Thursday, March 20, 2025

TCRA KUSHIRIKIANA NA TBN KUSADIA KUZALISHA MAUDHUI YENYE TIJA

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeahidi kufanyakazi na Mtandao wa Wana Blogu Tanzania (TBN) pamoja na vyama vingine vya waandishi wa habari ambavyo vinawakilisha mahitaji na matakwa ya wanachama wao.

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe  19 Machi 2025 Jijini Dar es Salaam na Meneja wa Huduma za Utangazaji wa TCRA, Mhandisi Andrew Kisaka, alipokutana na ujumbe wa TBN ofisini kwake, katika kikao cha kujadiliana changamoto mbalimbali zinazowakabili Bloga nchini.

“Sisi huwa tunapenda kufanya kazi na vyama ambavyo vinawakilisha mahitaji na matakwa ya wanachama wao, badala ya kufanyakazi na mwaandishi mmoja mmoja…tunafurahi sana kufanyakazi na waandishi kupitia vyama vyao,” amesema Mhandisi Kisaka.

Mhandisi Kisaka amesema kuwa TCRA imefurahi kukutana na TBN kwa kuwa wanafahamu kuwa Bloga wanasehemu kubwa sana kwenye maudhui ya ndani, na hata kwenye usajili wa TCRA Bloga wanachukua nafasi kubwa sana katika maudhui ya mtandaoni.

“Kwa hiyo TBN mtakuwa silaha moja wapo nzuri sana yakutuwezesha sisi kama Mamlaka ya Mawasiliano nchini, tunao simamia utangazaji pamoja na maudhui ya mtandaoni kuwa karibu na nyinyi na kuhakikisha maudhui ya mtandaoni yanaleta tija na maendeleo kwa wananchi,” amesema Mhandisi Kisaka.

Friday, March 14, 2025

RAIS MSTAAFU DK KIKWETE AFANYA ZIARA NCHINI JAPAN KUIMARISHA USHIRIKIANO KATI YA BODI YA SHIRIKA LA ELIMU LA KIMATAIFA (GPE) NA JAPAN


Rais mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa  Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Elimu la Kimataifa (GPE), yupo Tokyo nchini Japan kwa ziara maalum yenye lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya GPE na serikali ya Japan katika kutatua changamoto za elimu ya msingi katika nchi zinazoendelea.

Katika siku yake ya kwanza Tokyo, Dkt. Kikwete amefanya mazungumzo na Waziri wa Fedha wa Japan, Mhe. Shin-ichi Yokohama, pamoja na Naibu wake, Mhe. Atsushi Mimura. 

Mazungumzo hayo yalijikita katika ushirikiano wa kifedha ili kusaidia miradi ya elimu inayosimamiwa na GPE, ikiwemo upatikanaji wa rasilimali kwa ajili ya kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa watoto wa nchi zinazoendelea.

Baada ya mazungumzo hayo, Rais Mstaafu Kikwete alikutana na Bw. Akihiko Tanaka, Rais wa Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Japan (JICA). 

Shirika hili limekuwa na mchango mkubwa katika miradi ya maendeleo barani Afrika, na mazungumzo yalihusu namna JICA inaweza kusaidia jitihada za GPE katika kukuza elimu bora.

Dkt. Kikwete pia alikutana na Bw. Yohei Sasakawa, Mwenyekiti wa Taasisi ya Nippon. Bw. Sasakawa, mwenye umri wa miaka 86, ni mtu mashuhuri wa kusaidia miradi ya kijamii duniani. 

Katika mazungumzo yao, waligusia nafasi ya sekta binafsi katika kusaidia elimu, hasa kupitia taasisi zisizo za kiserikali. Vilevile, Bw. Sasakawa alishangaza dunia baada ya kufanikisha kupanda Mlima Kilimanjaro tarehe 12 Februari 2024, kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 85 ya kuzaliwa kwake – hatua inayothibitisha kuwa umri si kikwazo kwa ndoto kubwa.

Katika siku zinazofuata, Rais Mstaafu Kikwete anatarajiwa kukutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Mhe. T. Miyaji, pamoja na wabunge wa Bunge la Japan, ambapo ajenda kuu itakuwa nafasi ya elimu na teknolojia katika maendeleo ya jamii.

Pia, atashiriki mijadala maalum kuhusu elimu na teknolojia, kufanya mahojiano na vyombo vya habari, pamoja na kukutana na Mhe. Tetsuro Yano, Rais wa Taasisi ya AFRECO, ambayo inahusika na kukuza ushirikiano kati ya Japan na Afrika.

Ziara hii ni sehemu ya juhudi endelevu za Dkt. Kikwete katika kuboresha mifumo ya elimu duniani, hasa katika nchi zinazoendelea. 

Japan ni mshirika muhimu wa maendeleo ya elimu barani Afrika, na ushirikiano huu unaweza kuwa na mchango mkubwa katika kuhakikisha watoto wengi zaidi wanapata fursa ya elimu bora.

 


Thursday, March 13, 2025

KIWANDA CHA KEDS CHATOA MSAADA KWA WANAWAKE

KIWANDA cha kuzalisha sabuni cha Keds Tanzania Company Ltd cha Kibaha Mkoani Pwani kimetoa misaada ya sabuni kwa wanawake wa Mtaa wa Lulanzi ambao uko jirani na kiwanda hicho ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya sherehe ya siku ya wanawake Duniani.

Akizungumza kiwandani hapo mara baada ya kukabidhi msaada hiyo Mkurugenzi wa Kiwanda hicho Bob Cheng amesema kuwa wanaungana na jamii katika kusaidia wanawake ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya sherehe hizo.

Cheng amesema kuwa wamewapatia misaada hiyo ikiwa ni sehemu ya kuenzi mchango wa wanawake ambao ni mkubwa katika kuleta maendeleo kwenye jamii.

"Kiwanda kinaungana na wanawake katika maadhimisho haya hivyo tumeona turudishe kwa jamii ikiwa ni katika ushirikiano na wananchi katika kuleta maendeleo,"amesema Cheng.

Amesema kuwa kiwanda kitaendelea kushirikiana na jamii katika masuala mbalimbali ya maendeleo hususani kwa wananchi walio jirani na kiwanda na wananchi wote kwa ujumla.

Akishukuru kwa msaada huo wa sabuni za unga na vipande Jasmini Issa amesema kuwa wanashukuru kwa msaada huo kwani utawasaidia katika matumizi ya kila siku.

Issa amesema kuwa msaada huo umeonyesha jinsi kiwanda hicho kinavyoshirikiana na jamii katika suala zima la maendeleo ambapo wamekuwa wakisaidia miradi mbalimbali inayohusu wananchi.

Naye Meri Mkwizu amesema kuwa sabuni ni muhimu sana kwa familia na ni moja ya vitu muhimu katika mahitaji kwenye familia na hutumika muda wote.

Mkwizu amesema kuwa sabuni ina bajeti kubwa kutokana na matumizi yake ikiwa ni pamoja na kufulia nguo, kuoshea vyombo, kuogea na kufanyia usafi wa aina mbalimbali ambapo jumla ya wanawake 89 walipewa msaada huo.

KEDS KUENDELEA KUZALISHA BIDHAA BORA

KIWANDA cha Keds Tanzania Company Ltd kimesema kitaendelea kuzalisha bidhaa zenye ubora na bei nafuu kulingana na hali ya soko.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Mkurugenzi wa kiwanda hicho Bob Cheng alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.

Cheng amesema kuwa katika utengenezaji wa bidhaa zao wanazingatia ubora ili kuendelea kuwa na soko kwa kuwapatia wananchi kitu kilicho bora.

"Malengo ya kuanzishwa kiwanda ni kukuza uchumi wa wananchi kwa kutoa ajira kwa watu wengi pia kutengeneza bidhaa bora zinzokubalika,"amesema Cheng.

Amesema kuwa malengo yao ni kutengeneza bidhaa nyingine lakini kwa sasa wanafanya kwanza utafiti ili kujua ni bidhaa gani watakayoizalisha.

"Kiwanda kinajihusisha na uzalishaji wa sabuni za unga, vipande, pampasi na pedi za akinamama na kinashirikiana na serikali kwa kufuata taratibu zote za kisheria,"amesema Cheng.

Aidha amesema kuwa kiwanda kinashirikiana na jamii kwa kurudisha kwa jamii kwa kusaidia kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni pamoja na kwenye sekta za elimu, afya, barabara na sekta mbalimbali.

"Kuhusu maji yanayotoka kiwandani hayana athari zozote za kiafya na kimazingira ambapo hata wafanyakazi wetu wanaishi jirani na kiwanda ni asilimia 60 hivyo hayana tatizo lolote,"amesema Cheng.

Kiwanda hicho kinauza bidhaa zake kote nchini pamoja na nchi za jirani baadhi zikiwa ni Uganda, Kenya na Malawi.







TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA (THBUB) YATEMBELEA VIWANDA PWANI

TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imefanya ziara kutembelea viwanda kuangalia uzingatiwaji wa haki za binadamu ili zisivunjwe

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Kamishna wa Tume Nyanda Shuli wakati wa ziara ya kutembelea viwanda ili kufanya uchunguzi kujua kama kuna changamoto za uvunjifu wa haki.

Shuli amesema kuwa baadhi ya viwanda vimekuwa vikilalamikiwa kuvunja haki za binadamu kwa unyanyasaji wa wafanyakazi, uchafuzi taka maji na haki mbalimbali.

"Lengo la ziara ni kuangalia hali ya haki za binadamu na uzingatiwaji wa misingi ya utawala bora kuangalia usalama wa mazingira ya kazi na uzingatiaji wa viwango vya ajira,"amesema Shuli.

Amesema kuwa malalamiko waliyoyapokea watayafanyia kazi na kutoa majibu jambo kubwa ni kuona haki inatendeka ili kuondokana na uvunjifu wa haki za binadamu.

Kwa upande wake Bob Cheng ambaye ni Mkurugenzi wa kiwanda cha Keds Tanzania Company Ltd kinachojihusisha na uzalishaji wa sabuni za unga, vipande, pampasi na pedi za akinamama.

Cheng amesema kuwa kiwanda chao kinazingatia masuala ya haki za binadamu na lengo lake ni kukuza uchumi wa wananchi na hata maji ya kiwanda hicho hayana madhara ambapo asilimia 60 ya wafanyakazi wanaishi eneo jirani na kiwanda hivyo kama kungekuwa na changamoto yoyote wangefahamu.

Amesema kuwa wanafanya utafiti ili kuongeza bidhaa na uzalishaji wenye kuzingatia ubora na bei ambayo inaendana na soko.

Aidha kamishna aliambatana na Taasisi za Serikali ambazo ni OSHA, NEMC na Maofisa kutoka Ofisi ya RAS (Ofisa biashara, Ofisa Kazi na Ofisa Maendeleo ya jamii) kwa lengo la kuleta ufanisi katika ziara hiyo.


Wednesday, March 12, 2025

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA (THBUB) INAFANYA ZIARA KWENYE VIWANDA MKOANI PWANI KUANGALIA UZINGATIWAJI WA HAKI ZA BINADAMU

TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imefanya ziara kutembelea viwanda kuangalia uzingatiwaji wa haki za binadamu ili zisivunjwe.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Kamishna wa Tume Nyanda Shuli wakati wa ziara ya kutembelea viwanda ili kufanya uchunguzi kujua kama kuna changamoto za uvunjifu wa haki.

Shuli amesema kuwa baadhi ya viwanda vimekuwa vikilalamikiwa kuvunja haki za binadamu kwa unyanyasaji wa wafanyakazi, uchafuzi taka maji na haki mbalimbali.

"Lengo la ziara ni kuangalia hali ya haki za binadamu na uzingatiwaji wa misingi ya utawala bora kuangalia usalama wa mazingira ya kazi na uzingatiaji wa viwango vya ajira,"amesema Shuli.

Amesema kuwa malalamiko waliyoyapokea watayafanyia kazi na kutoa majibu jambo kubwa ni kuona haki inatendeka ili kuondokana na uvunjifu wa haki za binadamu.

Kwa upande wake Bob Cheng ambaye ni Mkurugenzi wa kiwanda cha Keds Tanzania Company Ltd kinachojihusisha na uzalishaji wa sabuni za unga, vipande, pampasi na pedi za akinamama.

Cheng amesema kuwa kiwanda chao kinazingatia masuala ya haki za binadamu na lengo lake ni kukuza uchumi wa wananchi na hata maji ya kiwanda hicho hayana madhara ambapo asilimia 60 ya wafanyakazi wanaishi eneo jirani na kiwanda.

Amesema kuwa wanafanya utafiti ili kuongeza bidhaa na uzalishaji wenye kuzingatia ubora na bei ambayo inaendana na soko 

Aidha kamishna aliambatana na Taasisi za Serikali ambazo ni OSHA, NEMC na Maofisa kutoka Ofisi ya RAS (Ofisa biashara, Ofisa Kazi na Ofisa Maendeleo ya jamii) kwa lengo la kuleta ufanisi katika ziara hiyo.


Wednesday, March 5, 2025

DOWEICARE YATOA YATOA MSAADA WA FEDHA UJENZI WA DARAJA LULANZI


KIWANDA cha Doweicare cha Kibaha Mkoani Pwani kimetoa fedha kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa daraja la Mtaa wa Lulanzi-Matunda ili kuboresha barabara ya mtaa huo.

Akikabidhi fedha hizo kwa uongozi wa Serikali ya Mtaa wa Lulanzi Mkurugenzi wa Kiwanda hicho Bob Chen amesema kuwa wameamua kutoa fedha hizo ili kukabili changamoto za jamii.

Amesema kuwa Kiwanda chao kimekuwa kikitoa misaada mbalimbali kwenye jamii ikiwa ni sehemu ya kurudisha kwa jamii kama sehemu ya huduma za jamii ambapo fedha hizo ni asilimia 57.5 ya fedha za mradi huo.

"Tunashirikiana na jamii kwenye masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja elimu, afya, barabara na masuala yanayohusu jamii,"amesema Chen.

Naye Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Lulanzi Thobias Shilole amesema kuwa wanakishukuru kiwanda hicho kwa msaada walioutoa utasaidia sana ujenzi wa daraja hilo.

Shilole amesema wananchi wamekuwa wakijitolea fedha kwa ajili ya ujenzi huo hivyo hiyo itakuwa imewaongezea nguvu kwenye kuanza ujenzi wa daraja ili kupunguza changamoto kwa wananchi wanaotumia barabara hiyo.

Amewataka wadau mbalimbali wa maendeleo kuendelea kuchangia ujenzi huo ili upunguze changamoto kwa watu wakiwemo wanafunzi wakati wakienda na kurudi shule.