Saturday, March 30, 2013

WALIMU WA RIADHA KUPEWA MAFUNZO


Na John Gagarini, Kibaha
IDARA ya Elimu na chama cha Riadha mkoa wa Pwani (RP) vimeandaa mafunzo kwa walimu wa mchezo wa riadha kutoka mikoa 10 kuanzia Aprili 6 hadi 17 mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Kibaha mkufunzi wa chama cha Riadha Tanzania (RT) Robert Kalyahe alisema kuwa mafunzo yatakuwa ya siku 10 na yatafanyika kwenye uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha –Tumbi.
Kalyahe alisema kuwa mafunzo hayo ya hatua ya kwanza yatasimamiwa na RT ambapo vyeti vya wahitimu vitatambuliwa na chama cha Riadha Duniani (IAAF).
“Washiriki watakuwa kutoka mikoa 10 walengwa zaidi wakiwa ni walimu wa shule za msingi, sekondari na wadau wengine wa mchezo huo sifa ikiwa ni elimu ya kidato cha nne na kuendelea,” alisema Kalyahe.
Alisema kuwa RT imeamua kushirikisha walimu zaidi kwani wao wana nafasi kubwa kuwaandaa wanafunzi shuleni na wakufunzi watakuwa ni Seleman Nyumbani, Samwel Tupa na yeye mwenyewe.
Kalyahe ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya ufundi ya mkoa wa Pwani alisema kuwa hadi sasa ni wadau 26 wamejitokeza kushiriki mafunzo hayo na kuwataka wadau wengi zaidi kujitokeza kupata elimu hiyo ili waweze kuendeleza mchezo huo.
Mwisho.
    

WANAKIJIJI WATAKA MAKUBALIANO

Na John Gagarini, Kibaha
WAKAZI wa Kijiji cha Gama wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wameitaka kampuni ya EcoEnergy ya Sweden inayotaka kuwekeza kilimo cha miwa kukaa pamoja ili kuingia makubaliano nao juu ya kuitumia ardhi yao  badala ya kuwatumia madalali wanaojifanya wanahusika na eneo hilo.
Wakizungumza Kijijini hapo jana kwenye mkutano wa hadhara uliaondaliwa na uongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Bagamoyo.
Moja ya wakazi wa Kijiji hicho Ramadhan Alawi alisema kuwa wao wanachokitaka ni kukaa meza moja na wao na si kuwatumia watu wa kati ambao hawahusiki na kuwasemea kwani ardhi hiyo ni vema kukawa na maelewano ya namna nao watakavyonufaika.
“Sisi hatukatai wawekezaji lakini tunachokitaka wawekezaji hao waje tukae meza moja na kukubaliana namna ya jinsi na sisi tutakavyoshiriki katika uwekezaji huo na hutataki watu wa kutusemea kwani sisi wenyewe tupo,” alisema Alawi.
Kwa upande wake Salum Yusuph alisema kuwa tatizo kubwa hapa ni wananchi kutoshirikishwa katika suala zima la uwekezaji huo kwa wakazi wa Kijiji chao na hawajui wao watanufaika vipi kwani waliambiwa waondoke kwenye eneo hilo.
“Hapa tunataka sisi na EcoEnergy tukae pamoja tukubaliane hasa ikizingatiwa kuwa hapa hatuna shule, zahanati wala huduma za kijamii na tungependa tuwe kama mashamba mengine ya Mtibwa na Kagera tukae tulime miwa wao waje kununua kwetu na si kutuondoa,” alisema Yusuph.
Akizungumzia suala hilo msimamizi wa wakulima wadogo wadogo wa kampuni hiyo Ian Sherry alisema kuwa wao wana lengo la kuwekeza katika kijiji hicho kwa manufaa ya wananchi na hawana lengo baya kwani kwenye vijiji walivyowekeza kupitia mradi huo wamenufaika na kuboresha huduma za kijamii.
“Wakazi wa eneo hili wasiwe na wasiwasi kwani taratibu zinafuatwa na kama kuna matatizo mambo yote yatawekwa sawa ili kuhakikisha manufaa ya mradi huo ambao utakuwa na uwekezaji mkubwa unaofikia zaidi ya bilioni saba,” alisema Sherry.
Naye mwenyekiti wa CCM wilaya ya Bagamoyo Shaibu Mtawa alisema kuwa kutokana na changamoto ya madai ya wananchi wataandaa mkutano baina ya pande zote hizo ili kuondoa tofauti zilizojitokeza.
Mtawa alisema kuwa hapa inaonekana wananchi hawajashirikishwa kikamilifu juu ya uwekezaji huo hivyo chama kitahakikisha mgogoro uliopo unamalizwa na kesi iliyo mahakamani inaondolewa ili kuleta mwafaka.
Mwisho.

DC ATAKA WLAIMU WAKAMATWE

Na John Gagarini, Bagamoyo
MWALIMU wa shule ya Msingi Msoga wilayani Bagamoyo mkoani Pwani anatuhumiwa kuwajaza mimba wanafunzi wa shule ya msingi na mwingine wa sekondari Msoga huku mwingne akifumaniwa na mwanafunzi.
Tuhuma hizo zilibainika wakati wa kikao cha pamoja kati ya wazee maarufu viongozi wa dini, wajumbe wa serikali ya Kijiji na watendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo na mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Ahmed Kipozi.
Mwalimu huyo alibainishwa kwenye kikao hicho ni Joel Mjema ambapo mwalimu mwingine ni Samwel Mjema yeye anatuhumiwa kufumaniwa na mwanafunzi wa sekondari ya Msoga lakini wazazi wa mwanafunzi huyo walilimaliza suala hilo kimya kimya.
Kutokana na tuhuma hizo ambazo zinawakabili walimu hao mkuu wa wilaya hiyo Kipozi alitaka walimu hao wakamatwe na kupelekwa kwenye vyombo vya kisheria ili hatua ziweze kuchukuliwa kutokana na matukio hayo.
Akizungumzia tuhuma za walimu hao Kipozi  alisema kuwa mwalimu Joel Mjema ana tuhuma za kumjaza mimba aliyekuwa mwanafunzi wa darasa la sita katika shule hiyo jina tunalo (Tatu Shaabani) hali iliyopelekea mwanafunzi huyo kushindwa kuendelea na masomo yake ya kuhitimu elimu ya msingi.
“Lakini kwa kuona hiyo haitoshi mwalimu huyo huyo akamjaza mimba na kupelekea kumkatisha  masomo mwanafunzi mwingine wa kidato cha tatu wa shule ya sekondari Lugoba na Latifa Shaaban,na kuamua kuishi naye kinyumba kitu ambacho ni kibaya sana kwa mwalimu aliyekabidhiwa dhima ya kulea watoto kimaadili,” alisema Kipozi.
Kuhusiana na mwalimu Samwel Mjema  alisema mwalimu huyo anatuhumiwa kutembea na mwanafunzi (Maimuna Hamis) ambapo alifumaniwa na wazazi wa binti huyo na kitu cha kushangaza suala hio lilimalizwa kimya kimya baina ya mwalimu huyo na wazazi na binti hali aliyosema haikubaliki  na kuagiza mara moja kuchukuliwa hatua kwa wazazi wote ambao wamekuwa wakifikia makubaliano ya kuvunja sheria.
Kipozi alisema kuwa walimu hao kwa nyakati tofauti wamekuwa wakikiuka maadili na kanuni za utumishi kwa kufanya ngono na wanafunzi wao kitu ambacho ni kinyume na kanuni na taratibu za utumishi na sheria za nchi.
“Kwa ujumla hatuwezi kuvumilia uchafu huu wa mtu anayepaswa kuheshimiwa kama mwalimu kuamua kuanza kuwashawishi na kufanya ngono na wanafunzi wake lakini mbaya zaidi ni kuwakatishia masomo watoto hao hivyo naagiza mara moja kukamatwa kwa walimu hao na kufikishwa katika mikono ya sheria,” alisema Kipozi.
Hata hivyo taarifa zilizotufikia zinasema kuwa mwalimu Samwel Mjema alikamatwa kuhusiana na tukio lake na kutarajiwa kufikishwa mahakamani huku mwalimu Joel Mjema akitoroka kuhusiana na tuhuma hizo zinazomkabili.
Mwisho.

Monday, March 25, 2013

WAIPONGEZA STARS


Na John Gagarini, Kibaha
WADAU wa soka mkoani Pwani wameipongeza timu ya Taifa kwa kuifunga Moroco kwa magoli 3-1 kwenye mchezo wa kufuzu kushiriki kombe la Dunuia nchini Brazil 2014 uliofanyika juzi kwenye uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na gazeti hili mjinin Kibaha moja ya wadau wa soka mkoani Pwani ambaye ni Mjumbe wa halmashauri Kuu ya Taifa Kibaha Mjini, Rugemalila Rutatina alisema kuwa timu hiyo imeonyesha kiwango kizuri kwa kuweza kukiangusha kigogo cha soka Barani Afrika.
Rutatina alisema kuwa Stars walionyesha mchezo mzuri ambao uliwavutia watu waliokwenda kuutazama na kusema sasa matumaini yameanza kuonekana kwenye soka la Tanzania.
“Tunawapongeza Vijana kwa kuonyesha kuwa wanaweza kwani waitoa Tanzania kimasomaso kwa kuwapa raha Watanzania kwa kuifunga Moroco ambao miaka ya nyuma walikuwa ni moja ya timu vigogo barani Afrika kutokana na uwezo wake kisoka,” alisema Rutatina.
Alisema kuwa miaka ya nyuma Watanzania walikuwa wakisikitishwa na matokeo yaliyokuwa yakitokea uwanjani kutokana na timu kufungwa mbele ya mashabiki wake lakini sasa wameweza kuibuka kidedea.
“Kwa kweli vijana wameitoa nchi kimasomaso na hichi ndicho Watanzania walichokuwa wakikitaka kwa miaka mingi tunawaomba wasibweteke na ushindi huu bali waongeze jitihada kwa kujituma zaidi kwenye michezo ijayo ili kwa mara ya kwanza Tanzania iweze kuingia kwenye ramani ya soka kwa kuingia kwenye kombe la dunia,” alisema Rutatina.
Aidha alisema kuwa jukumu lililobaki kwa shirikisho la soka nchini (TFF) ni kuitafutia Stars michezo mingi ya kirafiki hasa nje ya nchi ili kuwpaa uzoefu wachezaji hasa wale ambao bado hawajawa na uzoefu kwa michuano ya kimataifa.
“Stars itakuwa na michezo mingine ya nje hivyo lazima wachezaji wapate uzoefu mkubwa kama tunavyojua michezo ya ugenini huwa ni migumu kutokana na timu husika kutumia mazingira ya nyumbani kushinda,” alisema Rutatina.
Aliwataka wachezaji wa Stars kulinda viwnago vyao ili visishuke na kusababisha timu kufanya vibaya kwani bado kuna michezo migumu mbele yao ili kufuzu kucheza kombe la dunia.
Mwisho. 

 Na John Gagarini, Kibaha
BONDIA chipukizi Zumba Kukwe kutoka wilayani Kibaha mkoani Pwani anatarajiwa kupanda ulingoni dhidi ya Joseph Mbowe wa Jijini Dar es Salaam Aprili 7 mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini kibaha bondia huyo maarufu kama Chenchidola alisema kuwa pambano hilo litafanyika kwenye ukumbi wa CCM Mwinjuma Mwananyamala Jijini Dar es Salaam.
Chenchidola alisema kuwa pambano lao hilo litakuwa ni la utangulizi kabla ya pambano la kugombea ubingwa kati ya Shaban Madilu na Issa Omary.
“Mchezo huo utakuwa ni wa kujiweka sawa kwani malengo ni kucheza kwenye mashindano mbalimbali lakini kwa sasa nafanya mapambano ya kujipima nguvu ili kujiimarisha kabla ya kukutana kuwania ubingwa,” alisema Chenchidola.
Alisema kuwa kwa sasa yuko imara kupambana na bondia yoyote hapa nchini lakini kabla ya kufikia kupambana na mabingwa lazima ajiweke sawa.
“Natarajia kumpiga kwenye raundi ya pili au ya tatu na si zaidi ya hapo hivyo akae sawa kwani nimejiandaa vilivyo katika mchezo huo na endapo atanipiga basi itabidi niombe pambano la marudiano,” alisema Chenchidola.
Aidha alisema kuwa lengo lake ni kupigana kwenye mapambano ya ubingwa ambapo kwa sasa anatarajia kupambana na bondia mkubwa hapa nchini ili awaonyeshe Watanzania kuwa anaweza.
Aliwataka mapromota kujitokeza kuwasaidia chipukizi ili nao waweze kufikia kwenye viwango vya juu kwani wengi wako hasa mikoani lakini hawapati nafasi.
Mwisho.    

   
   

HABARI ZA P;WANI

 Na John Gagarini, Kibaha
KAMATI za Maadili kwenye klabu za waandishi wa habari nchini zimetakiwa kutumia busara katika kuwapatanisha waandishi na wadau mara kunapotokea migongano baina yao ili kumaliza pasipo kwenda mahakamani kuepusha vyombo vya habari kutozwa faini kubwa.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na ofisa kutoka baraza la habari Tanzania (MCT) Asterius Banzi wakati wa mafunzo ya siku moja kwa kamati ya maadili ya Chama Cha Waandishi wa habari mkoani Pwani (CRPC) yaliyofanyika kwenye ofisi za chama hicho.
Banzi alisema kuwa ni vema kamati hizo zikatumia uungwana kutatua migogoro kwani endapo malalamiko hayo yatapelekwa mahakamani athari zake ni kubwa hasa kwa upande wa vyombo vya habari kupigwa faini kubwa ambazo zitasababisha vyombo hivyo kufungwa.
“Baadhi ya walalamikaji wamedai fidia kubwa kwa vyombo vya habari na kupeleka vyombo hivyo kufungwa au kuyumba na kushindwa kuhudumia wananchi kupata taarifa ikiwa ni moja ya haki zao za msingi za kikatiba,” alisema Banzi.
Aidha alisema kuwa ni vema mambo hayo yakatatuliwa kirafiki kwani endapo yakifikishwa mahakamani athari zake ni kubwa kuliko yangemalizwa kwenye kamati hizo.
Pia alivitaka baadhi ya vyombo vya habari ambavyo vinakutana na matatizo ya kuwachafua wadau wao ndani ya jamii kukubali kukaa meza moja na walalamikaji ili kufikia muafaka kwa kujenga mahusiano mazuri.Banzi alisema kuwa vyombo vya habari na wananchi ni marafiki hivyo lazima kuwe na mahusiano mazuri kwa pande zote ili kuepuka migogoro isiyo na lazima.
Katika hatua nyingine kamati hiyo imemchagua wakili wa kujitegemea Saiwelo Kumwenda kuwa mwenyekiti wa kamati hiyo ambayo imetuliwa na chama hicho.
Nafasi ya makamu mwenyekiti ilikwenda kwa Elizabeth Ngai huku katibu wa kamati hiyo akiwa ni Athuman Mtasha.
Kamati hizo kwenye klabu za waandishi wa habari ziliundwa kwa lengo la kusuluhisha migogoro baina ya wanahabari na wadau ili kuzingatia maadili ya kazi za waandishi wa habari.
Mwisho.
 
Na John Gagarini, Kibaha
MBUNGE wa Jimbo la Kibaha Mjini mkoani Pwani Silvestry Koka amewataka waandishi wa habari mkoani humo kujiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwenye kambi ya Ruvu uiliyopo Mlandizi wilayani Kibaha yanayotarajiwa kuanza wakati wowote ili kujiimarisha kikakamavu na kujenga uzalendo wa nchi yao.
Aliyasema hayo hivi karibuni aliopoongea na waandishi wa habari mjini Kibaha na kusema kuwa mafunzo ya JKT ni muhimu hasa ikizingatiwa yanamfanya mshiriki kujua uzalendo wa nchi yake kama wanavyotarajia kwenda baadhi ya wabunge mafunzo hayo yatakapoanza.
Koka alisema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa watu wa aina yote na si kwa baadhi ya watu kwani waandishi wataweza kuielezea vizuri nchi yao pale watakapokuwa wakiandika habari zao.
“Kazi ya uandishi ni sawa na ya jeshi hivyo endapo watapata mafunzo hayo yatawasaidia kwa kiasi kikubwa katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku ambapo wamekuwa wakikutana na changamoto kubwa,” alisema Koka.
Aidha alisema kuwa kwa kipindi hichi waandishi wamekuwa wakishambuliwa hivyo endapo watapata mafunzo hayo yatawasaidia kujilinda na baadhi ya watu ambao wamekuwa wakiwateka waandishi na kuwadhuru.
“Zamani watu wengi walipitia mafunzo hayo kwa mujibu wa sheria hivyo kwa sasa kwa kuwa serikali imerejesha mafunzo hayo na waandishi nao wajitokeze ili waweze kupata mafunzo ambayo ni mazuri katika kuuweka mwili vizuri pia kuweza kujilinda,” alisema Koka.
Alibainisha kuwa waandishi kama baadhi ya wabunge waliojitokeza kushiriki mafunzo hayo nao wajitokeze, hivi karibuni serikali ilirudisha utaratibu wa mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria kuanzia mwaka huu.
Katika hatua nyingine alilaani baadhi ya watu ambao wamekuwa wakiwashambulia waandishi na kusema kuwa kufanya hivyo ni kunyanganya uhuru wa vyombo vya habari katika kufanya kazi zao.
Alisema inashangaza kuona waandishi wanashambuliwa pasipokuwa na sababu za msingi na kuwasababisha kufanya kazi zao kwa woga kuhofiwa kupigwa.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC-CCM) kutoka wilaya ya Kibaha mkoani Pwani Rugemalila Rutatina amewataka vijana kwenye wilaya hiyo kukitumia chuo cha ufundi Stadi (VETA) kilichopo wilayani humo ili kujiongezea ujuzi kuliko kuwaachia vijana kutoka mikoa mingine kusoma kwenye chuo hicho.
Aliyasema hayo hivi karibuni mjini Kibaha alipokutana na baadhi ya vijana kutoka kata mbalimbali kwenye wilaya ya Kibaha, kuzungumzia masuala ya kuboresha mazingira katika wilaya hiyo na kusema kuwa vijana wengi hawakitumii chuo hicho ambacho kimejengwa eneo la Kongowe.
Rutatina alisema kuwa inashangaza kuona vijana kwenye wilaya na mkoa wa Pwani kutokitumia chuo hicho licha ya wao kuwa jirani na chuo hicho huku vijana wengi kutoka mikoa mbalimbali nchini wakiwa wanakitumia ipasavyo chuo hicho.
“Changamoto kubwa inaonekana ni vijana wengi kutokukitambua chuo hicho kutokana na kukosa taarifa za uwepo wake jambo ambalo linawafanya washindwe kujiunga nacho hivyo vijana wanapaswa kutafuta taarifa na si kusubiri vijana toka nje ya mkoa wajae na kuanza kulalamika,” alisema Rutatina.
Alisema kuwa hiyo ni fursa ambayo vijana wa Kibaha na mkoa wanapaswa kuitumia kwani hata kama hawajafanikiwa kusoma masomo ya sekondari wana nafasi ya kujiunga na chuo hicho ambacho kinawapatia stadi za ufundi mbalimbali.
“Kama tujuavyo ufundi ni muhimu kwani kila kitu kinauhusiano na ufundi hivyo taaluma ya ufundi haiwezi kuepukika kwa maendeleo ya jambo lolote na hiyo ndiyo itakayowasaidia vijana katika mkoa wa Pwani kujikwamua na hali ngumu ya kiuchumi,” alisema Rutatina.
Aidha alisema kwamba hata masuala ya biashara na ujasiriamali yanafundishwa ambapo vijana wengi kwa sasa wamejiajiri na endapo watapata mafunzo ya chuo hicho wataweza kupata ujuzi na kuboresha shughuli zao.
“Maisha mazuri hayawezi kuja bila ya kujishughulisha kwani wakijiunga na mafunzo ya VETA wataweza kujiajiri na kukabiliana na tatizo la ajira kwa vijana kwani wataweza kujiajiri kupitia elimu watakayokuwa wameipata kwenye chuo hicho,” alisema Rutatina. Chuo hicho kilizinduliwa mwaka jana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Mwisho. 

Na John Gagarini, Kibaha
WAKAZI zaidi ya 1,500 wa Mtaa wa Zogowale, Kibaha Mjini mkoani Pwani, wanatarajia kunufaika na mradi wa maji ambao una uwezo wa kutoa maji lita 6,000 kwa saa.

Akizungumzia mradi huo wakati wa uzinduzi wa mradi huo ,mhandisi wa maji katika halmashauri ya mji wa Kibaha Grace Lyimo alisema idadi hiyo ya watakaonufaika ni sawa na asilimia 1.4 ya wananchi wa Kibaha Mjini hivyo kufanya jumla ya wanaopata maji kuwa ni asilimia 64.

Lyimo  alisema kuwa  ujenzi wa miundombinu ya mradi ulianza rasmi Mei 2012 na kukamilika mwaka huu kwa gharama ya zaidi ya shilingi Milioni 192 ambapo mkandarasi ameshakabidhiwa zaidi ya milioni 156 hadi sasa.

“Mradi  wa maji Zogowale uliibuliwa na jamii yenyewe na
wananchi walipaswa kuchangia zaidi ya milioni Nne ikiwa ni asilimia
2.5 ya gharama ya ujenzi ambapo waliweza kuchangia milioni moja na
laki saba na arobaini na tano, miasaba sabini na tano,” alisema Lyimo.

Aidha alisema kwa sasa mkandarasi anaendelea na umaliziaji wa kazi
ndogondogo zinazojitokeza na mfumo wa maji upo kwenye uangalizi kwa miezi sita.
Aliwataka wananchi kulinda miundombinu hiyo ya maji ili huduma hiyo iwe ya uhakika kwa lengo la kuondokana na kero ya maji katika mtaa huo.
Mwisho

Sunday, March 24, 2013

STORY ZA PWANI


 Na John Gagarini, Kibaha
KAMATI za Maadili kwenye klabu za waandishi wa habari nchini zimetakiwa kutumia busara katika kuwapatanisha waandishi na wadau mara kunapotokea migongano baina yao ili kumaliza pasipo kwenda mahakamani kuepusha vyombo vya habari kutozwa faini kubwa.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na ofisa kutoka baraza la habari Tanzania (MCT) Asterius Banzi wakati wa mafunzo ya siku moja kwa kamati ya maadili ya Chama Cha Waandishi wa habari mkoani Pwani (CRPC) yaliyofanyika kwenye ofisi za chama hicho.
Banzi alisema kuwa ni vema kamati hizo zikatumia uungwana kutatua migogoro kwani endapo malalamiko hayo yatapelekwa mahakamani athari zake ni kubwa hasa kwa upande wa vyombo vya habari kupigwa faini kubwa ambazo zitasababisha vyombo hivyo kufungwa.
“Baadhi ya walalamikaji wamedai fidia kubwa kwa vyombo vya habari na kupeleka vyombo hivyo kufungwa au kuyumba na kushindwa kuhudumia wananchi kupata taarifa ikiwa ni moja ya haki zao za msingi za kikatiba,” alisema Banzi.
Aidha alisema kuwa ni vema mambo hayo yakatatuliwa kirafiki kwani endapo yakifikishwa mahakamani athari zake ni kubwa kuliko yangemalizwa kwenye kamati hizo.
Pia alivitaka baadhi ya vyombo vya habari ambavyo vinakutana na matatizo ya kuwachafua wadau wao ndani ya jamii kukubali kukaa meza moja na walalamikaji ili kufikia muafaka kwa kujenga mahusiano mazuri.Banzi alisema kuwa vyombo vya habari na wananchi ni marafiki hivyo lazima kuwe na mahusiano mazuri kwa pande zote ili kuepuka migogoro isiyo na lazima.
Katika hatua nyingine kamati hiyo imemchagua wakili wa kujitegemea Saiwelo Kumwenda kuwa mwenyekiti wa kamati hiyo ambayo imetuliwa na chama hicho.
Nafasi ya makamu mwenyekiti ilikwenda kwa Elizabeth Ngai huku katibu wa kamati hiyo akiwa ni Athuman Mtasha.
Kamati hizo kwenye klabu za waandishi wa habari ziliundwa kwa lengo la kusuluhisha migogoro baina ya wanahabari na wadau ili kuzingatia maadili ya kazi za waandishi wa habari.
Mwisho.
 
Na John Gagarini, Kibaha
MBUNGE wa Jimbo la Kibaha Mjini mkoani Pwani Silvestry Koka amewataka waandishi wa habari mkoani humo kujiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwenye kambi ya Ruvu uiliyopo Mlandizi wilayani Kibaha yanayotarajiwa kuanza wakati wowote ili kujiimarisha kikakamavu na kujenga uzalendo wa nchi yao.
Aliyasema hayo hivi karibuni aliopoongea na waandishi wa habari mjini Kibaha na kusema kuwa mafunzo ya JKT ni muhimu hasa ikizingatiwa yanamfanya mshiriki kujua uzalendo wa nchi yake kama wanavyotarajia kwenda baadhi ya wabunge mafunzo hayo yatakapoanza.
Koka alisema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa watu wa aina yote na si kwa baadhi ya watu kwani waandishi wataweza kuielezea vizuri nchi yao pale watakapokuwa wakiandika habari zao.
“Kazi ya uandishi ni sawa na ya jeshi hivyo endapo watapata mafunzo hayo yatawasaidia kwa kiasi kikubwa katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku ambapo wamekuwa wakikutana na changamoto kubwa,” alisema Koka.
Aidha alisema kuwa kwa kipindi hichi waandishi wamekuwa wakishambuliwa hivyo endapo watapata mafunzo hayo yatawasaidia kujilinda na baadhi ya watu ambao wamekuwa wakiwateka waandishi na kuwadhuru.
“Zamani watu wengi walipitia mafunzo hayo kwa mujibu wa sheria hivyo kwa sasa kwa kuwa serikali imerejesha mafunzo hayo na waandishi nao wajitokeze ili waweze kupata mafunzo ambayo ni mazuri katika kuuweka mwili vizuri pia kuweza kujilinda,” alisema Koka.
Alibainisha kuwa waandishi kama baadhi ya wabunge waliojitokeza kushiriki mafunzo hayo nao wajitokeze, hivi karibuni serikali ilirudisha utaratibu wa mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria kuanzia mwaka huu.
Katika hatua nyingine alilaani baadhi ya watu ambao wamekuwa wakiwashambulia waandishi na kusema kuwa kufanya hivyo ni kunyanganya uhuru wa vyombo vya habari katika kufanya kazi zao.
Alisema inashangaza kuona waandishi wanashambuliwa pasipokuwa na sababu za msingi na kuwasababisha kufanya kazi zao kwa woga kuhofiwa kupigwa.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC-CCM) kutoka wilaya ya Kibaha mkoani Pwani Rugemalila Rutatina amewataka vijana kwenye wilaya hiyo kukitumia chuo cha ufundi Stadi (VETA) kilichopo wilayani humo ili kujiongezea ujuzi kuliko kuwaachia vijana kutoka mikoa mingine kusoma kwenye chuo hicho.
Aliyasema hayo hivi karibuni mjini Kibaha alipokutana na baadhi ya vijana kutoka kata mbalimbali kwenye wilaya ya Kibaha, kuzungumzia masuala ya kuboresha mazingira katika wilaya hiyo na kusema kuwa vijana wengi hawakitumii chuo hicho ambacho kimejengwa eneo la Kongowe.
Rutatina alisema kuwa inashangaza kuona vijana kwenye wilaya na mkoa wa Pwani kutokitumia chuo hicho licha ya wao kuwa jirani na chuo hicho huku vijana wengi kutoka mikoa mbalimbali nchini wakiwa wanakitumia ipasavyo chuo hicho.
“Changamoto kubwa inaonekana ni vijana wengi kutokukitambua chuo hicho kutokana na kukosa taarifa za uwepo wake jambo ambalo linawafanya washindwe kujiunga nacho hivyo vijana wanapaswa kutafuta taarifa na si kusubiri vijana toka nje ya mkoa wajae na kuanza kulalamika,” alisema Rutatina.
Alisema kuwa hiyo ni fursa ambayo vijana wa Kibaha na mkoa wanapaswa kuitumia kwani hata kama hawajafanikiwa kusoma masomo ya sekondari wana nafasi ya kujiunga na chuo hicho ambacho kinawapatia stadi za ufundi mbalimbali.
“Kama tujuavyo ufundi ni muhimu kwani kila kitu kinauhusiano na ufundi hivyo taaluma ya ufundi haiwezi kuepukika kwa maendeleo ya jambo lolote na hiyo ndiyo itakayowasaidia vijana katika mkoa wa Pwani kujikwamua na hali ngumu ya kiuchumi,” alisema Rutatina.
Aidha alisema kwamba hata masuala ya biashara na ujasiriamali yanafundishwa ambapo vijana wengi kwa sasa wamejiajiri na endapo watapata mafunzo ya chuo hicho wataweza kupata ujuzi na kuboresha shughuli zao.
“Maisha mazuri hayawezi kuja bila ya kujishughulisha kwani wakijiunga na mafunzo ya VETA wataweza kujiajiri na kukabiliana na tatizo la ajira kwa vijana kwani wataweza kujiajiri kupitia elimu watakayokuwa wameipata kwenye chuo hicho,” alisema Rutatina. Chuo hicho kilizinduliwa mwaka jana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Mwisho. 

Na John Gagarini, Kibaha
WAKAZI zaidi ya 1,500 wa Mtaa wa Zogowale, Kibaha Mjini mkoani Pwani, wanatarajia kunufaika na mradi wa maji ambao una uwezo wa kutoa maji lita 6,000 kwa saa.

Akizungumzia mradi huo wakati wa uzinduzi wa mradi huo ,mhandisi wa maji katika halmashauri ya mji wa Kibaha Grace Lyimo alisema idadi hiyo ya watakaonufaika ni sawa na asilimia 1.4 ya wananchi wa Kibaha Mjini hivyo kufanya jumla ya wanaopata maji kuwa ni asilimia 64.

Lyimo  alisema kuwa  ujenzi wa miundombinu ya mradi ulianza rasmi Mei 2012 na kukamilika mwaka huu kwa gharama ya zaidi ya shilingi Milioni 192 ambapo mkandarasi ameshakabidhiwa zaidi ya milioni 156 hadi sasa.

“Mradi  wa maji Zogowale uliibuliwa na jamii yenyewe na
wananchi walipaswa kuchangia zaidi ya milioni Nne ikiwa ni asilimia
2.5 ya gharama ya ujenzi ambapo waliweza kuchangia milioni moja na
laki saba na arobaini na tano, miasaba sabini na tano,” alisema Lyimo.

Aidha alisema kwa sasa mkandarasi anaendelea na umaliziaji wa kazi
ndogondogo zinazojitokeza na mfumo wa maji upo kwenye uangalizi kwa miezi sita.
Aliwataka wananchi kulinda miundombinu hiyo ya maji ili huduma hiyo iwe ya uhakika kwa lengo la kuondokana na kero ya maji katika mtaa huo.
Mwisho

Tuesday, March 12, 2013

UTENDAJI KAZI MAZOEA UNAANGAMIZA TAIFA

Na John Gagarini, Kibaha

IMEELEZWA kuwa utendaji kazi wa mazoea umesababisha Taifa kushindwa kusonga mbele katika kuwaletea maendeleo wananchi kutokana na utendaji wa mazoea wa baadhi ya viongozi na wafanyakazi.

Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Alafayo Kidata naibu katibu mkuu Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa (TAMISEMI), alipokuwa akizungumza na viongozi wa Shirika la Elimu Kibaha (KEC) baada ya ziara aliyoifanya kulitembelea Shirika hilo la Umma.

Kidata alisema kuwa baadhi ya watendaji kazi hasa kwenye mashirika na taasisi za serikali wamekuwa hawafanyi kazi ipasavyo na kufanya kazi kwa mazoea hali ambayo imekuwa haileti tija kwa maendeleo ya nchi.

"Tunapaswa kubadilika kama kweli tunataka kuleta mabadiliko ndani ya nchi yetu hatuwezi kufanya kazi kwa mazoea tu lazima kuwe na uwajibikaji vinginevyo tutazidi kulididimiza Taifa," alisema Kidata.

Alisema kuwa kwa upande wa mashirika ya Umma uzalishaji wake umekuwa ukishuka siku hadi siku kutokana na kutowajibika ipasavyo tofauti na mashirika binafsi ambayo yako makini katika utendaji kazi wake.

"Mashirika na taasisi binafsi zimekuwa zikifanikiw akutokana na kuwa makini katika utendaji kazi lakini kwa mashirika na taasisi za serikali hali imekuwa kinyume hii yote ni kutokana na watu kutowajibika ipasavyo," alisema Kidata.

Aidha alisema kwenye taasisi za Umma mfanyakazi anaweza kukaa mwezi mzima hajafanya kazi lakini mshahara unaingia kupitia ATM lakini hakuna mtu anayehoji je uwajibikaji hapo utakuwepo.

"Lazima wafanyakazi wa wajibike ipasavyo na kufanya kazi kama anavyoweza kuwajibika kwenye shughuli yake binafsi na uzalishaji wa kiwango kikubwa ndiyo utakaowaondoa kwenye matatizo mliyonayo hasa ya madeni," alisema Kidata.

Naye mkurugenzi wa KEC Dkt Cyprian Mpemba alisema kuwa changamoto kubw ailiyopo kwenye shirika hilo ni ukosefu wa fedha na madeni makubwa ya watumishi na watoa huduma katika shirika hilo ambalo lilianzishwa miaka ya 70.

mwisho.