Monday, September 21, 2015

SITA WAFA WANNE WAJERUHIWA

 Na John Gagarini, Mkuranga
WATU sita wamepoteza maisha na wanne kujeruhiwa baada ya basi dogo la abiria kugongana uso kwa uso na basi kubwa la kampuni ya Ibra.
Ajali hiyo ilitokea jana katika kijiji cha Njopeka wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani.
Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani Jafari Ibrahim alithibisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa katika ajali hiyo watu sita amekufa na wanne kujeruhiwa.
Ibrahim alisema basi hilo kubwa  lenye namba za usajili T 195 DCE aina ya YU TONG likiendeshwa na Alex Peter (46) liligongangana na gari ndogo iliyokua ikitokea Jaribu kuelekea Mbagala jijini Dar Es Salam lenye namba za  usajili T 782 DC.
Alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo kuwa ni dereva wa Basi la Ibra kuendesha zaidi kulia na hivyo kukutana uso kwa uso na kusababisha ajali hiyo.
Aidha alisema baada ya ajali hiyo wamelazimika kuweka askari katika eneo hilo, huku wakiwataka madereva kuwa makini na sheria za barabarani.
Ibrahim aliwasihi wananchi kutoa taarifa kwa Askari wa Usalama barabarani kwa namba zilizopo kwenye mabasi pindi wanapobaini kukiukwa kwa sheria za barabarani kabla ajali haijatokea.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment