MWENYEKITI wa Serikali ya Mtaa wa Sofu kata ya Sofu wilaya ya Kibaha Mkoni Pwani Catherine Lyimo ni moja ya viongozi wanawake aliyeweza kuwa na ushawishi mkubwa uliowafanya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumpa kura za kishindo na kumshinda aliyekuwa mwenyekiti wa Mtaa huo mwanaume aliyeongoza kwa kipindi cha miaka 10.Hayo inaonyesha jinsi gani watu wamenaza kubadilika na kuwaamini wanawake kuwa viongozi na hiyo inatokana na jinsi serikali ilivyoweka mazingira ya usawa baina ya wanaume na wanawake kuanzia kwenye elimu uongozi na sehemu mbalimbali ili kuwa na usawa wa kijinsia.
Hali hiyo imejidhihirisha ambapo kwenye Halmashauri ya Mji wa Kibaha wenyeviti wanawake kwenye mitaa ni 10 hali ambayo ni tofauti na ilivyokuwa miaka ya nyuma ambapo mila na desturi zilikuwa zikiwabana wanawake kuwa viongozi ambapo walikuwa hawapewi nafasi kabisa za kuwania uongozi au hata kwenye suala la elimu.
Lyimo aliondoa dhana hizo za wanwake kutoaminiwa na kuwa viongozi ambapo aliweza kuwashinda wanaume ambapo mwenyekiti aliyemaliza muda wake aliongoza kwa kipindi cha miaka 10 na mwingine alifanya kampeni kwa kipindi cha miaka zaidi ya miwli akijiandaa kutwaa nafasi hiyo.
“Yaani na wewe unataka kuwa mwenyekiti ungetuambia mapema sisi tumeshajipanga muda mrefu na wala huwezi kushinda na unajisumbua hivyo nafasi hii tuachie sisi wanawake hawawezi kuwa viongozi na hutajawahi kuongozwa na mwanamke,”alisema Lyimo.
Akizungumza na HabariLeo Lyimo alisema kuwa licha ya kuambiwa maneno hayo hayakumkatisha tamaa ambapo zikiwa zimesalia siku mbili huku akiona hakuna mwanamke yoyote aliyejitokeza kuwania nafasi ya kupata mwakilishi wa CCM kuwania nafsi ya uenyekiti yeye aliamua kujitosa.
Alisema kuwa kwenye uchaguzi huo yeye alipata kura 283 mpinzani wake akapata kura 119 na mshindi wa tatu alipata kura 83 ambapo jumla walikuwa wanaume wanne ambapo aliwabwaga na kupata nafasi ya kukiwakilisha chama kwenye uchaguzi wa Mtaa ambapo hata hivyo hakukuwa na chama cha upinzani na kuchukua nafasi hiyo na anamshukuru mume wake ambaye alimuunga mkono kwa kumpatia gari kwa ajili ya kufanya kampeni na hakuwa na wivu wa kimapenzi kwani anamwamini hivyo kutomzuia kufanya siasa.
“Mume wangu aliniruhusu kugombea lakini alikuwa na wasiwasi wa mimi kushinda lakini nilijipa moyo na kumwambia yeye anisaidie tu na matokeo atayaona mama yangu alikuwa akiunga mkono anapiga simu na kuniombea hata ndugu zangu nao waliniunga mkono na kupata baraka zao hivyo nikawa sina wasiwasi,”alisema Lyimo.
Alisema baada ya kufanikiwa kushika nafasi hiyo aliweka malengo ambayo ni kutatua changamoto za wananchi ikiwa ni pamoja na kujenga ofisi badala ya kutegemea ofisi za watu ambapo hazina nafasi kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi.
Alisema kuwa eneo tayari wanalo wanachofanya ni kuwaandikia wadau wa maendeleo kwenye mtaa huo kwa kushirikiana na wananchi kufanya ujenzi huo ambao ni ndoto yake kuhakikisha mkakati wa kuwa na ofisi unafanikiwa.
“Mpango mkakati wa mtaa kwa sasa ni kuwa na ofisi yake badala ya kutumia ofisi za watu wengine tunataka tuwe na ofisi yetu wenyewe ili tufanye kazi kwa uhuru badala ya kutegemea wengine kwani kutumia ofisi za watu wengine kuna changamoto zake,”alisema Lyimo.
Aidha alisema kuwa anamatumaini ofisi itajengwa kutokana na ushirikiano anaoupata kutoka kwa wananchi na wadau wa maendeleo kwani anaamini ushirikiano huo utafanikisha kupatikana kwa ofisi ya mtaa huo.
“Nataka kwa kushirikiana wananchi na wadau kuhakikisha tunaacha alama ya uongozi kwa kujenga ofisi yetu kwani tukiwa na ofisi yetu tutakuwa na uhuru na tutajenga kutokana na mahitaji ya mtaa wetu ambapo itakuwa na vyumba kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi,”alisema Lyimo.
Alibainisha kuwa jambo lingine ambalo atahakikisha linafanyika ni kuwagawia wananchi eneo la kufanyiabiashara kwa ananchi wa mtaa huo ili waweze kupata huduma ya soko karibu kwani wanataka liwe soko dogo ili kuwaongezea wananchi kipato na kutoa huduma.
“Tunahitaji tuwe na eneo ambalo litakuwa kama soko ambapo wananchi watauza bidhaa zao badala ya kwenda mbali kufuata mahitaji yao nyumbani tunataka wapate hapa jirani na pia itakuwa ni sehemu ya kujiongezea kipato,”alisema Lyimo.
Alisema kuwa nyingine ni kutafuta eneo kwa ajaili ya kujenga soko ambalo litatumiwa na wananchi wa mtaa huo ili waweze kujiongezea kipato kw akuinua uchumi wao badala ya kutumia masoko ya mtaa wa jirani wa Picha ya Ndege ambao ndiyo uliuzaa mtaa huo wa Sofu.
“Mimi mbali ya kuwa mjumbe pia nilikuwa mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Kata ya Sofu niliwasaidia sana watu kupata mikopo ya asilimia 10 kutoka Halmashauri kwani nilikuwa nikiwasaidia na hata kuwaandalia katiba na walifanikiwa kupata mikopo hiyo hivyo wengi walikuwa wakinipenda na nilipoingia kwenye kinyanganyiro sikupata shida sana kwani mimi sikufanya kampeni kama wenzangu na wala sikutoa rushwa ya fedha na wala sikuwa na fedha za kutoa,”alisema Lyimo.
Akizungumzia kuhusu rushwa ya ngono kwenye uchaguzi anasema hakukutana nayo kutokana na msimamo wake na changamoto kubwa ni wanawake kutojiamini wakifikiri kuwa uongozi ni wa wanaume kumbe hata wao wanaweza wanawenza kuongeza amewabadilisha wanawake wengi na kujiamini na kuomba nafasi mbalimbali za uongozi kwani wao ni jeshi kubwa. Aidha alisema kuwa mtu aliyemvutia na kuingia kwenye sisa ni Ester Matiko kutokana na jinsi anavyowasilisha hoja zake Bungeni na anatamani aje kuwa mbunge wa Viti maalumu baadaye na hata kuja kuwa waziri kwa miaka ijayo na Mtaa huo unazaidi ya wananchi 2,000.
No comments:
Post a Comment