Akizungumza na waandishiwa habari ofisini kwake Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) Robert Munis alisema kuwa vijana hao wamepatikana kutoka vituo vya soka vya Wilaya za Mkoa huo baada ya kufanyiwa mchujo na Tff na baadaye Fifa wanakwenda Tanga na wakifuzu wataendelezwa na Fifa.
Munis alisema kuwa Wilaya zote zilishiriki mchujo huo isipokuwa wilaya ya Mafia ambapo wataalamu hao walishindwa kwenda kutokana na changamoto ya usafiri wa kufika huko.
"Tunaishukuru Fifa na Tff kwa kuwachukua vijana hao ambao ni wanafunzi kwa lengo la kuwaendeleza kwani itakuwa ni faida ya baadaye kwa nchi na itawasaidia vijana hao kuendeleza vipaji vyao na familia zao zitanufaika kwani kwa sasa mpira ni ajira kubwa sana,"alisema Munis.
Alisema kuwa hiyo ni bahati kwa vijana hao kikubwa wanachotakiwa ni kuonyes ha vipaji vyao na kwao hilo ni fanikio kubwa kupeleka vijana hao kuuwakilisha mkoa huo kwenye kituo cha Tff cha Mnyanjani cha kuendeleza vipaj vya vijana.
"Wazaz wao wanapaswa kuwahamasisha vijana wao washiriki michezo na waache dhana kuwa mtoto akishiriki michezo hatafanya vizuri darasani hiyo siyo kweli kwa ninichezo na michezo vinakwenda pamoja ambapo michezo inafanya akili inakaa vizuri hivyo kufanya vizuri kwenye masomo,"alisema Munis.
Naye mmojawapo wa watoto hao Tariq Mkenda alisemia kuwa wänamshukuru Mungu kwa kuwapatia näfasi hiyo na watahakikisha wanaonesha vipaji vyao ili wafanye vizuri na wachaguliwe na kwenda mbele zaidi waje kuitumikia nchi yao.
Rashid Said alisema kuwa wanaishukuru Corefa Tff na Fifa kwa kuona vipaji vyao na kuviboresha kwani itawasaidia waweze kuonyesha uwezo wao ili waje kuwa wachezaji bora watakaoleta mageuzi ya soka hapa nchini na kuwoamba wazazi nao wawaunge mkono kwa kuwapatia vifaa na muda wa kushiriki michezo.
Aziz Mwashambwa alisema kuwa wamefurahishwa sana na mpango huo wakuwa endeleza watotoili waendeleze vipaji vyao kwani hiyo itawasaidia kufika mbali kisoka na kuja kuwa wachezaji bora wa baadaye.
Mwashambwa alisema kuwa soka la kisasa linawekezwa kwa vijana na itakuwa ni nafasi nzuri ya kubadi soka la Tanzania na kufungua ukurasa mpya wa mpira wa Tanzania kwani mpango huo wa kuwa endeleza vijana ambapo uko kwenye mikoa 14 hapa nchini ambapo watoto hao watakutana huko.
No comments:
Post a Comment