TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Pwani imefanikiwa kuongeza makusanyo kutoka kiasi cha shilingi milioni 4.6 hadi 12 kwa wiki kwenye kizuizi cha Maliasili cha Wilaya ya Kibiti.
Friday, January 31, 2025
TAKUKURU PWANI YAONGEZA MAPATO KUTOKA M 4.6 HADI M 12
Monday, January 27, 2025
KIBAHA SASA YAWA MANISPAA
MBUNGE wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Dk Samia Suluhu Hassan kuipandisha hadhi Halmashauri ya Mji Kibaha kuwa Manispaa.
Sunday, January 12, 2025
MANARA KUIUNGA MKONO SAMIA CUP KUTOA MILIONI 1
Manara alitoa ahadi hiyo kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Mtongani Mlandizi Kibaha wakati akizindua michuano hiyo ambayo itashirikisha timu 104 kutoka kwenye Kata zote za Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha yakiwa na lengo la kuhamasisha wananchi wakiwemo vijana kujiandikisha na kushiriki kwenye uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.
Alisema kuwa amevutiwa na vijana kuandaa mashindano kama hayo ambayo yanaunga mkono jitihada za Rais Dk Samia Suluhu Hassan kuchangia kwenye michezo kwani ni sehemu ya kuleta maendeleo nchini.
“Kutokana na kitu kizuri mlichokiandaa nitaunga mkono na nitawapatia kiasi cha shilingi milioni 1 ili mfanikishe mashindano haya yafanyike kwa ufanisi mkubwa na kufikisha vizuri ujumbe wa vijana kujiandikisha kwenye daftari la mpiga kura litakalofanyika Februari na kushiriki uchaguzi mkuu,”alisema Manara.
Kwa upande wake katibu wa hamasa wa UVCCM Godfrey Mwafulilwa alisema kuwa lengo la mashindano hayo ni kuhamasisha watu kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la mpiga kura na kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka huu kwa watu kuboresha taarifa zao.
Kwa kila kata watacheza hatua na kupata timu na kuingia hatua ya 16 bora ngazi Wilaya zawadi ambapo mshindi wa kwanza atapata zawadi ya guta la matairi matatu, mshindi wa pili atajinyakulia pikipiki na mshindi wa tatu atapata kiasi cha shilingi milioni 1.
Mwafulilwa alisema kuwa kwenye mashindano hayo hakutakuwa na kiingilio na kila timu itapatiwa jezi na mipira miwili huku zawadi nyingine ni mchezaji bora kipa mfungaji kila mmoja atapata ngao na shilingi 50,000 na timu yenye nidhamu shilingi 100,000.
Naye mwenyekiti wa chama cha soka mkoa wa Pwani COREFA Robert Munis alisema kuwa malengo yao ni kuhakikisha mpira Pwani unachezwa kwa kuzingatia taratibu na watashirikiana na wadau wanaoandaa mashindano mbalimbali lengo likiwa ni kuhakikisha vijana wanakuza vipaji vyao kwani soka ni ajira.
Munis alisema kuwa anawapongeza wadau hao kwa kuandaa mashindano hayo ambayo ni makubwa kwenye mkoa huo ambapo makubwa zidi ni yale yaliyoandaliwa na Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Omary Kipanga ambaye pia Mbunge wa Mafia.
Baadhi ya viongozi wa timu hizo waliwashukuru waandaaji wa mashindano hayo timu za Kujiandikisha na timu oresha taarifa zilitoka sare ya bao 1-1.
Mwisho.
VIJANA16 WENYE VIPAJI VYA SOKA KUWAKILISHA MKOA WA PWANI
Thursday, January 9, 2025
LICHA YA UNYNANYASAJI KIJINSIA NURU AWADH AWAANGUSHA VIGOGO WANAUME
WANAWAKE wanaowania nafasi za uongozi wanakabiliwa na changamoto za unyanyasaji wa kijinsia kutokana na baadhi ya watu au wagombea kuwa kejeli kuwa hawana uwezo wa kuongoza wao kazi yao ni kulea, kupika kumhudumia mume,”alisema Nuru Awadh.
Hiyo ni baadhi ya misemo wanayokutana nayo wanwake wanapoingia kwenye kuwania nafasi mbalimbali za uongozi dhana ambayo imekuwa ikiwakatisha tamaa baadhi ya wanawake hivyo kushindwa kujiingiza kwenye kuwania nafasi za uongozi.
Baadhi ya wanawake wameshindwa kuendelea na siasa au kuwania nafasi za uongozi wamekuwa wakizuliwa kashfa kuwa ni wahuni tu jambo ambalo siyo la kweli kwani wao nao wana uwezo wa kuongoza kama ilivyo kwa wanaume.Hayo ni maneno ambayo ymesmwa na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Miembe saba B Nuru Awadh kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati akiongea na mwandishi wa habari wa gazeti la HabariLeo ofisini kwake alisema kuwa ukatili wa kijinsia na mfumo dume bado upo na una warudisha nyuma wanwake kuwania nafasi za uongozi au kuingia kwenye siasa.
Kuna dhana imejengeka kuwa kiongozi lazima awe mwanaume na mwanamke hawezi kuwa kiongozi hali hiyo imekuwa ikiwarudisha nyuma wanawake ambapo jamii inapaswa iikemee na kuwapa wanwake nafasi sawa na wanaume.
“Namshukuru mama alinipambania nipate elimu lakini kwa upande wa baba hakuwa na msukumo kwa watoto wa kike kupata elimu hali ambayo ilisababisha nishindwe kwenda chuo cha ualimu baada ya kumaliza elimu ya sekondari,”alisema Awadh.
Awadh alisema kuwa wakati wa kuwania nafasi ya uenyekiti alikutana na unyanyasaji wa kijinisa kwani watu walimtolea kila aina ya kashfa lakini alipambana kwani alijua ni masuala ya kisiasa tu ili kumharibia asishinde kuanzia ndani ya chama hadi kwenye uchaguzi wa mtaa ambapo alishindana na kiongozi kutoka chama cha Chadema na yeye kumshinda na alikuwa mwanaume.
Alisema kuwa wanaume waachane na mfumo dume kwani unarudisha nyuma maendeleo kwani kuna viongozi wazuri wanawake na wana uwezo mkubwa wa kuongoza kuliko hata wanaume hivyo wasitumie nafasi hiyo kuwakandamiza wanawake.
“Nimetolewa maneno mengi ya kashfa na watu wa kawaida na baadhi ni viongozi ili tu kunidhoofisha lakini sikukata tamaa niliendelea kupambana na kushinda namshukuru na mume wangu kwani alinipa moyo na aliendelea kuniunga mkono hadi nikafanikiwa kushinda lakini kama huna moyo unaweza kuacha siasa,”alisema Awadh.
Alisema kuwa mume wake alipambana na kuna wakati alimuombea kura kwenye maeneo mbalimbali na hata wakati wa kampeni aliambatana naye ili kumsaidia aweze kushinda kwenye nafasi hiyo ya uenyekiti hivyo kumpa moyo na kutokata tamaa na hata kumsaidia kuhudumia watoto wakati yeye anapokuwa anayatekeleza majukumu yake.
Alisema kuwa amekuwa akitenga muda wa kuhudumia jamii na kuhudumia familia yake kwani anahakikisha kila kitu kinakwenda sawa na pia anatenga siku kwa ajili ya kwenda ofisini hasa ikizingatiwa kuwa yeye ni mjasiriamali ambapo hutenga muda kwa majukumu yote hayo bila kuathiri sehemu nyingine.
“Baada ya kushinda mikakati au malengo yangu ni kuhakikisha tunaboresha barabara ya Mtaa ambayo imeharibika sana na tumeanza kuweka vifusi sehemu korofi ila matarajio ni kuichonga kwani licha ya mvua kunyesha na kuiharibu haikubahatika kuchongwa hivyo kuwa kwenye hali mbaya,”alisema Awadh.
Alisema kuwa kipaumbele chake kingine ni ujenzi wa zahanati kwani wanatumia umbali mrefu kwenda kupata huduma za afya ambapo hupata huduma kwenye Zahanati ya Mwendapole ambako ni mbali na hutumia gharama kubwa ambapo ikijengwa hapo itakuwa imewasaidia wakazi wa mtaa huo.
“Malengo yangu mengine kwa kushirikiana na wananchi ni kukabiliana na migogorpo ya ardhi kwani kuna changamoto kubwa ya migogoro hivyo atashirikiana na wajumbe wake kuitatua migogoro hiyo ambayo imekuwa ikiwapotezea watu muda mwingi kuitatua na hiyo ni kero kubwa sana kwenye mtaa wangu,”alisema Awadh.
Aidha alisema kuwa baadhi ya maeneo yana changamoto ya maji hivyo atahakikisha anawasiliana na Dawasa ili watatue changamoto kwenye baadhi ya maeneo ili wananchi waweze kupata huduma hiyo kwa karibu na suala la mawasiliano kuna maeneo hayapati mawasiliano ya simu na kusababisha kero kwa wananchi.
“Katika kukabiliana na changamoto ndani ya mtaa nimeteua kamati ambazo zitafutailia changamoto hizo kulingana na sekta na kero hizo nilizipata wakati wa kampeni na uongozi utakuwa shirikisha kwa kuwashirikisha wananchi ambapo kwa sasa bado hatujakaa mkutano wa mtaa hivyo tunaanza kutatua kupitia kero tulizozipata wakati ule,”alisema Awadh. Alibainisha kuwa wananchi walimpa kura na kusema kuwa wamewapa uongozi wanaume kwa vipindi viwili hivyo ni wakati wa wanawake sasa kuongoza na anajivunia Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa uongozi wake nao ni chachu ya yeye kuingia kwenye nafasi hiyo ili naye aweze kuwasidia wananchi kutatua kero akiwa kama muongoza njia.
USAWA WA KIJINSIA WAWEZESHA CATHERINE KUSHINDA UENYEKITI LICHA YA VIKWAZO VYA WANAUMEA
MWENYEKITI wa Serikali ya Mtaa wa Sofu kata ya Sofu wilaya ya Kibaha Mkoni Pwani Catherine Lyimo ni moja ya viongozi wanawake aliyeweza kuwa na ushawishi mkubwa uliowafanya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumpa kura za kishindo na kumshinda aliyekuwa mwenyekiti wa Mtaa huo mwanaume aliyeongoza kwa kipindi cha miaka 10.Hayo inaonyesha jinsi gani watu wamenaza kubadilika na kuwaamini wanawake kuwa viongozi na hiyo inatokana na jinsi serikali ilivyoweka mazingira ya usawa baina ya wanaume na wanawake kuanzia kwenye elimu uongozi na sehemu mbalimbali ili kuwa na usawa wa kijinsia.
Hali hiyo imejidhihirisha ambapo kwenye Halmashauri ya Mji wa Kibaha wenyeviti wanawake kwenye mitaa ni 10 hali ambayo ni tofauti na ilivyokuwa miaka ya nyuma ambapo mila na desturi zilikuwa zikiwabana wanawake kuwa viongozi ambapo walikuwa hawapewi nafasi kabisa za kuwania uongozi au hata kwenye suala la elimu.
Lyimo aliondoa dhana hizo za wanwake kutoaminiwa na kuwa viongozi ambapo aliweza kuwashinda wanaume ambapo mwenyekiti aliyemaliza muda wake aliongoza kwa kipindi cha miaka 10 na mwingine alifanya kampeni kwa kipindi cha miaka zaidi ya miwli akijiandaa kutwaa nafasi hiyo.
“Yaani na wewe unataka kuwa mwenyekiti ungetuambia mapema sisi tumeshajipanga muda mrefu na wala huwezi kushinda na unajisumbua hivyo nafasi hii tuachie sisi wanawake hawawezi kuwa viongozi na hutajawahi kuongozwa na mwanamke,”alisema Lyimo.
Akizungumza na HabariLeo Lyimo alisema kuwa licha ya kuambiwa maneno hayo hayakumkatisha tamaa ambapo zikiwa zimesalia siku mbili huku akiona hakuna mwanamke yoyote aliyejitokeza kuwania nafasi ya kupata mwakilishi wa CCM kuwania nafsi ya uenyekiti yeye aliamua kujitosa.
Alisema kuwa kwenye uchaguzi huo yeye alipata kura 283 mpinzani wake akapata kura 119 na mshindi wa tatu alipata kura 83 ambapo jumla walikuwa wanaume wanne ambapo aliwabwaga na kupata nafasi ya kukiwakilisha chama kwenye uchaguzi wa Mtaa ambapo hata hivyo hakukuwa na chama cha upinzani na kuchukua nafasi hiyo na anamshukuru mume wake ambaye alimuunga mkono kwa kumpatia gari kwa ajili ya kufanya kampeni na hakuwa na wivu wa kimapenzi kwani anamwamini hivyo kutomzuia kufanya siasa.
“Mume wangu aliniruhusu kugombea lakini alikuwa na wasiwasi wa mimi kushinda lakini nilijipa moyo na kumwambia yeye anisaidie tu na matokeo atayaona mama yangu alikuwa akiunga mkono anapiga simu na kuniombea hata ndugu zangu nao waliniunga mkono na kupata baraka zao hivyo nikawa sina wasiwasi,”alisema Lyimo.
Alisema baada ya kufanikiwa kushika nafasi hiyo aliweka malengo ambayo ni kutatua changamoto za wananchi ikiwa ni pamoja na kujenga ofisi badala ya kutegemea ofisi za watu ambapo hazina nafasi kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi.
Alisema kuwa eneo tayari wanalo wanachofanya ni kuwaandikia wadau wa maendeleo kwenye mtaa huo kwa kushirikiana na wananchi kufanya ujenzi huo ambao ni ndoto yake kuhakikisha mkakati wa kuwa na ofisi unafanikiwa.
“Mpango mkakati wa mtaa kwa sasa ni kuwa na ofisi yake badala ya kutumia ofisi za watu wengine tunataka tuwe na ofisi yetu wenyewe ili tufanye kazi kwa uhuru badala ya kutegemea wengine kwani kutumia ofisi za watu wengine kuna changamoto zake,”alisema Lyimo.
Aidha alisema kuwa anamatumaini ofisi itajengwa kutokana na ushirikiano anaoupata kutoka kwa wananchi na wadau wa maendeleo kwani anaamini ushirikiano huo utafanikisha kupatikana kwa ofisi ya mtaa huo.
“Nataka kwa kushirikiana wananchi na wadau kuhakikisha tunaacha alama ya uongozi kwa kujenga ofisi yetu kwani tukiwa na ofisi yetu tutakuwa na uhuru na tutajenga kutokana na mahitaji ya mtaa wetu ambapo itakuwa na vyumba kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi,”alisema Lyimo.
Alibainisha kuwa jambo lingine ambalo atahakikisha linafanyika ni kuwagawia wananchi eneo la kufanyiabiashara kwa ananchi wa mtaa huo ili waweze kupata huduma ya soko karibu kwani wanataka liwe soko dogo ili kuwaongezea wananchi kipato na kutoa huduma.
“Tunahitaji tuwe na eneo ambalo litakuwa kama soko ambapo wananchi watauza bidhaa zao badala ya kwenda mbali kufuata mahitaji yao nyumbani tunataka wapate hapa jirani na pia itakuwa ni sehemu ya kujiongezea kipato,”alisema Lyimo.
Alisema kuwa nyingine ni kutafuta eneo kwa ajaili ya kujenga soko ambalo litatumiwa na wananchi wa mtaa huo ili waweze kujiongezea kipato kw akuinua uchumi wao badala ya kutumia masoko ya mtaa wa jirani wa Picha ya Ndege ambao ndiyo uliuzaa mtaa huo wa Sofu.
“Mimi mbali ya kuwa mjumbe pia nilikuwa mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Kata ya Sofu niliwasaidia sana watu kupata mikopo ya asilimia 10 kutoka Halmashauri kwani nilikuwa nikiwasaidia na hata kuwaandalia katiba na walifanikiwa kupata mikopo hiyo hivyo wengi walikuwa wakinipenda na nilipoingia kwenye kinyanganyiro sikupata shida sana kwani mimi sikufanya kampeni kama wenzangu na wala sikutoa rushwa ya fedha na wala sikuwa na fedha za kutoa,”alisema Lyimo.
Akizungumzia kuhusu rushwa ya ngono kwenye uchaguzi anasema hakukutana nayo kutokana na msimamo wake na changamoto kubwa ni wanawake kutojiamini wakifikiri kuwa uongozi ni wa wanaume kumbe hata wao wanaweza wanawenza kuongeza amewabadilisha wanawake wengi na kujiamini na kuomba nafasi mbalimbali za uongozi kwani wao ni jeshi kubwa. Aidha alisema kuwa mtu aliyemvutia na kuingia kwenye sisa ni Ester Matiko kutokana na jinsi anavyowasilisha hoja zake Bungeni na anatamani aje kuwa mbunge wa Viti maalumu baadaye na hata kuja kuwa waziri kwa miaka ijayo na Mtaa huo unazaidi ya wananchi 2,000.
LICHA YA KUKUTANA NA UKATILI WA KIJINSIA MBONI AUKABILI AWAGARAGAZA WANAUME
Monday, January 6, 2025
MTAA WA MIEMBE SABA WAWEKA VIFUSI KUBORESHA BARABARA YA MTAA
MTAA wa Miembe Saba B Wilayani Kibaha Mkoani Pwani umezanza zoezi la kuweka vifusi kwenye barabara ya Mtaa ili kuwaondolea kero wananchi wa Mtaa huo.
Sunday, January 5, 2025
WAHUKUMIWA MAISHA NA MIAKA 20 KWA UKATILI WA KIJINSIA
WATUHUMIWA wawili Mkoani Pwani waliokuwa wanakabiliwa kwa kesi za ukatili wa kijinsia wamehukimiwa vifungo tofauti ambapo mmoja amefungwa kifungo cha maisha jela na mwingine amefungwa kifungo cha miaka 20 jela.
Aidha jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani lilipeleka Mahakamani kesi 125 za makosa mbalimbali ambapo kati ya kesi hizo 47 zimepata mafanikio kwa watuhumiwa kuhukumiwa vifungo mbalimbali.
Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani ACP Salim Morcase alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya mafanikio ya jeshi hilo kwa kipindi cha mwezi Disemba 2024.
Morcase amesema kuwa jumla ya kesi za ukatili wa kijinsia kulikuwa na kesi tano za makosa ya kubaka na kulawiti.
"Watuhumiwa hao wawili walipata adhabu hizo ambapo wa kwanza alipatikana na hatia ya kubaka na kulawiti na wa pili alikutwa na hatia ya unyanyasaji wa kingono,"amesema Morcase.
Amesema kuwa watuhumiwa 52 wamehukumiwa vifungo tofauti tofauti kutokana na aina ya makosa yaliyokuwa yakiwakabili.
MADEREVA 11 MKOANI PWANIWAFUNGIWA LESENI
COREFA KUJENGA OFISI UWANJA WAKE
COREFA KUANDAA VIJANA KWENYE VITUO KILA WILAYA
CHAMA Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) kimesema kitahakikisha kila Wilaya inakuwa na kituo cha kuandaa vijana ili kuzalisha wachezaji watakaokuja kulitumikia Taifa.
COREFA KUANDAA VIJANA KUPITIA VITUO KILA WILAYA
CHAMA Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) kimesema kitahakikisha kila Wilaya inakuwa na kituo cha kuandaa vijana ili kuzalisha wachezaji watakaokuja kulitumikia Taifa.
VIONGOZI WA DINI NCHINI JAMHURI YA AFRIKA YA KATI WAISHUKURU JWTZ

Wakizungumza kwa nyakati tofauti mara baada ya kutembelewa na Kamanda wa Kikosi cha Nane cha Ulinzi wa Amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati Luteni Kanali Theofili Nguruwe wamesema uwepo wa JWTZ umekuwa na tija sana nchini humo kwani wamekuwa wakifanya kazi zao kwa weledi wa hali ya juu.
Akizungumza kwa niaba ya Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Berberati Mhashamu Koffi Denis, Karibu Mkuu wa Jimbo hilo Padre Jean Ancelimo amesema mbali na Ulinzi wa Amani pia limekuwa likitoa misaada mbalimbali ya hali na mali huku akitolea mfano wa ujenzi wa shule ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ambayo imepewa jina la Serengeti.
Naye Askofu Mkuu wa Kanisa la Evenjeliko (AEC) Mhashamu Lucian Nday amesema uwepo wa JWTZ nchini hapo umewafanya waishi kwa amani na zaidi ya yote limewezesha ukuaji wa lugha adhimu ya kiswahili.
Sheikh Rashid Mohamoud Arouna ni Imam wa Masjid Nuur amesema JWTZ limekuwa mstari wa mbele kwenye kila jambo ambalo wanaombwa kutoa msaada kwa ajili ya kuhakikisha nchi yao inakuwa na amani.
Kwa upande wa Kamanda wa Kikosi cha Nane cha Ulinzi wa Amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati Luteni Kanali Theofili Nguruwe amewashukuru viongozi hao na kuahidi kutekeleza majukumu yake kwa weledi wa hali ya juu.