Thursday, May 18, 2023

WIZARA VIWANDA NA BIASHARA KUANDAA MWONGOZO KWA WAFANYABIASHARA

MKURUGENZI wa uwezeshaji wananchi kiuchumi na maendeleo ya sekta binafsi ya TAMISEMI Conrad Milinga amesema kuwa Wizara ya Viwanda na Uwekezaji inaandaa mwongozo wa kuwawezesha wafanyabishara wajasiliamari kutambua kuwa wanapohitaji kuanzisha biashara sehemu ya kuanzia na kuishia.

Milingi ameyasema hayo Jijini Dodoma, katika kikao cha kuthibitisha rasimu ya muongozo wa wataalamu wa biashara na mpango wa kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini kilichofanyika katika ukumbi wa bodi ya wakandarasi.

Aidha amesema kuhusiana na taarifa za mwenendo wa bei za vyakula nchini wanahitaji kuzipata kuanzia kwao lakini zisitofautiane na zile zinazotolewa na wizara, hivyo waweke mfumo wa taarifa watakazo kuwa wanazipata kutoka kwao.

Kwa upande wake katibu tawala masidizi wa viwanda, biashara na uwekezaji mkoa wa Kigoma Deogratias Sangu, amesema kabla ya kuanzishwa kwa idara hiyo wizara ilikuwa ikifanya, kuunda, kupendekeza pamoja na kuanzisha sera ambapo utekelezaji wa chini haukuwa thabiti kwasababu haukuwa na wasimamizi, hivyo kupitia idara hiyo wasimamizi wana mwendelezo wa majukumu yaliyopangwa yatatimizwa.

Naye katibu tawala msaidizi viwanda, bishara na uwekezaji mkoa wa Morogoro Beatrice Njawa amesema kwakuwa wamepitishwa kwenye mpango wa kuboresha mazingira ya kufanyia bishara anaamini wanaenda kusimamia na kuondoa vikwazo vyote vya kibishara na uwekezaji katika mamlaka za serikali za mitaa na mikoani ili kuweza kutangaza uwekezaji unaopatikana katika maeneo hayo.

Njawa ameongeza kuwa wakiweza kuboresha eneo hilo hasa uwekezaji na ujenzi wa viwanda maana yake wanaenda kuzipa nguvu mamlaka za serikali za mitaa na wataongeza mapato na wanaenda kuimalisha mahusiano kati ya mikoa, halmashauri pamoja na sekta binafsi zilizopo katika maeneo yao.

WIZARA YA AFYA YAWEKA JITIHADA KUDHIBITI UGONJWA SHINIKIZO LA JUU LA DAMU

WAZIRI wa Afya Ummy Mwalimu amesema  pamoja na kuimarisha huduma za tiba hapa nchini, serikali imejipanga kuweka jitihada za kipekee ili kuzuia na kudhibiti ugonjwa wa shinikizo la juu la damu na magonjwa yasiyoambukiza.

Waziri Ummy ameyasema hayo leo Mei 17,2023 Jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari ikiwa ni maadhimisho ya siku ya shinikizo la damu Duniani.

Pia amekumbusha umuhimu wa kubadili mtindo wa maisha na kuhimiza wananchi kufanyaji wa mazoezi, kuepuka tabia bwete, kuepuka matumizi ya tumbaku na bidhaa zake, kupunguza matumizi ya vilevi, kuzingatia ulaji unaofaa wa mlo kamili wenye mboga mboga na matunda ya kutosha ili kuimarisha kinga ya mwili dhidi ya magonjwa.

Aidha, amesema kuwa takwimu kutoka kwenye mfumo wa ukusanyaji taarifa za Afya (DHIS2) zinaonesha kuwa jumla ya wagonjwa milioni 2.5 walitibiwa magonjwa yasiyoambukizwa kwenye vituo vya Afya nchini kwa mwaka 2017.

Waziri Ummy amesema kati yao, ugonjwa wa shinikizo la juu la damu ndio uliongoza miongoni mwa magonjwa yasiyoambukiza ambapo waliongezeka kutoka wagonjwa 688,901 kwa mwaka 2017, hadi kufikia wagonjwa milioni 1.3 kwa mwaka 2021 sawa na ongezeko la 95.4% katika kipindi hicho.

Amesema katika uchunguzi uliofanywa katika jamii kwenye mikoa ya Pwani, Arusha, Geita, Mtwara, Lindi, Zanzibar, Iringa na Dar es Salaam takwimu zinaonyesha watu 3-4 kati ya 10 wana shinikizo la juu la damu. 

Shinikizo la juu la damu ni ugonjwa unaosababishwa na nguvu ya msukumo wa damu katika mishipa kuwa kubwa kuliko kawaida kwa muda mrefu na ongezeko hilo huulazimu moyo kufanya kazi kupita kiasi ili uweze kusukuma damu katika mishipa kwa kiwango kilekile kinachohitajika mwilini.

MWENGE WAZINDUA MIRADI KIBAHA

KIONGOZI wa mbio za Mwenge Kitaifa Abdala Shaibu Kaim amewataka Watanzania kutunza mazingira ili kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi ambayo kwa asilimia 95 yanatokana na uharibifu wa mazngira.

Aidha aliwataka wananchi kuwa na utamaduni wa kula kwa mpangilio na kufanya mazoezi ili kujiepusha na magonjwa yasiyo ya kuambukiza.

Aliyasema hayo wakati akizungumza na viongozi na wananchi wa Halmashauri ya Mji Kibaha wakati wa kupokea Mwenge wa uhuru ukitokea Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha.

 Kaim alisema kuwa uharibifu huo wa mazingira unasababisha kushusha uchumi wa nchi kutokana na athari hizo hivyo kuna haja ya Watanzania kusimamia maingira ili yasiharibiwe.

"Tuhakikishe tunalinda mazingira yetu ili kukabiliana na athari hizo ambazo zinaleta changamoto za kimaendeleo,"alisema Kaim.

Alisema kuwa mazingira ni uhai hivyo mazingira  yanapaswa kulindwa kwa nguvu zote ili maisha yaendelee bila ya changamoto ambazo zimesababisha hali ya hewa kuwa mbaya.

Aliongeza kuwa ujumbe wa mwaka huu unasema kuwa Mabadiliko Tabianchi Hifadhi ya Mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji na kauli mbiu tunza mazingira okoa vyanzo vya maji kwa ustawi wa viumbe hai na ustawi wa uchumi wa Taifa.

"Tuendelee kukabiliana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza kwa kula vyakula kwa mpangilio ambavyo vinashauriwa na wataalamu na kuacha ulaji usio na mpangilio na kufanya mazoezi angalau kwa nusu saa,"alisema Kaim.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Simon John alisema kuwa Mwenge huo wa uhuru ulitembelea jumla ya miradi 12 yenye thamani ya shilingi bilioni 3.9.

John alisema kuwa fedha za miradi kati ya hizo milioni 520.2 ni mchango kutoka Halmashauri na milioni 683.7 ni kutoka serikali kuu na bilioni 2.4 ni michango ya wananchi.

Alisema kuwa fedha nyingine ni kutoka kwa wahisani ambapo ni kiasi cha shilingi milioni 293.3 na michango ya mwenge iliyoelekezwa katika miradi ya maendeleo ni shilingi milioni 2.5.

Mwisho.

Wednesday, May 17, 2023

WIZARA YA VIWANDA UWEKEZAJI KUANDAA MWONGOZO KWA WAFANYABIASHARA

 

MKURUGENZI wa uwezeshaji wananchi kiuchumi na maendeleo ya sekta binafsi ya TAMISEMI Conrad Milinga amesema kuwa Wizara ya Viwanda na Uwekezaji inaandaa mwongozo wa kuwawezesha wafanyabishara wajasiliamari kutambua kuwa wanapohitaji kuanzisha biashara sehemu ya kuanzia na kuishia.

Milingi ameyasema hayo Jijini Dodoma, katika kikao cha kuthibitisha rasimu ya muongozo wa wataalamu wa biashara na mpango wa kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini kilichofanyika katika ukumbi wa bodi ya wakandarasi.

Aidha amesema kuhusiana na taarifa za mwenendo wa bei za vyakula nchini wanahitaji kuzipata kuanzia kwao lakini zisitofautiane na zile zinazotolewa na wizara, hivyo waweke mfumo wa taarifa watakazo kuwa wanazipata kutoka kwao.

Kwa upande wake katibu tawala masidizi wa viwanda, biashara na uwekezaji mkoa wa Kigoma Deogratias Sangu, amesema kabla ya kuanzishwa kwa idara hiyo wizara ilikuwa ikifanya, kuunda, kupendekeza pamoja na kuanzisha sera ambapo utekelezaji wa chini haukuwa thabiti kwasababu haukuwa na wasimamizi, hivyo kupitia idara hiyo wasimamizi wana mwendelezo wa majukumu yaliyopangwa yatatimizwa.

Naye katibu tawala msaidizi viwanda, bishara na uwekezaji mkoa wa Morogoro Beatrice Njawa amesema kwakuwa wamepitishwa kwenye mpango wa kuboresha mazingira ya kufanyia bishara anaamini wanaenda kusimamia na kuondoa vikwazo vyote vya kibishara na uwekezaji katika mamlaka za serikali za mitaa na mikoani ili kuweza kutangaza uwekezaji unaopatikana katika maeneo hayo.



Njawa ameongeza kuwa wakiweza kuboresha eneo hilo hasa uwekezaji na ujenzi wa viwanda maana yake wanaenda kuzipa nguvu mamlaka za serikali za mitaa na wataongeza mapato na wanaenda kuimalisha mahusiano kati ya mikoa, halmashauri pamoja na sekta binafsi zilizopo katika maeneo yao.

Saturday, May 6, 2023

WIZARA ZA ELIMU NA UTAMADUNI ZIWASAIDIE VIJANA KUMFAHAMU ZAIDI MWL. NYERERE - MAJALIWA

 

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amezitaka Wizara za Elimu, Sayansi na Teknolojia na ile ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ziandae utaratibu utakaosaidia vijana kujifunza na kumfahamu zaidi hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kuanzia shule za msingi, hadi vyuo vikuu.

Ametoa wito huo leo (Jumamosi, Mei 6, 2023) alipomuwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye kongamano la kumbukizi ya miaka 101 ya hayati Mwalimu Nyerere lililofanyika katika ukumbi wa Chimwaga, Chuo Kikuu cha Dodoma.

Amesema kuwa kama lilivyo lengo la kongamano hilo ni muhimu kuwarithisha vijana wa Kitanzania fikra na falsafa za Baba wa Taifa. “Aidha, nyote mtakubaliana nami kwamba yapo mambo mengi ambayo tungetamani vijana wetu wayafahamu kuhusu urithi aliyotuachia Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.”

Mheshimiwa Majaliwa amesema baadhi ya mambo ambayo vijana wanapaswa kurithishwa ni kuyafahamu maisha ya Mwalimu Nyerere hasa baada ya kustaafu uongozi wa nchi na siasa za majukwaani, kutambua juhudi zake katika harakati za kuleta amani na kufanikisha ukombozi wa nchi za Kusini mwa Afrika na bara la Afrika.

Ameyataja masuala mengine kuwa ni kufahamu kipaji cha Mwalimu Nyerere katika harakati zake za kupigania uhuru na kuwaunganisha Watanzania na kuwa na uwezo wa kumfahamu na kumuelezea Mwalimu Nyerere alikuwa ni nani katika historia ya Tanzania.

“Miongoni mwa urithi huo ambao tungependa kizazi chetu kiufahamu ni pamoja na kuwa na uwezo wa kumfahamu na kumuelezea Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alikuwa ni nani katika historia ya Tanzania; kuzielewa na kuzitambua juhudi za zake katika kuimarisha ustawi wa Tanzania hususan kupitia falsafa yake ya kutokomeza maadui watatu yaani ujinga, umaskini na maradhi.”

Wakati huohuo, Mheshimiwa Majaliwa amesema kumekuwa na taarifa za malalamiko kuhusu kuongezeka kwa kelele na mitetemo katika sehemu mbalimbali nchini na maeneo yaliyoongoza kwa kulalamikiwa ni za nyumba za starehe, kumbi za burudani na nyumba za ibada.

Amesema katika kudhibiti kelele na mitetemo kutoka katika kumbi za starehe, Ofisi ya Makamu wa Rais ilitoa maelekezo mahususi yaliyolenga kudhibiti mitetemo iliyopitiliza katika kumbi za starehe hapa nchini. Pia, maelekezo hayo yaliainisha jinsi uratibu unavyopaswa kufanyika katika nyumba za ibada kwa kuwaomba viongozi wa dini kupitia Kamati za Amani kujadili suala la kelele na mitetemo iliyopitiliza kutoka kwa baadhi ya nyumba za ibada ili kupata namna bora ya kuendesha shughuli za ibada.

 Hata hivyo, Mheshimiwa Majaliwa amesema, kumejitokeza taharuki kwa baadhi ya viongozi wa dini wakati Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashughulikia malalamiko kuhusu ongezeko la kelele na mitetemo.

“Serikali ingependa kutoa ufafanuzi kwamba shughuli za dini ziendelee kufanyika kama kawaida na suala la uratibu wa jambo hilo katika nyumba za ibada liendelee kuratibiwa na viongozi wa dini wenyewe kupitia Jumuiya ya Maridhiano na Amani.”

“Serikali itaendelea kushauriana na jumuiya ya maridhiano na amani katika kuona namna bora ya kuendesha shughuli zao kwa kuzingatia mahitaji ya jamii na kulinda afya za Watanzania,” amesema.

Tanzania, Seattle Sounders, Seahawks, Trailblazers Kushirikiana Kutangaza Utalii



Tanzania, Seattle Sounders, Seahawks, Trailblazers Kushirikiana Kutangaza Utalii

Seattle, Washington State, Marekani

 SERIKALI ya Tanzania imeeleza azma yake ya kuongeza juhudi za kutangaza utalii kupitia michezo pia kushirikiana na taasisi mbalimbali duniani ili kuongeza idadi ya watalii kutoka nje na mapato zaidi kwa Serikali.

Azma hiyo imeelezwa na Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi, Mei 5, 2023, wakati wa hafla fupi iliyoandaliwa na kampuni ya Vulcan kwenye Uwanja wa Lumen jijini Marekani na kushirikisha wadau kutoka makampuni mbalimbali yaliyoko jijini Seattle ikiwemo wawakilishi kutoka Google, Starbucks, ofisi ya Meya wa Seattle, Boeing na jumuiya ya wafanyabiashara.

Taasisi ya Vulcan inamiliki hisa katika klabu kubwa za michezo mbalimbali katika ligi kuu za nchini Marekani za Seattle Sounders (mpira wa miguu); Seahawks (soka la Marekani) na Portland Trailblazers (Ligi ya NBA).

“Nimewahi kufika Tanzania, naweza kuwahakikishia kuwa kwa wale ambao hawajafika mfike ni nchi nzuri sana. Tuliwahi kwenda pia Sounders miaka ya 2000 ikacheza na Yanga, Simba na Timu ya Taifa,” alisema Bw. Adrian Hanauer, ambaye kwa sasa ni mmiliki mwenye hisa nyingi wa klabu ya Seattle Sounders akiahidi klabu hiyo na wadau wengine wako tayari kushirikiana kusukuma mbele utalii wa Tanzania.

Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) chini ya Mtendaji wake Mkuu, Damasi Mfugale, imeingia makubaliano ya awali kuelelea ishirikiano kamili na makampuni ya Vulcan.

MAKAMU WA RAIS DKT MPANGO AWASILI BURUNDI

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Melchoir Ndadaye uliopo Bujumbura nchini Burundi na kupokelewa na Makamu wa Rais wa Burundi Mheshimiwa Prosper Banzombaza leo tarehe 06 Mei 2023. 

Makamu wa Rais anamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa 11 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi Wanachama wa Mpango wa Amani, Usalama na Ushirikiano kwaajili ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Ukanda wa Maziwa Makuu unaofanyika Bujumbura nchini Burundi.