Wednesday, September 2, 2015

MWANAFUNZI AJERUHIWA KWA KIPIGO CHA MWALIMU

Na John Gagarini, Mafinga
MWANAFUNZI wa kidato cha sita wa Shule ya Sekondari ya JJ Mungai Octavian Luoga (20) amejeruhiwa kichwani kwa kupigwa fimbo na mwalimu wake kwa tuhuma za kushindwa kuingia darasani.
Akizungumza jana mjini Mafinga na waandishi wa habari mara baada ya kutoka kwenye Hospitali ya Mafinga wilaya ya Mufindi mkoani Iringa alipotoka kupatiwa matibabu mwanafunzi huyo alisema kuwa mbali ya kupigwa na fimbo kichwani pia alipigwa makofi na mateke.
Luoga alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya asubuhi Septemba  Mosi akiwa bwenini amepumzika kutokana na kuumwa na mishipa ya kichwa huku akiwa na wenzake wawili Wilson Due na Nsajigwa Moses ambao wote walikuwa wakiumwa jambo lililomfanya ashindwe kuingia darasani.
“Walimu wawili walikuja na kunitaka niende ofisini kwa ajili ya kupewa adhabu nikawaambia mimi naumwa ndiyo sababu ya kushindwa kuingia darasani mara wakaanza kunipiga nikawaambia nuamwa naomba mnisikilize wakakataa wakasema nimewajibu vibaya,” alisema Luoga.
Alisema kuwa kutokana na kipigo hicho ikabidi aende ofisini na kufika kule akaanza kupigwa makofi,mateke na fimbo maeneo mbalimbali ya mwili na mwalimu mkuu msaidizi Huruma Nyalusi akidai kuwa nawadharau walimu.
“Mwalimu alinipiga fimbo kichwani na damu zikaanza kunitoka hata hivyo hawakutaka kunipeleka hospitali ndipo wanafunzi wengine wakalazimisha nipelekwe ambapo tulienda polisi na baadaye hospitali kwa ajili ya matibabu nikashonwa nyuzi kadhaa,” alisema Luoga.
Aidha alisema kuwa walimu na wanafunzi wanafahamu matatizo yake na wiki moja iliyopita alilazwa kutokana na tatizo lake hilo hilo hali ambayo ilimfanya ashindwe kuingia darasani ambapo hata mahudhuria yake darasani ni mazuri lakini huwa anashindwa kuingia darasani kutokana na kuumwa kwake.
Baadhi ya wanafunzi walisema kuwa baadhi ya walimu wa shule hiyo wamekuwa na tabia ya kupiga wanafunzi kupita kiasi huku wakati mwingine wakiwapiga ngumi, makofi, vichwa mateke na kuwachapa fimbo zisizo na idadi.
Jitihahada za kumpata mwalimu Nyalusi aliyehusika na tukio hilo hazikuweza kufanikiwa kwani alikuwa akihojiwa kwenye kituo cha polisi cha Mafinga kuhusiana na tukio hilo baada ya wanafunzi wa kidato cha sita kuandamana kwenda polisi kulalamika.
Hata hivyo  jitihada za kumpata mwalimu mkuu wa shule hiyo Mariano Mwanyingu hazikuweza kufanikiwa kwani hakuwepo shuleni hapo kwani aliondoka kabla ya tukio hilo kutokea na haifahamiki atarudi baada ya muda gani.
Kwa upande wake mkuu wa polisi wilaya ya Mufindi Ambwene Mwanyasi alikiri kupokelewa kwa mwalimu huyo ambaye alihusika na tukio hilo kwa ajili ya kuhojiwa.
Mwisho.
MWANAFUNZI wa kidato cha sita wa Shule ya Sekondari ya JJ Mungai iliyopo kwenye Halmashauri ya Mji wa Mafinga wilaya ya Mufindi mkoani Iringa  Octavian Luoga (20) amejeruhiwa kichwani kwa kupigwa fimbo na mwalimu wake kwa tuhuma za kushindwa kuingia darasani.
Akizungumza jana mjini Mafinga na waandishi wa habari mara baada ya kutoka kwenye Hospitali ya Mafinga wilaya ya Mufindi mkoani Iringa alipotoka kupatiwa matibabu mwanafunzi huyo amesema kuwa mbali ya kupigwa na fimbo kichwani pia alipigwa makofi na mateke.
Luoga amesema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya asubuhi Septemba  Mosi akiwa bwenini amepumzika kutokana na kuumwa na mishipa ya kichwa huku akiwa na wenzake wawili Wilson Due na Nsajigwa Moses ambao wote walikuwa wakiumwa jambo lililomfanya ashindwe kuingia darasani.
Amesema kuwa walimu wawili walikwenda na kumtaka aende ofisini kwa ajili ya kupewa adhabu kwani hakwenda darasani akawaambia anaumwa ndiyo sababu ya kushindwa kuingia darasani mara wakaanza kumpiga licha ya kuwaomba wamsikilize wakakataa wakasema amewajibu vibaya.
Amesema kuwa kutokana na kipigo hicho ikabidi aende ofisini na kufika kule akaanza kupigwa makofi,mateke na fimbo maeneo mbalimbali ya mwili na mwalimu mkuu msaidizi Huruma Nyalusi akidai kuwa nawadharau walimu.
Aidha amesema kuwa mwalimu alimpiga fimbo kichwani na damu zikaanza kumtoka hata hivyo hawakutaka kumpeleka hospitali ndipo wanafunzi wengine wakalazimisha apelekwe ambapo walienda polisi na baadaye hospitali kwa ajili ya matibabu nikashonwa nyuzi kadhaa.
Amesema kuwa walimu na wanafunzi wanafahamu matatizo yake na wiki moja iliyopita alilazwa kutokana na tatizo lake hilo hilo hali ambayo ilimfanya ashindwe kuingia darasani ambapo hata mahudhuria yake darasani ni mazuri lakini huwa anashindwa kuingia darasani kutokana na kuumwa kwake.
Baadhi ya wanafunzi wamesema kuwa baadhi ya walimu wa shule hiyo wamekuwa na tabia ya kupiga wanafunzi kupita kiasi huku wakati mwingine wakiwapiga ngumi, makofi, vichwa mateke na kuwachapa fimbo zisizo na idadi.
Jitihahada za kumpata mwalimu Nyalusi aliyehusika na tukio hilo hazikuweza kufanikiwa kwani alikuwa akihojiwa kwenye kituo cha polisi cha Mafinga kuhusiana na tukio hilo baada ya wanafunzi wa kidato cha sita kuandamana kwenda polisi kulalamika.
Hata hivyo  jitihada za kumpata mwalimu mkuu wa shule hiyo Mariano Mwanyingu hazikuweza kufanikiwa kwani hakuwepo shuleni hapo kwani aliondoka kabla ya tukio hilo kutokea na haifahamiki atarudi baada ya muda gani.
Kwa upande wake mkuu wa polisi wilaya ya Mufindi Ambwene Mwanyasi alikiri kupokelewa kwa mwalimu huyo ambaye alihusika na tukio hilo kwa ajili ya kuhojiwa.

  
  


No comments:

Post a Comment