Sunday, November 26, 2017

WANAONUNUA KOROSHO KINYUME CHA UTARATIBU WAKAMATWE-RC

Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo akizindua ununuzi wa zao la korosho wilayani Kibiti 

 Baadhi ya viongozi wa wilaya za mkoa wa Pwani wakati wa uzinduzi wa zao la korosho wilayani Kibiti

 Baadhi ya wanunuzi waliohudhuria mnada wa kwanza wa uuuzaji zao la korosho uliofanyika Kibiti mkoani Pwani

 Wadau wa zao la korosho wakiptia taarifa mbalimbali juu ya uuzaji wa zao la korosho mkoani Pwani

Na John Gagarini, Mkuranga

MKUU wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo amewataka wakuu wa Polisi wa wilaya kuwakamata wafanyabiahara ambao watanunua zao la korosho la msimu huu kinyume cha utaratibu ikiwemo wale wanaonunua kwa njia ya “Kangomba”.

Ndikilo aliyasema hayo wilayani Mkuranga wakati wa mkutano na viongozi wa vyama vya wakulima wa zao la Korosho mkoani humo na kusema kuwa kwa msimu huu hataki kuona walanguzi wa zao hilo kwani wanawanyonya wakulima.

Alisema kuwa ununuzi kwa njia ya Kangomba ni marufuku na atakayekamatwa ananunua kwa njia hiyo ambayo inawanyonya wakulima haitakiwi.

“Ununuzi kwa njia ya Kangomba ni marufuku mauzo yote yafanyike kwa njia yam nada kwa kutumia stakabadhi ghalani hayo ndi maelekezo ya serikali atakayenunua tofauti na utaratibu huo akamatwe wakuu wa polisi wa wilaya fanyeni kazi msiwaonee huruma walanguzi wawekeni ndani,” alisema Ndikilo.

Aliitaka bodi ya korosho kuhakikisha inakabili changamoto za upatikanaji wa magunia ili korosho zilizovunwa zisiharibike na kuuzwa kwa bei ndogo kwenye soko la korosho ambapo unuzi unaanza Novemba 8 mwaka huu.

Kwa upande wake meneja wa bodi ya Korosho tawi la Dar es Salaam Mangile Malegesi alisema kuwa msimu wa zoa hilo kwa mkoa wa Pwani utazinduliwa wiki ijayo ambapo kwa mikoa ya Lindi na Mtwara msimu umeshazidnuliwa.

Malegesi alisema kuwa magunia yatapatikana kwa wakati ili wakulima waweze kuhifadhi korosho zao ambapo bei elekezi ni shilingi 1,460 kwa daraja la kwanza na 1,160 kwa daraja la pili.

Naye mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika Mkoa wa Pwani (CORECU) Rajabu Ngonema alisema kuwa changamoto kubwa iliyopo ni magunia na wakulima kutaka kuuza korosho zao kwenye maghala ya vyama vya msingi badala ya kuuza kwenye maghala makuu yaliyopitishwa na bodi ya Korosho.

Ngonema alisema kuwa maghala ni changamoto kubwa kwani wakulima wanahofia gharama na usumbufu na kutaka wauzie kwenye maghala ya vyama vya msingi.

Mwisho.  

No comments:

Post a Comment