Sunday, May 31, 2026

WAZIRI KAPINGA AITAKA TBPL KUZALISHA MBOLEA HAI YENYE UBORA

WAZIRI wa Viwanda na Biashara Judith Kapinga ametaka kiwanda cha Tanzania Biotech Production Ltd (TBPL) kuzalisha Mbolea hai kwa kuzingatia ubora.

Kapinga aliyasema hayo Mjini Kibaha wakati wa hafla ya utiaji saini za makubaliano baina ya TPBL kampuni tanzu ya NDC na TFC, TARI, TFRA na TPHPA juu ya ushirikiano wa pamoja.

Alisema kuwa mbolea hiyo inasoko kubwa kwani haina kemikali na pia inatunza mazingira hivyo ni salama kwa afya za binadamu hivyo izingatiwe ubora wake.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji Mwendeshaji wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) ambayo ndiyo wasimamizi wa kiwanda hicho Nicolaus Shombe alisema kuwa uzalishaji wa mbolea hiyo utaleta mapinduzi ya kilimo.

Mkurugenzi Mkuu wa TBPL Mhandisi Rafael Moya alisema kuwa mbolea itasaidia wakulima kutumua kemikali kwani kiupaumbele cha Taifa ni kulinda afya za watu.


No comments:

Post a Comment