Tuesday, June 25, 2024

FAMILIA ZISIONEA AIBU KUWAWAJIBISHA WANAOFANYA VITENDO VYA UKATILI KWA WATOTO





IMEELEZWA watu kuoneana aibu ndani ya familia kumesababisha vitendo vya ukatili kuendelea ndani ya jamii ambapo hali hiyo imezipeleka familia pabaya.

Aidha serikali ya Mkoa wa Pwani imesema kuwa itachukua hatua kali kwa watu wanaowafanyia ukatili watoto washindwe kufikia ndoto zao na kukosa haki zao.

Hayo yamesemwa na  Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Shangwe Twamala wakati wa Siku ya Mtoto wa Afrika kimkoa iliyofanyika Mjini Kibaha.

Twamala amesema kuwa baadhi ya taarifa zinaonyesha kuwa wanaofanya vitendo hivyo ni ndugu wa karibu.

"Ukatili unafanywa na ndugu wa karibu ambapo familia zinashindwa kuchukua hatua sababu ya kuoneana Muhali (Aibu) hili hatulikubali,"amesema Twamala.

Akisoma risala ya watoto wa mkoa wa Pwani Evelin Mhema amesema kuwa baadhi ya changamoto ni pamoja kufanyiwa vitendo vya ukatili mimba za utotoni, ubakaji, vipigo na vitendo vingine vinavyowanyima haki zao.

Mhema amesema kuwa watashirikiana na viongozi wakiwemo walimu ili waweze kufikia ndoto zao walizojiwekea kwa kusoma kwa bidii na kutii wazazi na walezi wao.

Kwa upande wake Said Mwinjuma amesema kuwa matumizi ya dawa za kulevya yamekuwa changamoto kwa vijana na kusababisha mmomonyoko wa maadadili.

Naye Mkurugenzi wa Kituo cha Msaada wa Kisheria Kibaha (KPC) Catherine Mlenga amesema kuwa watoto pia nao wajilinde kwa kutotembea usiku na kwenda kwenye mabanda ya video ma kulindana wao kwa wao.

Mlenga amesema kuwa pia wasipokee zawadi au kuomba fedha kwa watu wasiowafahamu na wazazi wawalinde watoto kwa kutokuwa wakali na

GRACE JUNGULU ATOA TOFALI 300

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Picha ya Ndege Grace Jungulu ametoa tofali 300 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya katibu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Kibaha Mjini.

Hayo yamesemwa na Katibu wa UWT Kibaha Mjini Cecilia Ndalu wakati wa kikao cha Baraza Kuu la Jumuiya hiyo kilichofanyika mjini Kibaha ambapo aliwashukuru wote waliochangia tofali ili kufanikisha ujenzi huo.

Ndalu amesema anawashukuru wanaccm waliojitolea kuchangia tofali ili ujenzi huo usichelewe na kukamilika kwa wakati kama malengo yaliyowekwa.

Ndalu amesema kuwa katika harambee hiyo jumla ya tofali 1,500 zilipatikana kwa ajili ya ujenzi huo ambapo mlezi wa UWT Selina Koka alitoa tofali 500 huku Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka akitoa mifuko ya simenti 100.

"Malengo yetu ni kuhakikisha ifikapo Desemba mwaka huu ujenzi huo uwe umekamilika ili kuepusha katibu kuishi kwenye nyumba ya kupanga ambapo pia itapunguza gharama,"amesema Ndalu. 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa UWT Kibaha Mjini Eline Mgonja amesema kuwa wamejipanga vizuri kuhakikisha mipango yote waliyojiwekea ikiwemo ujenzi huo na uchaguzi wa serikali za mitaa.

Mgonja amesema kuwa juu ya uchaguzi wamejipanga kuhakikisha CCM inashinda kwa kishindo kwenye uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.

Naye Mgeni rasmi kwenye Baraza hilo Mbunge Koka amesema kuwa ataendelea kushirikiana na umoja huo katika kuhakikisha chama kinapiga hatua na kuwaletea wananchi maendeleo.

Koka amesema kuwa ili kufanikisha ushindi wa chama wanawake lazima waungane washirikiane na kuacha kugawanyika kwani wasiposhirikiana watakigawanya chama.

Monday, June 24, 2024

HALMASHAURI YA MJI KIBAHA YAPATA HATI SAFI

MKUU wa Mkoa Pwani Abubakar Kunenge ameipongeza Halmashauri ya Mji Kibaha kwa kupata hati safi kutoka kwa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mji Kibaha kilichofanyika Kibaha wakati wa kupitia hoja za CAG.

Kunenge amesema kuwa Halmashauri imefanya vema kwa ukusanyaji wa mapato kutoka asilimia 54 Februari na kufikia asilimia zaidi 100 ambapo ni kazi kubwa imefanyika.

"Nawapongeza kwa kazi kubwa mliyoifanya lakini mnapaswa kudhibiti matumizi ya fedha kwani baadhi ya hoja zimetokana matumizi ya fedha na kutekeleza miradi kwa wakati,"amesema Kunenge.

Kwa upande wake katibu wa baraza hilo ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dk Rogers Shemwelekwa amesema kuwa kulikuwa na jumla ya hoja 69 zikiwemo za nyuma ambapo hoja 31 zimefungwa.

Shemwelekwa alisema kuwa hoja 38 ambazo hazijatekelezwa ni kutokana na masuala ya kisera lakini wanaendelea kuzifanyia kazi ili zisiwepo kabisa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kibaha Mussa Ndomba amesema kuwa wanaomba bajeti ya barabara iangaliwe kwani miundombinu imeharibika sana.

Ndomba amesema kuwa Halmashauri hiyo ipewe msukumo wa kuwa Manispaa kwani hapo ni Makao Makuu ya Mkoa huo kwani hata baadhi ya miradi inaweza kupatikana.

Naye Mkaguzi wa Mkuu wa nje wa Mkoa wa Owabi Pastory Massawe amesema kuwa baadhi ya changamoto zimeonekana kwenye eneo la ukusanyaji wa mapato.

Massawe amesema kuwa kinachokusanywa kitumike vizuri ili kuleta tija kwa wananchi na miradi izingatie sheria kanuni, utaratibu na kuzingatia miongozo.

Wednesday, June 19, 2024

KIBAHA KUKUSANYA CHUPA 800 KWA MWAKA

WILAYA ya Kibaha imejiwekea lengo la kukusanya chupa za damu 700 hadi 800 kwa mwaka ili ziweze kusaidia wahitaji wakiwemo akinamama wanaojifungua watoto na majeruhi wa ajali.

Hayo yamesemwa na mratibu wa damu salama wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Nyaisawa Birore alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kwenye zoezi la uchangiaji damu kwenye Kituo cha Afya Mlandizi.

Birore amesema kuwa wamejiwekea malengo ya kukusanya chupa 85 hadi 200 kwa kipindi cha robo mwaka ili ziweze kutumika kwa wagonjwa wenye mahitaji ya damu.

"Matumuzi ya damu kwa mwezi yalikuwa ni chupa 45 lakini yameongezeka na kufikia ni chupa 80 hadi 100 hivyo mahitaji ni makubwa sana na tunawaomba wananchi wajitokeze kwa wingi kujitolea,"amesema Birore.

Moja ya wachangiaji wa damu ambaye ni  katibu wa Umoja wa Vijana (UVCCM) Kibaha Vijijini Joel Kijuu amesema ameamua kujitolea ili kusaidia kuokoa maisha ya akinamama na wagonjwa wanaohitaji kuongezewa damu.

Kwa upande wake mhamasishaji uchangiaji damu Mariam Ngamila amesema kuwa baadhi ya wananchi wamekuwa na dhana kuwa damu inayochangwa inauzwa kitu ambacho siyo cha kweli.

Naye mhamasishaji uchangiaji damu Maria Ngamila amesema tone moja la damu linaweza kuokoa maisha ya watu wengi hivyo vijana wahamasike kuchangia damu.

Faudhi Kinanga ambaye yuko kwenye kambi ya uchangiaji damu amesema kuwa wamekuwa wakitoa elimu kwa vijana kushiriki zoezi la uchangiaji damu ili kuisaidia jamii.

Sunday, June 16, 2024

DK BITEKO AZINDUA TAARIFA ZA UTENDAJI SEKTA NDOGO UMEME, GESI ASILIA NA MAFUTA

Na Wellu Mtaki, Dodoma

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amezindua taarifa za utendaji katika Sekta ndogo ya Umeme, Gesi Asilia na Mafuta kwa mwaka 2022/2023 ambapo ametoa maelekezo mahsusi kwa Wizara na Taasisi mbalimbali kufanyia kazi taarifa hizo zinazoonesha mafanikio na changamoto katika Sekta Nishati.

Akizindua taarifa hizo tarehe 14 Juni, 2024 jijini Dodoma, Dkt. Biteko ameagiza Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati pamoja na Wizara ya Mipango na Uwekezaji kusoma taarifa hizo na kuzichambua na changamoto zilizoainishwa zipatiwe majibu ndani ya kipindi cha miezi mitatu.

Aidha ameagiza kuwa, kila aina ya fursa iliyoonekana kwenye taarifa hizo ichukuliwe kwa uzito mkubwa na itambuliwe nani ana uwezo wa kuitumia fursa hiyo ndani ya Serikali na katika taasisi binafsi.

“ Vilevile nawaagiza EWURA mhakikishe kuwa, tathmini ya mwaka ujao ihusishe utendaji wa Nishati Safi ya kupikia ili kuweza kujipima kwa usahihi kuhusu utekelezaji wa ajenda hii inayopewa kipaumbele na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan.” Amesema Dkt. Biteko.

Agizo jingine ni kuwa, matishio yote ya Sekta ya Nishati yaliyoainishwa katika ripoti kati ya mwaka 2023 hadi 2025 yawekewe mabunio ya suluhisho lake ili katika ripoti ijayo changamoto husika zisiwepo ikiwemo suala la kuongezeka kwa mahitaji ya umeme kila mwaka.

Dkt. Biteko pia ameitaka EWURA kupima uhusiano wa rasilimali zilizopo na mafanikio ya watu ambapo amesisitiza kuwa mafanikio ya sekta lazima yaendane na mabadiliko ya maisha ya watu.

Pia ametaka mifumo ya uagizaji mafuta iendelee kuboreshwa baada ya kufanyika utafiti wa kina na kueleza kwamba miundombinu ya mafuta bado inahitajika huku akisisitiza kuwa urasimu usiwepo kwenye Sekta ya Nishati.

Ameipongeza  EWURA kwa tathmini ambayo inaonesha kuwa Sekta ya Nishati inaendelea kuimarika, akitolea mfano kutolewa kwa leseni ya kuchimba gesi asilia katika kisima cha Ntorya kilichopo mkoani Mtwara kitakachotoa gesi futi za ujazo milioni 140 kwa siku ambapo leseni ya mwisho ya kuchimba gesi ilitolewa mwaka 2006.

Kuhusu sekta ndogo ya umeme amesema amesema Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kuiboresha ambapo leo ametoa taarifa kuwa mradi wa Julius Nyerere (JNHPP) umeingiza mtambo wa pili katika gridi ya Taifa kupitia mtambo namba 8 na hivyo kufanya mradi huo kuingiza megawati 470 katika gridi.

Kuhusu sekta binafsi amesema, “Sekta binafsi imetutoa kimasomaso, Serikali haiwezi kufanya kila kitu, wamefanya kazi kubwa mno kwenye mafuta, gesi na hata kwenye uzalishaji umeme, wito wangu kwenu msibaki nyuma changamkieni fursa, na kwa taasisi zilizo chini ya Wizara msione sekta binafsi kama watu wajanjawajanja, tuwape kipaumbele.” Amesema Dkt. Biteko

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, amemshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiimarisha Sekta ya Nishati na kusema kuwa Dodoma imeshuhudia matunda ya uimarishaji huo wa sekta kwani sasa umeme haukatiki.

Pia amepongeza utashi mkubwa wa uongozi wa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ambao unachangia kwa kiasi kikubwa katika kuiimarisha Sekta kwa ujumla.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba amesema kuwa katika tathmini iliyozinduliwa inaonesha Sekta ya Nishati  imepiga hatua kwenye maeneo megi ikiwemo uhakika wa upatikanaji umeme, upatikanaji na usambazaji wa mafuta kuimarika hasa baada ya Mhe. Dkt. Doto Biteko kuanza kuongoza Wizara ya Nishati, aidha upatikanaji na uwekezaji wa gesi unaendelea kuimarika na hii ikijumuisha usambazaji gesi kwenye maeneo mbalimbali kama katika magari, majumbani na viwandani.

Ameongeza kuwa, taarifa ya Benki ya Dunia kwa nchi za Dunia ya Tatu zinazofadhiliwa na Benki hiyo inaonesha kuwa Sekta ya Nishati kwa Tanzania inafanya vizuri zaidi katika nchi zote zinazoendelea na Bara la Afrika kwa ujumla na hii ni matunda ya usimamizi madhubuti wa Mhe.Dkt. Doto Biteko ambapo  eneo lililofanya vizuri zaidi ni usambazaji umeme vijijini na miradi mingine ya nishati kama JNHPP na mradi wa TAZA.

Ameongeza kuwa Benki ya Dunia imeidhinisha Dola.za Marekani milioni  300 ili ziendeleze sekta ya umeme kutokana na ufanisi huo wa Tanzania.

Akitoa taarifa za utendaji katika Sekta ya Nishati, Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Andilile alisema kuwa Sekta ya Nishati inaendelea kuimarika ikiwemo uwekezaji kwenye miundombinu ya mafuta, uwekezaji wa vituo vya mafuta na maghala umeongezeka, kuna ongezeko la uagizaji wa Gesi ya Mitungi (LPG) kwa asilimia 16 na ongezeko la uagizaji wa mafuta kwa asilimia 8.

 Amesema kuwa katika Sekta ya umeme uwekezaji umeongezeka katika uzalishaji, usafirishaji na usambazaji, upotevu wa umeme unazidi kupungua na wateja wa umeme wameongezeka kutoka milioni 3.8 mwaka 2021/22 hadi milioni 4.4 mwaka 2022/2023.

Baadhi ya  changamoto zilizoainishwa kwenye taarifa katika sekta ya umeme ni uchakavu wa miundombinu ambao unaendelea kufanyiwa kazi na uwekezaji endelevu kwenye sekta.

Saturday, June 15, 2024

WAZIRI JAFO ATUA KWA DC MAGOTI KUWEKA MIPANGO YA MAENDELEO

 

WAZIRI wa Nchi Ofisi Makamu wa Rais Muungano na  Mazingira na Mbunge wa Jimbo la Kisarawe Seleman Jafo amefika ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe kwa lengo la kwenda kumsalimia Mkuu mpya wa Wilaya hiyo Petro Magoti.

Waziri Jafo alikwenda kumtembelea mkuu huyo mpya wa Wilaya ikiwa imepita  siku moja tu baada ya kuapishwa rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge.

Waziri Jafo amesema kwamba ameamua kwenda kumtembelea mkuu huyo kwa lengo la kuweza kumpongeza kwa dhati baada ya kuteuliwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwenda kuwaongoza wananchi wa Kisarawe.

 Jafo amesema kwamba ana mfahamu Magoti kwa muda mrefu kutoka na kuwa mchapakazi hodari na anatekeleza majukumu yake ipasavyo kwa maslahi ya wananchi.

 "Kitu kikubwa nimekuja katika ofisi za Mkuu wa Wilaya lakini lengo kubwa ni kubadilisha mawazo katika Wilaya yetu ya Kisarawe na mimi nampongeza sana Magoti kwa kuletwa hapa,"amesema Waziri Jafo.

Pia Waziri Jafo alimshukuru kwa dhati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan  kwa kumteua Magoti nakumleta Kisarawe kwa lengo la kuwatumikia wananchi.

Sambamba na hilo Jaffo hakusita kumpa pongezi mkuu huyo wa Wilaya kwa kuchapa kazi kwa bidii zaidi kwani wanafahamiana tangu alipokuwa Waziri wa TAMISEMI waliweza i kufanya kazi kwa ushirikiano wa hali na mali.

Kwa upande wake Mkuu huyo wa Wilaya Petro Magoti amemwahidi waziri Jafo kumpa ushirikiano wa karibu zaidi lengo ikiwa ni kuwatumikia wananchi na kuwaletea maendeleo.


  

Friday, June 14, 2024

HALMASHAURI ZATAKIWA KUTENGA BAJETI YA MAFUTA KINGA KWA WATU WENYE UALBINO

 

SERIKALI imezitaka Halmashauri nchini kutenga bajeti kwa ajili ya kununua mafuta kinga ya kujipaka watu wenye ualbino ili kuepukana na mionzi ya jua ambayo inawasababishia kansa ya ngozi.

Hayo yalisemwa na Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu Deogratius Ndejembi ambapo hotuba yake ilisomwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya kuongeza uelewa juu ya Ualbino Duniani (IAAD) ambapo kitaifa ilifanyika Kibaha.

Ndejembi alisema kuwa serikali inafanya jitihada kubwa kuhakikisha watu wenye ulemavu wakiwemo watu wenye ualbino wanawekewa mazingira mazuri ili kupata huduma muhimu zikiwemo za kiafya.

"Tunaziagiza Halmashauri zote nchini kutenga bajeti kwa ajili ya kununulia mafuta hayo (sun screen lotion) ili ziweze kuwasaidia kukabiliana na mionzi ya jua ambayo imekuwa ikiwasababishia kansa ya ngozi,"alisema Ndejembi.

Alisema kuwa huduma za afya ni sehemu ya jukumu la serikali kama inavyotoa huduma nyingine na hiyo ni huduma mojawapo kwa wananchi.

"Pia ni vema kuwapatia vifaa zaidi kuliko fedha pale wanapokuwa wanahitaji vifaa kama vile vyerehani ili waweze kushonea kofia ambazo zinawasaidia kukabiliana na mwanga mkali na jua,"alisema Ndejembi.

Aidha alisema kuwa serikali iko makini katika kuangalia ustawi wa watu wenye ulemavu ambapo inawndelea na utaratibu wa kuboresha sheria ya watu wenye ulemavu na inalaani matukio ya kuwafanyia vitendo vya ujatili watu wenye ualbino.

"Jamii inapaswa kuthamini utu wa mtu na ni jukumu la kila mwananchi na kamati za usalama za mikoa zihakikishe vitendo hivyo vinakomeshwa na wao kwa wao waache migongano na washiriki uchaguzi kwa kuchagua na kuchaguliwa kwani ni haki yao,"alisema Ndejembi.

Aliwataka maofisa watendaji kuhakikisha wanafanya utambuzi wa watu wenye ualbino na kuhusu asilimia mbili ya mikopo ya Halmashauri kwa watu wenye ukemavu kwa mtu mmoja mmoja badala ya kukopa kwa vikundi serikali inalifanyia kazi suala hilo.

Kwa upande wake mwakilishi wa Mkuu wa Jeshi la Polisi, SACP Ralph Meela  alisema kuwa wataendelea kusimamia ulinzi na usalama hivyo watu wenye ualbino wasiwe na wasiwasi.

Meela alisema kuwa wanafanya jitihada mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwa na wakaguzi wa polisi ngazi ya kata zaidi ya 3,000 nchini na kuna makamishna wa polisi jamii kwenye mikoa hivyo kutakuwa na usalama wa kutosha.

Kwa upande waka katibu wa Chama Cha Watu Wenye Ualbino Tanzania (TAS) Batha Totei amesema kuwa wanaomba ruzuku kwa vyama vya watu wenye ulemavu na kuondoa gharama za matibabu ya kansa kwa watu wenye ualbino na kuwa na mpango wa bima ya afya.

Totei alisema kuwa serikali iweke mpango wa kuwa na kliniki kwenye hospitali za wilaya na kliniki tembezi na kuwashirikisha kwenye mikutano ya kampeni ili waweze kutoa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili kwa watu wenye ualbino.



MAGOTI KUSHIRIKIANA NA VIONGOZI KUWATUMIKIA WANAKISARAWE

MKUU mpya wa Wilaya ya Kisarawe Petro Magoti amesema kuwa atafanya kazi kwa ushirikiano na viongozi waliopo ili kuleta maendeleo kwa wabanchi wa wilaya hiyo. 

Magoti ameyasema hayo Mjini Kibaha alipokula kiapo cha kuwa Mkuu wa Wilaya ambapo aliapishwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge 

Amesema kuwa anamshukuru Rais kwa kumpa nafasi hiyo na hilo ni kama deni atalilipa deni hilo alilonalo kwa kuwatumikia wananchi wa Kisarawe katika kutatua changamoto zinazowakabili.

Kunenge amewataka wakuu wa Wilaya zote kuhakikisha wanasimamia mapato kwenye Halmashauri zao ili ziweze kuleta maendeleo kwa wananchi.

 Amewataka kutatua changamoto za wananchi kwa wakati na usimamizi kwenye utoaji huduma za afya na maji na usimamizi wa miradi ya elimu, barabara ili fedha zinazotolewa na serikali ziwe na tija.

Wednesday, June 12, 2024

WATU WENYE ULEMAVU WATAKA KUTEULIWA NAFASI NGAZI ZA MAAMUZI

CHAMA Cha Watu Wenye UalbinoTanzania (TAS) kimeiomba serikali iwateue kwenye nafasi za ngazi za maamuzi.

Aidha ametaja nafasi hizo za maamuzi kama vile Uwaziri, Ukuu wa Mikoa na Ukuu wa Wilaya kwani nao wanauwezo kama walivyo watu wengine.

Hayo yamesemwa na Mjumbe wa Bodi ya chama hicho Thomas Diwani wakati akitoa salama za chama kwenye kongamano la kuongeza uelewa juu ya Ualbino lililofanyika kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Kwa Mfipa Kibaha.

Naye Mkurugenzi kitengo cha huduma kwa watu wenye ulemavu Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Rasheed Maftah amesema kuwa serikali inaanda sera na miongozo mbalumbali kwa watu wenye ulemavu za kuweka usawa na haki.

Awali mwenyekiti wa Tas Godson Mollel amesema kuwa wanampongeza Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia Hospitali Rufaa ya KCMC kwa kuwapatia kiasi cha shilingi milioni 124 kwa ajili ya kuzalisha losheni zinazotumiwa na watu wenye ualbino.

Kwa upande wake kaimu mkuu wa mkoa wa Pwani Nickson John amesema kuwa watu wenye ualbino wapatao 368 wanapatiwa misaada mbalimbali na zimeundwa kamati za watu wenye ualbino.


MAHAKAMA YATAKIWA KUTOA ADHABU KALI WANAOWAFANYIA VITENDO VYA UKATILI WATU WENYE UALBINO



CHAMA cha watu wenye Ualbino Tanzania (TAS) kimeiomba Mahakama kutoa adhabu kali kwa watu wanaokutwa na hatia ya kuwakata viungo au kuwaua watu wenye Ualbino.

Hayo yamesemwa mjini Kibaha na Mwenyekiti wa Taifa wa TAS Godson Mollel alipozungumza na waandishi wa habari wakati wa maadhimisho ya kitaifa ya siku kuongeza uelewa juu ya Ualbino (IAAD) duniani.

Mollel amesema kuwa Mahakama ikotoa hukumu kali kwa wahusika hao itakuwa fundisho kwa watu wanaojihusisha na vitendo hivyo kuacha kuwadhuru watu wenye Ualbino.

Naye ofisa ustawi mkuu toka Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana na Watu wenye ulemavu Joy Maongezi amesema kuwa sheria namba 9 ya mwaka 2010 inataka kuwa na haki kwa watu wenye ulemavu ambapo watu wenye Ualbino ni sehemu yao.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Shangwe Twamala amesema kuwa wakati wa maadhimisho hayo huduma mbalimbali zinatolewa ikiwa ni pamoja na upimaji saratani ya ngozi, utoaji miwani, kofia na losheni ya kuzuia ngozi kuathirika, upimaji wa tezi dume na kansa ya kizazi.

Maadhimisho hayo hufanyika kila mwaka duniani ambapo kilele huwa tarehe 13 Juni kila mwaka na kwa mwaka huu kitaifa yanafanyika Kibaha Mkoani Pwani.


Monday, June 10, 2024

KAMPUNI YA REFUELLING TANZANIA LIMITED YATOA MABATI 72 KWA KIKUNDI CHA KUKAYA MIONO

KAMPUNI ya Refuelling Tanzania Ltd imekipatia mabati 72 kikundi cha KUKAYA-Miono Chalinze Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa ya shule ya msingi Miono.

Akipokea mabati hayo kwa niaba ya kikundi cha KUKAYA MIONO ,Mwenyekiti Omary Mtiga ameishukuru kampuni ya Refuelling kwa msaada huo.

Alieleza ujenzi una miezi sita kwa nguvu zao wananchi ,wameshapokea milioni 13.5 kutoka kwa wadau, lengo lilikuwa kujenga kuongeza darasa moja lakini wamefanikiwa kujenga madarasa mawili.

Mtiga alifafanua, kwasasa bado kuna mahitaji ya mabati 34 ,malori sita ya mchanga ,maroli manne ya kokoto na mifuko ya saruji 60 ili kukamilisha ujenzi huo.

"Tunashukuru uongozi wa kampuni hii, chini ya Mkurugenzi Mohsin Bharwani ambae ameguswa na jambo hili, Mohsin amekuwa akijitoa katika masuala ya kijamii kwenye maeneo mengi ndio na sisi tuliamua kumuomba msaada na tunashukuru kutusaidia "

Aidha Mtiga alitoa wito kwa makampuni na wadau wengine kuendelea kujitolea kwani bado kuna uhitaji.

Aliiomba jamii Miono kuendelea kushirikiana katika masuala ya maendeleo ili kujiinua kimaendeleo ikiwemo kuboresha sekta ya elimu.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa kampuni ya Refuelling Tanzania limited, Mohsin Bharwani, Meneja wa kampuni hiyo Renatus Kabeyo alisema wamekabidhi mabati 72 na kusafirisha jumla milioni mbili (mil.2).

Alifafanua kuwa, kampuni hiyo inashirikiana na jamii kwa kila jambo kulingana na uwezo wao.

"Nimeona kuna madarasa tunaona mnajenga ,vyoo ,niweze kuahidi tutajenga hoja ,pamoja na misaada inayokuja nikuombe ofisa elimu kata andika andiko ,ili mpate misaada mikubwa kutoka kwa wadau mbalimbali" alieleza Kabeyo.

Kabeyo alisema wanafunzi wanasoma ila wanatakiwa kusoma kwenye mazingira bora.

Sunday, June 9, 2024

375 WAFAULU BUNDIKANI SEC YAFUTA ZIRO

SHULE ya Sekondari ya Kata ya Maili Moja Bundikani Halmashauri ya Mji Kibaha imefanikiwa kufaulisha wanafunzi wote wa kidato cha nne 375 kufaulu na kuondoa daraja sifuri.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Bernard Muyenjwa alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake.

Muyenjwa alisema kuwa ufaulu huo ni asilimia 100 ya wanafunzi waliofanya mtihani wa kidato cha nne waliofanya mitihani yao mwaka jana.

"Wanafunzi 234 wamefaulu kwenda kidato cha tano na vyuo mbalimbali vya kati ambapi ufaulu huo ni sawa na asilimia 65 huku wengine wakisubiri uteuzi wa awamu ya pili,"alisema Muyenjwa.

Alisema kuwa jumla ya wanafunzi waliofanya mtihani walikuwa 375 wasichana wakiwa 218 wavulana 157 ambapo daraja la kwanza walikuwa 22 wasichana tisa wavulana 13.

"Daraja la pili 79 wasichana 53 wavulana 26 daraja la tatu 144 wasichana 73 wavulana 71 na daraja la nne ni 130 wasichana 83 wavulana 47 huku daraja sifuri kukiwa hakuna hata mmoja,"alisema Muyenjwa.

Aidha alisema kuwa mafanikio hayo yalitokana na mshikamano walionao walimu na kujitolea, kusimamia vizuri mipango iliyowekwa ya kufikia ufaulu.

"Ushirikiano kati ya shule, wazazi na bodi, kusimamia nidhamu kwa wanafunzi na kuhimiza walimu kufundisha kwa kasi na mazoezi ya mara kwa mara na ufuatiliaji, ufanyaji wa mitihani kila Jumamosi,"alisema Muyenjwa.

Aliongeza kuwa upande wa nidhamu ni kuweka uzio na walinzi ili kudhiti wanafunzi kutoka bila ya sababu zisizokuwa na msingi bali iwe ya msingi ndipo atoke au muda wa kuingia shuleni.

"Malengo ni kuhakikisha tunapunguza wanafunzi wanaopata daraja la nne na kuongeza ufaulu wa daraja la kwanza wafikie angala 60 au 70 na hilo linawezekana,"alisema Muyenjwa.

Alibainisha kuwa shule yao ambayo ni kinara kwa shule za Kata kwa kufaulisha kwenye Halmashauri ya Mji Kibaha ikiwa inazidiwa na shule ya Tumbi na Kibaha wasichana ambazo ziko chini ya Shirika la Elimu Kibaha.

"Tunaishukuru Serikali kwa kutoa kiasi cha shilingi milioni 120 kwa ujenzi wa vyumba vya madarasa vinne na changamoto zilizopo ni ndogondogo ambazo ziko ndani ya uwezo wetu walimu wapo wa kutosha zaidi ya 100,"alisema Muyenjwa.

Aliwaomba wazazi na wadau kuendelea kutoa ushirikiano ili shule hiyo iendelee kufanya vizuri kwenye matokeo ya kidato cha nne na kufikia malengo ya kuwa na kidato cha tano na sita.

Saturday, June 8, 2024

LAMI KUWEKWA SHELI MAILI MOJA






WANANCHI wanaopitiwa na mradi wa ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami ya BP Sheli-Maili Moja yenye urefu wa kilometa nne wametakiwa watoe ushirikiano ili kufanikisha ujenzi huo.
Hayo yamesemwa na Diwani wa Kata ya Maili Moja Ramadhan Lutambi alipokuwa akizungumza na wananchi wakati wa utoaji elimu juu ya mradi huo ambao kwa sasa uko kwenye hatua ya usanifu.

Lutambi amesema kuwa mradi huo unatekelezwa na benki ya dunia umeanza kwa kufanya usanifu hivyo wananchi wasiweke vikwazo ili hatua hiyo ambayo ni ya miezi nane iweze kwenda vizuri bila ya kikwazo chochote.

"Tunawaomba wananchi muonyeshe ushirikiano kwani kujengwa lami kwa barabara hii ni mkombozi kwa Kata yetu na italeta maendeleo na kurahisisha shughuli mbalimbali hasa za usafirishaji,"amesema Lutambi.

Amesema kuwa katika kutekeleza mradi huo hakutakuwa na fidia kwa sehemu ambazo nyumba zimejengwa barabarani itakapopita barabara hiyo ambayo inaanzia barabara kuu ya Dar es Salaam-Morogoro.

"Tusije tukakwamisha mradi ukikwama mradi utahamishiwa sehemu nyingine hivyo hii ni fursa kwetu tusiiache kwani kukwamisha ni kushindwa kujiletea maendekeo kwani barabara ni maendeleo na fursa zitajitokeza kwa wingi kupitia barabara,"amesema Lutambi. 

Kwa upande wake mwakilishi wa Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini TARURA Mhandisi Fredrick Nzogela amesema kuwa hatua ya usanifu itakamilika mwezi wa tisa ambapo mkandarasi atakabidhi taarifa ambayo itaonyesha baadhi ya maeneo yatakayo athirika.

Nzogela amesema kuwa barabara hiyo itakuwa na upana wa mita 8.5 na itakuwa na mitaro pande zote pamoja na kuwekwa taa na alama mbalimbali na matuta sehemu ambazo ni hatarishi hususani kwenye eneo la shule.

Kaimu Mtendaji wa Kata ya Maili Moja  Mwanawetu Said amewataka wananchi wasiwe na hofu kwani athari hazitakuwa kubwa kama wanavyofikiri na sehemu zitakazo athirika ni kidogo sana.

Said amesema kuwa sehemu zitakazo athirika wahusika wasikwamishe kufanyika kwa ujenzi huo kwani kuukwamisha ni kuyakataa maendeleo ndani ya maeneo yao.

Naye Mhandisi Kiza Mwesigwa ambaye anasimamia ujenzi wa barabara hiyo kwa ujenzi wa changarawe kabla ya kuwekwa lami amesema ujenzi wake utakuwa kuchonga na kuweka kifusi na kushindilia itakuwa na urrefu wa kilometa .

Mwesigwa amesema kuwa mradi huo utaanza mwezi huu kuanzia wiki ijayo na utakuwa wa miezi sita hadi mwezi Novemba itakuwa na urefu wa kilometa moja na mita 800.

Nao baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo wa elimu juu ya mradi huo waliitaka Halmashauri kutoa elimu ya kutosha juu ya utekelezaji mradi huo.

Wamesema wako tayari kutoa ushirikiano ili kufanikisha ujenzi wa barabara hiyo na kuwaweka wazi ili wajue maeneo ambayo yameonekana kuzidi ili waweze kuhamisha vitu vyao mapema.





Monday, June 3, 2024

WANAWAKE WA NDUMBWI WAASWA KUWAENZI WANAWAKE VINARA WAZALENDO







Ndugu Omary Abdul Punzi Afisa Mahusino wa Mradi wa Mazingira wa RAMATA (Rafiki wa Mazingira Tanzania) kutoka GBCF nchini Tanzania Tarehe 1.6.2024 awafunda wakina mama wa UWT tawi la Ndumbwi Mbezi Juu Kata ya Mbezi juu Wilaya ya Ubungo Jijini  Dar es Salaam.

Ndugu Omary Punzi aliwaelekeza kuwa Taifa hili limejengwa katika Misingi ya Kizalendo na walioitengeneza hii nchi ni wakina mama mfano Mwenyekiti wa kwanza Taifa wa Uwt  Sofia Kawawa na  Mwanasiasa Mashuhuri Bibi Titi Mohammed aliyejitoa kuchangia Mchango wake katika nchi hii.

Aliwaomba wanawake wamuunge mkono Mhe Dr Samia Suluhu Hassani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika sekta ya kutunza Mazingira na sekta nyingine za Kiuchumi.

Kwa kuzifuata hizi Falsa za TA TE TI TO TU
TA = Tangaza nchi yako bila uoga
TE= Tetea nchi yako bila uoga tusikubali idhalilike
TI= Timiza wajibu wako kwa kila hali
TO= Toa Ushauri kwa hali na Mali
TU= Tubu pale unapokosea

Pia aliwakumbisha sifa kuu ya kiongozi ni Kulalamikiwa na kuwa na Kiherehere chenye Manufaa kwa nchi yake

Naye Wakili msomi Godfrey Kizito Chambi alitoa mada ya Umuhimu wa wanawake katika kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mtaa wa mwaka 2024 na wasisite kwenda kujiandikisha katika Daftari la kudumu la kupiga kula  zoezi hilo  la kupata kitambulisho kwa ajili ya uchaguzi litakalo anza tarehe 1.7.2024 alisisitiza kuwa wasijitokeze kupokea au kutoa rushwa katika mchakato wa Uchaguzi utarudisha nyuma na kuwapata wagombea siyo sahihi na aliendelea kuwakumbusha wanawake hao juu ya Umuhimu wa kutunza Mazingira kwa kutumia rasilimali rafiki ili mazingira yetu yawe rafiki alisema shughuli za binadamu zinaongoza kuchochea kuharibu Mazingira.

Kwa upande Rehema Muya Mwenyekiti wa UWT Kata ambaye alikuwa Mgeni Rasmi katika Mkutano huo alimwaga sifa kwa Mwenyekiti  na katibu wa tawi la ndumbwi kwa kufanya jambo kubwa la kuandaa mada hizo na kuwakusanya Wanawake wa UWT hii inaonesha kuwa sasa CCM inakwenda kupata Ushindi wa Kishindo kwa Mhe Dkt Samia Suluhu Hassani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Katika uchaguzi wa 2024 na 2025

Naye Mhe Anna lukindo Diwani wa kata ya Mbezi Juu alisema kuwa Serikali Mhe Dk  Samia Suluhu Hassani imewasaidia wananchi wa Mbezi Juu kujenga Daraja Mito Miwili lengo kutatua kero ya muda mrefu ya kupita hapo Daraja  hilo likikamilika litakuwa chachu ya Maendeleo kutokana na Kasi inayofanywa na Mhe Josephat Gwajima na Timu nzima ya Viongozi wa Kinondoni sambamba na hilo alivutiwa na Mada za mkutano huo.

Katibu wa Tawi la Ndumbwi ndugu Witnes Ngowi alisema kuwa UWT katika Tawi hilo wamejipanga na kuhakikisha kuwa watashinda kwa kishindo katika Uchaguzi wa 2024 na  2025.

Kwa upande wa Catherine Mpangala Mwenyekiti wa Tawi la Ndumbwi alisema wameanda Mkutano huo   kwa lengo la kutekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi na kuwakumbusha watanzania kuwa mwaka 2024 kutakuwa na Uchaguzi wa serikali ya Mitaa hivyo wasisite kujitokeza kwa wingi katika zoezi la kujiandikisha katia Daftari la Kupiga kula litakalo anza Julai Mosi.

Aliwashukuru Bank ya NMB kuja kutoa Elimu ya Mikopo kwa wakina mama na na watoa mada ya Ujasiliamali kutoka kwa Estar Muhanga ,Mada Itifaki na Uzalendo iliyotolewa na ndugu Omary Punzi  na ile mada ya Utunzaji wa Mazingira na Umuhimu wa kushiriki Uchaguzi wa serikali za mita iliyotolewa na wakili Msomi Geoffrey Kizito 

Ndugu Catherine aliwawapongeza wanachama wa UWT kufika kwa wingi Sambamba na viongozi wa Chama kutoka Wilaya na kata kuja kushiriki Mkutano huo.

Sunday, June 2, 2024

CHAURU YACHAGUA VIONGOZI WAKE








CHAMA Cha Ushirika wa Umwagiliaji Mpunga Ruvu (CHAURU) cha Halmashauri ya Chalinze Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani kimefanikiwa kumchagua Mchujuko Mchujuko kuwa mwenyekiti atakayeongoza kwa kipindi cha miaka mitano.

Kwenye uchaguzi huo ambao ulisimamiwa na Ofisa Ushirika Halmashauri ya Chalinze alimtangaza Mchujuko aliyepata jumla ya kura 214 sawa na asilimia 91.8 kati ya kura 1,165 halali zikiwa 1,162 na kura zilizoharibika ni tatu ambapo mshindi alipaswa kupata angalau asilimia 50 ya kura.

Akitangaza washindi wa uchaguzi huo msimamizi huyo Raphael Kajale amemtangaza makamu wa mwenyekiti ni Otnel Mbura aliyepata kura 186 sawa na asilimia 79.8.

Kajale amewataja wagombea wengine kuwa ni Sade Mwakitalu alipata kura 173 sawa na asilimia 74, Renatha Mwaipopo alipata kura 171 sawa na asilimia 73.3 na Shea Bilali aliyepata kura 154 sawa na asilimia 67 hawa wote wataunda bodi ya ushirika huo.

Amewataja wajumbe wa kamati ya maadili waliochaguliwa ni Moses Polepole, Rajab Mfyome, Theresia Shayo, James Ole Njolay na Zuhura Matimbwa.

Akiwashukuru wajumbe wa mkutano huo mkuu wa uchaguzi uliompa ushindi mwenyekiti mpya Mchujuko amesema kuwa kikubwa atakachokifanya ni kuhakikisha wanaongeza uzalishaji kutoka tani tano za sasa hadi saba mpaka 10 na kukarabati miundombinu.

Awali mwenyekiti aliyemaliza muda wake Chacha Sadala akishukuru amesema pia wamefanikiwa kununua trekta na jembe lake ukarabati wa pampu nne kukarabati mashine mbili za kukoboa mpunga na tayari hekari 800 zimepandwa kati ya hekari 1,800 na hadi itakapofika Juni 30 wakulima wote watakuwa wamepanda mashamba yao.