Thursday, October 27, 2022
WAVAMIZI SOKO WAMACHINGA KUCHUKULIWA HATUA KISHERIA HATUA
WAVAMIVI WA SOKO LA WAMACHINGA COMPLEX DODOMA WATACHUKULIWA HATUA YA KISHERIA
Na Wellu Mtaki, Dodoma
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Sinyamule amewakata wale wote ambao awana sifa za machinga wasiingie kwenye soko ilo kwani soko limejengwa KWa ajiiri ya wanachinga tu KWa yoyote atakayebainika ameingia bila sifa za umachinga hatua za kisheria zitachukuliwa.
Pia amewataka wamachinga kuamia kwenye soko ilo KWa amani ,Uaminifu na uhadilifu pasipo kuibiana Pamoja na kuzingatia usafi wa Mazingira.
Hayo yamesemwa na mkuu wa Mkoa huyo wakati wa kusikiliza kero za wamachinga jijini dodoma kuhusu changamoto zinazowakabili wamachinga dodoma.
Sinyamule amesema Kuwa wapo ambao wamefanya maombi KWa kudanganya taarifa ili wapate nafasi ndani ya soko ilo, endapo wakibainika hatua za kisheria zitachukuliwa.
Aidha amewataka halmashauri ya jiji kutatua kero zote zinazojitokeza na ambazo zitajitokeza hapo baadae
" Jiji endeleeni kutatua kero hizi na zitakazojitokeza Ili kuhakikisha wafanyabiashara wadodo wadogo wanafanya biashara KWa amani na endapo kama kutajitokeza upungufu wa vizimba watapangwa maeneo mengine"Amesema Sinyamule.
Pamoja hayo Sinyamule ametangaza rasmi tarehe 28 hadi 30 octpbar mwaka huu ndiyo siku ya kuaza kuingia wamachinga kwenye soko ilo uku akiwataka viongozi wa Halmashauri ya jiji kukaa eneo ilo siku zote KWa ajiiri ya kusimamia zoezi ilo pamoja na kuwataka LATRA kuhakikisha kuwa kufikia tarehe 1 November daladala zinapitika njia ya soko hilo na kunakuwa na kituo cha kupitia na kushushia abiria.
Pia Sinyamule amewahakikishia Wamachinga fedha za mikopo zipo bali changamoto ya mikopo ni kuwa baadhi ya watu wanaunda vikundi vya watu watano ambapo ndani ya kundi ilo hakuna machinga hivyo ni vigumu kupata mkopo huo hivyo amewataka Wamachinga kuwa wahaminifu mwenye zoezi la kukopa na waunde vikundi fedha za mikopo zipo.
Kwa upande wake Katibu tawala Mkoa wa dodoma Dkt. Fatuma Mganga amesema Kuwa kuna mifuko zaidi ya 69 inatoa mikopo kwa wafanyabiashara wadogo wadogo pia kuna taasisi za fedha hivyo mikopo ipo kila mmoja atapata mkopo huo kwa kufata taratibu zilizopo.
Mwisho
BMH YATOA MATIBABU YA MOYO KWA WATOTO
Na Wellu Mtaki, Dodoma
BMH IMEAZA KUTOA MATIBABU YA MOYO KWA WATOTO.
HOSPITALI ya Benjamin Mkapa (BMH),
imeanza kufanya upasuaji wa moyo kwa watoto waliobainika kuzaliwa na matatizo ya moyo ambapo tayari watoto 10 wameshahudumiwa.
Pia Serikali imeokoa zaidi ya Shilingi bilioni 2.3 kutokana na huduma za upandikizaji wa figo kwa wagonjwa 31 ambao wametibiwa kwa gharama ya Shilingi milioni 25 ambapo wangeenda kutibiwa nje ya nchi ingegharimu milioni 100 kwa mtu mmoja.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Oktoba 26, 2022,Mganga mkuu wa BMH Dk. Alphonce Chandika wakati akitoa taarifa ya utekelezaji na vipaumbele vya hospitali hiyo kwa mwaka 2022/ 2023 amesema wamefanikiwa kutoa huduma za matibabu ya moyo kwa kuwa na maabara maalum inayotumika katika kutoa matibabu ya moyo pasipo kufungua kifua.
Dk. Chandika ameeleza kuwa kuna wagonjwa nane ambao mapigo yao ya moyo yanashuka sana, walihudumiwa katika Hospitali ya Benjamin Mkapa kwa kupandikizwa betri kwenye moyo na kupitia maabara hiyo wameweza kuhudumia watoto 14 waliozaliwa na matatizo ya moyo.
Amesema wagonjwa 39 waliobainika kuwa na matatizo makubwa ya moyo wamehudumiwa kwa kuwekewa vipandikizi na kati ya 39, wagonjwa wawili kati yao walihudumiwa kwa dharura ambapo kama ingekuwa ni kusafirishwa kwenda kupatiwa matibabu Dar es Salaam wangepoteza maisha.
Ameongeza kuwa hospitali BMH ni ya pili hapa nchini kutoa huduma hiyo na kwamba tangu mwaka 2019, na kwamba jumla ya wananchi 715 wamehudumiwa kwa kuchunguzwa.
Daktari huyo amebainisha kuwa tangu mwaka 2020, Hospitali ilifanikiwa kuanzisha upasuaji wa nyonga na magoti kwa kuweka vipandikizi na tayari wagonjwa 56 wamewekewa vipandikizi hivyo kwa wastani wa gharama ya shilingi milioni 12 ambapo gharama za huduma hizo nchi za nje ni takriban milioni 35.
Aidha ameongeza kuwa huduma hiyo imeshatolewa kwa wagonjwa 148 kwa gharama ya Shilingi milioni 1.2 kwa mgonjwa mmoja, kwa nje ya nchi gharama ni zaidi ya milioni 7 huku akieleza kwamba wagonjwa hao 148, Serikali imeokoa zaidi ya Shilingi milioni 850.
Ikumbukwe kuwa jitihada za Serikali kuhakikisha inawaletea wananchi huduma za afya zilizo bora, ilidhamiria kuiwezesha Hospitali ya Benjamini Mkapa kuwa na vifaa tiba vya kisasa na vinavyotumia teknolojia ya kisasa ili iweze kukidhi adhma yake ya kuwahudumia wananchi hao kwa kuwapatia matibabu ya kiwango cha juu.
Mwisho
HAZINA YAKUSANYA BILIONI 852.9
SERIKALI kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina katika mwaka wa fedha 2021/22 imekusanya 852.9 sawa na asilimia 109.5 ya lengo kutoka katika kampuni ambazo serikali inamiliki hisa.
Imesema ongezeko hilo linatokana na uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan ambapo ni zaidi ya kiasi kilichokusanywa Juni 30 mwaka jana ambacho ni sh. bilioni 638.87.
Hayo yalibainishwa jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Uwekezaji wa Umma, Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH), Lightness Mauki, wakati akizungumza na wandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa majukumu na mwelekeo wa ofisi hiyo katika mwaka huu wa fedha.
Alisema fedha hizo zimekusanywa katika mapato yasiyo na kodi ambayo yanajumuisha gawio, michango ya asilimia 15 ya mapato ghafi na mapato mengineyo kutoka katika taasisi 287 zilizo chini ya ofisi ya msajiri.
“Kuongezeka kwa makusanyo hayo kunatokana na kuimarisha usimamizi,ufuatiliaji na tathmini ya uwekezaji wa mitaji ya umma pamoja na hatua ambazo zilichukuliwa katika kukuza mapato na kudhibiti matumzi.
Aliongeza kuwa:"Hadi kufikia Juni 30 mwaka huu Ofisi ya Msajili wa hazina ilikuwa inasimamia mashirika ya umma 287 Kati ya mashirika hayo 237 serikali ina hisa zaidi ya asilimia 51, taasisi 40 serikali inahisa chache na 10 za nje ya Nchi ambazo serikali imeweka uwekezaji.
Lightness alisema serikali imewekeza kwenye mashirika hayo fedha sh.trilioni 70.
Alisema kuwa serikali kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina imeendelea na juhudi za kusimamia utendaji wa kampuni ambazo serikali inaumiliki wa hisa chache.
Pia, alisema serikali inafanya majadiliano na wabia wenza na kusimamia kwa ukaribu matumizi yasiyo ya lazima, hivyo kuchangia ongezeko la gawio.
"Mathalani mafanikio ya jitihada hizo yamejidhihirisha katika utendaji wa Banki ya NBC ambayo imeongeza faida kabla ya kodi kutoka sh. bilioni 7 mwaka 2020 hadi sh. bilioni 60 mwaka jana, ikiwa ni ongezeko la asilimia 757, ukuaji huu wa faida umewezesha benki kutoa gawio kwa serikali sh. bilioni 4.5 kiasi ambacho hakijawahi kufikiwa,"alieleza.
Akitaja mafaniko ya Ofisi hiyo Lightness alisema wameweza kufanya upanuzi wa kiwanda cha sukari cha Kilombero ambacho serikali inamiliki asilimia 25 ya hisa.
Alisema kutokana na kukua kwa mahitaji ya sukari nchini kulikuwa na uhitajio wa kupanua kiwanda cha sukari hicho ili kutimiza mahitaji.
“Bodi ya wakurugenzi baada ya kufanya upembuzi yakinifu iliwasilisha mapendekezo ya kupanua kiwanda hicho ambapo sh. bilioni 571.6 zilitumika, uwekezaji huo unatarajia kuongeza kiwango cha uzalishaji sukari hadi kufikia tani 271,000 kutoka tani 127,000 za sasa,” alisema.
.
Friday, May 20, 2022
KEDA YATOA MSAADA WA MARUMARU ZA MAMILIONI KWENYE SHULE ZA SEKONDARI
KIWANDA cha kutengeneza Marumaru cha Keda (T) Ceramics Co. Ltd kilichopo Pingo Halmashauri ya Chalinze wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani kimetoa Marumaru zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 20 kwa shule za Pera na Msata.
Akizungumza mara baada ya kuzikabidhi shule hizo Ofisa Tawala wa kiwanda hicho George Lulandala alisema kuwa maramaru hizo ni kwa ajili ya kuweka mazingira mazuri ya usomaji kwa wanafunzi.
Lulandala alisema kuwa wametoa vifaa hivyo ikiwa ni sehemu ya kurudisha mchango wao kwa jamii ambapo wamekuwa wakishiriki shughuli za wananchi ili kuwaletea maendeleo.
"Tumeamua kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan kwani ameonyesha kuwajali wananchi wakiwemo wanafunzi ambapo amefanya mambo mengi kwenye sekta ya elimu ikiwemo ujenzi wa madarasa na miundombinu,"alisema Lulandala.
Alisema kuwa wameamua kuunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan za kuboresha mazingira ya elimu ili wanafunzi wasome katika mazingira mazuri ambayo yatawafanya wapate uelewa vizuri.
"Sekondari ya Msata imepatiwa maboksi 203 huku Pera Sekondari wakipata maboksi 100 na bado tutaendelea kutoa misaada mbalimbali ili kuhakikisha kuboresha sekta mbalimbali,"alisema Lulandala.
Aidha alisema kuwa kwa kipindi cha nyuma walisaidia kituo cha afya cha Pera na huduma mbalimbali kwa wananchi kwenye maeneo mbalimbali kwenye wilaya na mkoa.
"Tunafanya jitihada mbalimbali kusaidia masuala ya jamii hivyo hata wadau wengine nao wanapaswa kuisaidia serikali ili iweze kuwahudumia wananchi wake,"alisema Lulandala.
Naye Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Iddi Ng'oka alisema kuwa wanashukuru kiwanda hicho kwa msaada walioutoa kwani bila ya kuweka Marumaru sakafu imekuwa ikiharibika mara kwa mara.
Ng'oka alisema kuwa wanaomba wapewe tena maramaru kwani kuna baadhi ya madarasa hayana Marumaru pamoja na ofisi hivyo wakipatiwa nyingine itasaidia sana.
Mwisho.
Thursday, September 12, 2019
CCM YACHANGIA MABATI 500 ELIMISHA KIBAHA
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM)Taifa kimekabidhi mabati 500 kwa ajili ya kuunga mkono kampeni ya wilaya ya Kibaha ya Elimisha Kibaha yenye lengo la kujenga madarasa ili kukabiliana na changamoto upungufu wa madarasa 65 unayoikabili wilaya hiyo.
Akikamkabidhi mabati hayo mkuu wa wilaya ya Kibaha Assumter Mshama ambaye ndiyo muasisi wa kampeni hiyo katibu Itikadi na Uenezi wa CCM Humphrey Polepole alisema kuwa wameamua kuunga mkono kampeni hiyo ambayo inaisaidia serikali na inatekeleza ilani ya chama ambayo inatekelezwa na Rais ya kutoa elimu bila ya malipo kwa shule za msingi na sekondari.
Polepole alisema kuwa tangu Rais Dk John Magufuli alivyotangaza elimu bure kumekuwa na ongezeko kubwa la wanafunzi zaidi ya mara tatu na hivyo kuongeza mahitaji ya uhaba wa madarasa, madawati na walimu ambalo serikali inalifanyia kazi na wamesha ongea na Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali ya Mitaa (TAMISEMI) ili Kibaha ipewe kipaumbele kwenye mgawanyo wa walimu.
“Wakuu wa chama wamefurahi sana kwa hili lililofanywa na waliridhia mimi kuja kushiriki nanyi na tunapopata watendaji na viongozi wa serikali wanaojituma wanapaswa kuungwa mkono na kusimama nao na ndiyo tuliweka ahadi ya chama ya kuchangia mabati 600 na tumeanza na mabati 500 kwa awamu hii ya kwanza na awamu ya pili tutatoa mabati 100 na mifuko ya saruji 100,” alisema Polepole.
Alisema kuwa wanafurahishwa na kazi inayofanyika kwani inatekeleza ilani ya chama na uongozi wa wilaya umepanda mbegu bora kwani kwani mkuu wa wilaya ya Kibaha amepanda kitu kizuri na viongozi wengine wamepata hamasa kwani wameanza kufanya kama yeye hiyo ni hamasa si lazima kusubiri fedha ya serikali kwani wananchi wako tayari kuchangia maendeleo yao wenyewe.
“Tunataka viongozi wahamasishe umma kama ulivyofanya wewe angalia tumeokoa shilingi ngapi kwa jitihada mlizozifanya kwa madarasa 26 ya mwanzo kati ya 65 yanayotarajiwa kujengwa kupitia kampeni hiyo ambapo fedha zilizookolewa zitakwenda kusaidia wale ambao hawajaweza kufanya kama mlivyofanya nyie Kibaha huu ndiyo uongozi unaotakiwa,” alisema Polepole.
Alisema viongozi wanapaswa kufanya mambo mema ya maendeleo kama hakuna watu wanaowaona hiyo ndiyo tafsiri ya uongozi au mtumishi mwadilifu usifanye ili watu waone kwani watakuwa si waadilifu bali wafanye kama jambo binafsi fanya kama lako mwenyewe na wakipatikana viongozi kama hao ambapo wapo tayari watamsaidia Rais kwa ndoto za kuibadilisha nchi zitatimia mapema kabla ya muda.
Awali mkuu wa wilaya ya Kibaha Assumter Mshama alisema kuwa baada ya uzinduzi wa kampeni hiyo iliyofanyika hivi karibuni walipata vifaa na fedha zilizokusanywa vitatosha ujenzi wa madarasa 26 kwa Halmashauri mbili za Kibaha Mjini na Wilaya ya Kibaha ambapo kila moja imeanza ujenzi wa madarasa 13.
Mshama alisema kuwa ujenzi wa madarasa hayo umeanza baada ya wakurugenzi wa Halmashauri hizo kupatiwa vifaa vya ujenzi ili kukabiliana na changamoto ya upungufu wa madarasa 65 ambayo thamani yake ni shilingi bilioni 1.3 na hii imetokana na idadi kubwa ya wanafunzi wanaofaulu darasa la saba.
Kumekuwa na ongezeko kubwa la wanafunzi wanaofaulu darasa la saba ambapo kwa mwaka 2017 jumla ya wanafunzi walifaulu 3,560, mwaka 2018 wanafunzi 3,938 walifaulu na mwaka 2019 wanafunzi waliongezeka na kufika 4,930 hali ambayo imesababisha kuwa na upungufu mkubwa wa madarasa hayo yanayohitajika.
Mwisho.
ReplyForward
|
Friday, December 29, 2017
RC NDIKILO AIPIGA TAFU KILUVYA UNITED MILIONI MBILI
Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo |
Baadhi ya wachezaji wa Kiluvya United inayoshiriki ligi daraja la kwanza wakimskiliza mkuu wa mkoa wa Pwani hayupo pichani walipomtembelea ofisini kwake mjini Kibaha |
Nahodha wa Timu ya Kiluvya United ya mkoani Pwani Ramadhan akishukuru baada ya kukabidhiwa fedha kwa ajili ya hamasa na mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo. |
Na John Gagarini, Kibaha
KUELEKEA mchezo wake wa ligi daraja la Kwanza leo dhidi ya
Ruvu kuwania kupanda Ligi Kuu unaotarajiwa kuchezwa kwenye uwanja wa Filbert Bayi wilayani Kibaha
mkoa wa Pwani umeipatia timu ya Kiluvya United kiasi cha shilingi milioni mbili
kwa ajili ya hamasa ili waweze kushinda mchezo huo.
Akizungumza wakati wa kukabidhi fedha hizo kwa viongozi wa
timu hiyo walioambatana na wachezaji ofisini kwake mjini Kibaha mkuu wa mkoa wa
Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo alisema kuwa lengo ni kuhakikisha wanashinda
mchezo huo.
Ndikilo alisema kuwa viongozi wa timu hiyo walifika ofisini
kwake na kuomba msaada wa kuisaidia timu yao ili iweze kufanya vizuri kwenye
michezo yake mitano iliyosalia ya ligi hiyo na endapo watashinda watafanikiwa
kupanda Ligi Kuu ya Voda Com.
“Tuko pamoja na timu yetu ambayo inawakilisha mkoa na leo tunawakabidhi
fedha ambazo zimetolewa na wadau wa mkoa ili kufanikisha malengo ya kupanda
Ligi Kuu kwani uwezekano huo upo,” alisema Ndikilo.
Alisema kuwa wadau wanachotaka ni timu yao kushinda kwani imeonyesha
ina uwezo wa kufanya hivyo kutokana na uwezo inaounyesha wanaamini inaweza
kufanya vizuri na kujiweka kwenye nafasi nzuri ya harakati zake za kiutaka
kupanda daraja ili kufikia Ligi Kuu ya Voda Com.
“Wadau wa soka wa mkoa wa Pwani wamejitolea fedha hizo kama
hamasa ya kufanya vyema kwenye mchezo wa leo ambao utakuwa na ushindani mkubwa
kwani timu hizo ziko kwenye nafasi nzuri ya kupanda Ligi Kuu ambapo Ruvu ndiyo
kinara wa kundi hilo na United wakiwa kwenye nafasi ya tatu,” alisema Ndikilo.
Aidha alisema kuwa mdau ambaye anataka kuipeleka timu ya
Kiluvya United nchi ya Ulaya ya Finland atafurahi kuona timu hiyo inashinda
mchezo huo na kutoa zawadi ya mwaka mpya kwa wadau wa mkoa wa Pwani.
Naye nahodha wa timu hiyo Ramadhan Ally alisema kuwa wao wkao
tayari kwa pambano hilo na watahakikisha wanapambana kwa nguvu zote ili wapate
ushindi na kujiweka vizuri kwenye harakati zao za kupanda daraja.
Ally alisema kuwa kutokana na kupewa fedha hizo zitawasaidia
kama morali kwao kwa ajili ya kupata ushindi huo ambao utakuwa muhimu ili
kuwapa raha watu wa mkoa wa Pwani.
Mwisho.
MWENYEKITI UVCCM AWASHUKIA WATENDAJI WA SERIKALI NA VIONGOZI WA KUCHAGULIWA
Moja ya Vijana wa UVCCM Kibaha Mjini akimvalisha skafu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Kheri James alipowasili wilayani Kibaha |
Baadhi ya Vijana wa UVCCM Mkoani Pwani wakishanglia jambo wakati wa mkutano huo |
Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo akiongea kwenye mkutano huo. |
Na John Gagarini, Kibaha
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha
Mapinduzi (UVCCM) Taifa Kheri James amewataka viongozi wa serikali na
wale wa kuchaguliwa nchini kuhakikisha wanashiriki kwenye mikutano ya
viongozi wa kitaifa ili waweze kupokea maagizo mbalimbali.
Aliyasema
hayo mjini Kibaha wakati wa sherehe za kumpongeza kwa kuchaguliwa
kwenye nafasi hiyo zilizoandaliwa na Uvccm Kibaha Mjini na kusema kuwa
maagizo yanayotolewa hayawezi kufanyiwa kazi kutokana na wahusika
kutokuwepo.
James alisema kuwa viongozi na watendaji wa serikali ambao hawashiriki vikao kama hivyo hawafai waondoke kwani wameshindwa kazi.
"Hapa
tunatoa maagizo na wao hawapo kwani maelekezo hayo yanapotolewa watu wa
kuyapokea hawapo kuanzia ngazi ya halmashauri za wilaya, wilaya na Mkoa
wanapaswa kujirekebisha kama wanaona hawawezi kazi watupishe," alisema
James.
Alisema kuwa
maelekezo yanayotolewa ni kuzikabili changamoto ambapo atendaji wa
serikali wanaposhindwa kutatua kero za wananchi ambazo ni ilani ya chama
kuna sababisha chama kuwa na wakati mgumu nyakati za uchaguzi kwa
wagombea wa ccm.
"Watendaji wanaohujumu waondoke kwani wao ndiyo watekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa ajili ya wananchi," alisema James.
"Viongozi
hawapaswi kulewa madaraka ambayo ni kitu kibaya sana na ni sawa na
ulevi na hutafsiriwa baada ya muda wa kuwa madarakani kwisha ambapo watu
watakuhukumu kwa matendo yako na kuwa bakora ya kukuchapia," alisema
James.
Alisema kuwa
hataki uongozi wa mitandao wa fb,insta, WhatsApp anataka viongozi wa
kufanya kazi kwani kazi ya kuongoza ni ngumu sana hasa wakati wa
kuhakiki mali za jumuiya hiyo watapambana na watu wenye vyeo vikubwa na
fedha nyingi hivyo ni vita kubwa.
Aidha
aliwata viongozi wa chama kutowatumia tu vijana wakati wa uchaguzi
wasiwafanye kama ngazi ya kupandia na kama hawatawashirikisha vijana
wampe taarifa na suala la ajira liangaliwe kwani baadhi ya wafanyakazi
wanaajiriwa toka nje kwa kazi zinazowezwa kufanywa na watanzania.
"Wamiliki
waangalie maslahi ya wafanyakazi vitendea kazi kwani baadhi wanafanya
kazi kwenye viwanda ambvyo huzalisha kwa kutumia kemikali ambazo
zinaweza kuwa maafa endapo hawatapewa vifaa vya kuwakinga kwani inaweza
kusababisha vifo kwani viwanda si kwa ajili ya kusababisha vifo,"
alisema James.
Aliwataka
wabunge wasiwe wa mifukoni wakichaguliwa wanaondoka na kusubiri hadi
muda wa uchaguzi kwa sasa hawana nafasi wanajitokeza muda huo na kuanza
vurugu wakidai fulani anampinga kumbe hawakuwajibika na kujiweka mbali
na wananchi pia viongozi wa chama pamoja madiwani kuhakikisha kuwa
asilimia tano ya vijana inakuwa agenda ya kudumu kwenye vikao
mbalimbali.
Kwa upande
wake Mwenyekiti wa ccm Mkoa Pwani Ramadhan Maneno alisema kuwa
watahikikisha wana hakiki mali za umoja huo wakiwa kama wasimamiaji wa
jumuiya zote za chama.
Awali
mwenyekiti wa umoja huo Chalangwa Seleman wa mkoa alitaka viongozi
kufuata maelekezo ya rais ili kufanya umoja huo kuwa kimbilio na
watayatrkeleza yale yote yaliyotolewa na mwenyekiti wao.
Subscribe to:
Posts (Atom)