mafanikio tuliyoyapata kwa mtu mmoja mmoja ni kuweza kuhudumia familia ambapo kwa wale walioolewa wanauwezo wa kushirikiana na waume zao katika kuendesha maisha na ambao hawajaolewa wanasomesha, wamejenga na wanafanya maendeleo makubwa,"alisema Ihema.

Aliongeza kuwa sifa ya mwanachama awe anaendesha chombo chochote cha moto ambapo baadhi ya wanachama wao ni marubani wa ndege, manahodha wa meli, madereva wa mitambo ya ujenzi, magari ya mizigo, mabasi makubwa, madereva wa treni, madereva wa uba, madereva wa mwendokasi na magari ya watu binafsi. Chama hicho kilianzishwa mwaka 2020 na kina wanachama 120.







CHAMA CHA MADEREVA WANAWAKE TANZANIA CHAJA NA MIKAKATI MIKUBWA

CHAMA Cha Madereva Wanawake Tanzania (CWMT) kinatarajia kuanzisha kampuni ya usafirishaji ili kujiongezea kipato na kutoa ajira kwa wanachama wake.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa chama hicho Naetwe Ihema alisema kuwa lengo ni kumkwamua mwanamke ili ajitegemee na asiwe tegemezi.

Ihema alisema kuwa madereva wanawake kwa sasa ni wengi ambao wanafanya kazi kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo kwenye Taasisi za serikali na binafsi lakini walikuwa hawana Umoja wao.

"Tumeanzisha chama hichi ambacho mwanzo ilikuwa ni kikundi tukaona tujiongeza na kuwa chama ambacho kimesajiliwa na moja ya malengo yetu ni kuwa na kampuni ya usafirishaji kwa mabasi ya kwenda mikoani na daladala ambapo wanachama wetu watakuwa ndiyo madereva,"alisema Ihema.

Alisema kuwa wanatarajia kuongea na watu wenye kampuni za mabasi kwa kuanzia mabasi madogo (daladala) ili waingie makubaliano kama ni kuwakopesha au njia yoyote ili waweze kupata mabasi ili waanze kufanya hiyo kazi.

"Tutaanzisha hiyo kampuni ya usafirishaji kwani ajira kwa madereva wanawake ni changamoto ambapo waajiri wanakuwa hawawaamini wanawake lakini ni madereva wazuri na uwezo wao ni mkubwa,"alisema Ihema.

Aidha alisema kuwa madereva wanawake hawasababishi ajali kutokana na kuwa makini na hofu ya kuogopa kupoteza uhai wa watu ndiyo sababu udereva wao ni wa kujihami na siyo kujiamini.

"Mafanikio tuliyoyapata kwa mtu mmoja mmoja ni kuweza kuhudumia familia ambapo kwa wale walioolewa wanauwezo wa kushirikiana na waume zao katika kuendesha maisha na ambao hawajaolewa wanasomesha, wamejenga na wanafanya maendeleo makubwa,"alisema Ihema.

Aliongeza kuwa sifa ya mwanachama awe anaendesha chombo chochote cha moto ambapo baadhi ya wanachama wao ni marubani wa ndege, manahodha wa meli, madereva wa mitambo ya ujenzi, magari ya mizigo, mabasi makubwa, madereva wa treni, madereva wa uba, madereva wa mwendokasi na magari ya watu binafsi. Chama hicho kilianzishwa mwaka 2020 na kina wanachama 120.




WEJISA WASHEREHEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI



WANAWAKE WA WEJISA WAJUMUIKA KUSHEHEREKEA SIKU YA WANAWAKE DAR

Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Weka Jiji Safi (WEJISA Company Ltd) kupitia kwa Mkurugenzi Mkuu wake Bi.Nuru Hassan amepongeza juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan katika kuweka mazingira mazuri ya kufanya kazi ikiwemo wafanyakazi wanawake jambo ambalo limeongeza uchapakazi kwa jinsia hiyo.

Nuru amesema hayo kwenye maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani ambayo inafanyika Machi 8 ya Kila mwaka.

"Rais wetu Samia tunamuunga mkono kwa sababu nafasi aliyonayo amesaidia kuongeza mwamko kwa wanawake kufanya kazi na wale ambao walikuwa hawana kazi na kutafuta shughuli zozote ili waweze kujiondoa kwenye utegemezi," alisema Nuru.

Amesema kuwa kampuni ya WEJISA itaendelea kushirikiana na Serikali bega kwa bega na ndiyo maana leo tumekuja hapa kusheherekea pamoja na kujifunza mengi kwa wafanyakazi wetu wanawake,"alisema Nuru Hassan

Aidha amesema kuwa amepata faraja kujumuika na Wanawake hao kwani wamekuwa chachu ya Maendeleo ya Kampuni hiyo.

Wanawake hao wa WEJISA wanatoka vitengo mbalimbali ikiwemo wanaosafisha maeneo ya Jiji, ikiwemo ufagiaji, ukusanyaji wa taka na usafi wa mazingira.

Lengo la tukio hilo ni kupeana moyo kama Wanawake katika kuamua mambo na kufanikisha utendaji bora wa kazi.

Kwa upande wake Patricia Kimelemeta Mwandishi Kinara wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Mtoto Mkoa wa Dar es Salaam ambaye alitoa mada ya malezi na makuzi kwa watoto katika tukio hilo la kusheherekea siku ya Wanawake, ambapo alitoa rai Kwa wazazi kuendelea kutoa elimu kwa watoto wao ikiwemo kujenga ukaribu wa kuwachunguza ilikujua changamoto wanazokutana nazo.

Kwa upande wao baadhi ya Wanawake wafanyakazi wa WEJISA waliishukuru kampuni hiyo kwani imekuwa mkombozi kwao na wamekuwa wakifanya kazi moyo.

"Mimi nina familia, nikitoka nyumbani naandaa kabisa chakula kwa wanangu.

Aidha, amewataka Wanawake kuzingatia sheria za Usalama barabarani kwani wamekuwa wakishuhudia matukio mengi, ikiwemo wao kugongwa.' Alisema Bi. Asha Salum.

Kwa upande wake. Bi. Sharifa Magombeka amesema kuwa, anafanya kazi ya kuzoa taka ilikupata kipato chake halali,

"Mwanamke ni kujitambua, nafanya kazi yangu ya kuzoa taka hii kupata kipato kihalali, tunamshukuru Mhe Rais kuendelea kuweka mazingira ya ufanyaji kazi na tumejumuika hapa tumepata elimu, lakini pia tumefurahia pamoja" alisema Sharifa.


Thursday, March 9, 2023

JWTZ WATANGAZA NAFASI KUJIUNGA NA JESHI

Na Mwandishi Wetu Dodoma

JESHI la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limetangaza nafasi za kujiunga na Jeshi kwa vijana wa Kitanzania wenye elimu ya kuanzia kidato cha nne hadi shahada ya uzamili ambao wamemaliza mkataba wa miaka miwili wa mafunzo ya kujitolea katika Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na kurudishwa majumbani.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiao wa (JWTZ) Luteni Kanali Gaudentius Ilonda wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu nafasi za kujiunga na Jeshi hilo.

Ilonda amesema kuwa nafasi hizo zinawahusu vijana wenye umri kuanzia miaka 18 hadi 26 kwa wenye elimu ya kidato cha 4 na cha sita na umri usiozidi miaka 27 kwa wenye elimu ya juu.

Amesema kuwa nafasi hizo haziwahusu vijana ambao bado wapo katika kambi mbalimbali za JKT kwa sasa bali zinawahusu wale ambao tayari wamemaliza mikataba yao ya mafunzo ya miaka miwili na kurudishwa majumbani na wenye vigezo vilivyotajwa vya kuomba nafasi hizo.

"Maombi yote yaandikwe kwa mkono na yawasilishwe makao makuu ya Jeshi hilo Dodoma kwanzia leo tarehe 9 Machi hadi tarehe 20 Machi 2023 yakiwa na viambatanisho kama vile nakala ya kitambulisho cha Taifa au namba ya Nida, nakala ya cheti cha kuzaliwa, vyeti vya shule na chuo, nakala cheti cha JKT na namba ya simu ya mkononi ya muombaji,"amesema Ilonda.

Aidha amewataka wananchi kuwa makini na matapeli kwani kumekuwa na tabia ya kuibuka matapeli pindi matangazo hayo ya nafasi ya kujiunga na Jeshi hilo zinapotangazwa. 

KIKWETE AOMBA USHIRIKIANO KUTIMIZA LENGO LA RAIS KUWA NA MUUNDO WA UTUMISHI KWA USTAWI WA TAIFA

MHE. RIDHIWANI KIKWETE AOMBA USHIRIKIANO KUTIMIZA LENGO LA MHE. RAIS LA KUWA NA SERA ZA KIUTUMISHI NA MIUNDO YENYE TIJA KWA USTAWI WA TAIFA

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

NAIBU Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amewataka watumishi wa Idara ya Uendelezaji Sera na Idara ya Uendelezaji Taasisi kumpa ushirikiano wa kutosha kwenye eneo la kusimamia uendelezaji wa sera katika Utumishi wa Umma na miundo ya Taasisi za Umma.

Mhe. Kikwete ametoa rai hiyo Jijini Dodoma wakati wa kikao kazi chake na watumishi wa Idara ya Uendelezaji Sera na Idara ya Usimamizi wa Taasisi kwa nyakati tofauti kilicholenga kufahamu majukumu yanayotekelezwa na Idara hizo pamoja na kuhimiza uwajibikaji.

 Amesema kuwa ili aweze kumsaidia vema Waziri mwenye dhamana kufikia lengo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuwa na sera za utumishi wa umma zenye tija na miundo inayotekelezeka kiutendaji kwa ustawi wa taifa.

Mhe. Kikwete amesema ameteuliwa na Mhe. Rais kumsaidia Waziri mwenye dhamana ya kusimamia utumishi wa umma na utawala bora, hivyo hana budi kufahamu kwa kina majukumu yanayotekelezwa na idara hizo ili aweze kuyazungumzia pale yanapohitaji ufafanuzi na uelewa kwa umma.

“Malengo ya kukutana nanyi leo ni kufahamiana na kujua majukumu yenu kwa kina kwa kuwa mimi nina jukumu la kumsaidia Mhe. Waziri kujibu maswali ya kiutumishi na utawala bora yanayoulizwa Bungeni,” Mhe. Kikwete amesisitiza.

Ameongeza kuwa, anatamani kujua kila kitu kinachofanyika katika idara hizo pamoja na changamoto wanazokabiliana nazo kiutendaji kwani kwa kufanya hivyo atakuwa kwenye nafasi nzuri ya kutekeleza kwa ufanisi lengo la Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan la kutoa huduma bora kwa wananchi.

Aidha Kikwete ameitaka Idara ya Undelezaji Sera kuhuisha sera za kiutumishi ili ziendane na wakati na ziweke mazingira rafiki ya kuzihusisha sekta binafsi kutoa mchango katika kuboresha utumishi wa umma kama Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan alivyoelekeza.

Wednesday, March 8, 2023

KIKWETE ATAKA USHIRIKIANO KUTIMIZA LENGO LA RAIS DK SAMOA SULUHU HASSAN KUWA NA SERA KWA USTAWI WA TAIFA

MHE. RIDHIWANI KIKWETE AOMBA USHIRIKIANO KUTIMIZA LENGO LA MHE. RAIS LA KUWA NA SERA ZA KIUTUMISHI NA MIUNDO YENYE TIJA KWA USTAWI WA TAIFA

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

NAIBU Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amewataka watumishi wa Idara ya Uendelezaji Sera na Idara ya Uendelezaji Taasisi kumpa ushirikiano wa kutosha kwenye eneo la kusimamia uendelezaji wa sera katika Utumishi wa Umma na miundo ya Taasisi za Umma.

Mhe. Kikwete ametoa rai hiyo jijini Dodoma wakati wa kikao kazi chake na watumishi wa Idara ya Uendelezaji Sera na Idara ya Usimamizi wa Taasisi kwa nyakati tofauti kilicholenga kufahamu majukumu yanayotekelezwa na Idara hizo pamoja na kuhimiza uwajibikaji.

 Amesema kuwa ili aweze kumsaidia vema Waziri mwenye dhamana kufikia lengo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuwa na sera za utumishi wa umma zenye tija na miundo inayotekelezeka kiutendaji kwa ustawi wa taifa.

Mhe. Kikwete amesema ameteuliwa na Mhe. Rais kumsaidia Waziri mwenye dhamana ya kusimamia utumishi wa umma na utawala bora, hivyo hana budi kufahamu kwa kina majukumu yanayotekelezwa na idara hizo ili aweze kuyazungumzia pale yanapohitaji ufafanuzi na uelewa kwa umma.

“Malengo ya kukutana nanyi leo ni kufahamiana na kujua majukumu yenu kwa kina kwa kuwa mimi nina jukumu la kumsaidia Mhe. Waziri kujibu maswali ya kiutumishi na utawala bora yanayoulizwa Bungeni,” Mhe. Kikwete amesisitiza.

Ameongeza kuwa, anatamani kujua kila kitu kinachofanyika katika idara hizo pamoja na changamoto wanazokabiliana nazo kiutendaji kwani kwa kufanya hivyo atakuwa kwenye nafasi nzuri ya kutekeleza kwa ufanisi lengo la Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan la kutoa huduma bora kwa wananchi.

Aidha, Mhe. Kikwete ameitaka Idara ya Undelezaji Sera kuhuisha sera za kiutumishi ili ziendane na wakati na ziweke mazingira rafiki ya kuzihusisha sekta binafsi kutoa mchango katika kuboresha utumishi wa umma kama Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan alivyoelekeza.