Friday, December 29, 2017

MWENYEKITI UVCCM AWASHUKIA WATENDAJI WA SERIKALI NA VIONGOZI WA KUCHAGULIWA

 
 Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Kheri James akisalimiana na mwenyekiti wa UVCCM Kibaha Mjini Azilongwa wakati alipowasili wilayani Kibaha kwenye mkutano wa kumpongeza kuchaguliwa kwenye nafasi hiyo uliofanyika kata ya Kongowe. 

 Moja ya Vijana wa UVCCM Kibaha Mjini akimvalisha skafu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Kheri James alipowasili wilayani Kibaha

 Baadhi ya Vijana wa UVCCM Mkoani Pwani wakishanglia jambo wakati wa mkutano huo

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo akiongea kwenye mkutano huo.
 
 
Na John Gagarini, Kibaha
 
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Kheri James amewataka viongozi wa serikali na wale wa kuchaguliwa nchini kuhakikisha wanashiriki kwenye mikutano ya viongozi wa kitaifa ili waweze kupokea maagizo mbalimbali.

Aliyasema hayo mjini Kibaha wakati wa sherehe za kumpongeza kwa kuchaguliwa kwenye nafasi hiyo zilizoandaliwa na Uvccm Kibaha Mjini na kusema kuwa maagizo yanayotolewa hayawezi kufanyiwa kazi kutokana na wahusika kutokuwepo.

James alisema kuwa viongozi na watendaji wa serikali ambao hawashiriki vikao kama hivyo hawafai waondoke kwani wameshindwa kazi.

"Hapa tunatoa maagizo na wao hawapo kwani maelekezo hayo yanapotolewa watu wa kuyapokea hawapo kuanzia ngazi ya halmashauri za wilaya, wilaya na Mkoa wanapaswa kujirekebisha kama wanaona hawawezi kazi watupishe," alisema James.

Alisema kuwa maelekezo yanayotolewa ni kuzikabili changamoto ambapo atendaji wa serikali wanaposhindwa kutatua kero za wananchi ambazo ni ilani ya chama kuna sababisha chama kuwa na wakati mgumu nyakati za uchaguzi kwa wagombea wa ccm.

"Watendaji wanaohujumu waondoke kwani wao ndiyo watekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa ajili ya wananchi," alisema James.

"Viongozi hawapaswi kulewa madaraka ambayo ni kitu kibaya sana na ni sawa na ulevi na hutafsiriwa baada ya muda wa kuwa madarakani kwisha ambapo watu watakuhukumu kwa matendo yako na kuwa bakora ya kukuchapia," alisema James.

Alisema kuwa hataki uongozi wa mitandao wa fb,insta, WhatsApp anataka viongozi wa kufanya kazi kwani kazi ya kuongoza ni ngumu sana hasa wakati wa kuhakiki mali za jumuiya hiyo watapambana na watu wenye vyeo vikubwa na fedha nyingi hivyo ni vita kubwa.

Aidha aliwata viongozi wa chama kutowatumia tu vijana wakati wa uchaguzi wasiwafanye kama ngazi ya kupandia na kama hawatawashirikisha vijana wampe taarifa na suala la ajira liangaliwe kwani baadhi ya wafanyakazi wanaajiriwa toka nje kwa kazi zinazowezwa kufanywa na watanzania.

"Wamiliki waangalie maslahi ya wafanyakazi vitendea kazi kwani baadhi wanafanya kazi kwenye viwanda ambvyo huzalisha kwa kutumia kemikali ambazo zinaweza kuwa maafa endapo hawatapewa vifaa vya kuwakinga kwani inaweza kusababisha vifo kwani viwanda si kwa ajili ya kusababisha vifo," alisema James.

Aliwataka wabunge wasiwe wa mifukoni wakichaguliwa wanaondoka na kusubiri hadi muda wa uchaguzi kwa sasa hawana nafasi wanajitokeza muda huo na kuanza vurugu wakidai fulani anampinga kumbe hawakuwajibika na kujiweka mbali na wananchi pia viongozi wa chama pamoja madiwani kuhakikisha kuwa asilimia tano ya vijana inakuwa agenda ya kudumu kwenye vikao mbalimbali.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa ccm Mkoa Pwani Ramadhan Maneno alisema kuwa watahikikisha wana hakiki mali za umoja huo wakiwa kama wasimamiaji wa jumuiya zote za chama.

Awali mwenyekiti wa umoja huo Chalangwa Seleman wa mkoa alitaka viongozi kufuata maelekezo ya rais ili kufanya umoja huo kuwa kimbilio na watayatrkeleza yale yote yaliyotolewa na mwenyekiti wao.

No comments:

Post a Comment