Saturday, July 29, 2023

PINDA KUZINDUA MAONYESHO NANE NANE KANDA YA MASHARIKI

 

WAZIRI Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye maonyesho ya wakulima nane nane Kanda ya Mashariki Mkoani Morogoro Agosti Mosi mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kuwa maonyesho hayo yanashirikisha mikoa minne ya Pwani, Dar es Salaam, Tanga na Morogoro.

Kunenge amesema kuwa hadi sasa tayari washiriki 589 wamejiandikisha kushiriki maonyesho hayo ambapo ni ongezeko la asilimia 22 ikilinganishwa na mwaka jana ambapo washiriki walikuwa 476.

Amesema kuwa maonyesho hayo ni ya 30 tangu kufanyika kwa kanda hiyo ya Mashariki ambapo kauli mbiu inasema Vijana na Wanawake ni msingi imara wa mifumo endelevu ya chakula.

Aidha amesema kuwa wakulima na wananchi wanakaribishwa kujitokeza kwa wingi ili kujifunza teknolojia za kisasa kwenye sekta za kilimo, ufugaji na uvuvi.

Friday, July 28, 2023

WAZIRI MKUU MSTAAFU PINDA MGENI RASMI NANE NANE KANDA YA MASHARIKI

WAZIRI Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye maonyesho ya wakulima nane nane Kanda ya Mashariki Mkoani Morogoro Agosti Mosi mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kuwa maonyesho hayo yanashirikisha mikoa minne ya Pwani, Dar es Salaam, Tanga na Morogoro.

Kunenge amesema kuwa hadi sasa tayari washiriki 589 wamejiandikisha kushiriki maonyesho hayo ambapo ni ongezeko la asilimia 22 ikilinganishwa na mwaka jana ambapo washiriki walikuwa 476.

Amesema kuwa maonyesho hayo ni ya 30 tangu kufanyika kwa kanda hiyo ya Mashariki ambapo kauli mbiu inasema Vijana na Wanawake ni msingi imara wa mifumo endelevu ya chakula.

Aidha amesema kuwa wakulima na wananchi wanakaribishwa kujitokeza kwa wingi ili kujifunza teknolojia za kisasa kwenye sekta za kilimo, ufugaji na uvuvi.

TASAC KUNUNUA BOTI ZA UOKOZI ZIWA VICTORIA

SHIRIKA la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limesema limejipanga kununua boti tatu za uokozi katika Ziwa Victoria ambazo zitakwenda kusaidia kutatua changamoto ambazo zimekuwa zikijitokeza pindi ajali zinapotokea

Hayo yamesemwa jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Bw.Kaimu Abdi Mkenyenge wakati  akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa majukumu ya mamlaka hiyo na mwelekeo wa utekelezaji wa mwaka wa fedha 2023/2024 .

Amesema  katika boti hizo tatu zitakazonunuliwa mbili zitakuwa ni za mwendonkasi kwaajili ya ukokozi na Moja itakuwa kwaajili ya kubebea majeruhi na wagonjwa (Ambulance) .

“Boti hizi tatu zitatumika kufanya uokozi katika ajali ambazo zimekuwa zikitokea katika Ziwa Victoria ambapo mbili zitakuwa ni za meendo kasi na Moja itatumika kama ambulance kwa ajili ya majeruhi”amesema

Aidha amesema TASAC  imeendelea kuimarisha udhibiti huduma za usafiri majini, na kuhakikisha kuna ushindani sawia miongoni mwa watoa huduma.

Amesema kuwa linafanya ufuatiliaji, tathmini na kutoa maelekezo kuhusu utekelezaji wa vigezo na viwango vya ubora wa huduma (performance standards and Benchmarks) kwa watoa huduma za bandari na usafiri majini.

“Tunaendelea kuratibu maombi ya tozo za usafiri wa meli katika Maziwa (Victoria na Nyasa) na kuhakikisha viwango vya tozo vinavyotumika haviathiri ushindani wa kibiashara;

“Lakini pia zoezi la urasimishaji wa bandari bubu Tanzania bara ambapo bandari bubu kumi na tatu (13) zilizowasilishwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) kwa ajili ya urasimishaji zilikaguliwa na kufanyiwa tathmini ya kina kwa kushirikiana na TPA, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Baraza la Usimamizi wa Mazingira (NEMC)”amesema Mkeyenge

Kadhalika amesema  bandari bubu kumi zilionekana kukidhi vigezo hivyo na kupendekezwa kwa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Uchukuzi) (WUU-U) kwa ajili ya kurasimishwa kwa mujibu wa sheria

“waendeshaji wa zilizokuwa bandari bubu binafsi tano (05) za Mwanza ambazo ni miongoni mwa zilizokuwa bandari bubu ishirini (20) zilizorasimishwa kupitia Tangazo la Serikali (GN) namba 293/2022 wamepewa leseni za uendeshaji huku TPA wakielekezwa kusimamia kwa karibu bandari kumi na tano (15) zilizobakia.

Akizungumzia kuhusu Kuboresha usalama, ulinzi kwa usafiri majini na kudhibiti uchafuzi wa mazingira baharini utokanao na meli amesema Shirika limetimiza lengo hilo la kimkakati kwa  kuendelea kusimamia usalama wa vyombo vya usafiri majini kwa kufanya ukaguzi wa meli kubwa na vyombo vidogo vya majini.

“Shirika lilifanya kaguzi za usalama kwa meli kubwa zibebazo tani 50 au zaidi ili kuhakikisha kuwa ni salama na zinaendeshwa na mabaharia wenye sifa katika mikoa ya Dar es Salaam, Mtwara, Tanga, Mwanza, Kagera, Kigoma na Mbeya ambapo katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Juni, 2023, Shirika lilifanya jumla ya kaguzi za meli kubwa 288 ambapo kaguzi 165 zilikuwa za meli za kigeni na kaguzi 123 zilikuwa meli za ndani.”amesema

Kuhusu uratibu Shughuli za Utafutaji na Uokoaji Majini amesema Kituo cha Utafutaji na Uokoaji Majini kilichopo Dar es Salaam kinachoratibiwa na TASAC kiliendelea kufanya shughuli zake  katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Juni, 2023 ambapo kituo kilipokea taarifa 4 za ajali zilizohusisha vyombo vya majini ambazo zilitokea katika eneo la maji ya Tanzania.

Katika ajali hizo  jumla ya watu 61 walihusika ambapo watu 58 sawa na 95% waliokolewa na watu 3 sawa na 5% walipoteza maisha.

Naye  Mkurugenzi wa Idara ya Habari -Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa amesema Serikali inataka kushirikiana na sekta binafsi kuendesha Bandari, mikataba nwatakaoendesha bado haijasainiwa.

“Sasa hivi ndio wataalamu wako mezani kuzungumza kuhusu mikataba, muda na gharama lakini hakuna bandari iliyouzwa, wataalamu watakapokamilisha majadiliano tutaangalia maslahi yetu yako wapi na maoni yanayotolewa na Watanzania yatazingatia Serikali iko macho wakati wote kuhakikisha maslahi ya Watanzania yanalindwa”amesema Msigwa.

Thursday, July 27, 2023

MRADI MKUBWA WA KILIMO CHA VANNILA WAZINDULIWA DODOMA UNAKWENDA KUGHARIMU ZAIDI YA BIL 30 ZA KITANZANIA.

 


KAMPUNI ya Vanilla international Limited imezindua Mradi wa kilimo cha Vanilla Mkoani Dodoma Vanilla village Dodoma katika Kitongoji cha Zamahero Kata ya Mayamaya Wilaya ya Bahi.

Uzinduzi huo umeambatana na utoaji Elimu kwa wananchi wa eneo hilo kuhusu kilimo cha Vanilla ambao umefanyika Julai 22 2023 katika shamba la kitalu (green House)kubwa ya kilimo hicho inayotumia njia za kisasa.

Mkurugenzi Mtendaji na muasisi wa makampuni ya Vanilla international Limited ,Simon Mkondya amesema shamba kitalu lipo kilomita 40 kutoka katikati  ya JIJI la Dodoma barabara kuu ya kwenda Arusha lenye ukubwa wa hekta 125.

Mkondya amesema uwekezaji huo unakuja baada ya mafanikio makubwa yaliyopatikana kupitia kilimo hicho katika kisiwa cha Zanzibar.

JWT YAVUTIWA UTALII UWEKEZAJI YAWATAKA WAFANYABIASHARA WAKAWEKEZE

 

KATIKA kuunga mkono jitihihada za Rais Dk Samia Suluhu Hassan kutangaza utalii Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) Mkoa wa Pwani imetembelea vivutio vya utalii na kutambua fursa za uwekezaji zilizopo Wilayani Bagamoyo.

Akizungumza mara baada ya kutembelea vivutio vya utalii na fursa za uwekezaji mwenyekiti wa Jwt Abdala Ndauka alisema kuwa baada ya ziara hiyo wameweza kutambua fursa mbalimbali kupitia utalii.

Ndauka alisema kuwa fursa kwa wafanyabiashara ni nyingi sana kwenye utalii pamoja na fursa nyingine kwenye sekta mbalimbali zikiwemo za utoaji huduma.

Kwa upande wake kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Majid Mhina alisema kuwa changamoto kubwa waliyonayo ni maeneo mengi yanamilikiwa na watu binafsi.

Naye ofisa biashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Magdalena Kitilla alisema kuwa kuhusu uwekezaji wametenga eneo lenye ukubwa wa hekta 9,800 ambalo linahitaji wawekezaji.

Kitilla alisema kuwa sekta ya utalii ina fursa nyingi ambapo kwenye sekta ya uvuvi kupitia uchumi wa buluu bado haujatumika ipasavyo ambapo kuna ufugaji wa vizimba baharini kunakofanyika ufugaji wa majongoo bahari ambapo ni mwekezaji ni mmoja tu.

Moja ya wafanyabiashara Fihiri Msangi alisema kuwa ziara hiyo wamejifunza mambo mengi ambayo watayafanyia kazi ili waangalie namna ya kuweza kuwekeza.

Msangi alisema kuwa fursa hizo watazitumia vizuri ili kuinua uchumi wa Mkoa huo ambao unategemea uwekezaji kwenye maeneo mbalimbali na pia unauwekezaji mkubwa wa viwanda.

JWT WAVUTIWA NA VIVUTIO VYA UTALII NA UWEKEZAJI BAGAMOYO

KATIKA kuunga mkono jitihihada za Rais Dk Samia Suluhu Hassan kutangaza utalii Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) Mkoa wa Pwani imetembelea vivutio vya utalii na kutambua fursa za uwekezaji zilizopo Wilayani Bagamoyo.

Akizungumza mara baada ya kutembelea vivutio vya utalii na fursa za uwekezaji mwenyekiti wa Jwt Abdala Ndauka alisema kuwa baada ya ziara hiyo wameweza kutambua fursa mbalimbali kupitia utalii.

Ndauka alisema kuwa fursa kwa wafanyabiashara ni nyingi sana kwenye utalii pamoja na fursa nyingine kwenye sekta mbalimbali zikiwemo za utoaji huduma.

Kwa upande wake kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Majid Mhina alisema kuwa changamoto kubwa waliyonayo ni maeneo mengi yanamilikiwa na watu binafsi.

Naye ofisa biashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Magdalena Kitilla alisema kuwa kuhusu uwekezaji wametenga eneo lenye ukubwa wa hekta 9,800 ambalo linahitaji wawekezaji.

Kitilla alisema kuwa sekta ya utalii ina fursa nyingi ambapo kwenye sekta ya uvuvi kupitia uchumi wa buluu bado haujatumika ipasavyo ambapo kuna ufugaji wa vizimba baharini kunakofanyika ufugaji wa majongoo bahari ambapo ni mwekezaji ni mmoja tu.

Moja ya wafanyabiashara Fihiri Msangi alisema kuwa ziara hiyo wamejifunza mambo mengi ambayo watayafanyia kazi ili waangalie namna ya kuweza kuwekeza.

Msangi alisema kuwa fursa hizo watazitumia vizuri ili kuinua uchumi wa Mkoa huo ambao unategemea uwekezaji kwenye maeneo mbalimbali na pia unauwekezaji mkubwa wa viwanda.

Wednesday, July 26, 2023


KATIKA kuhakikisha wafanyabiashara wanaondokana na changamoto mbalimbali Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) imejipanga kuhakikisha inakabili kero na kuzifikisha sehemu husika.

Hayo yamesemwa na  Mwenyekiti wa Jumuiya ya  Wafanyabiashara Tanzania Hamis Livembe wakati wa mkutano wa wafanyabiashara mkoani Tanga.

Amewataka wafanyabiashara hao kuungana na kuwa na sauti ya pamoja katika kuhakikisha wanajenga jumuiya yao kwa kutetea masilahi ya biashara zao.

Livembe amesema kuwa umoja wa wafanyabiashara unasaidia katika kutatua kero na kuisaidia serikali katika kutatua changamoto za wafanyabiashara pamoja na kuundwa kwa sera bora ya biashara.

"Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ipo katika kusaidia na kutatua kero za wafanyabiashara kwa makundi siyo kwa mtu mmoja mmoja ndiyo maana waliunda kamati maalum ambayo lengo lake lilikuwa ni kukusanya na kuchakata na kuwasilisha kwa serikali," amesema Livembe.

Awali katibu wa JWT Mkoa wa Tanga Ismail Masod amesema kuwa hadi sasa bei ya vitenge imeshuka ambapo awali ilikuwa kati ya shilling milioni 200 na milioni 300 lakini kwa sasa ni shilingi milioni 60 kwa kontena ambayo hiyo ni kazi ya kamati iliyoundwa.

Masod amewataka wafanyabiashara wa Tanga watumie fursa ambazo serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imeziweka kwa kuagiza mizigo China kutokana na mfumo mzuri ambao serikali wameutengeneza.

Naye Mwenyekiti wa Kariakoo Martin Mbwana amesema kuwa serikali ipo pamoja na Jumuiya hiyo hivyo ametoa wito kwa wafanyabiashara watambue fursa na thamani ambayo Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan ambayo ameitoa kwa wafanyabiashara hao.