Thursday, March 14, 2024

CCWT YATANGAZA MUDA WA KUCHUKUA FOMU ZA UCHAGUZI


Na Wellu Mtaki, Dodoma.

Chama Cha Wafugaji Tanzania (CCWT) kimetangaza muda wa kuchukua fomu za kugombea nafasi za uongozi kwa wanachama wake wanaotaka kugombea huku wakibainisha kuwa malipo ya uchukuaji wa fomu hizo yanapaswa kufanyika kupitia akaunti ya tume ya uchaguzi na sio kwenye akaunti ya chama hicho.

Hayo yameelezwa leo Machi 12, 2024 Jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi ya CCWT Bw. Charles Lyuba alipokutana na waandishi wa habari katika ofisi ya chama hicho ambapo amesema kuwa lisiti za malipo zinapaswa kuambatanishwa katika fomu wakati wa kuzirejesha.

“Tangu mwaka jana tumeanza mchakato wa uchaguzi na hadi sasa tunaendelea na chaguzi za ngazi mbalimbali ikiwemo za wilaya, nawatangazia wafugaji na wanachama wote kuwa fomu za kugombea uongozi ndani ya chama chetu ngazi ya kanda na taifa zitaanza kutolewa Machi 13 - 25,2024 na mwanachama yeyote mwenye nia ya kugombea nafasi yeyote ya kanda anapaswa kuzingatia ratiba na kalenda nzima inayotolewa na tume,”amesema.

Amesema wanachama wao ni muhimu kuwa na taarifa sahihi zinazohusu uchaguzi ili kuepuka mikanganyiko na hasa wanapotoa ratiba isije kuonekana kuna watu wana ratiba zao binafsi.

“Hii ndio ratiba ya tume ya uchaguzi na sisi tunasema hiyo tarehe 13 kwa yaani kesho hadi tarehe hadi tarehe 25, Machi tunaanza kutoa hizo fomu za kanda sambamba na fomu za ngazi ya taifa,” amesema.

Aidha Bw. Lyuba amewasisitiza wagombea wote kufuata ratiba ya tume ipasavyo na kuchukua fomu kwa wakati kwa ngazi ya taifa uchaguzi utaanza Aprili 8,2024 utakao wahusisha viongozi wote wa wilaya na walaya ambayo haitakuwa imefanya uchaguzi wa ngazi haitaruhusiwa kufanya uchaguzi wa ngazi ya kanda pamoja na taifa kwasababu watakuwa hawajatimiza takwa la katiba ya wanachama hicho.

Kwa upande wake mjumbe wa tume ya uchaguzi George Kifuliko amewasisitiza wagombea na wanachama wote kuzingatia ratiba ili kuepusha vikwazo vitakavyojitokeza.

Wednesday, March 13, 2024

MADALALI WA KUPIGIA DEBE WAGOMBEA WATAKIWA KUACHA MARA MOJA



CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Picha ya Ndege Wilayani Kibaha imewataka watu wanaojifanya madalali wa watu wanaotaka kugombea nafasi za uenyekiti wa serikali za mitaa waache kwani muda wa viongozi walio madarakani haujaisha.

Aidha kimewataka watu kuacha kuwasemea vibaya viongozi walioko madarakani kwani nikukiharibia chama kwani wanatokana na chama hicho.

Hayo yamesemwa na Katibu Mwenezi wa Kata ya Picha ya Ndege Said Namamba wakati wa ziara kwa mabalozi wa Kata hiyo.

Namamba amesema kuwa kuna baadhi ya watu wanajifanya wanawapigia debe baadhi ya watu wanaotaka kuwania nafasi za uongozi huku muda wa kuwania nafasi hizo ukiwa bado.

Naye Mjumbe Mkutano Mkuu kutoka Kata  Subira Said amesema kuwa wametumia fursa hiyo kuwafundisha mabalozi hao kujua wajibu na majukumu yao.

Said amesema kuwa pia wamewaelekeza namna ya kutunza kumbukumbu za wanachama na kuhifadhi taarifa mbalimbali za mashina yao na kutoa taarifa juu ya changamoto kwa balozi wanazoziongoza.

Kwa upande wake Katibu wa Hamasa wa Vijana wa Kata Lenatus Mkude amesema kuwa wao wanataka mabalozi wasikubali kupotoshwa na watu wanaotaka kuwatumia kuwapigia debe wakati muda haujafika.

Mkude amesema wao wanataka utaratibu wa chama ufuatwe ili mgombea atakayechaguliwa kupitia kura za maoni apeperushe bendera ya chama na siyo vinginevyo.


Tuesday, March 12, 2024

WAFANYABIASHARA WA DODOMA WAIOMBA SERIKALI KUBORESHA MIUNDOMBINU YA BIASHARA





Na Anna Misungwi, Dodoma 

WAFANYABIASHARA wa Mkoa wa Dodoma waiomba serikali kurekebisha miundombinu ya soko la Machinga Complex pamoja  soko la Mavunde  lililopo Kata ya Chang'ombe ambapo kipindi cha mvua maji huingia na biashara kuharibika.

Hayo yamesemwa na wafanyabiashara wa masoko hayo Tarehe 11 Machi 2024 wakati wa ziara ya mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) Hamis Livembe, kwenye ziara iliyolenga kupokea changamoto, kero na maoni ya wafanyabiashara.

Mmoja wa wafanyabiashara Abdalla Ramadhan amesema kuwa kumekuwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na miundombinu ya soko kwani maji yanaingia na hivyo kusababisha bidhaa kuharibika.

Ramadhan amesema kuwa pia wanaomba kushushwa kwa ushuru kutoka 1,000 na kuwa 500 kwenye kizimba kwenye soko la Machinga Complex ambapo kizimba kimoja kinaweka wafanyabiashara wawili kwani ushuru wanaolipa unasababisha kushuka kwa biashara zao.

"Wafanyabiashara kipato chetu kinashuka tunaimomba serikali itusaidie kwani kizimba kimoja tunakaa watu wawili na kila mtu kwenye kizimba analipa shilling 1,000 ambapo watu wawili ni shilling 2,000 tunaomba tupunguziwe tulipe shilling 500 kwa kila mtu,"amesema Ramadhan.

Amesema wanaiomba serikali kuacha kuwafungia vizimba kutokana na hali ya wafanyabiashara kudaiwa kulipia ushuru kwani kizimba kikifungwa husababisha kukosa mapato kwa wafanyabiashara na serikali kwa ujumla.

"Tunafungiwa vizimba sababu ya mtu kama hajalipa ushuru siku moja au mbili kitendo ambacho wengi wanashidwa kuja kugomboa maana unapofungiwa lazima uje utoe fedha ndo ufunguliwe tunaomba serikali itusaidie,"wamesema wafanyabiashara hao.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania Hamis Livembe amesema kuwa lengo la kuja ni kupokea changamoto, kero na maoni na changamoto ambazo zinaweza kutolewa majibu zinatolewa ufafanuzi na ambazo majibu hawana watazipeleka sehemu husika ili kuzitafutia ufumbuzi.

Livembe ametoa wito kwa wafanyabiashara kuhakikisha wanakuwa wamoja katika kushughulikia matatizo kwa umoja.

EWURA KUMTUA MWANAMKE KUNI KICHWANI

Na Wellu Mtaki, Dodoma

MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Dkt. James Andilile,amesema mamlaka hiyo ina wajibu kuhakikisha wanamtua mwanamke kuni na mkaa kichwani kwa kuhakikisha wanatoa leseni kwa wakati kwa wawekezaji wanaokuja nchini kuwekeza katika nishati safi ya kupikia.

Dkt. Andilile ameyasema hayo Machi 9,2024 jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari katika banda la Mamlaka hiyo kwenye Kongamano la wanawake la kugawa mitaji na vitendea kazi vya nishati safi ya kupikia.

Amesema taifa bado linatumia nishati isiyosafi kwa kupikia hivyo EWURA itahakikisha ina wajibu wa kuhakikisha inatekeleza mikataba ya kukabiliana na changamoto zinazojitokeza ikiwemo uharibifu wa mazingira na madhara ya afya yanayosababidhwa na moshi wakati wa matumizi ya kuni na mkaa.

“EWURA tutahakikiha tunahamasisha uwekezaji katika nishati safi kwa kutoa leseni kwa wawekezaji kwa wakati ili wawekeze katika eneo hilo, pia tunaangalia upatikanaji wake katika maeneo mengi kwa kuangalia mwenendo wa bei za bidhaa hiyo,” amesema Dkt. Andilile.

Ameongeza kuwa:”Sisi kama EWURA tutahakikisha kama ilivyo dhamira ya Rais kumtua ndoo mama kichwani, tutamtua mwanamke kuni kichwani kwa kuhakikisha anatumia nishati ambayo itamrahisishia kupata maendeleo badala ya kuhangaika na nishati chafu ya kupikia,”.

Monday, March 11, 2024

TISA WAFA AJALINI BAGAMOYO

WATU tisa wamefariki dunia na wengine watatu kujeruhiwa baada ya basi dogo la abiria aina ya Toyota Coaster kugongana uso kwa uso na lori.

Kwa mujibu wa kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani SACP Pius Lutumo amesema kuwa ajali hiyo ilitokea Machi 10 majiira ya saa 11:15 jioni huko Kiromo Wilaya ya Bagamoyo barabaraba kuu ya Bagamoyo Dar es Salaam.

Lutumo amesema kuwa ajali hiyo ilihusisha basi hilo dogo lenye namba za usajiliT676 DSM likiendeshwa na dereva aitwaye Juma Mackey akitokea Dar es Salaam kuelekea Bagamoyo ambapo dereva huyo na yule wa lori ni miongoni mwa waliofariki dunia.

Ametaja gari lingine lililohusika na ajali hiyo kuwa ni lori aina ya Howo mali ya VGK Limited lenye namba za usajili T 503 DRP na tela namba T 733 DUa likierndeshwa na dereva aitwaye Apolo Mgomela (52) mkazi wa Kibaha likitoka Bagamoyo kwenda Dar es Salaam.

Waliokuta ni wanaume saba na wanawake yawawili ambapo majeruhi walipelekwa Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo kwa matibabu na pamoja na marehemu," amesema Lutumo.

Ametaja chanzo cha ajali hiyo kuwa ni uzembe wa dereva wa lori kuyapita magari menginep asipokuchukua tahadhari na kuligonga basi ambalo lilikuwa linakuja mbele yake ambapoa metoa wito kwa wananchi na watumiaji wote wa barabara hasa madereva kufuata sheria zau salama barabarani ili kuepusha ajali zinazogharimu maisha ya watu.

KATA YA MAILI MOJA WAELEZEA MAFANIKIO NA CHANGAMOTO

KATA ya Maili Moja Wilayani Kibaha Mkoani Pwani imeelezea mafanikio na changamoto huku wakiitaka Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) kukarabati miundombinu ya barabara ambayo imeharibika vibaya.

Diwani wa Kata hiyo Ramadhan Lutambi ameelezea baadhi ya mafanikio na changamoto mbele ya Katibu Tawala wa Wilaya ya Kibaha Moses Magogwa ambaye alimwakilisha mkuu wa Wilaya ya Kibaha wakati wa mkutano wa hadhara kwenye mtaa wa Uyaoni.

Lutambi amesema baadhi ya mafanikio ni kwenye sekta ya elimu ambapo kwenye sekondari ya Bundikani kwenye matokeo ya kidato cha nne mwaka jana wamefanikiwa kuondoa daraja sifuri na ujenzi wa madarasa mapya.

Amesema kwa upande wa shule za msingi wamefanikiwa kuanzisha shule mpya ya Muheza, shule za Maendeleo na Maili Moja zimejengewa madarasa mapya, kwa upande wa serikali za mitaa kujenga ofisi zake badala ya kupanga.

"Kuna baadhi ya changamoto lakini kubwa ni miundombinu ya barabara hii ni tatizo kwa mitaa yote suala la urasimishaji, umeme kukatika mara kwa mara, baadhi ya maeneo kukosa maji na umeme na mikopo ya kausha damu,"amesema Lutambi.

Kwa upande wake katibu tawala wa Wilaya ya Kibaha Moses Magogwa amesema kuhusu changamoto ya barabara atawaelekeza Tarura ili wakae na wananchi ili kuangalia vipaumbele vya barabara ili zianze kufanyiwa marekebisho.

Magogwa amesema kuhusu urasimishaji wote waliopewa hiyo kazi wakutane naye ofisini ili kuangalia namna ya kutatua changamoto hiyo ili kuondoa malalamiko ya wananchi.

Amesema kuhusu mikopo ya kausha damu viongozi wa mitaa wakae na wamiliki wa taasisi hizo za mikopo ili kuangalia namna ya kudai marejesho badala ya kuwadhalilisha watu.

Ameongeza kuwa serikali inasikiliza kero za wananchi ili kuzitatua kwani Rais Dk Samia Suluhu Hassan anapambana kuhakikisha wananchi wanaishi kwenye mazingira mazuri.

Saturday, March 9, 2024

BAWACHA YAWATAKA WANAWAKE WANAOLEA WATOTO PEKE YAO KUOMBA MSAADA


Na, Wellu Mtaki, Dodoma 

Mwenyekiti wa Baraza la wanawake wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA (BAWACHA) Sharifa Suleiman amewakumbusha wazazi wanaoleo watoto peke yao kuomba msaada wa malezi  kwani kumekuwa na wimbi kubwa la watoto kukosa malezi ya wazazi wote wawili

Bi. Sharifa ameyasema hayo Jijini Dodoma wakati wa maadhimisho ya  siku ya Wanawake Duniani ambapo kitaifa yamefanyika Jijini Dodoma huku akiongeza kuwa suala la malezi na makuzi linahitajika kwa pande zote mbili kwani wanategemeana kwenye malezi.

Aidha ameongeza kuwa changamoto ya afya ya akili imefanya wazazi wengi kukimbia familia zao jambo linalofanya hali ya familia kwasasa kuwa katika hali mbaya.

Naye Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe amewasisitiza wanawake kuwa na udhubutu wa kugombea nafasi mbalimbali za uongozi serikalini.

Nao baadhi ya wahudhuriaji katika maadhimisho hayo wamezungumzia kuhusiana na kitu kinachosababisha wanaume wengi kukimbia familia zao na kushindwa kutimiza jukumu lao la malezi.