MTAA wa Miembe Saba B Wilayani Kibaha Mkoani Pwani umezanza zoezi la kuweka vifusi kwenye barabara ya Mtaa ili kuwaondolea kero wananchi wa Mtaa huo.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mwenyekiti wa Mtaa huo Nuru Awadhi amesema kuwa barabara hiyo yenye urefu wa kilometa saba imeharibika sana kutokana na kuharibiwa na mvua kubwa zilizonyesha mwaka jana.
Awadhi amesema kuwa wameanza kusambaza vifusi hivyo ambavyo wameviomba kutoka kwa wadau mbalimbali wa maendeleo wa mtaa huo ili kufanikisha uboreshaji wa barabara hiyo ya vumbi.
"Nawashukuru wadau wa maendeleo katika mtaa ambao wamejitolea kupatikana kwa kifusi hichi ambacho kitatusaidia ili kupunguza kero kwa wananchi wanayoitumia barabara hii,"amesema Awadhi.
Amesema kuwa wameweka kifusi sehemu na bado kinahitajika kifusi zaidi ambapo tunaweka kwanza kwenye maeneo korofi ili kupunguza changamoto ya ubovu wa barabara.
"Tumepata changamoto kubwa ya ubovu wa barabara kwani sisi kwa bahati mbaya barabara yetu haikuchongwa kama baadhi ya barabara za mitaa mingine zilibahatika kuchongwa hivyo kupunguza athari za ubovu tofauti na kwetu,"amesema Awadhi.
Aidha amesema kuwa wanaendelea kuwahamasisha wananchi kuendelea kusaidia ili wakabiliane na changamotro hiyo ili kuongeza vifusi zaidi ili kuweza kuvisambaza kwenye barabara yote.
"Tuliongea na diwani ambapo alisema watafanya mpango wa kutuletea greda lakini majibu ni kuwa ni bovu hivyo tutatasubiri hadi litengenezwe ndipo tulilete kwetu lakini hiyo itakuwa ni muda mrefu ndipo tukaona njia ya haraka ni kumwaga kwanza kifusi kwenye sehemu korofi,"amesema Awadhi.
Aliongeza kuwa wao walipata bahati mbaya kutochongewa barabara yao lakini mitaa mingine ilichongewa barabara zao ambazo zilichongwa mwaka jana angalau imepunguza changamoto za ubovu.
"Mtaa wetu una wananchi zaidi ya 4,000 hivyo kila mmoja wetu akipambana tutaweza kuboresha miundombinu yetu ya barabara ambapo kuna shule za Msingi tatu na moja ya sekondari hivyo inaonyesha jinsi gani changamoto ya ubovu wa barabara inavyokuwa shida,"amesema Awadhi.
No comments:
Post a Comment