Thursday, December 19, 2024
KAMPUNI YA PPM GROUP YAHAMASISHA NISHATI SAFI NA UTUNZAJI MAZINGIRA
STAMICO YATAKA WATANZANIA WATAKIWA KUTUMIA NISHATI SAFI NA SALAMA YA MKAA WA RAFIKI BRIQUETTES
KATIKA kuhamasisha matumizi ya nishati safi na salama Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limewataka Watanzania kutumia Mkaa wa Rafiki Briquettes.
TAASISI YA ANJITA YATAKA USHIRIKIANO KUKABILIANA NA UKATILI WA KIJINSIA
Wednesday, December 18, 2024
KINGLION KUTOA AJIRA
KIWANDA cha kuzalisha malighafi zitumikazo kwenye uzalishaji vyuma na mabati na usambazaji wa pikipiki cha Kinglion kinatarajia kutoa ajira kwa watu 1,500 ajira za kudumu na ajira za muda zaidi ya 5,000.
MLEZI WA KAMATI YA USALAMA BARABARANI ACP MORCASE AONGOZA KIKAO CHA KAMATI
Mlezi wa Kamati ya usalama barabarani Mkoa wa Pwani, Kamishina Msaidizi wa Polisi Salim Morcase Disemba 17 amekiongoza kikao cha kamati ya usalama barabarani ambacho kimejadili maswala mbalimbali ikiwemo kuondoa msongamano wa foleni kwenye barabara kuu za Mkoa wa Pwani na kuweka mikakati ya pamoja ya kumaliza foleni hizo ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua kali kwa madereva watakaobainika kupandisha nauli za mabasi kwenye kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka pamoja na madereva wanaokaidi kutii Sheria za usalama barabarani kwa watumiaji wengine wa barabara.
Saturday, December 14, 2024
VITENDO VYA UKATILI PWANI VYAPUNGUA
CATHERINE MWENYEKITI MTAA WA SOFU NA MKAKATI WA KUJENGA OFISI SERIKALI YA MTAA.
Lyimo akizungumza na mwandishi wa habari hizi amesema kuwa hilo ndiyo jambo ambalo ni kipaumbele chake mara baada ya kuchguliwa kwenye uchaguzi wa serikali za mita uliofanyika hivi karibuni na yeye kushinda nafasi hiyo.
Amesema kuwa eneo tayari wanalo wanachofanya ni kuwaandikia wadau wa maendeleo kwenye mtaa huo kwa kushirikiana na wananchi kufanya ujenzi huo ambao ni ndoto yake kuhakikisha mkakati wa kuwa na ofisi unafanikiwa.
“Mpango mkakati wa mtaa kwa sasa ni kuwa na ofisi yake badala ya kutumia ofisi za watu wengine tunataka tuwe na ofisi yetu wenyewe ili tufanye kazi kwa uhuru badala ya kutegemea wengine kwani kutumia ofisi za watu wengine kuna changamoto zake,”amesema Lyimo.
Aidha amesema kuwa anamatumaini ofisi itajengwa kutokana na ushirikiano anaoupata kutoka kwa wananchi na wadau wa maendeleo kwani anaamini ushirikiano huo utafanikisha kupatikana kwa ofisi ya mtaa huo.
“Nataka kwa kushirikiana wananchi na wadau kuhakikisha tunaacha alama ya uongozi kwa kujenga ofisi yetu kwani tukiwa na ofisi yetu tutakuwa na uhuru na tutajenga kutokana na mahitaji ya mtaa wetu ambapo itakuwa na vyumba kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi,”amesema Lyimo.
Amebainisha kuwa jambo lingine ambalo atahakikisha linafanyika ni kuwagawia wananchi eneo la kufanyiabiashara kwa ananchi wa mtaa huo ili waweze kupata huduma ya soko karibu kwani wanataka liwe soko dogo ili kuwaongezea wananchi kipato na kutoa huduma.
“Tunahitaji tuwe na eneo ambalo litakuwa kama soko ambapo wananchi watauza bidhaa zao badala ya kwenda mbali kufuata mahitaji yao nyumbani tunataka wapate hapa jirani na pia itakuwa ni sehemu ya kujiongezea kipato,”amesema Lyimo.
Lyimo alifanikiwa kushinda nafasi hiyo baada ya kumshinda aliyekuwa mwenyekiti wa Mtaa huo Lazaro Joseph ambaye aliongoza kwa vipindi viwili vya miaka 10 huku yeye akiwa ni mjumbe wa serikali ya mtaa huo ambapo alishindwa kwenye nasafi hiyo na mtangulizi wake mwaka 2019 na alikuwa ni mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania Kata ya Sofu na Mjumbe wa mtaa.